ARUSHA: Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiAfrica, Maxence Melo amesema “JamiiAfrica ipo tayari kuwapokea Watu kutoka Vyuoni kuwajengea Uwezo wa masuala ya Uhakiki wa Taarifa kwa Wanahabari, tunapoelekea katika Uchaguzi Mkuu ni wakati muhimu ambao tunaweza kutoa Elimu hiyo.”
Ameongeza “Tuna Mkataba wa ushirikiano na Vyuo kadhaa ikiwemo UDSM, SAUT na UDOM. Tunapoelekea hatuwezi kufanya kila kitu peke yetu, ndio maana tuna Mikataba na Redio za Kijamii 15 kwaajili ya kutoa Elimu hiyo, hatuwezi kufanikiwa kupitia ushirikiano wa UTPC peke yake"
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #FactChecking
Ameongeza “Tuna Mkataba wa ushirikiano na Vyuo kadhaa ikiwemo UDSM, SAUT na UDOM. Tunapoelekea hatuwezi kufanya kila kitu peke yetu, ndio maana tuna Mikataba na Redio za Kijamii 15 kwaajili ya kutoa Elimu hiyo, hatuwezi kufanikiwa kupitia ushirikiano wa UTPC peke yake"
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #FactChecking
👍1
ARUSHA: Akizungumzia kuhusu kuwawezesha Wanawake kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 katika masuala ya Uhakiki wa Taarifa, Mkurugenzi Mtendaji wa #JamiiAfrica, Maxence Melo amesema Taasisi hiyo imekuwa ikitoa mafunzo ya kuwajengea uwezo Wadau wa Habari Wanawake na programu hizo zimekuwa zikiendelea
Amesema “Tulikuwa na Mradi maalumu pamoja na WiLDAF kuhusu kuwajengea uwezo Wanawake, pia kama kuna mapendekezo mengine yoyote kutoka kwa Wadau tupo tayari kuyapokea na ikiwezekana kushirikiana nao.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis04
Amesema “Tulikuwa na Mradi maalumu pamoja na WiLDAF kuhusu kuwajengea uwezo Wanawake, pia kama kuna mapendekezo mengine yoyote kutoka kwa Wadau tupo tayari kuyapokea na ikiwezekana kushirikiana nao.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis04
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
BUNGENI: Mbunge wa Viti Maalum, Christina Mnzava amehoji mpango wa Serikali wa kuja na sera ya kuwapatia posho Wazee wote wa Tanzania Bara, kama ilivyo Visiwani Zanzibar
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Patrobas Katambi amesema wamelipokea na wataendelea kulifanyia kazi kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara husika ili kuona hali ya Kiuchumi kama itaruhusu basi litatekelezwa
Zaidi https://jamii.app/PoshoWazee
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #ServiceDelivery #Governance
Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Patrobas Katambi amesema wamelipokea na wataendelea kulifanyia kazi kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara husika ili kuona hali ya Kiuchumi kama itaruhusu basi litatekelezwa
Zaidi https://jamii.app/PoshoWazee
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #ServiceDelivery #Governance
ARUSHA: Akisoma maazimio ya Wadau wa Habari katika kuadhimisha Miaka 32 ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2025, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiAfrica, Maxence Melo amesema Wadau wa Sekta ya Habari Nchini wanaungana kuendeleza na kulinda misingi ya Uhuru, Uwazi na Kujisimamia kwa Vyombo vya Habari
Amesema Kaulimbiu ya Mwaka 2025 ya “Uhabarishaji katika Dunia Mpya: Mchango wa Akili Mnemba kwenye Uhuru wa Vyombo vya Habari,” inaakisi mabadiliko makubwa ya Kidigitali yanayoendelea kuibadilisha Tasnia ya Habari Duniani kote
Ameeleza kuwa Teknolojia ya Akili Mnemba (AI) inabadilisha kwa kasi namna taarifa zinavyokusanywa, kuchakatwa na kusambazwa.
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Amesema Kaulimbiu ya Mwaka 2025 ya “Uhabarishaji katika Dunia Mpya: Mchango wa Akili Mnemba kwenye Uhuru wa Vyombo vya Habari,” inaakisi mabadiliko makubwa ya Kidigitali yanayoendelea kuibadilisha Tasnia ya Habari Duniani kote
Ameeleza kuwa Teknolojia ya Akili Mnemba (AI) inabadilisha kwa kasi namna taarifa zinavyokusanywa, kuchakatwa na kusambazwa.
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
ARUSHA: Maazimio ya Wadau wa Habari katika kuadhimisha Miaka 32 ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2025 yanaeleza kuwa Teknolojia inaleta fursa kubwa katika kuongeza ufanisi wa Uandishi wa Habari, Upatikanaji wa taarifa na kutatua changamoto ya utofauti katika Lugha
Akisoma maazimio hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiAfrica, Maxence Melo ameeleza Teknolojia inaibua changamoto mpya kama vile upendeleo wa kimfumo, (Algorithmic bias), taarifa potofu, Migogoro ya Maadili na hatari kwa Uadilifu wa habari
Kwa muktadha huo, kuna haja ya kuweka uwiano sahihi kati ya ubunifu wa Kiteknolojia na Uwajibikaji ili kuhakikisha Uhuru wa Vyombo vya Habari unadumishwa katika zama hizi za Kidijitali.
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Akisoma maazimio hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiAfrica, Maxence Melo ameeleza Teknolojia inaibua changamoto mpya kama vile upendeleo wa kimfumo, (Algorithmic bias), taarifa potofu, Migogoro ya Maadili na hatari kwa Uadilifu wa habari
Kwa muktadha huo, kuna haja ya kuweka uwiano sahihi kati ya ubunifu wa Kiteknolojia na Uwajibikaji ili kuhakikisha Uhuru wa Vyombo vya Habari unadumishwa katika zama hizi za Kidijitali.
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
ARUSHA: Nuzulack Dausen, Mkurugenzi wa Nukta Africa anasema kuna Watu wanaanzisha taarifa potoshi wakiwa na lengo la kujiingizia kipato kutokana na kuamini wanapofanya hivyo wakitumia njia za kuvutia inaweza kuwavutia Watu kubonyeza au kufuatilia taarifa zao
Ameeleza kuwa wengine wanafanya taarifa hizo makusudi kwasababu zao za Kisiasa. Wanaweza kufanya hivyo kwa lengo la kuhamisha fikra za Watu ili waache kujadili kitu fulani na wajadili suala analotaka yeye
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #FactChecking
Ameeleza kuwa wengine wanafanya taarifa hizo makusudi kwasababu zao za Kisiasa. Wanaweza kufanya hivyo kwa lengo la kuhamisha fikra za Watu ili waache kujadili kitu fulani na wajadili suala analotaka yeye
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #FactChecking
Filamu ya Makala ya #BloodParliament inaonesha ushahidi wa video na picha zaidi ya 5,000, ikiwemo Matukio ya Polisi wakifyatua risasi kwa #Waandamanaji karibu na majengo ya Bunge Juni 25, 2024. Pia, inawataja Maafisa wa Usalama wanaodaiwa kutoa amri za kuua, pamoja na wale waliotekeleza mauaji hayo
Katika Maandamano hayo ya #RejectFinanceBill2024 ya Juni na Julai 2024, zaidi ya Watu 60 waliuawa huku Polisi wakitumia nguvu kupita kiasi dhidi ya Waandamanaji, wengi wao wakiwa #GenZ
Wananchi wametoa wito kwa Mamlaka kuwawajibisha Maafisa wote waliohusika na mauaji hayo na kuhakikisha Haki inatendeka kwa waathiriwa na Familia zao
Zaidi https://jamii.app/BloodParliament
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #SocialJustice
Katika Maandamano hayo ya #RejectFinanceBill2024 ya Juni na Julai 2024, zaidi ya Watu 60 waliuawa huku Polisi wakitumia nguvu kupita kiasi dhidi ya Waandamanaji, wengi wao wakiwa #GenZ
Wananchi wametoa wito kwa Mamlaka kuwawajibisha Maafisa wote waliohusika na mauaji hayo na kuhakikisha Haki inatendeka kwa waathiriwa na Familia zao
Zaidi https://jamii.app/BloodParliament
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #SocialJustice
Amani ni zawadi ya thamani isiyolipika. Hakuna mafanikio, uhusiano au nafasi yoyote inayostahili kuipoteza
Chagua yale yanayokuinua, yanayokutuliza na yanayokusaidia kuwa toleo bora la 'wewe'
#JamiiForums #JamiiAfrica #Goodmorning #AmkaNaJF #Maisha
Chagua yale yanayokuinua, yanayokutuliza na yanayokusaidia kuwa toleo bora la 'wewe'
#JamiiForums #JamiiAfrica #Goodmorning #AmkaNaJF #Maisha
👍2
Mdau wa JamiiForums.com ameshauri Watu kutofanya siri kwenye mambo yanayohusu Familia. Amesema fikiria umejenga, huna uliyemshirikisha; una pesa Benki, Biashara, hata Mtoto nje ya Ndoa ila hakuna Ndugu anayemjua. Likitokea la kutokea ghafla, kila kitu kinapoteza maana
Amesema tujifunze kushirikishana, tuache siri zisizo na tija
Mdau, ni jambo gani huwezi kumshirikisha Mtu au Watu wako wa karibu?
Mjadala https://jamii.app/TupunguzeSiri
#JamiiAfrica #JamiForums #Maisha
Amesema tujifunze kushirikishana, tuache siri zisizo na tija
Mdau, ni jambo gani huwezi kumshirikisha Mtu au Watu wako wa karibu?
Mjadala https://jamii.app/TupunguzeSiri
#JamiiAfrica #JamiForums #Maisha
👍1
DAR: Mdau wa JamiiForums.com anadai Desemba 2024, Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, alitoa Miezi Mitatu kwa Mkandarasi wa Barabara ya Msongola - Mbande, kukamilisha Barabara hiyo kabla Mvua za masika kuanza, lakini hadi sasa ujenzi haujaisha na hali inazidi kuwa mbaya
Ametoa Wito kwa Wizara ya Ujenzi kufuatilia changamoto hiyo kwani Wananchi wengi wanategemea njia hiyo lakini kwa sasa wanaweza kutumia hadi Saa 3 kwenye kipande hicho
Zaidi https://jamii.app/BarabaraKisewe
#JamiForums #JamiiAfrica #HudumaZaKijamii #ServiceDelivery #JFMdau2025 #Accountability #Governance
Ametoa Wito kwa Wizara ya Ujenzi kufuatilia changamoto hiyo kwani Wananchi wengi wanategemea njia hiyo lakini kwa sasa wanaweza kutumia hadi Saa 3 kwenye kipande hicho
Zaidi https://jamii.app/BarabaraKisewe
#JamiForums #JamiiAfrica #HudumaZaKijamii #ServiceDelivery #JFMdau2025 #Accountability #Governance
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
#HUDUMAZAKIJAMII: Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko jana, Aprili 29, 2025 akihitimisha kujibu hoja za Wabunge waliochangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara hiyo kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, amesema hakuna jambo linakera Wananchi kama kukatikiwa na Umeme
Amesema "Hakuna jambo linakera Wananchi kama kukatika Umeme hasa kama hawajapewa taarifa na ndio maana tumeamua Kituo chetu cha Huduma kwa wateja tukiimarishe, Umeme unapokatika Watu wapewe taarifa. Tumeamua kila Wilaya na kila Mkoa kuwe na 'magroup' ya WhatsApp, Meneja awe 'admin' kwenye yale magroup kwaajili ya kuwapa taarifa Watu".
Vipi Mdau, upo kwenye 'group' la TANESCO la Wilaya au Mkoa unaoishi? Mara yako ya mwisho kupata taarifa ya kukatika kwa Umeme ni lini?
Mjadala https://jamii.app/KukatikiwaUmeme
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Uwajibikaji #ServiceDelivery
Amesema "Hakuna jambo linakera Wananchi kama kukatika Umeme hasa kama hawajapewa taarifa na ndio maana tumeamua Kituo chetu cha Huduma kwa wateja tukiimarishe, Umeme unapokatika Watu wapewe taarifa. Tumeamua kila Wilaya na kila Mkoa kuwe na 'magroup' ya WhatsApp, Meneja awe 'admin' kwenye yale magroup kwaajili ya kuwapa taarifa Watu".
Vipi Mdau, upo kwenye 'group' la TANESCO la Wilaya au Mkoa unaoishi? Mara yako ya mwisho kupata taarifa ya kukatika kwa Umeme ni lini?
Mjadala https://jamii.app/KukatikiwaUmeme
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Uwajibikaji #ServiceDelivery
Mshiriki wa Stories of Change 2024 anapendekeza kufanyika kwa Kilimo cha Nyasi ambacho kitaongeza Uzalishaji wa Nyasi na kupunguza Migogoro inayojitokeza kati ya Wakulima na Wafugaji na kwenye Maeneo ya Hifadhi na Misitu
Kusoma zaidi Andiko lake tembelea https://jamii.app/KilimoNyasiSOC04
#JamiiForums #JamiiAfrica #SOC2024
Kusoma zaidi Andiko lake tembelea https://jamii.app/KilimoNyasiSOC04
#JamiiForums #JamiiAfrica #SOC2024