This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia Katibu Mkuu wake, John Mnyika kimetoa wito kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP), Camillus Wambura kuwajibika kutokana na tukio la Wanachama na Viongozi wa Chama hicho kudaiwa kukamatwa, kupigwa na kuumizwa na Polisi
Mnyika amesema "Tunamtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), kama haya matendo hayana baraka zake ajitokeze yeye mwenyewe atoe taarifa kwa Umma, juu ya matukio ya kupigwa, kuteswa na kuumizwa kwa Wanachama na Viongozi wa CHADEMA, akitaja idadi halisi, akitaja sababu ya hali hizo na kuwajibika kutokana na hayo"
Zaidi https://jamii.app/MnyikaPressApr30
#JamiiForums #Uwajibikaji #HumanRights #Governance #Democracy
Mnyika amesema "Tunamtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania (IGP), kama haya matendo hayana baraka zake ajitokeze yeye mwenyewe atoe taarifa kwa Umma, juu ya matukio ya kupigwa, kuteswa na kuumizwa kwa Wanachama na Viongozi wa CHADEMA, akitaja idadi halisi, akitaja sababu ya hali hizo na kuwajibika kutokana na hayo"
Zaidi https://jamii.app/MnyikaPressApr30
#JamiiForums #Uwajibikaji #HumanRights #Governance #Democracy
โค1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, John Mnyika amewaonesha Waandishi wa Habari, video ya mtu aliyemtaja kwa jina la Noel akiwa amelala chini baada ya kudaiwa kupigwa rungu la kichwa, kung'atwa na mbwa na kuvunjwa Mguu na Polisi katika eneo la Mahakama ya Kisutu, Aprili 24
Zaidi https://jamii.app/UshahidiCHADEMA
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #Uwajibikaji
Zaidi https://jamii.app/UshahidiCHADEMA
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #Uwajibikaji
Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) imekumbusha Taasisi zote za Umma na binafsi Nchini zinazohusika na kuchakata taarifa binafsi za Watu, kuhakikisha zinajisajili kwenye Mfumo wa Usajili wa #RCMIS kabla ya tarehe ya mwisho, 30 Aprili 2025
Kwa mujibu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya Mwaka 2022 (Sura ya 44), Taasisi yoyote inayokusanya au kuchakata taarifa binafsi, ikiwemo Mashirika ya Umma, Kampuni, Sekta ya 'hospitality', NGOs, Vyombo vya Habari, Shule, Vyuo, pamoja na watoa Huduma za Afya, inatakiwa kuwa imesajiliwa rasmi na PDPC ili kuzingatia matakwa ya Sheria
Imeelezwa, kushindwa kujisajili ni ukiukwaji wa Sheria ambapo mhusika anaweza kutozwa faini ya kati ya Tsh. 100,000 hadi Tsh. 5,000,000 au kifungo cha hadi Miaka Mitano, au vyote kwa pamoja
Soma https://jamii.app/SikuYaMwishoYaUsajili
#JamiiForums #DigitalRights #Governance #HakiYaFaragha #UlinziWaTaarifaBinafsi
Kwa mujibu wa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya Mwaka 2022 (Sura ya 44), Taasisi yoyote inayokusanya au kuchakata taarifa binafsi, ikiwemo Mashirika ya Umma, Kampuni, Sekta ya 'hospitality', NGOs, Vyombo vya Habari, Shule, Vyuo, pamoja na watoa Huduma za Afya, inatakiwa kuwa imesajiliwa rasmi na PDPC ili kuzingatia matakwa ya Sheria
Imeelezwa, kushindwa kujisajili ni ukiukwaji wa Sheria ambapo mhusika anaweza kutozwa faini ya kati ya Tsh. 100,000 hadi Tsh. 5,000,000 au kifungo cha hadi Miaka Mitano, au vyote kwa pamoja
Soma https://jamii.app/SikuYaMwishoYaUsajili
#JamiiForums #DigitalRights #Governance #HakiYaFaragha #UlinziWaTaarifaBinafsi
๐1
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia Tawi lake la Bonyokwa kimemvua rasmi uanachama John Mrema aliyekuwa Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa chama hicho kwa tuhuma za utovu wa nidhamu, dharau kwa mamlaka halali za chama na kukaidi misingi na maadili ya Chama
Kwa mujibu wa barua rasmi ya Aprili 30, 2025 iliyosainiwa na Katibu wa Tawi, Solomini Kagaruki ni kuwa Kamati Tendaji ya Tawi hilo ilikutana Aprili 29, 2025 na kufikia uamuzi huo kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA ya mwaka 2006, toleo la 2019, ibara ya 5.4.3.
Miongoni mwa Tuhuma dhidi ya Mrema ni pamoja na kusambaza barua ya Wito ya Kamati ya Nidhamu kwenye mitandao ya kijamii badala ya kuitikia rasmi. Hata hivyo, Mrema amepewa haki ya kukata rufaa kwa ngazi ya juu endapo hataridhika na uamuzi huo
Zaidi https://jamii.app/JonMremaCDM
#JamiiForums #JamiiAfrica #Democracy #Accountability
Kwa mujibu wa barua rasmi ya Aprili 30, 2025 iliyosainiwa na Katibu wa Tawi, Solomini Kagaruki ni kuwa Kamati Tendaji ya Tawi hilo ilikutana Aprili 29, 2025 na kufikia uamuzi huo kwa mujibu wa Katiba ya CHADEMA ya mwaka 2006, toleo la 2019, ibara ya 5.4.3.
Miongoni mwa Tuhuma dhidi ya Mrema ni pamoja na kusambaza barua ya Wito ya Kamati ya Nidhamu kwenye mitandao ya kijamii badala ya kuitikia rasmi. Hata hivyo, Mrema amepewa haki ya kukata rufaa kwa ngazi ya juu endapo hataridhika na uamuzi huo
Zaidi https://jamii.app/JonMremaCDM
#JamiiForums #JamiiAfrica #Democracy #Accountability
#MAISHA: Unampa Ushauri gani Mdau huyu wa JamiiForums.com ili aweze kuyashinda Mawazo ya kuona anaelekea kufeli Maisha
Mjadala zaidi https://jamii.app/KutoboaMshaharaSerikali
#JamiiForums #LifeLessons #JFStories #JFChitChats #JamiiAfrica
Mjadala zaidi https://jamii.app/KutoboaMshaharaSerikali
#JamiiForums #LifeLessons #JFStories #JFChitChats #JamiiAfrica
๐1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Baada ya kusambaa kwa taarifa za kushambuliwa kwa Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Charles Kitima na Watu wasiojulikana, usiku wa jana Aprili 30, 2025, Jeshi la Polisi limesema linamshikilia Rauli Mahabi โHarajaโ, Mkazi wa Kurasini kutokana na tukio hilo na uchunguzi unaendelea
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema tukio limetokea Saa Nne Usiku maeneo ya TEC - Kurasini, Temeke na kwamba alishambuliwa kichwani na kitu butu akiwa maliwatoni pembeni ya kantini
Muliro amesema Padre Kitima anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan
Soma https://jamii.app/KitimaUpdates
#JFMatukio #JamiiForums #Governance #HumanRights
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro amesema tukio limetokea Saa Nne Usiku maeneo ya TEC - Kurasini, Temeke na kwamba alishambuliwa kichwani na kitu butu akiwa maliwatoni pembeni ya kantini
Muliro amesema Padre Kitima anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan
Soma https://jamii.app/KitimaUpdates
#JFMatukio #JamiiForums #Governance #HumanRights
KENYA: Mbunge wa Chama cha ODM, Charles Were amepoteza maisha baada ya kupigwa risasi akiwa kwenye gari katika mzunguko wa Hifadhi ya City kwenye Barabara ya Ngong Jijini Nairobi kutoka kwa Watu wawili waliokuwa kwenye pikipiki ambao bado hawajatambulika
Mbunge huyo wa Kasipul ambaye chama chake kinaongozwa na Raila Odinga amepigwa risasi Saa 1:30 Usiku, jana Aprili 30, 2025 ambapo mashuhuda wamesema mtu aliyempiga risasi alisogea karibu kabisa katika dirisha la gari na kufyatua risasi kisha kutokomea kusikojulikana
Alikimbizwa Hospitali lakini baadaye ikatangazwa amefariki, Jeshi la Polisi la Kenya bado halijatoa tamko kuhusu tukio hilo
Soma https://jamii.app/RIPCharlesWere
#JamiiForums #KenyanPolitics #HumanRights
Mbunge huyo wa Kasipul ambaye chama chake kinaongozwa na Raila Odinga amepigwa risasi Saa 1:30 Usiku, jana Aprili 30, 2025 ambapo mashuhuda wamesema mtu aliyempiga risasi alisogea karibu kabisa katika dirisha la gari na kufyatua risasi kisha kutokomea kusikojulikana
Alikimbizwa Hospitali lakini baadaye ikatangazwa amefariki, Jeshi la Polisi la Kenya bado halijatoa tamko kuhusu tukio hilo
Soma https://jamii.app/RIPCharlesWere
#JamiiForums #KenyanPolitics #HumanRights
๐1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akizungumzia uamuzi wa baadhi ya kesi kufanyika kwa njia ya Mtandao, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa ametolea mfano Viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA) walitoa tamko linaloashiria uvunjifu wa Amani na Usalama, hali iliyosababisha baadhi ya Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao kwa njia ya Mtandao
Amesema "Watanzania waelewe kuwa Jeshi linapokuwa na taarifa za Kiusalama linashirikiana na Mahakama kutoa Haki ile ile lakini kwa kutumia Teknologia ya Mahakama Mtandao ili kuzuia fujo Mtaani, naomba Watanzania watuelewe.โ
Soma https://jamii.app/BashungwaAprili29
#JamiiForums #Accountability #Governance #HumanRights #CivilRights
Amesema "Watanzania waelewe kuwa Jeshi linapokuwa na taarifa za Kiusalama linashirikiana na Mahakama kutoa Haki ile ile lakini kwa kutumia Teknologia ya Mahakama Mtandao ili kuzuia fujo Mtaani, naomba Watanzania watuelewe.โ
Soma https://jamii.app/BashungwaAprili29
#JamiiForums #Accountability #Governance #HumanRights #CivilRights
โค1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, ameliagiza Jeshi la Magereza kusimamia Sheria na taratibu kwa wanaotaka kuwaona Wafungwa na Mahabusu, akieleza taratibu hizo lazima ziheshimiwe bila upendeleo na hakuna wanaotakiwa kupewa Huduma Maalum (V.I.P)
Soma https://jamii.app/BashungwaAprili29
#JamiiForums #Accountability #Governance #HumanRights #CivilRights
Soma https://jamii.app/BashungwaAprili29
#JamiiForums #Accountability #Governance #HumanRights #CivilRights
JamiiAfrica inawatakia Wafanyakazi wote Maadhimisho mema ya Siku ya Wafanyakazi Duniani
Tukumbuke, nyuma ya kila Huduma bora, Bidhaa nzuri na Maendeleo ya Taifa kuna jasho, Maarifa na Bidii ya Mfanyakazi
Tuendelee kusimamia Haki, Mazingira salama ya Kazi na Maslahi bora kwa Wafanyakazi wote. Bila Mfanyakazi, hakuna Mafanikio
#JamiiAfrica #JamiiForums #MeiMosi2025 #WorkersDay
Tukumbuke, nyuma ya kila Huduma bora, Bidhaa nzuri na Maendeleo ya Taifa kuna jasho, Maarifa na Bidii ya Mfanyakazi
Tuendelee kusimamia Haki, Mazingira salama ya Kazi na Maslahi bora kwa Wafanyakazi wote. Bila Mfanyakazi, hakuna Mafanikio
#JamiiAfrica #JamiiForums #MeiMosi2025 #WorkersDay
โค2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa amesema Jeshi la Magereza kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania litaendelea kuwawezesha Wafungwa na Mahabusu kusikiliza mashauri yao wakiwa Magerezani kupitia Mahakama Mtandao, hasa kunapokuwepo na viashiria vya matishio ya kiusalama
Ameyasema hayo Aprili 30, 2025 alipoambatana na Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), kukagua Makasha ya kisasa ya Mahakama Mtandao yanayowezesha usikilizaji wa mashauri kwa njia ya Kiteknolojia katika Gereza la Isanga -Dodoma
Soma https://jamii.app/BashungwaAprili29
#JamiiForums #Accountability #Governance #HumanRights #CivilRights
Ameyasema hayo Aprili 30, 2025 alipoambatana na Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama (NUU), kukagua Makasha ya kisasa ya Mahakama Mtandao yanayowezesha usikilizaji wa mashauri kwa njia ya Kiteknolojia katika Gereza la Isanga -Dodoma
Soma https://jamii.app/BashungwaAprili29
#JamiiForums #Accountability #Governance #HumanRights #CivilRights
๐1
DAR: Akizungumzia tukio la Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima kujeruhiwa, Rais wa TEC, Askofu Wolfgang Pisa amesema eneo alikoshambuliwa hulitumia kufanyia kazi zake baada ya shughuli za pamoja na hakuwa anapata kinywaji, wala si sehemu kunakopatikana kinywaji chochote
Askofu Pisa amesema Padri Kitima alikuwa na Mapadri wenzake katika kikao, walipomaliza wenziwe waliondoka, akabaki eneo la mgahawa anakofanyia shughuli zake siku zote na kuwa hakuna baa wala vinywaji na kama kuna anayehitaji kupata vinywaji kwa kawaida angeenda nje ya eneo hilo
Ameongeza โMaana ukisema Mtu alikuwa anakunywa kwa saa zote hizo maana yake alikuwa anakunywa pombe, si hivyo. Wakati anatoka kurejea ndani kuna uchochoro wenye giza, hapo ndipo akavamiwa na kujeruhiwa na kitu kizito kichwani na kidevuniโ
Soma https://jamii.app/TECPadriKitima
#JFMatukio #JamiiForums
Askofu Pisa amesema Padri Kitima alikuwa na Mapadri wenzake katika kikao, walipomaliza wenziwe waliondoka, akabaki eneo la mgahawa anakofanyia shughuli zake siku zote na kuwa hakuna baa wala vinywaji na kama kuna anayehitaji kupata vinywaji kwa kawaida angeenda nje ya eneo hilo
Ameongeza โMaana ukisema Mtu alikuwa anakunywa kwa saa zote hizo maana yake alikuwa anakunywa pombe, si hivyo. Wakati anatoka kurejea ndani kuna uchochoro wenye giza, hapo ndipo akavamiwa na kujeruhiwa na kitu kizito kichwani na kidevuniโ
Soma https://jamii.app/TECPadriKitima
#JFMatukio #JamiiForums
๐3๐ฅ1
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema kimepokea kwa mshtuko na masikitiko makubwa taarifa za kushambuliwa kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padre Dkt. Charles Kitima, tukio lililotokea usiku wa Aprili 30, 2025, katika eneo la Kurasini, Dar es Salaam
Padre Kitima alivamiwa na watu Wawili wasiojulikana na kushambuliwa kichwani na mwilini na kusababishiwa majeraha mbalimbali
CCM imesema inalaani vikali kitendo hicho cha kikatili na kisicho na utu dhidi ya kiongozi wa dini, ambaye kimesema amejitolea maisha yake kuhudumia jamii kwa upendo na uadilifu
CCM imetoa wito kwa vyombo vya usalama kufanya uchunguzi wa kina na wa haraka ili kuwabaini na kuwachukulia hatua kali wahusika wa tukio hilo
Soma https://jamii.app/CCMKitima
#JamiiForums #Governance #Accountability #HumanRights
Padre Kitima alivamiwa na watu Wawili wasiojulikana na kushambuliwa kichwani na mwilini na kusababishiwa majeraha mbalimbali
CCM imesema inalaani vikali kitendo hicho cha kikatili na kisicho na utu dhidi ya kiongozi wa dini, ambaye kimesema amejitolea maisha yake kuhudumia jamii kwa upendo na uadilifu
CCM imetoa wito kwa vyombo vya usalama kufanya uchunguzi wa kina na wa haraka ili kuwabaini na kuwachukulia hatua kali wahusika wa tukio hilo
Soma https://jamii.app/CCMKitima
#JamiiForums #Governance #Accountability #HumanRights
Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) limelaani vikali tukio la kushambuliwa kwa Padre Charles Kitima, Katibu Mkuu wa baraza hilo lililotokea usiku wa Aprili 30, 2025 katika Makao Makuu ya TEC, Kurasini, Dar es Salaam
Kwa mujibu wa taarufa ya Baraza hilo, Padre Kitima kwa sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan
Aidha, TEC imetoa wito kwa Jeshi la Polisi na Vyombo vya Usalama kuhakikisha wahusika wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria. Vilevile uchunguzi wa tukio hili ufanyike kwa haraka, kwa uwazi na bila upotoshaji ili kurejesha imani ya wananchi
Soma https://jamii.app/TamkoTECMei1
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #SocialJustice
Kwa mujibu wa taarufa ya Baraza hilo, Padre Kitima kwa sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan
Aidha, TEC imetoa wito kwa Jeshi la Polisi na Vyombo vya Usalama kuhakikisha wahusika wanakamatwa na kufikishwa mbele ya sheria. Vilevile uchunguzi wa tukio hili ufanyike kwa haraka, kwa uwazi na bila upotoshaji ili kurejesha imani ya wananchi
Soma https://jamii.app/TamkoTECMei1
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #SocialJustice
Hatua ndogo ni hatua bado. Usijione mdogo kwa sababu hujafika kule unapotamani kufika
Acha kujilaumu kwa kile ambacho hujafanya jana, leo ni nafasi nyingine ya kujaribu tena, kujifunza tena na kusonga mbele
#Goodmorning #JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF
Acha kujilaumu kwa kile ambacho hujafanya jana, leo ni nafasi nyingine ya kujaribu tena, kujifunza tena na kusonga mbele
#Goodmorning #JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF