DODOMA: Kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na aliyekuwa Kada wa CCM, Mchungaji Dkt. Godfrey Malisa ambayo ilipangwa kusikilizwa Agosti 14, 2025 imeahirishwa hadi Jumanne Agosti 19, 2025.
Shauri hilo linapinga uhalali wa mchakato uliotumika kumpata mgombea wa Urais wa CCM pamoja na Mgombea Mwenza. Dkt. Malisa alipotafutwa kwa simu, amesema shauri hilo limesogezwa hadi Agosti 19, ambapo mawakili wa CCM watatoa utetezi wao.
Awali, kesi hiyo ilisikilizwa kwa mara ya kwanza Agosti 5, 2025 ambapo Mahakama ilibainisha kuwa ina hoja za msingi zinazostahili kuamuliwa Mahakamani.
Soma https://jamii.app/KesiYaMalisaNaSamia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
Shauri hilo linapinga uhalali wa mchakato uliotumika kumpata mgombea wa Urais wa CCM pamoja na Mgombea Mwenza. Dkt. Malisa alipotafutwa kwa simu, amesema shauri hilo limesogezwa hadi Agosti 19, ambapo mawakili wa CCM watatoa utetezi wao.
Awali, kesi hiyo ilisikilizwa kwa mara ya kwanza Agosti 5, 2025 ambapo Mahakama ilibainisha kuwa ina hoja za msingi zinazostahili kuamuliwa Mahakamani.
Soma https://jamii.app/KesiYaMalisaNaSamia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
❤1
Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la JF Chit-Chats and Jokes, ameuliza kwenye ajira, Waajiri huwa wanaangalia nini zaidi wakati wa usaili wa kazi? Je, ni CV yako ilivyoandikwa? Uzoefu wa kazi ulionao? Kipaji? Ufaulu wako (GPA)? Au ni Chuo ulichosoma ndicho chenye uzito mkubwa?
Wewe unaamini nini huwa kinaamua zaidi hatma ya muombaji?
Kushiriki mjadala huu bonyeza https://jamii.app/SifaZaKuajiriwa
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats
Wewe unaamini nini huwa kinaamua zaidi hatma ya muombaji?
Kushiriki mjadala huu bonyeza https://jamii.app/SifaZaKuajiriwa
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa onyo kwa watoaji maudhui mtandaoni wanaokiuka Sheria za huduma za Utangazaji na kusema haitasita kuchukua hatua kali kwa wanaojihusisha na utoaji wa huduma hizo bila leseni.
Taarifa ya Mamlaka hiyo ya Agosti 16, 2025 imesema Watoa huduma za Mawasiliano ya Simu wanatakiwa kuhakikisha Maudhui ya arafa za mkupuo (bulk messages) kuelekea, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu 2025 yanazingatia Sheria na Kanuni zote za mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, Uhakiki wa maudhui ufanywe kabla ya kusambaza arafa za mkupuo zinazohusika.
Pia, TCRA imewataka watoa huduma kuhakikisha Maudhui yote yanayohusiana na shughuli za Uchaguzi Mkuu yanapata idhini kutoka kwa taasisi au uongozi wa chama cha #Siasa husika na wanapaswa kuhifadhi kumbukumbu za arafa zote zinazotumwa kwa wingi kwa kipindi kinachotakiwa kisheria kwa ajili ya uthibitisho endapo utahitajika.
Soma https://jamii.app/HudumaMaudhuiBilaLeseni
#JamiiForums #JamiiAfrica #Democracy #DigitalRights #KuelekeaUchaguzi2025
Taarifa ya Mamlaka hiyo ya Agosti 16, 2025 imesema Watoa huduma za Mawasiliano ya Simu wanatakiwa kuhakikisha Maudhui ya arafa za mkupuo (bulk messages) kuelekea, wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu 2025 yanazingatia Sheria na Kanuni zote za mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, Uhakiki wa maudhui ufanywe kabla ya kusambaza arafa za mkupuo zinazohusika.
Pia, TCRA imewataka watoa huduma kuhakikisha Maudhui yote yanayohusiana na shughuli za Uchaguzi Mkuu yanapata idhini kutoka kwa taasisi au uongozi wa chama cha #Siasa husika na wanapaswa kuhifadhi kumbukumbu za arafa zote zinazotumwa kwa wingi kwa kipindi kinachotakiwa kisheria kwa ajili ya uthibitisho endapo utahitajika.
Soma https://jamii.app/HudumaMaudhuiBilaLeseni
#JamiiForums #JamiiAfrica #Democracy #DigitalRights #KuelekeaUchaguzi2025
❤2
DAR: Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA), leo Agosti 17, 2025 kimetoa taarifa kikieleza Jeshi la Polisi Kanda Maalum lilivamia kikao cha Chama hicho kilichokuwa kikifanyika, Agosti 16, 2025, Kibaha - Pwani na kuwakamata Wanachama Sita na raia waliokuwa jirani na eneo la kikao.
Taarifa ya Brenda Rupia, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa Chama hicho, imeeleza waliokamatwa ni Pendo Msechu, Pendo Kyosi, Mary Mushi, Samson Mzambia, Focus Laurent na Alfred Bundala ambao wamepelekwa Kituo Kikuu cha Polisi (Central), lakini Polisi wa kituo hicho walikana kuendelea kuwashikilia.
Upande wa Jeshi la Polisi limetoa taarifa kuwa Agosti 16, 2025, limewakamata Watu 10 waliokuwa katika Ukumbi wa Mwitongo, Mailimoja Shule kwa maelezo kuwa walikuwa wakipanga njama za kufanya uhalifu.
Zaidi soma https://jamii.app/ChademaKibaha
#JamiiForums #JamiiAfrica #Democracy #JFMatukio #UchaguziMkuu2025
Taarifa ya Brenda Rupia, Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa Chama hicho, imeeleza waliokamatwa ni Pendo Msechu, Pendo Kyosi, Mary Mushi, Samson Mzambia, Focus Laurent na Alfred Bundala ambao wamepelekwa Kituo Kikuu cha Polisi (Central), lakini Polisi wa kituo hicho walikana kuendelea kuwashikilia.
Upande wa Jeshi la Polisi limetoa taarifa kuwa Agosti 16, 2025, limewakamata Watu 10 waliokuwa katika Ukumbi wa Mwitongo, Mailimoja Shule kwa maelezo kuwa walikuwa wakipanga njama za kufanya uhalifu.
Zaidi soma https://jamii.app/ChademaKibaha
#JamiiForums #JamiiAfrica #Democracy #JFMatukio #UchaguziMkuu2025
ENGLAND: Timu ya #ManchesterUnited imeanza vibaya msimu wa 2025/26 kwa kukubali kichapo cha Goli 1-0 kutoka kwa Arsenal kwenye Uwanja wa Old Trafford ikiwa ni mchezo wa kwanza kwa timu hizo katika Premier League.
Goli pekee limewekwa wavuni na beki Riccardo Calafiori akimalizia mpira wa kona dakika ya 13.
Mechi ijayo ya United ni dhidi ya Fulham (Agosti 24, 2025), #Arsenal itavaa Leeds United (Agosti 23, 2025).
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports #JFEPL2025
Goli pekee limewekwa wavuni na beki Riccardo Calafiori akimalizia mpira wa kona dakika ya 13.
Mechi ijayo ya United ni dhidi ya Fulham (Agosti 24, 2025), #Arsenal itavaa Leeds United (Agosti 23, 2025).
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports #JFEPL2025
Tembelea JamiiForums.com kusoma kwa undani habari hizi na mengine mengi yaliyojiri juma lililopita.
#JamiiAfrica #JamiiForums #YaliyojiriJumaLililopita #JFToons
#JamiiAfrica #JamiiForums #YaliyojiriJumaLililopita #JFToons
DAR: Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo Agosti 18, 2025 imepanga kutoa amri kuhusu kurushwa mubashara (LIVE) kwa maelezo ya mashahidi wa siri katika kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa #CHADEMA, #TunduLissu sambamba na kusikiliza vielelezo vitakavyotumika.
Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga alieleza kuwa kurushwa mubashara mwenendo huo ni sawa na kuchapisha ushahidi na kunaweza kukiuka uamuzi wa Mahakama Kuu wa Agosti 4, 2025 uliolenga kulinda utambulisho wa mashahidi.
Lissu alipinga hoja hiyo akieleza uamuzi huo ulikataza kufichua majina na anuani za mashahidi pekee, hivyo akaomba kesi iendelee kurushwa mubashara bila kuathiri usiri wao.
Zaidi soma https://jamii.app/KesiYaLissuLive
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga alieleza kuwa kurushwa mubashara mwenendo huo ni sawa na kuchapisha ushahidi na kunaweza kukiuka uamuzi wa Mahakama Kuu wa Agosti 4, 2025 uliolenga kulinda utambulisho wa mashahidi.
Lissu alipinga hoja hiyo akieleza uamuzi huo ulikataza kufichua majina na anuani za mashahidi pekee, hivyo akaomba kesi iendelee kurushwa mubashara bila kuathiri usiri wao.
Zaidi soma https://jamii.app/KesiYaLissuLive
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mvutano umezuka ndani ya Ukumbi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu baada ya eneo linalotakiwa kukaliwa na viongozi na wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA) kujazwa na watu wanaodaiwa kuwa ni askari wa Jeshi la Polisi waliovaa nguo za kiraia, kinyume na utaratibu.
Hali hiyo ilisababisha wanachama hao kushindwa kupata nafasi ya kukaa ili kufuatilia mwenendo wa Kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wao, Tundu Lissu.
Soma zaidi https://jamii.app/MvutanoMahakamani
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
Hali hiyo ilisababisha wanachama hao kushindwa kupata nafasi ya kukaa ili kufuatilia mwenendo wa Kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wao, Tundu Lissu.
Soma zaidi https://jamii.app/MvutanoMahakamani
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
❤1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akitoa amri kuhusu kesi dhidi ya Tundu Lissu kurushwa moja kwa moja (#LiveStreaming), Agosti 18, 2025 Hakimu Mkazi Mfawidhi, Franco Kiswaga amesema Mahakama imesitisha matangazo ya moja kwa moja (LIVE), utangazaji, usambazaji wa moja kwa moja au aina nyingine ya uenezaji wa moja kwa moja kwa umma ikijumuisha na mitandao ya kijamii hadi pale itakapotolewa amri nyingineyo.
Soma zaidi https://jamii.app/KuripotiLissuKibaliMahakamani
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
Soma zaidi https://jamii.app/KuripotiLissuKibaliMahakamani
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akitoa amri kuhusu kesi dhidi ya Tundu Lissu kurushwa moja kwa moja (#LiveStreaming), Agosti 18, 2025 Hakimu Mkazi Mfawidhi, Franco Kiswaga amesema kuchapisha na kusambaza nakala zenye ushahidi au ushahidi wowote utakaoweza kufichua mashaidi wa kiraia kesi ya Lissu inakatazwa na ni marufuku bila idhini ya Mahakama.
Pia ameongeza kwa kusema “Mtu au Vyombo vya Habari vinavyotaka kuchapisha habari kuhusu mwenendo wa kesi ya Lissu “committal proceedings” au mashahidi ni lazima vipeleke maombi mahakamani ili kuonesha kuhariri na kuondolewa kwa utambulisho na Mahakama kuu umekamilika na uchapishaji hautafichua utambulisho wa mashahidi wanaolindwa na Mahakama”
Soma https://jamii.app/VibaliMahakamaKesiLissu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
Pia ameongeza kwa kusema “Mtu au Vyombo vya Habari vinavyotaka kuchapisha habari kuhusu mwenendo wa kesi ya Lissu “committal proceedings” au mashahidi ni lazima vipeleke maombi mahakamani ili kuonesha kuhariri na kuondolewa kwa utambulisho na Mahakama kuu umekamilika na uchapishaji hautafichua utambulisho wa mashahidi wanaolindwa na Mahakama”
Soma https://jamii.app/VibaliMahakamaKesiLissu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Imam wa Msikiti wa Manyema, Sheikh Hameed Jongo akizungumza wakati wa kutoa hotuba ya Ijumaa Agosti 15, 2025 amesema kuwa Rais Samia anatenda haki na kufanya vizuri katika uongozi wake ndiyo maana wafanyabiashara wamechangia kikubwa walichochangia.
Ameongeza kuwa kuna Wanawake wana uwezo wa kuongoza kuliko wanaume, uongozi uliopita tumeona jinsi wanaume walivyoongoza, awamu hii ya sita Rais Samia anaongoza 'Fantastic'.
Soma https://jamii.app/HarambeeCCMAmani
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSiasa #UchaguziMkuu2025
Ameongeza kuwa kuna Wanawake wana uwezo wa kuongoza kuliko wanaume, uongozi uliopita tumeona jinsi wanaume walivyoongoza, awamu hii ya sita Rais Samia anaongoza 'Fantastic'.
Soma https://jamii.app/HarambeeCCMAmani
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSiasa #UchaguziMkuu2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mahakama Kuu ya Tanzania imetupilia mbali maombi ya Bodi ya Wadhamini na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA) ya kutaka kutenguliwa kwa uamuzi wa Juni 10, 2025, uliowazuia kuendelea na shughuli za Kisiasa kwa kutumia mali za Chama.
Uamuzi huo mdogo umetolewa leo Agosti 18, 2025 na Jaji Hamidu Mwanga katika kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Zanzibar, Said Issa Mohammed na wenzake dhidi ya Bodi ya Wadhamini na Katibu Mkuu wa CHADEMA kuhusu mgawanyo wa rasilimali kati ya Chama hicho Bara na Upande wa Zanazibar.
Wakili wa CHADEMA, Hekima Mwasipu amesema Jaji Mwanga baada ya kukataa maombi yao, pande zote zimekubaliana kuendelea na shauri ambapo Mahakama imeahirisha kesi hadi Agosti 28, 2025 kwa mapitio ya hoja zinazobishaniwa na kupanga utaratibu wa kuendelea na kesi kuu.
Zaidi soma https://jamii.app/OmbiLaChadema
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
Uamuzi huo mdogo umetolewa leo Agosti 18, 2025 na Jaji Hamidu Mwanga katika kesi ya madai iliyofunguliwa na aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Zanzibar, Said Issa Mohammed na wenzake dhidi ya Bodi ya Wadhamini na Katibu Mkuu wa CHADEMA kuhusu mgawanyo wa rasilimali kati ya Chama hicho Bara na Upande wa Zanazibar.
Wakili wa CHADEMA, Hekima Mwasipu amesema Jaji Mwanga baada ya kukataa maombi yao, pande zote zimekubaliana kuendelea na shauri ambapo Mahakama imeahirisha kesi hadi Agosti 28, 2025 kwa mapitio ya hoja zinazobishaniwa na kupanga utaratibu wa kuendelea na kesi kuu.
Zaidi soma https://jamii.app/OmbiLaChadema
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mkuu wa Kitengo cha Sheria Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Muhidin Mapejo ameeleza ukomo wa matumizi ya fedha kwa Wagombea mbalimbali katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025 ambapo katika nafasi za Urais ni Tsh. Bilioni 9, Udiwani Tsh. Milioni 16 na katika majimbo imezingatiwa idadi ya Watu, ukubwa wa majimbo na miundombinu na ukomo wa juu ni Tsh. Milioni 136.
Ameeleza hayo katika mafunzo kuhusu Sheria ya Gharama za Uchaguzi kwa Viongozi wa Kitaifa wa Vyama vya Siasa yaliyofanyika leo Jumatatu Agosti 18, 2025 kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (#JNICC).
Zaidi soma https://jamii.app/UkomoPesaUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFSiasa #UchaguziMkuu2025 #JFDemocracy
Ameeleza hayo katika mafunzo kuhusu Sheria ya Gharama za Uchaguzi kwa Viongozi wa Kitaifa wa Vyama vya Siasa yaliyofanyika leo Jumatatu Agosti 18, 2025 kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (#JNICC).
Zaidi soma https://jamii.app/UkomoPesaUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFSiasa #UchaguziMkuu2025 #JFDemocracy
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
ZANZIBAR: Tume ya Uchaguzi (ZEC), leo Agosti 18, 2025, imesema kuwa kampeni za Uchaguzi Mkuu zitaanza rasmi Septemba 11, 2025, Saa 10:01 Jioni mara baada ya uteuzi wa Wagombea na zitaendelea hadi siku ya mwisho kabla ya upigaji kura Oktoba 29, 2025.
Mwenyekiti wa ZEC, Jaji Goerge Joseph Kazi amesema mchakato wa kuchukua na kurejesha fomu za Wagombea wa Urais, Baraza la Wawakilishi na Udiwani utafanyika kuanzia Agosti 28 hadi Septemba 10, 2025 Saa 10:00 Jioni, na uteuzi rasmi kufanyika Septemba 11, 2025 Saa 10:00 Jioni kabla ya kuanza kwa kampeni.
Zaidi soma https://jamii.app/UchaguziZbar
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
Mwenyekiti wa ZEC, Jaji Goerge Joseph Kazi amesema mchakato wa kuchukua na kurejesha fomu za Wagombea wa Urais, Baraza la Wawakilishi na Udiwani utafanyika kuanzia Agosti 28 hadi Septemba 10, 2025 Saa 10:00 Jioni, na uteuzi rasmi kufanyika Septemba 11, 2025 Saa 10:00 Jioni kabla ya kuanza kwa kampeni.
Zaidi soma https://jamii.app/UchaguziZbar
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Democracy #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MWANZA: Mkuu wa Mkoa, Said Mtanda, leo Jumatatu Agosti 18, 2025 amefafanua suala la Mtoto Mkazi wa Nyakato, Wilayani Ilemela aliyesemekana kulawitiwa na Steven Ibasa (Baba Claudia), kwa kueleza kuwa suala hilo limefikishwa Mahakamani na kwamba mtuhumiwa amekosa mtu wa kumdhamini, amepelekwa Gerezani Butimba.
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akizungumza katika Mafunzo kuhusu Sheria ya Gharama za Uchaguzi kwa Viongozi wa Kitaifa wa Vyama vya Siasa kwenye Ukumbi wa #JNICC, Mwenyekiti wa Chama cha Alliance for Democratic Change (#ADC), Shaban Itutu amelalamikia kile alichodai ni unyanyasaji wa Polisi dhidi ya Wagombea wasiotokana na dola.
Ametoa wito kwa mamlaka kuwaalika katika Mikutano inayohusisha Vyama vya Siasa ili wajifunze kuwa kazi yao siyo kuwatisha na kuwakamata Wanasiasa.
Soma https://jamii.app/PolisiUchaguziWanasiasa
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFSiasa #UchaguziMkuu2025
Ametoa wito kwa mamlaka kuwaalika katika Mikutano inayohusisha Vyama vya Siasa ili wajifunze kuwa kazi yao siyo kuwatisha na kuwakamata Wanasiasa.
Soma https://jamii.app/PolisiUchaguziWanasiasa
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFSiasa #UchaguziMkuu2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MOROGORO: Zaidi ya wanachama 50 wa CCM kutoka Kata ya Minepa, Wilaya ya Ulanga mkoani Morogoro, wametishia kurudisha kadi zao za uanachama baada ya kulalamikia mchakato wa kura za maoni za udiwani. Wanachama hao wanadai kuwa Mtia nia aliyeshinda, Marugu Manosu hajapewa barua ya utambulisho badala yake amepewa mshindi wa nafasi ya pili.
Wanachama hao walifika katika Ofisi ya CCM Mkoa Morogoro wakitaka majibu ya wazi kuhusu hatua hiyo. Kwa upande wake, Manosu amesema licha ya kufuatilia suala hilo katika ngazi mbalimbali za chama, ameambiwa mchakato bado unaendelea bila kuelekezwa mwisho wake, hali ambayo imezidisha sintofahamu kwa wafuasi wake.
Soma zaidi https://jamii.app/WanachamaCCM
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Demokrasia
Wanachama hao walifika katika Ofisi ya CCM Mkoa Morogoro wakitaka majibu ya wazi kuhusu hatua hiyo. Kwa upande wake, Manosu amesema licha ya kufuatilia suala hilo katika ngazi mbalimbali za chama, ameambiwa mchakato bado unaendelea bila kuelekezwa mwisho wake, hali ambayo imezidisha sintofahamu kwa wafuasi wake.
Soma zaidi https://jamii.app/WanachamaCCM
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Demokrasia
Kushiriki kwenye mijadala mingine tembelea JamiiForums.com
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
NJOMBE: Mkuu wa Wilaya ya Makete, Kissa Kasongwa amewataka Vijana waliohitimu mafunzo ya Jeshi la Akiba (Mgambo) kuwa wazalendo na kuilinda Nchi kwa wivu mkubwa ambapo pia ametoa ahadi ya Serikali kuwatumia kwa ajili ya kutazama usalama katika kipindi cha Uchaguzi.
DC Kissa ameeleza hayo Agosti 17, 2025 wakati akifunga mafunzo ya miezi mitatu kwa vijana zaidi ya 50 wa Kata ya Tandala wilayani humo.
Soma zaidi
https://jamii.app/MgamboKutumikaUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025
DC Kissa ameeleza hayo Agosti 17, 2025 wakati akifunga mafunzo ya miezi mitatu kwa vijana zaidi ya 50 wa Kata ya Tandala wilayani humo.
Soma zaidi
https://jamii.app/MgamboKutumikaUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Mdau hii kitaalamu tunaiitaje? 😃
Kushiriki kwenye mijadala mingine kama hii tembelea JamiiForums.com
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats
Kushiriki kwenye mijadala mingine kama hii tembelea JamiiForums.com
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats