MICHEZO: Mtibwa Sugar Sports Club yenye makazi yake Mkoani Morogoro, Wilaya ya Mvomero, ilianzishwa na Wafanyakazi wa Kiwanda cha Sukari cha Mtibwa. Madhumuni ya awali yalikuwa kushiriki Ligi katika Ngazi ya Wilaya na kutoa burudani kwa Wafanyakazi, baadaye iliendelea na kushiriki Ligi Daraja la Nne (4th Division League).
Mtibwa Sugar ni moja ya timu yenye historia kubwa katika soka la #Tanzania, iliwahi kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara mbele ya vigogo wa ligi #Simba na #Yanga mara mbili mfululizo.
Tukumbuke #MtibwaSugar ilipobeba taji la Bara na Mdau una kumbukumbu ipi kuhusu wakati huo?
Soma Zaidi https://jamii.app/MtibwaSugar
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFSports #JFKumbukizi
Mtibwa Sugar ni moja ya timu yenye historia kubwa katika soka la #Tanzania, iliwahi kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara mbele ya vigogo wa ligi #Simba na #Yanga mara mbili mfululizo.
Tukumbuke #MtibwaSugar ilipobeba taji la Bara na Mdau una kumbukumbu ipi kuhusu wakati huo?
Soma Zaidi https://jamii.app/MtibwaSugar
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFSports #JFKumbukizi
MWANZA: Mdau wa JamiiForums.com aliyejitambulisha kuwa Mkazi wa Mtaa wa Kaseze, Kata ya Mkolani, Wilaya ya Nyamagana anadai Wakazi wa eneo hilo hasa Mlimani wanakabiliwa na ukosefu mkubwa wa Huduma ya Maji, hali inayowalazimisha baadhi ya Watu kujisaidia vichakani.
Anatahadharisha kuwa mvua inaponyesha, uchafu husambaa na kwamba unaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa ya kuambukiza.
Mdau, hali ya Huduma ya Maji Mtaani kwako ipoje?
Kushiriki mjadala soma https://jamii.app/KeroMajiMwanza
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #Uwajibikaji #JFMdau2025
Anatahadharisha kuwa mvua inaponyesha, uchafu husambaa na kwamba unaweza kusababisha mlipuko wa magonjwa ya kuambukiza.
Mdau, hali ya Huduma ya Maji Mtaani kwako ipoje?
Kushiriki mjadala soma https://jamii.app/KeroMajiMwanza
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #Uwajibikaji #JFMdau2025
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Sehemu ya Hotuba ya Mwalimu Julius Nyerere akizungumzia kuhusu Azimio la Arusha pamoja na umuhimu wa uwepo wa mfumo wa vyama vingi nchini #Tanzania.
Alinukuliwa akisema “Chama ambacho hakina mpinzani wake anayekisukuma ambaye kinamuogopa kinasema kama tusipoangalia, kama tusipokuwa karibu na Watu tukajipanga vizuri tutapoteza Uchaguzi ujao, chama cha namna hiyo unakijengaje na unakipaje nguvu?”
Soma zaidi https://jamii.app/MwalimuNyerereVyamaVingi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFKumbukizi #Governance
Alinukuliwa akisema “Chama ambacho hakina mpinzani wake anayekisukuma ambaye kinamuogopa kinasema kama tusipoangalia, kama tusipokuwa karibu na Watu tukajipanga vizuri tutapoteza Uchaguzi ujao, chama cha namna hiyo unakijengaje na unakipaje nguvu?”
Soma zaidi https://jamii.app/MwalimuNyerereVyamaVingi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFKumbukizi #Governance
ARUSHA: Waendeshaji Akaunti ya Mtandaoni ya “Wachokonozi”, Jackson Kabalo na Joseph Mrindoko leo Julai 21, 2025 wameachiwa huru na Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha baada ya upande wa Jamhuri kueleza haupo tayari kuendelea na shauri hilo kwa sababu ambazo hawakuziweka wazi.
Mara baada ya kuachiwa huru, walikamatwa tena na kupelekwa Mahakama ya Wilaya ya Meru, wakasomewa upya mashtaka yaleyale ya awali. Baada ya Hakimu kusikiliza hoja za pande zote, ameitaka Jamhuri kukamilisha upelelezi kabla ya Agosti 13, 2025 ambapo shauri litasikilizwa.
Watuhumiwa wameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ambapo wanatuhumiwa kuchapisha taarifa za uongo kwa njia ya Mtandao na kutoa maudhui Mtandaoni bila kuwa na leseni.
Zaidi soma https://jamii.app/WachokoziWaachiwaWakamatwa
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMatukio #DigitalRights #CivilRights
Mara baada ya kuachiwa huru, walikamatwa tena na kupelekwa Mahakama ya Wilaya ya Meru, wakasomewa upya mashtaka yaleyale ya awali. Baada ya Hakimu kusikiliza hoja za pande zote, ameitaka Jamhuri kukamilisha upelelezi kabla ya Agosti 13, 2025 ambapo shauri litasikilizwa.
Watuhumiwa wameachiwa kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ambapo wanatuhumiwa kuchapisha taarifa za uongo kwa njia ya Mtandao na kutoa maudhui Mtandaoni bila kuwa na leseni.
Zaidi soma https://jamii.app/WachokoziWaachiwaWakamatwa
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMatukio #DigitalRights #CivilRights
Watu watakuona kwa kile unachofanya na matokeo yake, si kwa ndoto wala hadithi unazojisemea au mipango unayoahirisha kila mara.
Anza na kile kidogo ulichonacho, fanya kila siku na hapo ndipo utaona mabadiliko.
Tembela https://jamii.app/JukwaaJamiiForums
#JamiiAfrica #JamiiForums
#AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
Anza na kile kidogo ulichonacho, fanya kila siku na hapo ndipo utaona mabadiliko.
Tembela https://jamii.app/JukwaaJamiiForums
#JamiiAfrica #JamiiForums
#AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
❤1
Mdau wa JamiiForums.com anaeleza kuwa haridhishwi na utendaji wa Baraza la Wauguzi na Ukunga Tanzania (#TNMC) akidai halisimamii vizuri uhuishaji wa leseni, anatoa mfano kwamba Wauguzi wanatakiwa kupata pointi nje ya Mtandao kupitia Mafunzo na Semina wakati Watumishi wengi wa chini hawapewi nafasi ya kushiriki katika fursa hizo.
Mdau anadai Baraza halijatatua changamoto ya Mishahara akieleza kuwa Wauguzi wa Shahada wanalipwa ngazi ya TGHS C ilhali kisheria walitakiwa kulipwa TGHS D sawa na Mfamasia au Biomedical ambapo wote wamesoma kwa Miaka Minne
Soma https://jamii.app/WauguziKukimbiaFani
#JamiiForums #JFHuduma #Governance #JFUwajibikaji #PublicHealth
Mdau anadai Baraza halijatatua changamoto ya Mishahara akieleza kuwa Wauguzi wa Shahada wanalipwa ngazi ya TGHS C ilhali kisheria walitakiwa kulipwa TGHS D sawa na Mfamasia au Biomedical ambapo wote wamesoma kwa Miaka Minne
Soma https://jamii.app/WauguziKukimbiaFani
#JamiiForums #JFHuduma #Governance #JFUwajibikaji #PublicHealth
Mdau wa JamiiForums.com kutoka Jukwaa la JF Garage anadai baadhi ya madereva wakifika vituo vya mafuta huwaambia Wahudumu 'Jaza mafuta mpaka gari litapike', tena hufikia hadi kulitikisatikisa.
Anaonya kuwa kujaza mafuta kupita kiwango huathiri mfumo wa EVAP (Evaporative Emission Control System) unaodhibiti mvuke wa mafuta kutoka nje, hivyo mafuta yanaweza kuingia kwenye bomba la mvuke na kuharibu 'charcoal canister' na kusababisha harufu ya mafuta, kupunguza ufanisi wa injini na kuwasha taa ya “Check Engine”.
Anashauri kila unapojaza mafuta, kuacha pampu ikomee pale inaposimama yenyewe (auto stop) bila kuendelea kujaza mafuta kupita kiwango (Overfilling Fuel Tank).
Zaidi shiriki https://jamii.app/GariMafutaKupitiliza
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFGarage #JFMdau2025
Anaonya kuwa kujaza mafuta kupita kiwango huathiri mfumo wa EVAP (Evaporative Emission Control System) unaodhibiti mvuke wa mafuta kutoka nje, hivyo mafuta yanaweza kuingia kwenye bomba la mvuke na kuharibu 'charcoal canister' na kusababisha harufu ya mafuta, kupunguza ufanisi wa injini na kuwasha taa ya “Check Engine”.
Anashauri kila unapojaza mafuta, kuacha pampu ikomee pale inaposimama yenyewe (auto stop) bila kuendelea kujaza mafuta kupita kiwango (Overfilling Fuel Tank).
Zaidi shiriki https://jamii.app/GariMafutaKupitiliza
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFGarage #JFMdau2025
❤1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akizungumza na Clouds TV, leo Julai 22, 2025, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro amesema Kauli Mbiu ya ''No Reforms No Election'' inayotumiwa na #CHADEMA haina msingi wa Kisheria na haiwezekani kutumika kuzuia Uchaguzi, akisisitiza Jeshi la Polisi linasimamia Sheria na siyo kauli za Kisiasa.
Soma https://jamii.app/CHADEMAHaiweziZuiaUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #Democracy #Uchaguzi2025 #Siasa #Governance
Soma https://jamii.app/CHADEMAHaiweziZuiaUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #Democracy #Uchaguzi2025 #Siasa #Governance
❤1
Malawi: Mahakama Kuu, Julai 16, 2025, ilitangaza kufuta Kifungu cha 200 cha Kanuni ya Adhabu kinachofanya kashfa kuwa kosa la jinai, kwa kusema kinakiuka haki ya uhuru wa kujieleza. Kesi hiyo ilifunguliwa na Joshua Chisa Mbele dhidi ya Mkurugenzi wa Mashtaka na Mwanasheria Mkuu akipinga kifungu hicho kwa misingi ya Kikatiba na Haki za Binadamu.
Mahakama ilieleza kuwa kuchukulia kashfa kama kosa la jinai inazuia na kufifisha haki ya kujieleza na mijadala ya umma katika Jamii huru, ilihimiza matumizi ya njia za madai za Kiraia badala ya kifungo.
Wanasheria na Watetezi wa Haki za Binadamu wamepongeza uamuzi huo kama hatua muhimu kwa uhuru wa kujieleza. SALC imeitaka Bunge kufuta rasmi kifungu hicho na kupitia Sheria nyingine kandamizi.
Soma Zaidi https://jamii.app/MalawiKifungu
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #Accountability
Mahakama ilieleza kuwa kuchukulia kashfa kama kosa la jinai inazuia na kufifisha haki ya kujieleza na mijadala ya umma katika Jamii huru, ilihimiza matumizi ya njia za madai za Kiraia badala ya kifungo.
Wanasheria na Watetezi wa Haki za Binadamu wamepongeza uamuzi huo kama hatua muhimu kwa uhuru wa kujieleza. SALC imeitaka Bunge kufuta rasmi kifungu hicho na kupitia Sheria nyingine kandamizi.
Soma Zaidi https://jamii.app/MalawiKifungu
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #Accountability
MWANZA: Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Habari na Hoja Mchanganyiko amedai kusikitishwa na hali ya kero ya vumbi katika barabara ya muda inayotumika kupita eneo la ujenzi wa Daraja la Mkuyuni, ambapo siku mbili mfululizo, hakuna maji yanayomwagwa kudhibiti vumbi.
Anadai ni jambo ambalo linaathiri afya za Wananchi, pia Watumiaji wa vyombo vya moto wanapata changamoto ya kuona vumbi linapotawala eneo hilo.
Ameiomba Mamlaka husika kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha usalama na ustawi wa Watumiaji wa barabara hiyo unazingatiwa.
Soma https://jamii.app/KeroDarajaLaMkuyuniMwanza
#JamiiAfrica #JamiiForums #ServiceDelivery #Uwajibikaji #ServiceDelivery #JFHuduma
Anadai ni jambo ambalo linaathiri afya za Wananchi, pia Watumiaji wa vyombo vya moto wanapata changamoto ya kuona vumbi linapotawala eneo hilo.
Ameiomba Mamlaka husika kufuatilia kwa karibu na kuhakikisha usalama na ustawi wa Watumiaji wa barabara hiyo unazingatiwa.
Soma https://jamii.app/KeroDarajaLaMkuyuniMwanza
#JamiiAfrica #JamiiForums #ServiceDelivery #Uwajibikaji #ServiceDelivery #JFHuduma
👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amehoji kauli ya baadhi ya wanasiasa wanaodai “watalinda kura” wakati wa uchaguzi, akitaka waeleze kwa sheria ipi na kwa namna gani wanakusudia kufanya hivyo.
"Wewe kama unahoja unaona kuna udhaifu sehemu fulani ingiza kwenye mifumo ya kisheria, lakini kama haipo kisheria mimi Jukumu langu ni kuhakikisha usalama unaimarika pia kwa kufuata mifumo ya kisheria"
Muliro ametoa kauli hiyo Julai 22, 2025, wakati wa mahojiano na Clouds TV, Dar es Salaam
Soma Zaidi https://jamii.app/MuliroKulindaKura
#JamiiAfrica #JamiiForums #Democracy #UchaguziMkuu2025 #Accountability
"Wewe kama unahoja unaona kuna udhaifu sehemu fulani ingiza kwenye mifumo ya kisheria, lakini kama haipo kisheria mimi Jukumu langu ni kuhakikisha usalama unaimarika pia kwa kufuata mifumo ya kisheria"
Muliro ametoa kauli hiyo Julai 22, 2025, wakati wa mahojiano na Clouds TV, Dar es Salaam
Soma Zaidi https://jamii.app/MuliroKulindaKura
#JamiiAfrica #JamiiForums #Democracy #UchaguziMkuu2025 #Accountability
Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Siasa ameandika “Wagombea wengi wanaahidi mambo makubwa wakati wa Uchaguzi zikiwemo kujenga barabara, kutoa ajira kwa Vijana, kutoa huduma bora kwa Wananchi, hata kama hawana uwezo."
Ameeleza, wapo Wagombea wa Ubunge na Udiwani ambao Kikatiba hawana mamlaka ya moja kwa moja kutekeleza baadhi ya mambo hayo lakini wao wamekuwa wakiahidi tu licha ya kwamba wanajua ukweli.
Hivyo, Mdau anahoji, Je, kutoa ahadi zisizotekelezeka wakati wa Uchaguzi ni kosa Kisheria na adhabu zake ni zipi?
Soma Zaidi https://jamii.app/UongoKampeniUchaguzi
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025 #TaarifaZaUchaguzi2025
Ameeleza, wapo Wagombea wa Ubunge na Udiwani ambao Kikatiba hawana mamlaka ya moja kwa moja kutekeleza baadhi ya mambo hayo lakini wao wamekuwa wakiahidi tu licha ya kwamba wanajua ukweli.
Hivyo, Mdau anahoji, Je, kutoa ahadi zisizotekelezeka wakati wa Uchaguzi ni kosa Kisheria na adhabu zake ni zipi?
Soma Zaidi https://jamii.app/UongoKampeniUchaguzi
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025 #TaarifaZaUchaguzi2025
Uraia sio tu kupiga Kura au kudai Haki zako, ni pia kujitokeza kwa vitendo. Unaposaidia kusafisha mtaa, kuwasaidia watoto shuleni au kuwasaidia ambao wapo kwenye hali ngumu, unajenga jamii bora zaidi.
Mdau, wewe kama Raia unayewajibika huwa una tabia ya kujitolea kwenye jamii yako?
Tembela https://jamii.app/JukwaaJamiiForums
#JamiiAfrica #JamiiForums #RestlessDevelopment #RaiaWajibika #CivicEducation #SautiYaRaia #UraiaWenyeUelewa
Mdau, wewe kama Raia unayewajibika huwa una tabia ya kujitolea kwenye jamii yako?
Tembela https://jamii.app/JukwaaJamiiForums
#JamiiAfrica #JamiiForums #RestlessDevelopment #RaiaWajibika #CivicEducation #SautiYaRaia #UraiaWenyeUelewa
Mdau, kwani hii nayo inahitaji "D Mbili?"
Tuambie kama umeshamfahamu?
Kushiriki mjadala huu bonyeza
https://jamii.app/UmemtambuaMwanasiasaHuyu
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFPhotos
Tuambie kama umeshamfahamu?
Kushiriki mjadala huu bonyeza
https://jamii.app/UmemtambuaMwanasiasaHuyu
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFPhotos
Mdau wa Jukwaa la Elimu ndani ya JamiiForums.com anadai anasikitishwa na mabadiliko ya Mitaala ya Elimu ya Vyuo Vikuu ikiwemo hatua ya kufungia baadhi ya fani au programu kwa kutoa maagizo ya ghafla yasiyozingatia muda wa kitaaluma unaohitajika ili kuandaa mabadiliko yenye ubora na tija.
Anasema “Sera ya Elimu huandaliwa kwa muda mrefu kupitia tafiti, mijadala ya kina na michakato thabiti ya Kitaalamu, leo tunaona Vyuo vinaamrishwa kufanya mabadiliko ya mitaala kwa muda mfupi bila tafakuri ya kina wala maandalizi ya Kisayansi, ni jambo linalotia wasiwasi.”
Mdau anadai hali hiyo inachangia kuwaweka Wahadhiri na Vyuo katika presha ya Kisiasa au ya Watu wachache wanaotaka kuonekana wanafanya kazi, ilhali wanavuruga msingi wa elimu bora.
https://jamii.app/MitaalaYaVyuo
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFElimu #JFMdau2025 #Accountability
Anasema “Sera ya Elimu huandaliwa kwa muda mrefu kupitia tafiti, mijadala ya kina na michakato thabiti ya Kitaalamu, leo tunaona Vyuo vinaamrishwa kufanya mabadiliko ya mitaala kwa muda mfupi bila tafakuri ya kina wala maandalizi ya Kisayansi, ni jambo linalotia wasiwasi.”
Mdau anadai hali hiyo inachangia kuwaweka Wahadhiri na Vyuo katika presha ya Kisiasa au ya Watu wachache wanaotaka kuonekana wanafanya kazi, ilhali wanavuruga msingi wa elimu bora.
https://jamii.app/MitaalaYaVyuo
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFElimu #JFMdau2025 #Accountability
👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
TANZIA: Anastazia Mwamongi, kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA), amekutwa ameuawa na mwili wake kupatikana ndani ya nyumba yake ukiwa na majeraha kichwani.
Mwenyekiti wa mtaa wa Mkimbizi D, Mgimba Wigeni, amesema mwili huo uligunduliwa baada ya taarifa kutoka kwa mtoto wake, aliyepata wasiwasi kwa kutompata mama yake kwa siku kadhaa. Mwili wake umezikwa leo Jumanne, Julai 22, 2025, katika makaburi ya Igeleke, kata ya Mkimbizi, Kihesa Kilolo.
Marehemu aliwahi kuwa Mweka Hazina wa Baraza la Wanawake CHADEMA na Mratibu wa Elimu Manispaa ya Iringa.
Soma https://jamii.app/AnastaziaMwamongiAuawa
#JamiiAfrica #JamiiForums
Mwenyekiti wa mtaa wa Mkimbizi D, Mgimba Wigeni, amesema mwili huo uligunduliwa baada ya taarifa kutoka kwa mtoto wake, aliyepata wasiwasi kwa kutompata mama yake kwa siku kadhaa. Mwili wake umezikwa leo Jumanne, Julai 22, 2025, katika makaburi ya Igeleke, kata ya Mkimbizi, Kihesa Kilolo.
Marehemu aliwahi kuwa Mweka Hazina wa Baraza la Wanawake CHADEMA na Mratibu wa Elimu Manispaa ya Iringa.
Soma https://jamii.app/AnastaziaMwamongiAuawa
#JamiiAfrica #JamiiForums