JamiiForums
βœ”
34K subscribers
37.3K photos
2.98K videos
32.8K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema hakitambui Ripoti ya Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani Yaliyotokea Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025 ambayo imewasilishwa leo Aprili 23, 2026 chini ya uongozi wa Jaji Chande.

Aidha, chama hicho kimeeleza kuwa kinaendelea kuchambua ripoti hiyo na kitatoa msimamo rasmi baada ya kikao cha Kamati Kuu kitakachofanyika Aprili 28 na 29, 2026.

Zaidi https://jamii.app/ChademaTume

#JamiiForums #Uwajibikaji #Demokrasia
🀬1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Balozi, ambaye pia ni Mshauri wa Rais, Lazaro Nyalandu ameyasema hayo Aprili 23, 2026 wakati alipokuwa akihojiwa na Kituo cha Sky News baada ya kutoka kwa Ripoti ya Tume ya Rais ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyotokea Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025.

Zaidi https://jamii.app/NyalanduWaandamaji

#JamiiForums #Uwajibikaji #Utawala
Aprili 24, 2026: Moja ya mijadala mingi inayoendelea ndani ya JamiiForums.com wakati huuπŸ“Œ

Zaidi https://jamii.app/ACTRipotiChande

#JamiiForums #Uwajibikaji
UTEUZI: Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu kuhusu uteuzi uliofanywa na Rais Samia, leo, Aprili 24, 2026 imeeleza amemteua Angela Charles Kizigha kuwa Mshauri wa Rais, Masuala ya Jamii.

Zaidi  https://jamii.app/KizighaMshauriRais

#JamiiForums #Governance #JFMatukio
⚑1🀬1
UTEUZI: Rais Samia Suluhu amemteua Mhandisi Mwasalyanda kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), kabla ya uteuzi huo, alikuwa Mtendaji Mkuu wa Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), anachukua nafasi ya Dkt. Jabiri Kuwe Bakari ambaye amemaliza.

Pia, Rais amemteua Dkt. Jabiri Kuwe Bakari kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), anachukua nafasi ya Salim Ramadhani Msangi ambaye atapangiwa majukumu mengine. Uteuzi huo umefanyika leo, Aprili 24, 2026.

Zaidi https://jamii.app/PeterMkurugenziTCRA

#JamiiForums #Governance #JFMatukio
πŸ‘Ž3
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Akifanya Mahojiano na BBC, Aprili 24, 2026, Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira ametoa Kauli hiyo kufuatia Matamko yaliyotolewa na Vyama vya Siasa, ACT-Wazalendo na CHADEMA kutokubaliana na Ripoti ya Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani Yaliyotokea Wakati na Baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba, 2025, iliyowasilishwa Aprili 23, 2026.

Zaidi tembelea https://jamii.app/WasiraMaridhiano

Nini maoni yako Mdau?

#JamiiForums #Uwajibikaji #Governance
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira, amesema hayo wakati akifanya Mahojiano na BBC Aprili 24, 2026.

Nini maoni yako Mdau?

Zaidi tembelea https://jamii.app/WasiraTakwimu

#JamiiForums #Uwajibikaji
❀1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Katibu Mkuu wa CHAUMMA na aliyekuwa mgombea wa Urais wa chama hicho katika uchaguzi mkuu wa 2025, Salum Mwalim, amesema hayo Aprili 23, 2026 baada ya Tume ya Kuchunguza Matukio ya Wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025 kuwasilisha na kukabidhi Ripoti yake kwa Rais Samia.

Zaidi https://jamii.app/SalumTumeChande

#JamiiForums #Uwajibikaji
DAR: Mdau anatoa angalizo kuwa baadhi ya Watu wenye uwezo wa kifedha wamekuwa wakinunua ardhi maeneo ya Mwenge na Sinza, hivyo Serikali iwe macho Watu wachache wasije kutumia mradi wa Sinza wenye nia nzuri kujineemesha wao binafsi badala ya malengo yaliyowekwa na Serikali.

Zaidi tembelea https://jamii.app/SinzaMipango

#JamiiForums #CivilRights #Governance
❀1
Moja ya mjadala unaoendelea ndani ya JamiiForums.com kuhusu matumizi ya nishati ya gesi.

Zaidi tembelea https://jamii.app/MatumiziGesi

#JamiiForums #JFMdau2026 #Uwajibikaji
Please open Telegram to view this post
VIEW IN TELEGRAM
ENGLAND: Goli pekee lililofungwa na Eze katika dakika ya 9 limeipa #ArsenalFC ushindi dhidi ya #NewcastleUnited na hivyo kurejea nafasi ya kwanza katika Ligi Kuu ya England β€œ#PremierLeague”, huku Newcastle ikibaki nafasi ya 14 kati ya timu 20.

Arsenal imefikisha alama 73 katika michezo 34 na hivyo kuishusha Manchester City hadi nafasi ya pili ikiwa na alama 70 katika michezo 33.

Wakati huohuo, Man City imefuzu Fainali ya FA Cup baada ya kuifunga Southampton Magoli 2-1 katika Nusu Fainali, leo Aprili 25, 2026.

Zaidi https://jamii.app/MichezoJF2026

#JamiiForums #JFEPL2026 #JFSports
MUUNGANO CUP: Yanga imetangulia kuingia Fainali baada ya kuifunga Azam FC Magoli 2-1 katika Nusu Fainali kwenye Uwanja wa Amaani, Zanzibar, hivyo inasubiri mshindi wa mchezo wa Simba dhidi ya Mlandege utakaochezwa Aprili 26, 2026.

Walioifungia ya Yanga katika mchezo wa leo Aprili 25, 2026 ni Prince Dube na Maxi Zengeli wakati Feisal Salum β€œFei Toto” alifunga upande wa Azam FC.

Zaidi https://jamii.app/YangaFainali

#JamiiForums #JFSports #JFMuunganoCup2026
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (TATOA) na Chama cha Mawakala wa Forodha Tanzania (TAFFA) kwa pamoja wamesema wanachama wao wanapata changamoto ya kutokana na ucheleweshaji wa uhamishaji wa makontena kutoka bandarini kwenda bandari kavu (ICDs).

Wameeleza badala ya makontena kuhamishwa ndani ya Saa 48 kama Sheria inavyotaka, baadhi huchukua kati ya siku 7 hadi 40.

Zaidi https://jamii.app/ForodhaBandariDar

#JamiiForums #Uwajibikaji #JFHuduma