JamiiForums
34.9K subscribers
37.2K photos
2.94K videos
32.8K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
SONGWE: Aprili 13, 2026, Mdau wa JamiiForums.com aliandika kuhusu michezo "michafu" katika Machinjio ya Mji wa Tunduma, leo Aprili 17, 2026, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Tunduma, Mariam Chaurembo ameeleza hatua zilizochukuliwa na kuongeza kuwa Serikali imetenga Tsh. Milioni 850 ya ujenzi wa Machinjio mpya sababu ya sasa imekuwa ndogo.

Zaidi tembelea https://jamii.app/MachinjioTundumaKujengwa

#JamiiForums #JFMdau2026 #Uwajibikaji #JFHuduma #PublicHealth

Nawe unaweza kuwasilisha Kero yako kupitia FichuaUovu ndani ya JamiiForums.com 📌
Aliyekuwa Waziri Mkuu wa Gabon, Alain-Claude Bilie-By-Nze, amekamatwa Aprili 16, 2026 kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya tamasha la utamaduni la Mwaka 2008, baada ya mtoa huduma aliyeandaa tamasha hilo kufungua malalamiko akidai hakulipwa japo Bilie By Nze alipokea fedha hizo,

Chama chake cha EPG kimepinga kukamatwa kwake kikidai ni mbinu za kumnyamazisha kwa sababu yeye ni mkosoaji Mkuu wa Serikali ya Kijeshi ya sasa chini ya Brice Oligui Nguema, kikisisitiza kuwa deni hilo ni la Serikali na si la kwake binafsi.

Zaidi: https://jamii.app/GabonWaziri

#JamiiForums #Accountability #AfricanPolitics
1
Unamshauri nini Mdau katika hii changamoto?

Toa ushauri wako kupitia https://jamii.app/ChooKigumuHewaChafu

#JamiiForums #Maisha #JFAfya #PublicHealth #JFMdau2026
Licha ya ukuaji wa 4.5% mwaka 2025, uchumi wa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara unatarajiwa kushuka hadi 4.3% mwaka 2026. Vita vya Mashariki ya Kati na kupungua kwa misaada ya kigeni vinatajwa kama tishio jipya kwa usalama wa chakula na hali ya maisha ya wananchi.

Fuatilia zaidi mjadala https://jamii.app/IMFUchumi

#JamiiForums #Uchumi #JFEconomy #GlobalEconomy
KAGERA: Mamlaka ya Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) imesema Kitongoji cha Akajiji (Kijiji cha Nyakayanja) kilikuwa na changamoto ya pampu, hivyo kushindwa kupata maji, tayari Chombo cha Utoaji Huduma ya Maji Ngazi ya Jamii (LUNYANYABIRWA) kimegharamikia matengenezo na maji yanapatikana.

Awali, Mdau wa JamiiForums.com aliandika “Afya za Wananchi Kata Nyaishozi Wilayani Karagwe zipo hatarini, wanatumia maji ya madimbwi”, akatoa wito kwa mamlaka kushughulikia changamoto hiyo haraka.

Fuatilia zaidi https://jamii.app/MajiNyaishozi

#JamiiForums #JFMdau2026 #Uwajibikaji #JFHuduma

Nawe unaweza kuwasilisha KERO yako kupitia WhatsApp +255743440000 au FichuaUovu kwenye App ya JamiiForums📌📌
Aprili 18, 2026: Moja kati ya mijadala mingi inayoendelea ndani ya JamiiForums.com wakati huu📌

Fuatilia mjadala👉🏾 https://jamii.app/IranStraitHormuz

#JamiiForums #GlobalPolitics
Please open Telegram to view this post
VIEW IN TELEGRAM