JamiiForums
33.4K subscribers
37.4K photos
2.99K videos
32.9K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MWANZA: Mdau wa JamiiForums.com anadokeza kuwa kuna Vijana wanafanya kazi bila kuwa na vifaa maalum vya usalama kazini kwenye jengo la ghorofa Mitaa ya Ghana, Mkabala na Hoteli ya Kingdome hali inayotishia usalama wao.

Anahoji "Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) mko wapi? Hamuoni hayo yanayoendelea?"

Zaidi https://jamii.app/OshaVifaaKazi

#JamiiForums #JFMdau2026 #Uwajibikaji
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
KATAVI: Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Tulieni, Manispaa ya Mpanda amesema shule hiyo inakabiliwa na upungufu wa madawati kwani yapo 169 ikilinganishwa na idadi ya Wanafunzi 2,500.

Ameyasema hayo alipokuwa aliwasilisha changamoto hizo mbele ya Mwenyekiti wa CCM, Tawi la Tulieni walipotembelea, Aprili 24, 2026 ili kujua mwenendo wa shule hiyo pamoja na kuzipeleka maeneo husika.

Zaidi https://jamii.app/TulieniUhabaWalimu

#JamiiForums #Uwajibikaji #JFElimu

Video: KINYOGOTO JR
Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Rugemeleza Nshala amesema leo asubuhi Aprili 30, 2026, Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu alifikishwa Mahakamani na uamuzi uliotolewa umetupilia mbali hoja za kutaka kuunganishwa katika kesi ya mgawanyo wa mali za CHADEMA.

Zaidi: https://jamii.app/MahakamaKesiCHADEMA

#JamiiForums #Uwajibikaji #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
LINDI: Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa wa Chama cha ACT Wazalendo, Abdul Omary Nondo akizungumzia orodha ya wanufaika wa maombi ya mkopo kupitia mfuko wa Maendeleo ya Vijana chini ya Wizara ya Maendeleo ya Vijana iliyotolewa Aprili 28, 2026.

Zaidi https://jamii.app/MikopoYaWizara

#JamiiForums #Uwajibikaji #UtawalaBora
DAR: Mdau wa JamiiForums.com anatoa wito kwa Mamlaka za juu kufanya uchunguzi kwenye Kituo cha Afya Mbande kilichopo Temeke akidai kuna mazingira ambayo sio mazuri kwa Watendaji kutokana na uwepo wa matukio kadhaa yasiyoendana na maadili ya kazi.

Zaidi https://jamii.app/MbandeUbadhirifu

#JamiiForums #Uwajibikaji #JFMdau2026
Changamoto ya nyayo kuwa na ngozi ngumu kisha kuchanika inajulikana kwa jina gani kwenu? Ni mbinu ipi unayoijua inafaa kuondoa au kutibu hali hiyo?

Zaidi https://jamii.app/GagaMiguuni

#JamiiForums #JFMdau2026 #Maisha #JFAfya #PublicHealth
Balozi wa China nchini Nigeria, Yu Dunhai ameeleza kuwa jengo hilo ni mradi wa kielelezo unaolenga kuimarisha uwezo wa ECOWAS na kusisitiza kuwa ushirikiano wa China na Afrika unazingatia sera ya "kutojiingiza katika mambo ya ndani" na kwamba msaada huo hauna masharti yoyote ya Kisiasa.

Zaidi: https://jamii.app/ChinaECOWAS

#JamiiForums #Diplomasia
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mdau ndani ya JamiiForums.com ametoa wito kwa mamlaka husika kushughulikia kero ya Barabara ya Kitunda Kivule akidai ni kero kwa wakazi wa eneo hilo, akieleza kuwa kuna hospitali kubwa ambapo Wananchi wanapata tabu wanapokuwa wanapita kuelekea au kutoka eneo hilo.

Zaidi https://jamii.app/BarabaraKitundaMbovu

#JamiiForums #Uwajibikaji #JFMdau2026
Mdau wa JamiiForums.com anatoa wito kwa Mamlaka zinazosimamia mfumo wa Ajira Portal kurekebisha vigezo katika maombi ya ajira kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ili kuwawezesha Watu wengi zaidi kupata fursa ya kufikisha maombi yao ya kazi.

Zaidi https://jamii.app/TAKUKURUAjira

#JamiiForums #Uwajibikaji #JFMdau2026 #DigitalWorld