JamiiForums
33.4K subscribers
37.4K photos
2.99K videos
32.9K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
UEFA: Baada ya PSG na Bayern Munich kuonesha mchezo mkali jana Aprili 28, 2026, leo Aprili 29, 2026, Arsenal itakuwa ugenini kuivaa Atletico Madrid, baada ya hapo mechi ya marudiano itapigwa Jumanne, Mei 5, 2026 kwenye Uwanja wa Emirates Jijini London, England. Mshindi wa jumla ataingia fainali kukutana na Paris Saint-Germain au Bayern Munich.

Soma https://jamii.app/AtleticoVsArsenal

#JamiiForums #JFSports #JFUEFA2026
ZANZIBAR: Goli pekee lililofungwa na mshambuliaji Selemani Mwalimu kwa penati baada ya Clatous Chotta Chama kuchezewa faulo ndani ya boksi limeipa Simba ushindi wa 1-0 dhidi ya Yanga katika Fainali ya Kombe la Muungano na hivyo kubeba ubingwa.

Mchezo huo uliopigwa kwa dakika 120 kwenye Uwanja wa New Amaan Complex umemaliza ‘uteja’ kwa Simba ambayo katika mechi saba zilizopita imefungwa sita na sare moja.

Kabla ya kufika Fainali hiyo, Yanga iliifunga Makumbi City magoli 4-0 kisha ikaichapa Azam FC 2-1 wakati Simba iliichapa Mafunzo 1-0 na kuitoa Mlandege kwa magoli 3-0.

Zaidi https://jamii.app/SimbaBingwaMuungano

#JamiiForums #JFSports #JFMuunganoCup2026
UHISPANIA: Nusu Fainali ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya timu kutoka Jiji la Madrid na ile ya London imemalizika kwa sare ya 1-1, Viktor Gyökeres akianza kuifungia Arsenal kisha Julián Alvarez akasawazisha.

Mchezo huo uliopigwa kwenye Uwanja wa Metropolitano Jijini Madrid umeshuhudia magoli yakiwekwa wavuni kwa njia ya penati, huku Julián Alvarez akiweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa Atletico kufikisha magoli 10 katika msimu mmoja wa ligi hiyo.

Mchezo wa pili baina ya timu hizo unatarajiwa kupigwa Mei 5, 2026 kwenye Uwanja wa Emirates.

Zaidi https://jamii.app/AtleticoArsenal

#JamiiForums #JFSports #JFUEFA2026
Mdau wa JamiiForums.com ametoa wito kwa Viongozi wa Taasisi za Umma kuheshimu ratiba ya likizo na kuweka kipaumbele Afya ya Akili kwa kuwaruhusu Watumishi kupata muda wa mapumziko na kubadili mazingira tofauti na kazi kwa mujibu wa Kanuni na Sheria za Kazi, sababu hiyo inaweza kuchangia kuongeza ufanisi.

Fuatilia mjadala huu https://jamii.app/LikizoWatumishiUmmaMateso

#JamiiForums #JFMdau2026 #UtawalaBora
ARUSHA: Jeshi la Polisi limeeleza kuwa linamshikilia Salmin Rajab mwenye umri wa Miaka 29, fundi ujenzi, Mkazi wa Sinoni kwa tuhuma za mauaji ya Mtoto wake aitwaye Sahiri Salmin mwenye umri wa miezi 8, kwa kumchinja shingoni na kutenganisha kichwa na kiwiliwili.

Kamanda wa Polisi Mkoa, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP, Justine Masejo amesema mtuhumiwa huyo alitenda kosa hilo Aprili 28, 2026 katika maeneo ya Sinoni na kwamba uchunguzi wa tukio hilo unaendelea ikiwa ni pamoja na kubaini chanzo chake.

Zaidi https://jamii.app/AmuuaMtotoMiezi8

#JamiiForums #HumanRights #JFMatukio
1
ZIMBABWE: Kando na Sean, Rais Emmerson Mnangagwa mnamo Septemba 2023 alim­teua mtoto wake David Kudakwashe Mnangagwa kuwa Naibu Waziri wa Fedha na Maendeleo ya Kiuchumi, na mpwa wake Tongai Mnangagwa kuwa Naibu Waziri wa Utalii.

Zaidi: https://jamii.app/RaisMnangagwa

#JamiiForums #Uwajibikaji #AfricanPolitics #Governance
MWANZA: Mdau wa JamiiForums.com anadokeza kuwa kuna Vijana wanafanya kazi bila kuwa na vifaa maalum vya usalama kazini kwenye jengo la ghorofa Mitaa ya Ghana, Mkabala na Hoteli ya Kingdome hali inayotishia usalama wao.

Anahoji "Wakala wa Usalama na Afya Mahala pa Kazi (OSHA) mko wapi? Hamuoni hayo yanayoendelea?"

Zaidi https://jamii.app/OshaVifaaKazi

#JamiiForums #JFMdau2026 #Uwajibikaji
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
KATAVI: Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Tulieni, Manispaa ya Mpanda amesema shule hiyo inakabiliwa na upungufu wa madawati kwani yapo 169 ikilinganishwa na idadi ya Wanafunzi 2,500.

Ameyasema hayo alipokuwa aliwasilisha changamoto hizo mbele ya Mwenyekiti wa CCM, Tawi la Tulieni walipotembelea, Aprili 24, 2026 ili kujua mwenendo wa shule hiyo pamoja na kuzipeleka maeneo husika.

Zaidi https://jamii.app/TulieniUhabaWalimu

#JamiiForums #Uwajibikaji #JFElimu

Video: KINYOGOTO JR
Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Rugemeleza Nshala amesema leo asubuhi Aprili 30, 2026, Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu alifikishwa Mahakamani na uamuzi uliotolewa umetupilia mbali hoja za kutaka kuunganishwa katika kesi ya mgawanyo wa mali za CHADEMA.

Zaidi: https://jamii.app/MahakamaKesiCHADEMA

#JamiiForums #Uwajibikaji #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
LINDI: Mwenyekiti wa Ngome ya Vijana Taifa wa Chama cha ACT Wazalendo, Abdul Omary Nondo akizungumzia orodha ya wanufaika wa maombi ya mkopo kupitia mfuko wa Maendeleo ya Vijana chini ya Wizara ya Maendeleo ya Vijana iliyotolewa Aprili 28, 2026.

Zaidi https://jamii.app/MikopoYaWizara

#JamiiForums #Uwajibikaji #UtawalaBora