Mshiriki wa Stories of Change (#SoC) 2022 Kupitia andiko lake ameelezea Wajibu na dhamana ya Wabunge kuleta maendeleo kwa Wananchi akisisitiza kuwa wanatakiwa kusikiliza na kufuatilia changamoto za Wananchi wao kisha kuwasilisha Serikalini ili kuweza kutatuliwa wakishirikiana na Viongozi wa ngazi za Vijiji, Kata na Halmashauri.
Ametoa wito kwa Wabunge nchini kutambua nafasi yao kama Viongozi wa Wananchi na sio Watumishi wa Serikali.
Soma zaidi https://jamii.app/Wabunge
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #SoC2022
Ametoa wito kwa Wabunge nchini kutambua nafasi yao kama Viongozi wa Wananchi na sio Watumishi wa Serikali.
Soma zaidi https://jamii.app/Wabunge
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #SoC2022
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Akizungumza katika Kampeni za Chama Cha Mapinduzi (#CCM), jana Septemba 4, 2025, Profesa Palamagamba Kabudi amesema Rais Samia Suluhu ametekeleza mambo makubwa ambayo Baba wa Taifa, Hayati Mwl. Julius Nyerere aliyatamani lakini hakuweza kuyafanya, na huko aliko Baba wa Taifa atakuwa anajivunia utekelezwa wake.
Zaidi Soma https://jamii.app/KabudiSamia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Democracy
Zaidi Soma https://jamii.app/KabudiSamia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Democracy
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Sumbawanga Mjini kupitia Chama cha #ACTWazalendo, Edwin Kachoma ametangaza kujiondoa katika kinyang’anyiro cha Uchaguzi Mkuu akidai amekosa ushirikiano kutoka Makao Makuu ya chama hicho, ikiwemo kushindwa kumpatia vifaa vya kampeni kama bendera na nyenzo nyingine muhimu.
Soma https://jamii.app/KachomaUbungeSumbawanga
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Democracy #JFUchaguzi2025
Soma https://jamii.app/KachomaUbungeSumbawanga
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Democracy #JFUchaguzi2025
❤1
ChatGPT inaoongoza kwa matumizi ya Akili Mnemba (AI) kote Ulimwenguni kwa Mwaka 2025, Watu wameitembelea mara bilioni 46.6 hali inayofanya kuwa na 48.36% ya soko zima la matumizi ya teknolojia hiyo.
Vilevile, kulingana na takwimu za Statcounter za Julai 2025, matumizi ya AI Tanzania yanaongozwa na ChatGPT, ambayo inatumiwa na Asilimia 86.3 ya watumiaji wote wa AI ambapo kati ya kila watumiaji 10 wa AI, zaidi ya 8 wanatumia ChatGPT.
Soma https://jamii.app/TakwimuMatumiziAI
#DigitalWorld #JamiiAfrica #JamiiForums #DigitalRights
Vilevile, kulingana na takwimu za Statcounter za Julai 2025, matumizi ya AI Tanzania yanaongozwa na ChatGPT, ambayo inatumiwa na Asilimia 86.3 ya watumiaji wote wa AI ambapo kati ya kila watumiaji 10 wa AI, zaidi ya 8 wanatumia ChatGPT.
Soma https://jamii.app/TakwimuMatumiziAI
#DigitalWorld #JamiiAfrica #JamiiForums #DigitalRights
❤4
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
ZANZIBAR: Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema, yeyote atakayezungumza kinyume na kuhubiri amani huyo hataki mema, akisisitiza kuwa kila Mwanasiasa na kiongozi wa dini akizungumza jambo lolote ambalo linaashiria uvunjifu wa amani huyo hafai.
Ameyasema hayo Septemba 4, 2025 wakati akifungua Soko na Kituo cha Mabasi cha Kisasa Chuini, Wilaya ya Magharibi A.
Zaidi soma https://jamii.app/RaisMwinyiAmani
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance #Siasa
Ameyasema hayo Septemba 4, 2025 wakati akifungua Soko na Kituo cha Mabasi cha Kisasa Chuini, Wilaya ya Magharibi A.
Zaidi soma https://jamii.app/RaisMwinyiAmani
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance #Siasa
❤1
DRC: Serikali imethibitisha mlipuko mpya wa Virusi vya Ebola, Kusini mwa Mji wa Kasai ambapo hadi sasa kuna Wagonjwa 28 wanaoshukiwa kuambukizwa, idadi ya vifo ikiwa ni 15.
Wizara ya Afya imesema mlipuko ulianza mwishoni mwa Agosti 2025 baada ya Mwanamke mjamzito kulazwa katika Hospitali ya Bulape akiwa na dalili za kutokwa na damu, na kufariki ndani ya wiki moja, baadaye wahudumu wa afya na wataalamu wa maabara waliomhudumia nao walianza kuonyesha dalili.
Ikumbukwe Septemba 4, 2025 Wizara ya Afya ilitangaza kuwa Ebola imerejea na inaenea katika eneo hilo ikiwa ni baada ya miaka 3 kupita. Rekodi zinaonesha Mwaka 2018 - 2020 Watu 2,300 walipoteza maisha kutokana na virusi hivyo.
Soma zaidi https://jamii.app/Ebola
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFAfya #PublicHealth
Wizara ya Afya imesema mlipuko ulianza mwishoni mwa Agosti 2025 baada ya Mwanamke mjamzito kulazwa katika Hospitali ya Bulape akiwa na dalili za kutokwa na damu, na kufariki ndani ya wiki moja, baadaye wahudumu wa afya na wataalamu wa maabara waliomhudumia nao walianza kuonyesha dalili.
Ikumbukwe Septemba 4, 2025 Wizara ya Afya ilitangaza kuwa Ebola imerejea na inaenea katika eneo hilo ikiwa ni baada ya miaka 3 kupita. Rekodi zinaonesha Mwaka 2018 - 2020 Watu 2,300 walipoteza maisha kutokana na virusi hivyo.
Soma zaidi https://jamii.app/Ebola
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFAfya #PublicHealth
🤬1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
SHINYANGA: Mgombea Urais kupitia Chama cha Wananchi (#CUF), Gombo Samandito Gombo amesema endapo atashinda katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, atamuachia huru Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA), Tundu Lissu, na kumjumuisha kwenye Kamati Maalum ya kutengeneza Katiba mpya.
Amesema hayo Septemba 4, 2025 wakati wa kampeni za chama chake.
Soma https://jamii.app/GomboAchiaLissu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Democracy #UchaguziMkuu2025
Amesema hayo Septemba 4, 2025 wakati wa kampeni za chama chake.
Soma https://jamii.app/GomboAchiaLissu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Democracy #UchaguziMkuu2025
❤1
Mdau, una maoni gani kuhusiana na mistari ya wimbo huu?
Tembelea JamiiForums.com kushiriki kwenye mijadala mbalimbali yenye tija.
Zaidi bofya https://jamii.app/JukwaaJamiiForums
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
Tembelea JamiiForums.com kushiriki kwenye mijadala mbalimbali yenye tija.
Zaidi bofya https://jamii.app/JukwaaJamiiForums
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
Turejee enzi zile za shule, pale tulipowapa Walimu wetu majina ya utani yaliyojaa ubunifu na ucheshi, bila shaka kila mmoja anakumbuka jina moja au mawili yaliyobaki kuwa kumbukumbu zetu mpaka leo.
Kushiriki mjadala https://jamii.app/MajinaWalimuUtani
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFChitChat
Kushiriki mjadala https://jamii.app/MajinaWalimuUtani
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFChitChat
❤2
GUINEA-BISSAU: Rais Umaro Sissoco Embaló ameingia katika mgogoro wa Kisiasa baada ya muhula wake kumalizika rasmi Usiku wa Septemba 4, 2025 bila ya kukabidhi madaraka. Ameendelea kushikilia madaraka, jambo ambalo upinzani umelitafsiri kama kunyakua madaraka kinyume cha Sheria.
Rais Embaló ameahidi kuendelea na majukumu yake hadi uchaguzi utakapofanyika Novemba 23, 2025 ambapo anatarajiwa kugombea muhula wa pili. Katiba ya Guinea-Bissau inaeleza muhula wa Urais ni Miaka mitano na unaweza kuongezwa mara moja pekee.
Upinzani unadai muhula wa Embaló ulipaswa kumalizika Februari 27, 2025 lakini Mahakama Kuu iliamua uendelee hadi Septemba 4, 2025. Hata hivyo, kwa miezi kadhaa, Vyama vya Upinzani vimekataa kumtambua Embaló kama Rais halali.
Soma zaidi https://jamii.app/GuineaBissau
#JamiiAfrica #JamiiForums #AfricanPolitics #Democracy #Governance
Rais Embaló ameahidi kuendelea na majukumu yake hadi uchaguzi utakapofanyika Novemba 23, 2025 ambapo anatarajiwa kugombea muhula wa pili. Katiba ya Guinea-Bissau inaeleza muhula wa Urais ni Miaka mitano na unaweza kuongezwa mara moja pekee.
Upinzani unadai muhula wa Embaló ulipaswa kumalizika Februari 27, 2025 lakini Mahakama Kuu iliamua uendelee hadi Septemba 4, 2025. Hata hivyo, kwa miezi kadhaa, Vyama vya Upinzani vimekataa kumtambua Embaló kama Rais halali.
Soma zaidi https://jamii.app/GuineaBissau
#JamiiAfrica #JamiiForums #AfricanPolitics #Democracy #Governance
❤2
Baada ya Mdau wa JamiiForums.com kulalamikia huduma za Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL) hasa ile ya TTCL Fiber kuwa ni changamoto, inachukua muda mrefu na pia kuna mazingira ya rushwa, hoja ambazo ziliungwa na Wachangiaji wengine kupitia Instagram, TTCL imesema inafanyia kazi maoni hayo kwa ajili ya kuboresha huduma zao.
TTCL imeomba radhi na kueleza kuwa hatua za ndani zitachukuliwa kwa yeyote aliyeshiriki na kusisitiza kuwa huduma ya kufungiwa "Faiba" ni bure na kwamba Mteja atapaswa kulipia kifurushi kulingana na mahitaji yake ambapo bei ya kifurushi kinaanzia Tsh. 55, 000.
Soma zaidi https://jamii.app/TTCL
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #JFMdau2025 #Uwajibikaji
TTCL imeomba radhi na kueleza kuwa hatua za ndani zitachukuliwa kwa yeyote aliyeshiriki na kusisitiza kuwa huduma ya kufungiwa "Faiba" ni bure na kwamba Mteja atapaswa kulipia kifurushi kulingana na mahitaji yake ambapo bei ya kifurushi kinaanzia Tsh. 55, 000.
Soma zaidi https://jamii.app/TTCL
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #JFMdau2025 #Uwajibikaji
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imesitisha Leseni ya Maudhui Mtandaoni ya JamiiForums kwa muda wa siku 90 na kuzuia upatikanaji wa jukwaa hilo, kwa maelezo ya kukiuka Kanuni za Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta kuhusu maudhui mtandaoni
TCRA imesema uamuzi huu umetokana na JamiiForums kuchapisha taarifa ya Mwanasiasa Humphrey Polepole kuhusu Rostam kumiliki mgodi wa makaa ya mawe kwa asilimia 70 na taarifa za uhusiano kati ya Rais wa Tanzania na "Mfanyabiashara" Wicknell Chivayo bila kuzingatia mizania.
Kwa mujibu wa TCRA, JamiiForums ilishindwa kutafuta maoni ya Mamlaka husika/Msemaji wa Rais/Serikali, kuthibitisha uhalisia wa picha (za Rais na Chivayo) zilizotumika, na hivyo kuuaminisha Umma taarifa za upande mmoja.
Aidha, TCRA imeeleza kuwa jukwaa la JamiiForums halikudhibiti maudhui yenye lugha ya matusi, kashfa na kejeli dhidi ya Rais wa Tanzania, na kuendelea kuhifadhi maudhui hayo ambayo bado yanapatikana kwa umma.
#JamiiForums
TCRA imesema uamuzi huu umetokana na JamiiForums kuchapisha taarifa ya Mwanasiasa Humphrey Polepole kuhusu Rostam kumiliki mgodi wa makaa ya mawe kwa asilimia 70 na taarifa za uhusiano kati ya Rais wa Tanzania na "Mfanyabiashara" Wicknell Chivayo bila kuzingatia mizania.
Kwa mujibu wa TCRA, JamiiForums ilishindwa kutafuta maoni ya Mamlaka husika/Msemaji wa Rais/Serikali, kuthibitisha uhalisia wa picha (za Rais na Chivayo) zilizotumika, na hivyo kuuaminisha Umma taarifa za upande mmoja.
Aidha, TCRA imeeleza kuwa jukwaa la JamiiForums halikudhibiti maudhui yenye lugha ya matusi, kashfa na kejeli dhidi ya Rais wa Tanzania, na kuendelea kuhifadhi maudhui hayo ambayo bado yanapatikana kwa umma.
#JamiiForums
❤17🤬17👎1