Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
ZANZIBAR: Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa tisa wa Chama cha Walimu Zanzibar (ZATU), Wilaya ya Mjini Unguja Agosti 13, 2025, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar, Lela Mohammed Mussa amesema kumfundisha Mtoto ndani ya chumba hakumpi nafasi Mwanafunzi kujifunza kwani Watoto wanahitaji eneo la kutosha ili kujifunza.
Waziri Lela amesema hayo yanafanyika kutokana na baadhi ya Wazazi kuendelea kuwapeleka Watoto wao katika maeneo hayo ambayo hayakidhi vigezo vya kuwafundisha Watoto hasa ngazi ya awali, hivyo Serikali imepiga marufuku shule ambazo zipo ndani ya nyumba (skuli nyumba) na kuwataka wamiliki kujenga majengo yanayokidhi utoaji wa huduma kwa Wanafunzi wao.
Ikumbukwe, Mwaka 2023, Ripoti ya Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ilionesha vitendo vya ukatili wa kijinsia vimeripotiwa kuongezeka #Zanzibar kutoka matukio 1,222 Mwaka 2021 hadi 1,360 Mwaka 2022, ambapo kati ya hayo matukio 1,173 yalijumuisha Watoto.
Soma zaidi https://jamii.app/SkuliNgumbaMarufuku
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFElimu #Uwajibikaji #Accountability #Governance
Waziri Lela amesema hayo yanafanyika kutokana na baadhi ya Wazazi kuendelea kuwapeleka Watoto wao katika maeneo hayo ambayo hayakidhi vigezo vya kuwafundisha Watoto hasa ngazi ya awali, hivyo Serikali imepiga marufuku shule ambazo zipo ndani ya nyumba (skuli nyumba) na kuwataka wamiliki kujenga majengo yanayokidhi utoaji wa huduma kwa Wanafunzi wao.
Ikumbukwe, Mwaka 2023, Ripoti ya Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali ilionesha vitendo vya ukatili wa kijinsia vimeripotiwa kuongezeka #Zanzibar kutoka matukio 1,222 Mwaka 2021 hadi 1,360 Mwaka 2022, ambapo kati ya hayo matukio 1,173 yalijumuisha Watoto.
Soma zaidi https://jamii.app/SkuliNgumbaMarufuku
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFElimu #Uwajibikaji #Accountability #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
GEITA: Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (#TAKUKURU) imewakamata Wajumbe wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), Kata ya Nyankumbu walioonekana katika picha mjongeo wakigawana rushwa Agosti 2, 2025 katika mchakato wa uchaguzi ndani ya #CCM.
TAKUKURU imeeleza kuwa baada ya tukio hilo kusambaa, ofisi ya mkoa ilichukua hatua ya haraka kwa kuwatambua na kuwakamata wajumbe waliokuwa wakionekana kwenye picha hizo na kwamba Inadaiwa kuwa vitendo hivyo vilifanyika mara baada ya zoezi la kuwanadi wagombea Ubunge kukamilika.
Aidha, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa, James Ruge amesema kutokana na matukio hayo na mengine, ofisi imeanzisha uchunguzi unaoelekea kukamilika, ikiwa ni hatua ya kukusanya ushahidi ili kuthibitisha tuhuma za rushwa dhidi ya wahusika.
Zaidi soma https://jamii.app/WajumbeUWTTuhumaRushwa
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #UchaguziMkuu2025 #KataaRushwa
TAKUKURU imeeleza kuwa baada ya tukio hilo kusambaa, ofisi ya mkoa ilichukua hatua ya haraka kwa kuwatambua na kuwakamata wajumbe waliokuwa wakionekana kwenye picha hizo na kwamba Inadaiwa kuwa vitendo hivyo vilifanyika mara baada ya zoezi la kuwanadi wagombea Ubunge kukamilika.
Aidha, Mkuu wa TAKUKURU Mkoa, James Ruge amesema kutokana na matukio hayo na mengine, ofisi imeanzisha uchunguzi unaoelekea kukamilika, ikiwa ni hatua ya kukusanya ushahidi ili kuthibitisha tuhuma za rushwa dhidi ya wahusika.
Zaidi soma https://jamii.app/WajumbeUWTTuhumaRushwa
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #UchaguziMkuu2025 #KataaRushwa
❤2
GEITA: Jeshi la Polisi linawashikilia Askari wanne wa Jeshi la Uhifadhi (JESHI USU) kwa tuhuma za mauaji ya Eziboni Fikiri (20), Mkulima, Mkazi wa Kijiji cha Msonga, Wilaya ya Bukombe ambaye walimkuta akikata mti eneo la Pori la Hifadhi ya Kigosi, Wilaya ya Bukombe, Agosti 13, 2025.
Taarifa ya Polisi imesema Mwili umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya kwa ajili ya uchunguzi huku Watuhumiwa wakihojiwa na kwamba uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.
Ikumbukwe hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni saa chache tangu Mdau wa JamiiForums.com awasilishe andiko akitoa wito kwa Jeshi la Polisi na TFS kufuatilia tukio hilo akidai kuna ukimya na hatua hazijachukuliwa.
Soma https://jamii.app/Askari4MauajiGeita
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji
Taarifa ya Polisi imesema Mwili umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya kwa ajili ya uchunguzi huku Watuhumiwa wakihojiwa na kwamba uchunguzi utakapokamilika watafikishwa Mahakamani.
Ikumbukwe hatua hiyo imechukuliwa ikiwa ni saa chache tangu Mdau wa JamiiForums.com awasilishe andiko akitoa wito kwa Jeshi la Polisi na TFS kufuatilia tukio hilo akidai kuna ukimya na hatua hazijachukuliwa.
Soma https://jamii.app/Askari4MauajiGeita
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji
🤬1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Baadhi ya Wanachama wa CCM Kata ya Bereko na Kisese Wilayani Kondoa wametaka mchakato wa kura za maoni za Udiwani na Ubunge wa Kondoa Vijijini urudiwe, wakisema mchakato huo uligubikwa na madai ya #Rushwa na kwamba Viongozi waliochaguliwa kwenye mchakato huo walipendelewa.
Akijibu tuhuma hizo Katibu wa CCM Wilaya ya Kondoa, Abdulrahim Dogo alipozungumza na ITV amesema “Kura za maoni haimaanishi aliyeongoza kwenye Kura za maoni ndio mshindi na ndio Kanuni yetu ya Uchaguzi, isipokuwa tu kura hizo zimepigwa kwa ajili ya kuvisaidia vikao vya juu vifanye uteuzi wa mwisho.”
Zaidi Soma https://jamii.app/KuraZaMaoniKondoa
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Accountability #Democracy
Akijibu tuhuma hizo Katibu wa CCM Wilaya ya Kondoa, Abdulrahim Dogo alipozungumza na ITV amesema “Kura za maoni haimaanishi aliyeongoza kwenye Kura za maoni ndio mshindi na ndio Kanuni yetu ya Uchaguzi, isipokuwa tu kura hizo zimepigwa kwa ajili ya kuvisaidia vikao vya juu vifanye uteuzi wa mwisho.”
Zaidi Soma https://jamii.app/KuraZaMaoniKondoa
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Accountability #Democracy
Mdau wa JamiiForums.com ametoa wito kwa mamlaka zinazohusika na Sekta ya Elimu kuheshimu uhuru wa Vyuo Vikuu katika kuandaa na kusimamia mitaala ili kuondoa mkanganyiko na mabadiliko yasiyo na tija kwenye mitaala hiyo na fani mbalimbali.
Amedai maelekezo yasiyo wazi kutoka mamlaka za udhibiti wa mitaala yamesababisha mkanganyiko na baadhi ya fani kufutwa, akitoa mfano wa Chuo cha #UDOM ambapo Programu ya Education with Psychology ilisitishwa bila ya alichokiita “mashauriano ya kutosha” kati ya chuo na mamlaka husika kufanyika.
Ameshauri mamlaka zishauriane na Vyuo Vikuu na kuhusisha wabobezi pamoja na Sekta Binafsi kabla ya kubadilisha au kusitisha mitaala ili kuhakikisha mitaala hiyo ina manufaa ya muda mrefu na ushindani wa Kimataifa.
Mjadala zaidi Soma https://jamii.app/FaniVyuoni
#JamiiForums #JFElimu #JFMdau2025 #Accountability
Amedai maelekezo yasiyo wazi kutoka mamlaka za udhibiti wa mitaala yamesababisha mkanganyiko na baadhi ya fani kufutwa, akitoa mfano wa Chuo cha #UDOM ambapo Programu ya Education with Psychology ilisitishwa bila ya alichokiita “mashauriano ya kutosha” kati ya chuo na mamlaka husika kufanyika.
Ameshauri mamlaka zishauriane na Vyuo Vikuu na kuhusisha wabobezi pamoja na Sekta Binafsi kabla ya kubadilisha au kusitisha mitaala ili kuhakikisha mitaala hiyo ina manufaa ya muda mrefu na ushindani wa Kimataifa.
Mjadala zaidi Soma https://jamii.app/FaniVyuoni
#JamiiForums #JFElimu #JFMdau2025 #Accountability
MWANZA: Mdau wa JamiiForums.com anatoa wito kwa Mamlaka kufuatilia tukio analodai linadalili za ‘kuminywa’ linalohusu Mtoto wa Kiume wa Miaka Minne Mkazi wa Nyakato kulawitiwa na jirani yake na kwamba suala hilo lilipofikishwa Kituo cha Polisi Kirumba kumekuwa na hali ya sintofahamu kuhusu kinachoendelea.
Mdau anadai Mtoto anaishi na bibi yake, alipofanyiwa ukatili huo mara mbili mtuhumiwa alimwambia asiseme kwa kuwa akisema bibi yake ‘atamchapa sana’. Bibi alipoona mjukuu anatembea kwa kuchechemea akamlazimisha kusema nini kimemsibu, ndipo Mtoto akaelezea na kumtaja jirani yao.
Mdau anaongeza kuwa Bibi na Mtoto walipoenda kuripoti Kituo cha Polisi Nyakato walimkuta Mtuhumiwa eneo hilo pia akipiga ‘stori’ na Askari, Mtoto akaonesha aliyemfanyia ukatili yupo eneo hilo, mtuhumiwa akakamatwa lakini baada ya kesi kuhamishiwa Kituo cha Polisi Kirumba ndipo kukatokea ‘sintofahamu’ na haijulikani nini kinachoendelea.
Soma zaidi https://jamii.app/UkatiliNyakato
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Mdau anadai Mtoto anaishi na bibi yake, alipofanyiwa ukatili huo mara mbili mtuhumiwa alimwambia asiseme kwa kuwa akisema bibi yake ‘atamchapa sana’. Bibi alipoona mjukuu anatembea kwa kuchechemea akamlazimisha kusema nini kimemsibu, ndipo Mtoto akaelezea na kumtaja jirani yao.
Mdau anaongeza kuwa Bibi na Mtoto walipoenda kuripoti Kituo cha Polisi Nyakato walimkuta Mtuhumiwa eneo hilo pia akipiga ‘stori’ na Askari, Mtoto akaonesha aliyemfanyia ukatili yupo eneo hilo, mtuhumiwa akakamatwa lakini baada ya kesi kuhamishiwa Kituo cha Polisi Kirumba ndipo kukatokea ‘sintofahamu’ na haijulikani nini kinachoendelea.
Soma zaidi https://jamii.app/UkatiliNyakato
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
❤2
MWANZA: Baada ya Mdau wa JamiiForums.com kuhoji Kiongozi gani wa juu anayemlinda mtuhumiwa wa Ulawiti kwa Mtoto katika Kituo cha Polisi Kirumba, Mkuu wa Mkoa, Said Mtanda ametoa maelekezo kwa Mwananchi huyo kuhusu kipi anachotakiwa kukifanya.
RC Mtanda ameandika “Namshauri huyo aliyedhurumiwa haki yake kufika pia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya au Mkoa, kwa Mwanza kila Jumanne tunakutana na Wananchi wenye changamoto za namna hizo, anaweza kuwa hajasikilizwa na taasisi moja lakini Kiongozi wa Serikali katika Wilaya ya Nyamagana ni Mkuu wa Wilaya amuone, yawezekana hajui. Kama hatasikilizwa aje Ofisi ya Mkuu wa Mkoa siku ya Jumanne.”
Ikumbukwe Mdau alisema Mtu huyo ambaye amemlawiti Mtoto wa Miaka minne eneo la Nyakato, alifikishwa Kituo cha Polisi akahojiwa, Mtoto akatoa maelezo, vipimo vya Hospitali ya Sekou Toure vikaonesha ameingiliwa lakini hakuna kinachoendelea, akidai kuna mazingira ya Mtuhumiwa kulindwa na Kiongozi wa ‘juu’.
Zaidi soma https://jamii.app/RCMtandaUfafanuzi
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
RC Mtanda ameandika “Namshauri huyo aliyedhurumiwa haki yake kufika pia Ofisi ya Mkuu wa Wilaya au Mkoa, kwa Mwanza kila Jumanne tunakutana na Wananchi wenye changamoto za namna hizo, anaweza kuwa hajasikilizwa na taasisi moja lakini Kiongozi wa Serikali katika Wilaya ya Nyamagana ni Mkuu wa Wilaya amuone, yawezekana hajui. Kama hatasikilizwa aje Ofisi ya Mkuu wa Mkoa siku ya Jumanne.”
Ikumbukwe Mdau alisema Mtu huyo ambaye amemlawiti Mtoto wa Miaka minne eneo la Nyakato, alifikishwa Kituo cha Polisi akahojiwa, Mtoto akatoa maelezo, vipimo vya Hospitali ya Sekou Toure vikaonesha ameingiliwa lakini hakuna kinachoendelea, akidai kuna mazingira ya Mtuhumiwa kulindwa na Kiongozi wa ‘juu’.
Zaidi soma https://jamii.app/RCMtandaUfafanuzi
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
KATAVI: Mwakilishi wa Wafanyabiashara Mjini Mpanda, Aman Mahella amehoji kwanini mikopo kwa Vijana na akinamama hutolewa karibu na Uchaguzi huku ikiambatana na ujumbe wa Kisiasa jambo linaloashiria rushwa?
Akizungumza katika mafunzo ya kupambana na #Rushwa kuelekea #UchaguziMkuu2025, yaliyotolewa na #TAKUKURU, Ijumaa Agosti 15, 2025, Mahella ametoa wito kwa Serikali kuimarisha mifumo ya kudhibiti rushwa ili kuondoa mianya hiyo wakati wa Uchaguzi.
Soma https://jamii.app/RushwaMikopoUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #Governance
Akizungumza katika mafunzo ya kupambana na #Rushwa kuelekea #UchaguziMkuu2025, yaliyotolewa na #TAKUKURU, Ijumaa Agosti 15, 2025, Mahella ametoa wito kwa Serikali kuimarisha mifumo ya kudhibiti rushwa ili kuondoa mianya hiyo wakati wa Uchaguzi.
Soma https://jamii.app/RushwaMikopoUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #Governance
DAR: Mdau wa JamiiForums.com amedai kuna changamoto ya upatikanaji wa kadi zinazotumika kununua tiketi katika usafiri wa Mabasi ya Mwendokasi na kutoa wito hatua zichukuliwe haraka kwa kuwa hali hiyo ni kero na inawakosesha baadhi ya Watu huduma.
Ikumbukwe Julai 26, 2025 Mdau mwingine alidai kuna kero kubwa ya kutopatikana kwa kadi hizo siku za wikiendi, Agosti 6, 2025, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), Dkt. Athumani Kihamia alisema sio lengo lao kuuza kadi wakati wa Siku za Jumamosi na Jumapili, abiria anaweza kupata kadi kwa siku tano za wiki ambazo ni Jumatatu hadi Ijumaa.
Mjadala zaidi https://jamii.app/TiketiMwendokasi
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
Ikumbukwe Julai 26, 2025 Mdau mwingine alidai kuna kero kubwa ya kutopatikana kwa kadi hizo siku za wikiendi, Agosti 6, 2025, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), Dkt. Athumani Kihamia alisema sio lengo lao kuuza kadi wakati wa Siku za Jumamosi na Jumapili, abiria anaweza kupata kadi kwa siku tano za wiki ambazo ni Jumatatu hadi Ijumaa.
Mjadala zaidi https://jamii.app/TiketiMwendokasi
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
❤1
Mdau wa JamiiForums.com kupitia jukwaa la Siasa ameibua hoja kuhusu magari yenye plate number za aina ya SSH 25-30 au SSH 2530, akisema kuna magari mengi yenye namba zinazofanana na wengi mtaani wanajiuliza iwapo wamiliki wake ni viongozi au la!
Amehoji iwapo tukio kama ajali au uhalifu likitokea litahusianishwa na gari lipi? Je, hii si aina ya kampeni ya mapema?
Kushiriki mjadala huu https://jamii.app/PlateNumberZaSamia
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji #Misinformation #Disinformation #MisDis2025 #TaarifaZaUchaguzi2025
Amehoji iwapo tukio kama ajali au uhalifu likitokea litahusianishwa na gari lipi? Je, hii si aina ya kampeni ya mapema?
Kushiriki mjadala huu https://jamii.app/PlateNumberZaSamia
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji #Misinformation #Disinformation #MisDis2025 #TaarifaZaUchaguzi2025
❤3
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
ARUSHA: Akizungumza na Waandishi wa Habari, Agosti 16, 2025, Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM, Saipulan Ramsey amesema “Chama Cha Mapinduzi hakijatoa kwa Mwanachama yeyote wala Mwananchi yeyote wala kutoa ruksa ya utengenezaji wa Namba za 'SSH 2530'. Ziko mamlaka husika zinazohusika na utoaji wa vibao vya namba za magari.”
Ameongeza “Chama hakina mamlaka ya kutengeneza vibao vya namba za magari, zipo mamlaka husika zinazoshughulika na jukumu hilo. Naomba mamlaka zinazohusika na utoaji wa namba za magari pamoja na usafirishaji zifuatilie yeyote aliyeweka namba hizo awaeleze amezipata wapi.”
Video Credit: Arusha Zone
Soma zaidi https://jamii.app/NambaZaSSH2530
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
Ameongeza “Chama hakina mamlaka ya kutengeneza vibao vya namba za magari, zipo mamlaka husika zinazoshughulika na jukumu hilo. Naomba mamlaka zinazohusika na utoaji wa namba za magari pamoja na usafirishaji zifuatilie yeyote aliyeweka namba hizo awaeleze amezipata wapi.”
Video Credit: Arusha Zone
Soma zaidi https://jamii.app/NambaZaSSH2530
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MWANZA: Mkuu wa Mkoa, Said Mtanda, leo Jumatatu Agosti 18, 2025 amefafanua suala la Mtoto Mkazi wa Nyakato, Wilayani Ilemela aliyesemekana kulawitiwa na Steven Ibasa (Baba Claudia), kwa kueleza kuwa suala hilo limefikishwa Mahakamani na kwamba mtuhumiwa amekosa mtu wa kumdhamini, amepelekwa Gerezani Butimba.
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Akizungumza Agosti 18, 2025, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime amesema "Tukiona moshi unafuka hatutasubiri moto uwake, tutachukua hatua. Tukiona matamshi ambayo hayastahili, tunajua huku anakoelekea huyu siyo sahihi, lazima tuzuie kabla ya kutokea madhara."
Soma https://jamii.app/MishimeMoshi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
Soma https://jamii.app/MishimeMoshi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
❤1👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MWANZA: Kulwa Steven Ibasa (37) anayetuhumiwa kumlawiti Mtoto wa Kiume (4), amefikishwa Mahakama ya Ilemela, jana Agosti 18, 2025 na baada ya shauri lake kutajwa alikosa Mtu wa kumdhamini akapelekwa Gerezani Butimba.
Hati ya Mashtaka imesomwa na Wakili wa Serikali, Mwanahawa Changali mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Juma Opudo imeeleza Kesi hiyo Namba 20028/2025, Ibasa ameshtakiwa kwa shtaka la kulawiti, kinyume na Kifungu cha 154(1)(a)(2) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16, marejeo ya Mwaka 2023.
Mshtakiwa alikana mashtaka ambapo kesi imepangwa kutajwa tena Septemba 1, 2025 kwa ajili ya kuanza kusikilizwa upande wa mashahidi.
Ikumbukwe, Agosti 15, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alihoji ukimya wa Mamlaka kuhusu tukio hilo, Mkuu wa Mkoa, Saidi Mtanda, akatoa maelekezo suala hilo lifanyiwe kazi ndipo Agosti 18 mtuhumiwa akafikishwa Mahakamani.
Zaidi soma https://jamii.app/NyakatoMatukio
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Hati ya Mashtaka imesomwa na Wakili wa Serikali, Mwanahawa Changali mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Juma Opudo imeeleza Kesi hiyo Namba 20028/2025, Ibasa ameshtakiwa kwa shtaka la kulawiti, kinyume na Kifungu cha 154(1)(a)(2) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16, marejeo ya Mwaka 2023.
Mshtakiwa alikana mashtaka ambapo kesi imepangwa kutajwa tena Septemba 1, 2025 kwa ajili ya kuanza kusikilizwa upande wa mashahidi.
Ikumbukwe, Agosti 15, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alihoji ukimya wa Mamlaka kuhusu tukio hilo, Mkuu wa Mkoa, Saidi Mtanda, akatoa maelekezo suala hilo lifanyiwe kazi ndipo Agosti 18 mtuhumiwa akafikishwa Mahakamani.
Zaidi soma https://jamii.app/NyakatoMatukio
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akizungumza Agosti 18, 2025 kwenye Baraza la Wafanyakazi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza S. Johari ametoa onyo kwa Watumishi wanaovujisha siri za Serikali, akibainisha kuwa ofisi yake itawafuatilia kwa ukaribu na kuchukua hatua za kinidhamu kwani ni kinyume na miongozo, Kanuni na Sheria za nchi, pia kufanya hivyo ni sawa na kujipiga risasi mwenyewe.
Pia, alieleza kusikitishwa na uwepo wa Mawakili wa Serikali wenye tabia za uongo, akisema jambo hilo linaweza kuipunguzia heshima taaluma ya Sheria na kuichafua taswira ya Serikali mbele ya umma.
Soma zaidi https://jamii.app/MwanasheriaSerikali
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
Pia, alieleza kusikitishwa na uwepo wa Mawakili wa Serikali wenye tabia za uongo, akisema jambo hilo linaweza kuipunguzia heshima taaluma ya Sheria na kuichafua taswira ya Serikali mbele ya umma.
Soma zaidi https://jamii.app/MwanasheriaSerikali
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
ARUSHA: Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Habari na Hoja Mchanganyiko ametoa ushauri kwa Mamlaka za Jiji kuangalia changamoto ya baadhi ya Maafisa wa Usalama katika Barabara kati ya Soko Kuu na Sokoine, akidai hawatendi haki kwa baadhi ya madereva wanaopita njia hiyo kiasi kwamba wengine wanatengeneza mazingira ya usumbufu ili 'wamalizana pembeni'.
Soma zaidi https://jamii.app/FainiArusha
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #JFMdau2025 #Accountability
Soma zaidi https://jamii.app/FainiArusha
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #JFMdau2025 #Accountability
👍1
KATAVI: Mdau wa JamiiForums.com aliyejitambulisha kuwa Mkazi wa Wilaya ya Mpanda anatoa wito kwa Shirika la Umeme Tanzania (#TANESCO) kushughulikia changamoto ya umeme kukatika mara kwa mara, akihoji mbona wanapodai madai yao hutumia magari ya matangazo kuzunguka Mtaani kufikisha ujumbe, lakini suala la kukata umeme hutumia makundi ya WhatsApp ambayo Wananchi wengi hawana au hawatumii?
Zaidi soma https://jamii.app/UmemeMpanda
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
Zaidi soma https://jamii.app/UmemeMpanda
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
ETHIOPIA: Wizara ya Elimu imetoa mwongozo unaopiga marufuku utoaji wa Shahada za Heshima (Honorary Doctorate) kwa Viongozi wa Serikali na Wanasiasa walioko madarakani, agizo hilo limetiwa saini na Waziri wa Elimu, Profesa Berhanu Nega, na limeelekezwa kwa Vyuo Vikuu na taasisi zote za elimu.
Mwongozo huo umeweka masharti mapya, ukiwataka wanaotunukiwa wawe ni waliotoa mchango mkubwa katika taaluma au kazi zao. Viongozi walioko kazini na Wafanyakazi wa Vyuo Vikuu na Wajumbe wa Seneti, hawataruhusiwa kupokea shahada hizo wakiwa bado kazini.
Aidha, vyuo vitakavyotoa shahada ya heshima vinapaswa kutoa kozi za PhD, viwe na angalau awamu nane za wahitimu, na viwe vinatambulika Kitaifa na Kimataifa.
Upande wa Tanzania, miongoni mwa waliotunukiwa Shahada za Heshima na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni Hayati Mwalimu Julius Nyerere (1966, 1986), Balozi Juma Mwapachu (2005), na Rais Mstaafu Hayati Benjamin Mkapa (2006). Licha ya mchango wao mkubwa, hawakuwahi kutumia cheo cha “Daktari wa Heshima”.
Zaidi soma https://jamii.app/EthiopiaMarufukuPhD
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
Mwongozo huo umeweka masharti mapya, ukiwataka wanaotunukiwa wawe ni waliotoa mchango mkubwa katika taaluma au kazi zao. Viongozi walioko kazini na Wafanyakazi wa Vyuo Vikuu na Wajumbe wa Seneti, hawataruhusiwa kupokea shahada hizo wakiwa bado kazini.
Aidha, vyuo vitakavyotoa shahada ya heshima vinapaswa kutoa kozi za PhD, viwe na angalau awamu nane za wahitimu, na viwe vinatambulika Kitaifa na Kimataifa.
Upande wa Tanzania, miongoni mwa waliotunukiwa Shahada za Heshima na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni Hayati Mwalimu Julius Nyerere (1966, 1986), Balozi Juma Mwapachu (2005), na Rais Mstaafu Hayati Benjamin Mkapa (2006). Licha ya mchango wao mkubwa, hawakuwahi kutumia cheo cha “Daktari wa Heshima”.
Zaidi soma https://jamii.app/EthiopiaMarufukuPhD
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Siasa ameibua hoja kuhusu wimbi la baadhi ya Watu maarufu na Wanasiasa kujipendekeza kwa Watawala maarufu kama ‘uchawa’ hali ambayo imeonekana kuzidi kushamiri kadri joto la Uchaguzi linavyopanda.
Amedai kuwa tabia hiyo haimfurahishi kwani inaleta madhara kwa Taifa, ikiwemo kupotosha Wapiga Kura na kuharibu mwelekeo wa Demokrasia.
Je, Wanasiasa wanaojipendekeza wanatafuta nafasi za Uongozi kwa maslahi ya Taifa na Wananchi, au ni kwa ajili ya maslahi yao binafsi?
Zaidi Soma https://jamii.app/KujipendekezaWagombea
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025
Amedai kuwa tabia hiyo haimfurahishi kwani inaleta madhara kwa Taifa, ikiwemo kupotosha Wapiga Kura na kuharibu mwelekeo wa Demokrasia.
Je, Wanasiasa wanaojipendekeza wanatafuta nafasi za Uongozi kwa maslahi ya Taifa na Wananchi, au ni kwa ajili ya maslahi yao binafsi?
Zaidi Soma https://jamii.app/KujipendekezaWagombea
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025
❤1👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Askofu Gervas Nyaisonga amewaasa vijana kutojishughulisha na dhambi ya mauaji pamoja na matukio ya utekaji akisisitiza kuwa hakuna mtu mwenye haki juu ya uhai wa mtu mwingine.
Ameyasema hayo leo Agosti 20 wakati wa mahubiri kwenye Misa Takatifu ya Ufunguzi wa Kongamano la 6 la Viwawa Taifa ambalo linafanyika Jimbo kuu la Mbeya katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mbeya.
Zaidi soma https://jamii.app/MshirikiDhambiMauaji
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji
Ameyasema hayo leo Agosti 20 wakati wa mahubiri kwenye Misa Takatifu ya Ufunguzi wa Kongamano la 6 la Viwawa Taifa ambalo linafanyika Jimbo kuu la Mbeya katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mbeya.
Zaidi soma https://jamii.app/MshirikiDhambiMauaji
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji