JamiiForums
52.6K subscribers
34.4K photos
2.46K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Afisa Mtendaji Mkuu wa Media Council Kenya, David Omwoyo amesema kuwawezesha Wananchi kutambua habari zinazofaa, kufichua upotoshaji, na kuwaelimisha juu ya athari za kushiriki katika upotoshaji wa habari na kusambaza habari potofu ni muhimu zaidi kuliko kuwafuata watu mitandaoni na kuwashughulikia kwa nguvu

Amesema "Teknolojia inabadilika kwa kasi zaidi kuliko uwezo wa wasimamizi kuweka Sheria hivyo ni muhimu kuwapa Wananchi ujuzi wa habari ili waweze kutambua habari za uongo, upotoshaji na teknolojia za uundaji wa video za kughushi"

Ameongeza "Tunahitaji kupunguza udhibiti na badala yake kuwawezesha Watu kuchambua ukweli na kujielewa wenyewe"

Soma https://jamii.app/EACA2024

#JamiiForums #PressFreedom #FreedomOfExpression #MisInformation #FactsChecking #Democracy
👍31
JIUNGE NA 'CHANNEL' YA WHATSAPP YA JAMIICHECK UWE WA KWANZA KUPATA TAARIFA ZILIZOHAKIKIWA

JamiiForums kupitia Jukwaa lake la JamiiCheck.com inaendelea kukupa nafasi ya Kuhabarika, Kuelimika, Kuburudika pamoja na Kushiriki mchakato wa Kuhakiki Taarifa kila wakati na kwa haraka zaidi, ambapo hivi sasa imekuongezea sehemu nyingine ya kupata taarifa hizo kupitia Mtandao wa #WhatsApp 

Jiunge sasa na 'Channel' ya JamiiCheck kwa kubofya https://jamii.app/JConWhatsApp

#JamiiForums #HakikiTaarifa #Misinformation #Disinformation #FactsChecking #VisitJamiiCheck
👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Mdau wa JamiiCheck.com alitaka kufahamu Uhalisia wa Video inayosambaa katika Mitandao ya Kijamii ikimuonesha Makamu Mwenyekiti wa #CHADEMA (Bara), Tundu Lissu akizomewa wakati akizungumza na Waandishi wa Habari Septemba 11, 2024

#JamiiCheck imefanya Uhakiki wa Video hiyo na kubaini kuwa imehaririwa kwa kuongezewa sauti zinazosikika zikisema "Toka wee, Yuda huyo, tunamtaka Mwenyekiti" ambazo hazipo kwenye Video Halisi ya mkutano huo uliorushwa mbashara kupitia baadhi ya chaneli za Youtube.

Soma https://jamii.app/TunduLissuMkutanoni

#JamiiCheck #HakikiTaarifa #FactsCheck #FactsChecking #VisitJamiiCheck #MisDis04
👍2
Mdau wa JamiiCheck.com alihitaji kufahamu Uhalisia wa chapisho linalosambaa mtandaoni linalodaiwa kuwa la #TheChanzo likionesha kuwa Mwenyekiti wa #CHADEMA, Freeman Mbowe amemshukuru Rais Samia kwa kuungana na CHADEMA kuomboleza kifo cha Mzee Ali Kibao

Ufuatiliaji wa #JamiiCheck kwa kutumia #GoogleReverseImage umebaini kuwa Taarifa hiyo Si ya Kweli na haijachapishwa katika kurasa rasmi za Mitandao ya Kijamii ya The Chanzo. Pia, kupitia kurasa zake, The Chanzo imekanusha kuhusika na Taarifa hiyo

Aidha, JamiiCheck imebaini uwepo wa utofauti wa Nembo inayotambulisha mtandao wa X ambapo chapisho hilo limetumia nembo ya zamani ya alama ya Ndege wakati mtandao huo ukijulikana kama #Twitter tofauti na The Chanzo ambao hutumia nembo yenye herufi X

Soma https://jamii.app/MboweAmshukuruSamia

#JamiiCheck #HakikiTaarifa #FactsCheck #FactsChecking #VisitJamiiCheck #MisDis04
👍3👏1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akizungumza katika hafla ya Utoaji wa Tuzo za umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania, (#EJAT), Naibu Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu, ametoa wito kwa Jamii kuwa makini na matumizi ya Akili Mnemba (AI), ili kuondoa Upotoshaji, Uzushi na kuepuka kusababisha taharuki

Soma https://jamii.app/EJATAwards2024

#JamiiForums #JFMatukio #EJATAwards #UhuruWaHabari #FactsChecking #FactsCheck #HakikiTaarifa #VisitJamiiCheck
JIUNGE NA 'CHANNEL' YA TELEGRAM YA JAMIICHECK UWE WA KWANZA KUPATA TAARIFA ZILIZOHAKIKIWA

JamiiForums kupitia Jukwaa lake la JamiiCheck.com inaendelea kukupa nafasi ya Kuhabarika, Kuelimika na Kushiriki mchakato wa Kuhakiki Taarifa kila wakati na kwa haraka zaidi, ambapo hivi sasa imekuongezea sehemu nyingine ya kupata taarifa hizo kupitia Mtandao wa #Telegram

Jiunge sasa na 'Channel' yetu ya Telegram kwa kubofya hapa https://t.me/JamiiCheck

#JamiiCheck #Misinformation #Disinformation #FactsChecking #VisitJamiiCheck
Uvumi wa Taarifa zisizo za Kweli kuhusu Afya unaweza kuwafanya Wananchi kupuuza ushauri wa wataalamu, hali inayoweza kusababisha madhara makubwa kwa afya za Watu.

Hakikisha Unathibitisha Taarifa zinazogusa Sekta ya Afya kabla ya kuziamini ili Kuhakikisha usalama wako na Jamii kwa ujumla

Soma https://jamii.app/ThibitishaKablaHujaamini

#VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis04
Upotoshaji hufanyika kwa njia nyingi ikiwemo kusambazwa kwa jumbe zinazodaiwa kuwa ni zawadi kutoka kwa Mashirika ya Kimataifa.

Ukutanapo na Taarifa za aina hii hakikisha Unathibitisha kuona kama ni Kweli imetolewa na chanzo husika ili kufanya maamuzi yaliyo sahihi na kujiepusha na #Upotoshaji.

Tumia Jukwaa la JamiiCheck.com kupata Uhalisia wa Taarifa mbalimbali.

Soma https://jamii.app/ZawadiMashirikaYaKimataifa

#VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis05
1
Ni muhimu kuthibitisha Picha unazokutana nazo Mtandaoni zikihusishwa na Matukio tofautitofauti ili kupata Uhalisia wake kabla ya kuendelea kuwasambazia wengine kwani baadhi ya Watu hutumia Picha za Matukio ya zamani kupotosha Umma

Kumbuka unapofanya Uhakiki wa maudhui unawalinda Watu wengi dhidi ya Upotoshaji unaosambaa ndani na nje ya Mtandao.

Soma https://jamii.app/ThibitishaPicha

#VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis05
Kumekuwapo na Jumbe zinazotumwa katika Makundi Sogozi ya #WhatsApp na Mitandao mingine ya kijamii zinazoelekeza kubofya 'Links' (Viungo) ili upate zawadi ya MB ama Pesa

Link hizo mara nyingi zimekuwa si salama zikiwa na lengo la kulaghai na kuchukua Taarifa zako na wakati mwingine kupelekea Udukuzi wa Akaunti yako

Thibitisha links za aina hiyo kila unapokutana nazo ili kuepuka kupotoshwa. Hakikisha pia huendelei kusambaza links za aina hiyo ili kuwalinda wengine.

Soma https://jamii.app/LinksZaOfaNaZawadi

#VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis05
Upotoshaji umekuwa ukifanyika katika namna tofauti tofauti ikiwemo kuhariri Maudhui halisi yaliyo kwenye grafiki na kuleta maana tofauti.

Ili kuthibitisha uhalisia wa grafiki unayoitilia mashaka, angalia utofauti katika aina ya mwandiko(Fonts), maneno kupishana, au tafuta chanzo halisi kuona iwapo wamechapisha grafiki hiyo.

Unaweza pia kutumia Jukwaa la JamiiCheck.com kuwasilisha Taarifa unazohitaji uhalisia wake.

Soma https://jamii.app/GrafikiKuhaririwa

#VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis05
👍1
Wakati wa uchaguzi, Taarifa Potofu zinaweza kusambazwa kwa kutumia vipande vya Video ili kuwasafisha au kuwachafua wanasiasa. Hakikisha Unathibitisha kila Taarifa kabla ya Kuiamini.

Tumia jukwaa la JamiiCheck.com kujifunza namna ya Kuthibitisha Maudhui ya Video, na kupata msaada wa Uhakiki kwa Taarifa zinazokutia mashakani.

Soma https://jamii.app/ThibitishaKipandeChaVideo

#VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis05
ARUSHA: Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2025, Balozi wa Sweden-Tanzania, Charlotta Ozaki Macias amesema Dunia inabadilishwa na Akili Mnemba (AI) ambayo ina faida nyingi lakini pia ina changamoto zake ikiwemo upotoshaji wa taarifa na kupungua kwa nafasi ya kiraia

Balozi Charlotta amesema AI zinasisimua na zinatisha pia, zinaweza kuwasaidia Wanahabari kwa kurahisisha kazi na kuchakata kiasi kikubwa cha taarifa n.k hiyo inasaidia kutengeneza habari za ubora wa juu na zenye ushahidi wa kutosha

Anaongeza “AI inaweza pia kutumiwa kufanya upotoshaji wa taarifa, Picha, Video na Maandishi bandia, inazidi kuwa vigumu kujua ukweli ni upi. Hili si tatizo la Kiteknolojia tu, ni tatizo la Uaminifu."

Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
ARUSHA: Balozi wa Sweden-Tanzania, Charlotta Ozaki Macias anasema “Nchini Sweden, tumejaribu kuelekeza Maendeleo ya Akili Mnemba (AI) kwa njia ya kimaadili. Mkakati wetu wa kitaifa kuhusu AI unalenga mambo matatu kwa kuwa AI inapaswa kufanya kazi kwa ajili ya Watu, si dhidi yao.”

Ameyataja mambo hayo kuwa ni Kulinda faragha na kuhakikisha usalama wa taarifa za Watu, Kufanya AI iwe wazi, ili Watu waelewe jinsi maamuzi yanavyofanyika na Kupambana na upendeleo ili kuhakikisha AI haisaidii kuendeleza Ubaguzi.

Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
ARUSHA: Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2025, Balozi wa Sweden-Tanzania, Charlotta Ozaki Macias amesema “Tunapoingia kwenye enzi hii ya Kidijitali, Waandishi wa Habari lazima wakabiliane na mashambulizi Mtandaoni, ufuatiliaji wa Kidijitali na taarifa za uongo. Pia, wanapaswa kutafuta njia za kutumia Teknolojia ili kuelimisha na kuhamasisha.”

Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
Mtaalamu wa Mawasiliano na Vyombo vya Habari wa EAC, Lilian Kiarie akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2025 amesema Teknolojia imeimarisha Uandishi wa kiraia huku Watu wa kawaida wakipewa uwezo wa kuripoti matukio kwa wakati halisi, jambo ambalo limepanua Demokrasia ya upatikanaji wa habari

Ametoa wito kwa Waandishi wa Habari kuendelea kushikilia misingi ya ukweli, uadilifu na uwazi, pamoja na Serikali na wadau kulinda Uhuru wa Kujieleza na kukuza ubunifu, ili kuhakikisha Uandishi wa habari unabaki kuwa nguzo ya Demokrasia hata katika enzi za Akili Mnemba

Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Media Foundation, Dastan Kamanzi akizungumza katika Siku ya Kwanza ya Maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani ameyataja mambo matatu muhimu wanayohitaji Waandishi wa Habari ili kuboresha kazi zao

Amesema “Waandishi wanahitaji mambo matatu muhimu ili kuboresha kazi zao, kwanza ni Shauku inayohusisha kubadilika na kukua. Pili, ni Utayari unaohusisha Uwekezaji wa maarifa na Uwekezaji wa muda, tatu wanahitaji kudhamiria na kujikita kwenye Majukumu yao”

Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
1
ARUSHA: Akizungumzia kuhusu kuwawezesha Wanawake kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 katika masuala ya Uhakiki wa Taarifa, Mkurugenzi Mtendaji wa #JamiiAfrica, Maxence Melo amesema Taasisi hiyo imekuwa ikitoa mafunzo ya kuwajengea uwezo Wadau wa Habari Wanawake na programu hizo zimekuwa zikiendelea

Amesema “Tulikuwa na Mradi maalumu pamoja na WiLDAF kuhusu kuwajengea uwezo Wanawake, pia kama kuna mapendekezo mengine yoyote kutoka kwa Wadau tupo tayari kuyapokea na ikiwezekana kushirikiana nao.”

Soma https://jamii.app/WPFD2025DayTwo

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis04
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Wakili Onesmo Olengurumwa, amesema Waandishi wa Habari wanao wajibu wa kusaidia umma kubaini Taarifa za ukweli na uongo, na wanaweza kutumia Teknolojia ya Akili Mnemba (AI) kuongeza tija licha ya kuwa nayo inachangia kuzalishwa kwa Taarifa za uongo

Ameyasema hayo Mei 2, 2025 katika mafunzo ya Siku moja ya Wanahabari 150, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, ambayo inaadhimishwa Mei 3, ambapo Kaulimbiu ya Mwaka 2025 ni “Uhabarishaji kwenye Dunia Mpya: Mchango wa Akili Mnemba/Unde kwenye Uhuru wa Vyombo vya Habari.”

Aidha, ametoa kongole kwa #JamiiAfrica ambayo imekuwa ikishughulikia kubaini Taarifa sahihi na zisizo sahihi kupitia Jukwaa la #JamiiCheck

Soma https://jamii.app/WPFD2025

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis04
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji wa Serikali, Gerson Msigwa ametoa wito kwa Wanahabari kuwa na kawaida ya kuhakiki Taarifa kabla ya kusambaza kama ambavyo imekuwa ikifanywa na JamiiCheck.com

Msigwa amezungumza hayo wakati akichangia mada katika Mkutano wa Wadau kujadili Mchango wa Sekta ya Habari kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 uliofanyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City, leo Julai 9, 2025

Amesema “Nimeona Watu wa JamiiForums wana kitu kinaitwa JamiiCheck, wanachofanya ndio kilekile tulichojifunza shuleni kwamba unachotaka kukichapisha jiridhishe kuwa ni sahihi?”

Soma https://jamii.app/MsigwaOnJamiiCheck

#JamiiCheck #HakikiTaarifa #FactsCheck #FactsChecking #VisitJamiiCheck
2