This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Kiongozi Mkuu Mstaafu wa Chama cha #ACTWazalendo, Zitto Kabwe amesema amefunguliwa kesi na Harbinder Singh Seth akidaiwa kumkashifu mtu huyo na kumvunjia heshima mbele ya jamii wakati Zitto alipozungumzia sakata linalohusu Kampuni ya Ufuaji Umeme ya IPTL
Zitto ambaye amesema anashutumiwa akidaiwa kutoa kauli ya kukashifu na kumchafua Sethi kupitia ukurasa wake wa X, amesema “Nipo tayari kwa kesi, nitaweka ukweli wote wazi na mwisho kufukia kabisa huu mzoga unaoitwa Sakata la IPTL.”
Ameongeza “Ninampongeza sana (Sethi) na kumshukuru kwa ujasiri wake wa kunishtaki kwasababu kesi hii itatoa fursa ya kumaliza jambo hili lililoweka wingu kwa muda mrefu sana katika Taifa letu."
Soma https://jamii.app/ZittoKabweMei18
#JamiiForums #JFMatukio
Zitto ambaye amesema anashutumiwa akidaiwa kutoa kauli ya kukashifu na kumchafua Sethi kupitia ukurasa wake wa X, amesema “Nipo tayari kwa kesi, nitaweka ukweli wote wazi na mwisho kufukia kabisa huu mzoga unaoitwa Sakata la IPTL.”
Ameongeza “Ninampongeza sana (Sethi) na kumshukuru kwa ujasiri wake wa kunishtaki kwasababu kesi hii itatoa fursa ya kumaliza jambo hili lililoweka wingu kwa muda mrefu sana katika Taifa letu."
Soma https://jamii.app/ZittoKabweMei18
#JamiiForums #JFMatukio
AFYA: Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Mohamed Janabi amechaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Kanda ya Afrika, katika uchaguzi uliofanyika leo Mei 18, 2025, Geneva-Uswisi
Prof. Janabi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkurugenzi Mteule wa Kanda hiyo, Dkt. Faustine Ndugulile, aliyefariki dunia Novemba 2024
Wagombea wengine waliowania nafasi hiyo lakini hawakufanikiwa ni pamoja na Prof. Moustafa Mijiyawa kutoka Togo, Dkt. N’Da Konan Michel Yao kutoka Ivory Coast, Dkt. Boureima Hama Sambo wa Niger na Mohamed Lamine Dramé kutoka Guinea
Aidha, Kwa mujibu wa utaratibu wa WHO, Prof. Janabi anatarajiwa kuhudumu katika nafasi hiyo kwa kipindi cha Miaka Mitano, huku akiwa na fursa ya kuchaguliwa tena kwa muhula mwingine mmoja pekee
Soma https://jamii.app/JanabiAshinda
#JamiiForums #JamiiForums #ServiceDelivery #HudumaZaKijamii #Governance
Prof. Janabi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkurugenzi Mteule wa Kanda hiyo, Dkt. Faustine Ndugulile, aliyefariki dunia Novemba 2024
Wagombea wengine waliowania nafasi hiyo lakini hawakufanikiwa ni pamoja na Prof. Moustafa Mijiyawa kutoka Togo, Dkt. N’Da Konan Michel Yao kutoka Ivory Coast, Dkt. Boureima Hama Sambo wa Niger na Mohamed Lamine Dramé kutoka Guinea
Aidha, Kwa mujibu wa utaratibu wa WHO, Prof. Janabi anatarajiwa kuhudumu katika nafasi hiyo kwa kipindi cha Miaka Mitano, huku akiwa na fursa ya kuchaguliwa tena kwa muhula mwingine mmoja pekee
Soma https://jamii.app/JanabiAshinda
#JamiiForums #JamiiForums #ServiceDelivery #HudumaZaKijamii #Governance
❤4
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Makamu Mwenyekiti wa #CHADEMA, John Heche amedai aliyekuwa Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa chama, John Mrema ameondoka na Akaunti ya X (Twitter) na YouTube na kudai alikuwa akijinufaisha kwa kuingiza kipato yeye na Msaidizi wake
Akijibu madai hayo, Mrema amesema “Nilikuwa Kiongozi wa Kitengo lakini waliohusika kuposti ni Maafisa wengine, Apolo alisimamia X wakati YouTube ilikuwa chini ya Abdulkarim, binafsi sikuwa hata na ‘password’, nilipotaka kutuma ujumbe, niliandika na kuwakabidhi hao.”
Ameongeza “Nilichosikia, kulikuwa na majaribio mengi ya kuingia kimakosa, akaunti zikafungwa, wao (CHADEMA) hawana password ya email iliyotumika kufungua, pia Abdulkarim ana madai yake, aliwasilisha kwa Heche akaambiwa anadai fedha nyingi, wataangalia namna, so wanajua kilichotokea mimi sihusiki.”
Soma https://jamii.app/MajibuYaJohnMrema
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Akijibu madai hayo, Mrema amesema “Nilikuwa Kiongozi wa Kitengo lakini waliohusika kuposti ni Maafisa wengine, Apolo alisimamia X wakati YouTube ilikuwa chini ya Abdulkarim, binafsi sikuwa hata na ‘password’, nilipotaka kutuma ujumbe, niliandika na kuwakabidhi hao.”
Ameongeza “Nilichosikia, kulikuwa na majaribio mengi ya kuingia kimakosa, akaunti zikafungwa, wao (CHADEMA) hawana password ya email iliyotumika kufungua, pia Abdulkarim ana madai yake, aliwasilisha kwa Heche akaambiwa anadai fedha nyingi, wataangalia namna, so wanajua kilichotokea mimi sihusiki.”
Soma https://jamii.app/MajibuYaJohnMrema
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili mzunguko wa pili na uwekaji wazi wa Daftari la awali linaendelea katika mikoa 16, linafanyia Mei 16 - 22, 2025
Mikoa husika ni Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba
Mkurugenzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhani Kailima amesema Daftari la Wapiga Kura linawekwa wazi katika vituo vya kuandikisha Wapiga Kura vilivyotumika Awamu ya Kwanza, moja kati ya takwa la kufanya hivyo ni kukidhi matakwa ya Kisheria na kutoa fursa ya Watu kukagua kama kuna dosari
Soma https://jamii.app/UboreshajiDaftari
#JamiiForums #Democracy #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Mikoa husika ni Arusha, Manyara, Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Pwani, Singida, Dodoma, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Mjini Magharibi, Kaskazini Unguja, Kusini Unguja, Kaskazini Pemba na Kusini Pemba
Mkurugenzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhani Kailima amesema Daftari la Wapiga Kura linawekwa wazi katika vituo vya kuandikisha Wapiga Kura vilivyotumika Awamu ya Kwanza, moja kati ya takwa la kufanya hivyo ni kukidhi matakwa ya Kisheria na kutoa fursa ya Watu kukagua kama kuna dosari
Soma https://jamii.app/UboreshajiDaftari
#JamiiForums #Democracy #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Finland inakadiriwa kuwa na Sauna (Bafu la Mvuke) Milioni 3.2 huku likiwa ni Taifa lenye idadi ya Watu zaidi ya Milion 5.5 (Takwimu za Mwaka 2023), hali ambayo inaonesha uwepo wa mabafu hayo sio fasheni au kitu cha gharama kubwa kwa Watu fulani kama ilivyo katika baadhi ya Nchi nyingi, bali kwao ni sehemu ya maisha na sehemu ya tamaduni
Baadhi ya faida za Sauna zinazoaminiwa na Wakazi wa #Finland ni kuwa: Matumizi ya mara kwa mara yanazuia matatizo makubwa ya Kisaikolojia, yanapunguza hatari ya kupata Ugonjwa wa Akili ikiwemo wa Dementia (kupoteza ufahamu)
Pia, inaongeza mabadiliko ya mapigo ya moyo na kuboresha kazi ya moyo, huboresha mzunguko wa damu na kuimarisha ulegevu wa mishipa ya damu. Wanaotumia mara kwa mara huwa na mfumo wa kinga wenye nguvu zaidi
#JamiiAfrica #JamiiForums #NordicWeek
Baadhi ya faida za Sauna zinazoaminiwa na Wakazi wa #Finland ni kuwa: Matumizi ya mara kwa mara yanazuia matatizo makubwa ya Kisaikolojia, yanapunguza hatari ya kupata Ugonjwa wa Akili ikiwemo wa Dementia (kupoteza ufahamu)
Pia, inaongeza mabadiliko ya mapigo ya moyo na kuboresha kazi ya moyo, huboresha mzunguko wa damu na kuimarisha ulegevu wa mishipa ya damu. Wanaotumia mara kwa mara huwa na mfumo wa kinga wenye nguvu zaidi
#JamiiAfrica #JamiiForums #NordicWeek
❤2
Kusoma kwa undani habari hizi na nyingine zilizojiri juma lililopita bofya https://jamii.app/YaliyojiriJumaLililopita
#JamiiForums #YaliyojiriJumaLililopita #JFToons
#JamiiForums #YaliyojiriJumaLililopita #JFToons
Kuna wakati unaweza kujikuta umetembea umbali mrefu kwa miguu, ama kwa hiyari yako au kutokana na mazingira uliyokuwa nayo wakati husika kukulazimisha ufanye hivyo, je, imewahi kukutokea na ilikuwaje?
Soma https://jamii.app/KutembeaDar
#JamiiForums #JFChitChats
Soma https://jamii.app/KutembeaDar
#JamiiForums #JFChitChats
DAR: Mwenyekiti wa #CHADEMA – Taifa, Tundu Lissu amefikishwa Mahakama ya Mkazi Kisutu, leo Mei 19, 2025 kwa ajili ya kesi kusikiliza kesi mbili zinazomkabili ambapo viongozi kadhaa wa chama hicho nao wamefika kufuatilia
Ikumbukwe Mei 6, 2025 mchakato wa kesi hiyo uliendeshwa kwa njia ya Mtandao ambapo Mahakama ilitoa uamuzi wa kesi hiyo kusikilizwa leo na kuruhusu Wananchi kuhudhuria
Aidha, Jaji Mkuu Mstaafu wa Kenya, Willy Mutunga na baadhi ya Waandishi wa Habari na Wanasiasa kutoka Kenya waliosafiri kufuatilia kesi hii inadaiwa wameshikiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere tangu Saa 9 Usiku
Zaidi https://jamii.app/KesiYaLissuLeo
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
Ikumbukwe Mei 6, 2025 mchakato wa kesi hiyo uliendeshwa kwa njia ya Mtandao ambapo Mahakama ilitoa uamuzi wa kesi hiyo kusikilizwa leo na kuruhusu Wananchi kuhudhuria
Aidha, Jaji Mkuu Mstaafu wa Kenya, Willy Mutunga na baadhi ya Waandishi wa Habari na Wanasiasa kutoka Kenya waliosafiri kufuatilia kesi hii inadaiwa wameshikiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere tangu Saa 9 Usiku
Zaidi https://jamii.app/KesiYaLissuLeo
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
❤2
DAR: Wananchi wamejitokeza kwa wingi leo Mei 19, 2025 katika Mahakama ya Kisutu kufuatilia kesi inayomkabili Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu
Ulinzi umeimarishwa Mahakamani hapo ambapo kuna idadi kubwa ya Askari Polisi na Askari wa Jeshi la Magereza
Awali, kesi hiyo iliendeshwa kwa njia ya Mtandao, Mei 6, 2025 Mahakama iliruhusu Umma kuhudhuria kesi hiyo ambapo Lissu anakabiliwa na tuhuma za Uhaini na Kutoa Taarifa za Uongo
Soma https://jamii.app/KesiYaLissuLeo
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025 #CitizenParticipation #Transparency
Ulinzi umeimarishwa Mahakamani hapo ambapo kuna idadi kubwa ya Askari Polisi na Askari wa Jeshi la Magereza
Awali, kesi hiyo iliendeshwa kwa njia ya Mtandao, Mei 6, 2025 Mahakama iliruhusu Umma kuhudhuria kesi hiyo ambapo Lissu anakabiliwa na tuhuma za Uhaini na Kutoa Taarifa za Uongo
Soma https://jamii.app/KesiYaLissuLeo
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025 #CitizenParticipation #Transparency
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu alivyowasili ndani ya Mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kuanzia kusikiliza kesi zinazomkabili, leo Mei 19, 2025
Soma https://jamii.app/KinachojiriKesiLissu
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
Soma https://jamii.app/KinachojiriKesiLissu
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
🔥2👎1
DAR: Upande wa Jamhuri umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa shauri la kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Wakili Tundu Lissu haujakamilika hivyo kuomba kesi hiyo ihairishwe hadi Juni 02, 2025
Aidha, Jopo la Mawakili wa utetezi likiongozwa na Mawakili Mpale Mpoki, Dkt. Rugemeleza Nshala na Peter waliwasilisha maombi Mahakamani ikiwemo kuomba Mahakama 'kulazimisha' upande wa Jamhuri ueleze nini hasa kinachokwamisha upelelezi kwa sababu mwanzo ilidaiwa Mahakamani hapo kuwa ushahidi wote kuhusiana na shauri hilo upo mtandaoni
Mawakili wa Serikali upande wa Jamhuri wamejibu kuwa hakuna sehemu yoyote ya Kisheria na Kikatiba inayowalazimisha kueleza hatua ya upelelezi waliyofikiwa na kwamba mambo ya upelelezi sio ya kuwekwa hadharani
Soma https://jamii.app/KesiLissuKusogezwa
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
Aidha, Jopo la Mawakili wa utetezi likiongozwa na Mawakili Mpale Mpoki, Dkt. Rugemeleza Nshala na Peter waliwasilisha maombi Mahakamani ikiwemo kuomba Mahakama 'kulazimisha' upande wa Jamhuri ueleze nini hasa kinachokwamisha upelelezi kwa sababu mwanzo ilidaiwa Mahakamani hapo kuwa ushahidi wote kuhusiana na shauri hilo upo mtandaoni
Mawakili wa Serikali upande wa Jamhuri wamejibu kuwa hakuna sehemu yoyote ya Kisheria na Kikatiba inayowalazimisha kueleza hatua ya upelelezi waliyofikiwa na kwamba mambo ya upelelezi sio ya kuwekwa hadharani
Soma https://jamii.app/KesiLissuKusogezwa
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
❤2👏1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Jopo la Mawakili wa utetezi likiongozwa na Mawakili Waandamizi Mpale Mpoki, Dkt. Rugemeleza Nshala na Peter Kibatala wamewasilisha ombi Mahakamani kutoa amri ya kuwaondoa Askari wote 'wanaomlinda' mteja wao, Tundu Lissu ndani ya chumba cha Mahakama
Mawakili hao wamedai kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, Mahakama haimtambui mtuhumiwa kama 'mkosaji' na kwamba kitendo cha mteja wao kuzungukwa na Askari wengi hakikubaliki
Aidha, upande wa Jamhuri umeieleza Mahakama kuwa licha ya kwamba Katiba imeeleza hivyo lakini haijatoa maelekezo ya aina gani ya ulinzi unahitajika kwa mtuhumiwa na kwamba ikiwezekana wanaomba ulinzi huo uongezwe kwani suala la ulinzi lina faida kwa mtuhumiwa mwenyewe, Mahakama na Maafisa wa Mahakama kwa ujumla
Soma https://jamii.app/KesiLissuKusogezwa
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
Mawakili hao wamedai kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, Mahakama haimtambui mtuhumiwa kama 'mkosaji' na kwamba kitendo cha mteja wao kuzungukwa na Askari wengi hakikubaliki
Aidha, upande wa Jamhuri umeieleza Mahakama kuwa licha ya kwamba Katiba imeeleza hivyo lakini haijatoa maelekezo ya aina gani ya ulinzi unahitajika kwa mtuhumiwa na kwamba ikiwezekana wanaomba ulinzi huo uongezwe kwani suala la ulinzi lina faida kwa mtuhumiwa mwenyewe, Mahakama na Maafisa wa Mahakama kwa ujumla
Soma https://jamii.app/KesiLissuKusogezwa
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
❤1
Kitambulisho chako (ID) kinachukuliwa kuwa Taarifa Binafsi kwasababu kina taarifa zako kama Jina, Nambari ya Utambulisho, Picha, Tarehe ya Kuzaliwa, n.k.
Unamshauri Mdau afanye nini hapo?
Mjadala zaidi https://jamii.app/MkopoSimuKitambulisho
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #PersonalDataProtection #DataPrivacy
Unamshauri Mdau afanye nini hapo?
Mjadala zaidi https://jamii.app/MkopoSimuKitambulisho
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #PersonalDataProtection #DataPrivacy