JamiiForums
52.4K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
NIGERIA: MAREKANI KUKABIDHI TSH. BILIONI 53 ZILIZOCHUKULIWA NA SANI ABACHA

Fedha hizo zilizochukuliwa na mtawala wa zamani wa Kijeshi zitakabidhiwa kwa Serikali ya #Nigeria baada ya Nchi hizo kufanya makubaliano

- Inadaiwa Sani Abacha alichukua Fedha za Umma zinazofikia Tsh. Trilioni 10 na hakushtakiwa

Soma - https://jamii.app/AbachaPesa

#Accountability
👍8😁3
UGANDA: SERIKALI KUONGEZA VITUO 2,000 VYA 'WIFI' YA BURE

- Lengo ni kuongeza ufikiaji wa huduma ya #Intaneti maeneo ya pembezoni kwa watakaohitaji huduma za Serikali

Hadi sasa #Uganda imeweka vituo 600 ambapo 300 vipo #Kampala

Zaidi - https://jamii.app/InternetUganda

#DigitalRights
👍21
USIMPIGE PICHA WALA KUMCHUKUA VIDEO KARANI WA #SENSA BILA IDHINI YAKE

Kutokana na kusambazwa kwa Picha na Video za Makarani, tungependa kuukumbusha umma kuwa suala la faragha na ulinzi wa taarifa zao na zetu ni jukumu letu sote

Ibara ya 16 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza: Kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafsi, maisha binafsi na familia na unyumba wake, heshima na hifadhi ya maskani na mawasiliano yake

Soma https://jamii.app/PersonalDataPrivacy

#DataPrivacy
👍14
Hati za Ukaguzi ni maoni ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali kuhusu Hesabu za Taasisi inayokaguliwa

Maoni haya yanalenga kuonesha kama Hesabu zilizokaguliwa zimeandaliwa kwa kuzingatia Viwango vya Kihasibu vya Kimataifa (IPSAs) na matamko yanayotolewa na Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA)

Uzingatiaji wa viwango hivi unaziba mianya ya ubadhirifu kwenye matumizi ya Umma na athari zake kwa upatikanaji Huduma kwa Wananchi

#JFUwajibikaji
ROMBO: ASHIKILIWA NA POLISI KWA KUSHIRIKIANA NA MPENZI KUMUUA MAMA YAKE

- Felister Silayo amefariki kwa kupigwa na Kitu kizito Kichwani kutokana na Mgogoro wa Ardhi

- Marehemu aligawa mashamba kwa Watoto wake (kike na kiume) lakini Binti alitaka kupewa maeneo yote

Soma - https://jamii.app/MauajiRombo
😢9🤔5👍2
#JFDATA: Kwa mujibu wa Takwimu za Umoja wa Mataifa, uhaba wa Maji unaathiri zaidi ya 40% ya Watu wote

Watu 3 kati ya 10 wanakosa Huduma za Maji safi ya kunywa

Aidha, Takwimu zinaonesha takriban Watoto 1,000 hufariki dunia kutokana na Magonjwa yanayohusishwa na Maji/Usafi

Zaidi, soma - https://jamii.app/WWWeek2022

#WorldWaterWeek
👍6
SERIKALI KUWACHUNGUZA WAFANYABIASHARA WAKUBWA WANAOWATUMIA MACHINGA KUKWEPA KODI

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Dkt. Dorothy Gwajima amesema hatua hiyo imefikiwa baada ya Machinga wengi kudaiwa kutoyatumia maeneo waliyotengewa kurudi Barabarani

Soma - https://jamii.app/BiasharaNdogondogo
👍8😁1
NIGERIA: Watu wenye Silaha wamewaachia huru Watawa 4 wa Kikatoliki waliotekwa nyara mapema Wiki hii katika Jimbo la #Imo

Polisi hawajaweka wazi iwapo kuna malipo yamefanyika kwa Watekaji ili kuwaachia huru Watawa hao

Soma https://jamii.app/WatawaWaachiwa

#HumanRights
👍6
#THAILAND: MAHAKAMA YAMSIMAMISHA KAZI WAZIRI MKUU

Mahakama ya #Katiba imemsimamisha kazi Prayuth Chan-ocha baada ya kuwekewa pingamizi na Vyama vya Upinzani vilivyodai Kiongozi huyo amemaliza muhula wake wa Miaka minne

Soma - https://jamii.app/ThaiPM

#Democracy
👍1🎉1
MICHEZO: GEITA GOLD KUMSAJILI RAIA WA JAPAN

Geita Gold ipo katika hatua za mwisho kukamilisha vibali vya Mchezaji Shinobu Sakai ambaye ni raia wa Japan

> Kocha Mkuu wa Geita Gold, Fred Felix Minziro amesema anaimani kubwa na Mjapani huyo

Soma https://jamii.app/UsajiliGeita

#JFSports
😁28👍8👎2🤮2
DAR: MTOTO WA WAZIRI SIMBACHAWENE APIGWA FAINI TSH. 250,000

Mahakama imemhukumu James Simbachawene (24) kulipa faini hiyo baada ya kukiri kusababisha ajali kwa kugonga magari matatu

> Aidha, Leseni yake ya Udereva imefungiwa kwa Miezi 6

Soma - https://jamii.app/JemesSimbachawene

#JamiiForums
👎12👍6😁3
#DATAPRIVACY: Shirika la Ulinzi wa Taarifa la Ufaransa linaituhumu Kampuni ya #Google kwa kuwatumia matangazo Watumiaji wa Gmail bila idhini yao

> Hii ni kinyume na Sera ya Faragha na maamuzi ya Mahakama ya Haki ya Umoja wa Ulaya

Zaidi - https://jamii.app/MalalamikoGoogle

#JamiiForums
👍10
AFRIKA KUSINI: Wafanyakazi wameitisha maandamano nchi nzima kupinga kupanda kwa Gharama za Maisha

> Madai mengine ni Ruzuku ya Mapato, Kima cha Chini cha Mshahara, Kikomo cha Bei ya Mafuta na Viwango vya Riba

Soma - https://jamii.app/UnrestSA

#Uwajibikaji
👍13
KENYA: Mbunge Mteule, Didmus Barasa, anayedaiwa kumuua kwa Risasi Brian Olunga amekana mashtaka na kuachiwa kwa dhamana ya takriban Tsh. 191,671,000

Mahakama imemzuia kutembelea eneo la tukio kwani anaweza kuwashawishi mashahidi wa kesi hiyo

Soma - https://jamii.app/BarassaAshtakiwa
👍6🤔3👎1
- Kiungulia ni moja ya changamoto inayosumbua Mfumo wa Chakula. Hutokea pale tindikali ya Tumboni inapopanda juu mpaka Mdomoni na kusababisa kuungua kwa Tishu laini za Koo

- Sababu nyingi zinapelekea kupata Kiungulia ikiwemo Kula Vyakula vinavyowasha mfano pilipili. Huwa unatumia njia gani kutuliza hali hii?

#JamiiForums #Afya
👍7🔥3
Taasisi ya Twaweza inazindua ripoti yake leo, Agosti 25, 2022 kupitia 'Sauti za Wananchi' ikieleza Maoni ya wananchi kuhusu hali ya Uchumi wa #Tanzania, na Tozo za Miamala ya Pesa kupitia Simu za Mkononi

Takwimu zimekusanywa kutoka kwa wahojiwa 3,000 kuanzia Oktoba na Novemba 2021 na Juni na Julai 2022 kupitia jopo maalum la Sauti za Wananchi

Fuatilia Mubashara uzinduzi huu kupitia - https://jamii.app/TwawezaTozo

#SautiZaWananchi #TakwimuHuru
👍4
Miongoni mwa yaliyomo kwenye Ripoti ya Twaweza ni pamoja na Nusu ya Wananchi waliohojiwa wataja masuala ya Kiuchumi kuwa changamoto kubwa inayokabili Kaya zao

Gharama kubwa za Maisha (48%), ukosefu wa Ajira au fursa za Mapato (29%) na uhaba wa Chakula (26%) ziliongoza kwenye orodha ya mambo yanayowapa wasiwasi

Soma zaidi - https://jamii.app/TozoTwaweza

#JamiiForums #SautiZaWananchi #TakwimuHuru
👍5
Wananchi wanaosema Nchi iko kwenye mwelekeo sahihi ni 30%, haiko kwenye mwelekeo sahihi ni 25% na wenye hali ya sintofahamu ni 44%

Matumaini yao kuhusu suala la Uchumi yako chini sana. Wanaosema hali ya uchumi ni mbaya ni 41% na wanaosema uchumi ni mzuri ni 9%

#SautiZaWananchi #TakwimuHuru
Vipaumbele vikuu ambavyo Wananchi wangependa Rais ashughulikie ni gharama kubwa za Maisha (46%) na ubovu wa Vituo vya #Afya (42%)

Soma zaidi - https://jamii.app/TozoTwaweza

#JamiiForums #SautiZaWananchi #TakwimuHuru
Aidha, Wananchi wanasema wameona kuboreshwa kwa Huduma za Kijamii katika kipindi cha Miezi 6 iliyopita, hasa Sekta ya Elimu (68%)

Pia, Uhuru wa Kujieleza umeboreshwa (60%), Uhuru wa Kisiasa umeimarika (56%), Ulinzi na Usalama (59%)

#JamiiForums #SautiZaWananchi #Twaweza #TakwimuHuru
👍2