JamiiForums
52.4K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
WAZIRI NAPE: KAZI YA KAMPUNI YA MAWASILIANO SIO KUOMBA RIDHAA KWA WANANCHI

Akitolea ufafanuzi upandaji wa gharama za vifurushi vya #intaneti Nchini, Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema kazi ya Kampuni siyo kuomba ridhaa kwa Wananchi, isipokuwa ni kuwapa tu taarifa juu ya bidhaa mpya wanazotoa

Amefafanua kuwa Mtoa huduma hawezi tu kupandisha bei pasipo kuleta mapendekezo kwa Mamlaka (TCRA).

#JamiiForums #DigitalRights
👍1
UGANDA: SERIKALI KUONGEZA VITUO 2,000 VYA 'WIFI' YA BURE

- Lengo ni kuongeza ufikiaji wa huduma ya #Intaneti maeneo ya pembezoni kwa watakaohitaji huduma za Serikali

Hadi sasa #Uganda imeweka vituo 600 ambapo 300 vipo #Kampala

Zaidi - https://jamii.app/InternetUganda

#DigitalRights
👍21
Migawanyiko ya #Kidijitali kama kati ya Wanaume na Wanawake, Vijana na Wazee, Mijini na Vijijini inasababisha baadhi ya makundi kubaki nyuma

Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Mawasiliano Duniani (ITU), asilimia 5 ya Watu Duniani hawajaunganishwa kwenye #Intaneti. Barani Afrika, ni asilimia 18 ya Watu wake bado hawawezi kufikia Huduma hiyo

Soma - https://jamii.app/DigitalRights

#DigitalRights
FRANCIS NYONZO: KUNA VITU VINGI VINAVYOGUSA TAIFA LAKINI HAVITOLEWI TAARIFA

Amesema mpaka leo hatujapata kauli ya Serikali juu ya kilichotokea Oktoba 2020 ambapo #Facebook, #WhatsApp na #JamiiForums zilikuwa hazipatikani, akisema kukaa kimya kunaibua Taarifa nyingi Mtaani juu ya nini kilitokea wakati huo

Akizungumzia kuhusu gharama za vifurushi vya #Intaneti amesema, "Tunasema tuna viwango nafuu vya Vifurushi lakini tunapoangalia gharama ni vizuri kuzingatia uhalisia wa maisha ya Watu, siyo kulinganisha na gharama za Nchi nyingine. Nashauri tathmini iangalie kiwango cha Maisha na siyo mlinganisho wa hivyo"

#KongamanoHabari2022 #DigitalRights #JamiiForums
👍10👏2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
#MaxenceMelo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums anasema “Kazi ya #Intaneti ni kuunganisha vifaa vya Digitali ili kazi iwe rahisi zaidi. Pia, Watu wengi wanaaminia Serikali inamiliki Intaneti, si kweli bali inaweza kudhibiti Miundombinu.”

Anaeleza “Intaneti ni uvumbuzi uliotokana na Jeshi la Marekani wakati likitafuta njia rahisi ya kuwasiliana, baadaye Teknolojia hiyo ikatoka Jeshini na kuingia kwa Raia.”
-
#DigitalWorld #DataPrivacy #JamiiForums
👍21
Kwa mujibu wa Mtandao wa cable.co.uk Watumiaji wa #Intaneti katika Nchi nyingi za Afrika wanakabiliwa na gharama kubwa za Mtandao, Miundombinu isiyo thabiti pamoja na huduma isiyo nzuri ikiwemo Kasi ndogo ya Intaneti

Licha ya takwimu za ufikiaji wa Huduma za Intaneti kuonesha Watumiaji wa Intaneti Barani Afrika walifikia Milioni 570 hadi Desemba 2022, bado ni 43.1% tu ya Watu wanapata huduma hiyo Afrika wakati wastani wa Kimataifa ni angalau iwe 66.2%.

#JamiiForums #FIFAfrica23 #InternetFreedomAfrica #DigitalRights #HakiZaKidijitali #InternetAccess #JFDATA
👍42
Kabla ya kugunduliwa kwa #Intaneti na Mitandao ya Kijamii, watu walikuwa wakitumia njia mbalimbali kusambaza #HabariPotofu kwa lengo la kufikia Malengo yao, iwe ni Kisiasa, Kiuchumi au Kijamii

Hata hivyo, Ugunduzi wa Intaneti na Mitandao ya Kijamii vimeongeza urahisi wa usambazaji wa Habari Potofu kwa kufanya zifikie Watu wengi ndani ya Muda mfupi

Katika kipindi chote cha Historia, Suala la Elimu, Uhuru wa kujieleza na Ukweli wa Habari vimekuwa nyenzo muhimu katika kukabiliana na Changamoto hii

Soma https://jamii.app/IntanetiNaHabari

#JamiiForums #JamiiCheck #HakikiHabari #Misinformation #Disinformation #FactsChecking #FactCheck
👍5
Kuongezeka kwa gharama za #Intaneti kunaathiri Uwezo wa Watu kupata #Elimu, kufanya #Biashara, kuwasiliana na Kupata taarifa Muhimu kupitia Mtandao hivyo kukwamisha Ukuaji wa Sekta ya Digitali

Vipi Mdau? Unaathiriwaje na Gharama za Intaneti Nchini?

Kwa Maoni zaidi, shiriki pamoja nasi katika Mjadala wa namna Sera, Gharama, Bajeti na Matamko ya Viongozi vinachochea ukuaji wa Sekta ya Digitali Nchini, utakaofanyika Juni 13, 2024, kuanzia Saa 12 Jioni - Saa 2:00 Usiku kupitia #XSpaces ya JamiiForums

Mjadala https://jamii.app/DigitalSpaces

#JamiiForums #DigitalTransformation #DigitalSpace #DigitalRights #HakiZaKidigitali #Digitalization #MjadalaSektaDigitali
👍31
Kuwafuatilia Watoto wako wanachofanya Mtandaoni inahitaji jitihada. Chukua hatua za kuwachunguza wanawasiliana na nani, wanaangalia nini, na wanapakua (download) nini

Pia, ni vizuri kujadili nao mara kwa mara kuhusu Matumizi ya #Intaneti ili kuwalinda na kuwajengea tabia salama Mtandaoni

#JamiiForums #DigitalRights #JFDigitali #ChildOnlineSafety #ChildSafety24 #ChildSafety
👍2
Kuongezeka kwa gharama za #Intaneti kunaathiri uwezo wa Watu kupata #Elimu, kufanya #Biashara, kuwasiliana na Kupata taarifa Muhimu kupitia Mtandao hivyo kukwamisha Ukuaji wa Sekta ya Digitali

Vipi mdau, unaathiriwaje na Gharama za Intaneti Nchini?

Kutoa maoni yako, shiriki Mjadala wa namna Sera, Gharama, Bajeti na Matamko ya Viongozi vinachochea ukuaji wa Sekta ya Digitali Nchini, leo Alhamisi ya Juni 20, 2024, kuanzia Saa 12:00 Jioni - Saa 2:00 Usiku kupitia #XSpaces ya JamiiForums

Link ya Mjadala https://jamii.app/DigitaliSpaces

#JamiiForums #DigitalTransformation #DigitalSpace #DigitalRights #HakiZaKidigitali #Digitalization #MjadalaSektaDigitali
👍41