This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Mdau wa JamiiForums.com anasema tukio la Waamuzi kubughudhiwa na kunusurika kupigwa kama ilivyotokea katika mchezo wa Ligi Kuu ya Wanawake kati ya Simba Queens na Mashujaa Queens, Mei 12, 2025, halitakiwi kuachwa kama lilivyo kwani ikiwa hivyo inaweza kutokea makubwa zaidi ya hapo
Anaeleza kuwa tukio hilo lililohusisha baadhi ya memba wa Benchi la Ufundi wa Simba Queens kuanzisha vurugu baada ya mchezo huo linaweza kuwa ni ishara kuna baadhi ya matukio ambayo sio mazuri yanayoendelea nyuma ya kamera
Mdau anasema kama mtu anaweza kufanya hivyo hadharani kukiwa na kamera, je Waamuzi ambao kawaida sio wazungumzaji katika Vyombo vya Habari, usalama wao upoje?
Soma https://jamii.app/WaamuziViwanjani
Video Credits: Tuzo Online
#JamiiForums #JFSports #JamiiAfrica
Anaeleza kuwa tukio hilo lililohusisha baadhi ya memba wa Benchi la Ufundi wa Simba Queens kuanzisha vurugu baada ya mchezo huo linaweza kuwa ni ishara kuna baadhi ya matukio ambayo sio mazuri yanayoendelea nyuma ya kamera
Mdau anasema kama mtu anaweza kufanya hivyo hadharani kukiwa na kamera, je Waamuzi ambao kawaida sio wazungumzaji katika Vyombo vya Habari, usalama wao upoje?
Soma https://jamii.app/WaamuziViwanjani
Video Credits: Tuzo Online
#JamiiForums #JFSports #JamiiAfrica
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo amesema Sheria ya Tanzania inaeleza Mtanzania yeyote aliye nje ya mipaka akiwa na Hati ya Kusafiria (Passport) ni Mtanzania kama wengine lakini Diaspora ni yule ambaye ni Mzaliwa wa Tanzania anayeenda nje na kuukana uraia wake
Soma https://jamii.app/DiasporaUfafanuzi
#JamiiForums #Governance #Diplomacy
Soma https://jamii.app/DiasporaUfafanuzi
#JamiiForums #Governance #Diplomacy
#TANZIA: Sifa Bujuni aliyeimba wimbo wa “Tanzania Inaelekea Wapi?” yenye kionjo cha “Mnatuona Nyani tu” amefariki Dunia hospitali ya Muhimbili alikokuwa akipatiwa matibabu. Baba Mzazi wa Marehemu amethibitisha taarifo za kifo chake
Ikumbukwe, Septemba 13, 2023, Sifa na wenzake Wawili walikamatwa huko Isyesye - Mbeya wakidaiwa kuandaa wimbo wenye maudhui ya uchochezi dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuusambaza kupitia mitandao ya kijamii pamoja na mtandao wa kurusha maudhui wa YouTube
Septemba 19, 2023, Sifa na wenzake Salome Mwampeta (Mwimbaji) na Mtayarishaji wa Wimbo huo, Hezekiel Millyashi George walipandishwa Mahakamani na kusomewa Shtaka la Kusambaza Taarifa za Uongo kwa njia ya Mtandao ambapo wote walikana na baadaye kesi yao kufutwa
Soma https://jamii.app/SifaAfariki
#JamiiAfrica #JamiiForums #FreedomOfExpression #Demokrasia #UhuruWaKujieleza
Ikumbukwe, Septemba 13, 2023, Sifa na wenzake Wawili walikamatwa huko Isyesye - Mbeya wakidaiwa kuandaa wimbo wenye maudhui ya uchochezi dhidi ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuusambaza kupitia mitandao ya kijamii pamoja na mtandao wa kurusha maudhui wa YouTube
Septemba 19, 2023, Sifa na wenzake Salome Mwampeta (Mwimbaji) na Mtayarishaji wa Wimbo huo, Hezekiel Millyashi George walipandishwa Mahakamani na kusomewa Shtaka la Kusambaza Taarifa za Uongo kwa njia ya Mtandao ambapo wote walikana na baadaye kesi yao kufutwa
Soma https://jamii.app/SifaAfariki
#JamiiAfrica #JamiiForums #FreedomOfExpression #Demokrasia #UhuruWaKujieleza
👍1
DAR: Shirika la Reli Tanzania (TRC) limetoa taarifa kuwa ajali ya treni ya Mjini kwenda Pugu, iliyotokea Stesheni ya KAMATA kwenye makutano ya reli na Barabara ya Kawawa, jana Mei 13, 2025 imejeruhi Watu 10
TRC imesema ajali hiyo iliyohusisha mabehewa 12 yaliyobeba abiria takribani 1,200 na kuwa Wataalamu wa Shirika na Timu ya Afya ya Shirika, walifika kutoa msaada wa huduma ya kwanza, waliojeruhiwa wawili ni Wanaume na nane Wanawake walikimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Amana
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Uhusiano wa TRC, Fredy Mwanjala amesema chanzo cha ajali hiyo ambayo imesababisha mabehewa 6 kuathirika bado hakijafahamika lakini huduma ya usafiri wa treni ya Mjini kwenda Pugu inaendelea kama kawaida leo Mei 14, 2025
Soma https://jamii.app/TreniYaMjini
#JamiiForums #JFMatukio
TRC imesema ajali hiyo iliyohusisha mabehewa 12 yaliyobeba abiria takribani 1,200 na kuwa Wataalamu wa Shirika na Timu ya Afya ya Shirika, walifika kutoa msaada wa huduma ya kwanza, waliojeruhiwa wawili ni Wanaume na nane Wanawake walikimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Amana
Mkuu wa Kitengo cha Habari na Uhusiano wa TRC, Fredy Mwanjala amesema chanzo cha ajali hiyo ambayo imesababisha mabehewa 6 kuathirika bado hakijafahamika lakini huduma ya usafiri wa treni ya Mjini kwenda Pugu inaendelea kama kawaida leo Mei 14, 2025
Soma https://jamii.app/TreniYaMjini
#JamiiForums #JFMatukio
👎1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Mei 13, 2025 katika Ibada ya kumuaga aliyekuwa Msemaji Mkuu wa Serikali ya Zanzibar, Charles Hillary, Askofu Jackson Sosthenes (wa Kanisa la Anglikani - DSM), alizungumzia Matukio ya watu kuvamiwa, kutekwa na kuuawa, akisema wote wanaofanya vitendo hivyo, wanapora haki na Mamlaka ya Mungu ya kuchukua uhai wa binadamu
Zaidi https://jamii.app/MamlakaYaMungu
#JamiiForums #JamiiAfrica #SocialJustice #HumanRights #Accountability #Governance
Zaidi https://jamii.app/MamlakaYaMungu
#JamiiForums #JamiiAfrica #SocialJustice #HumanRights #Accountability #Governance
👍1
UHISPANIA: Nyota wa #RealMadrid, Rodrygo inadaiwa hana mpango wa kuendelea kuichezea Timu hiyo kutokana na nafasi anayocheza kutawaliwa na Jude Bellingham na Kylian Mbappe wanaopewa nafasi zaidi
Mtandao wa Marca umeeleza kuwa anataka kuondoka ili kwenda kutafuta sehemu nyingine atakayopata nafasi ya kucheza Mechi nyingi
Inadaiwa kilichomkera zaidi Rodrygo ni kitendo cha kutojumuishwa kwenye kikosi kilichocheza El Clasico (dhidi ya Barcelona), hivyo anajiona hana umuhimu
Soma https://jamii.app/RodrygoTransfer
#JamiiForums #JFSports #Michezo
Mtandao wa Marca umeeleza kuwa anataka kuondoka ili kwenda kutafuta sehemu nyingine atakayopata nafasi ya kucheza Mechi nyingi
Inadaiwa kilichomkera zaidi Rodrygo ni kitendo cha kutojumuishwa kwenye kikosi kilichocheza El Clasico (dhidi ya Barcelona), hivyo anajiona hana umuhimu
Soma https://jamii.app/RodrygoTransfer
#JamiiForums #JFSports #Michezo
UHISPANIA: Kipa wa #FCBarcelona, Wojciech Szczesny amesema anasubiri mwongozo wa Mkewe na Familia yake kabla ya kusaini Mkataba mpya wa kuendelea kubaki Klabuni hapo au kuondoka
Kipa huyo wa zamani wa Arsenal, alisajiliwa Oktoba 2024 ikiwa ni Mwezi mmoja tangu atangaze kustaafu akitokea Juventus, alipewa nafasi hiyo baada ya kipa chaguo la kwanza Marc-Andre ter Stegen kuumia goti
Szczesny na Luczenko walifunga Ndoa Mwaka 2016 baada ya kuwa kwenye uhusiano kwa Miaka mitatu, walikutana wakati akiwa anaichezea #Arsenal
Soma https://jamii.app/SzczesnyTransfer
#JamiiForums #JFSports #Michezo
Kipa huyo wa zamani wa Arsenal, alisajiliwa Oktoba 2024 ikiwa ni Mwezi mmoja tangu atangaze kustaafu akitokea Juventus, alipewa nafasi hiyo baada ya kipa chaguo la kwanza Marc-Andre ter Stegen kuumia goti
Szczesny na Luczenko walifunga Ndoa Mwaka 2016 baada ya kuwa kwenye uhusiano kwa Miaka mitatu, walikutana wakati akiwa anaichezea #Arsenal
Soma https://jamii.app/SzczesnyTransfer
#JamiiForums #JFSports #Michezo
👍2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Spika wa Bunge la Tanzania, Dkt. Tulia Ackson aliyasema hayo jana, Mei 13, 2025 wakati wa ibada ya mazishi ya aliyekuwa Waziri Mkuu na Makamu wa Rais wa Kwanza, Cleopa David Msuya huko Usangi - Mwanga
Zaidi https://jamii.app/KwendaMbinguni
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Kuelekea2025
Zaidi https://jamii.app/KwendaMbinguni
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Kuelekea2025
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa kichama wa Kinondoni, Henry Kilewo ametangaza kujiondoa rasmi ndani ya chama hicho na kueleza “Hatuendi kuanza upya, tunabadili Jukwaa.”
Akizungumza na Wanahabari, leo Mei 14, 2025, Kilewo ambaye pia ni Mwanachama wa Kundi la G-55 ndani ya chama hicho amesema “Chama kama kimepoteza mwelekeo wa Kiuongozi, kimepoteza mwelekeo wa kutovumiliana Kidemokrasia. Nimekubaliana na nafsi yangu kuwa dhana iliyonivutia kujiunga CHADEMA haipo tena.”
Soma https://jamii.app/G55Mei14
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Akizungumza na Wanahabari, leo Mei 14, 2025, Kilewo ambaye pia ni Mwanachama wa Kundi la G-55 ndani ya chama hicho amesema “Chama kama kimepoteza mwelekeo wa Kiuongozi, kimepoteza mwelekeo wa kutovumiliana Kidemokrasia. Nimekubaliana na nafsi yangu kuwa dhana iliyonivutia kujiunga CHADEMA haipo tena.”
Soma https://jamii.app/G55Mei14
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
👍1
Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini, Mrisho Gambo amesema yeye pamoja na Viongozi wengine wa Chama cha Mapinduzi wametembelea Kivuko cha Mto Rajabu ambapo Awamu ya Kwanza imekamilika na wapo kwenye utaratibu wa kuanza Awamu ya Pili
#Gambo, kupitia kurasa zake za Mitandao ya Kijamii ameandika “Jana pamoja na Viongozi wa Chama tulitembelea Kivuko cha Mto Rajabu kwenye Kata ya Sakina. Kivuko hiki Awamu ya Kwanza imekamilika na sasa tupo kwenye utaratibu wa kuanza awamu ya pili! Kazi na Utu: Tunasonga Mbele”
Soma https://jamii.app/GamboKivuko
#JamiiAfrica #JamiiForums #Kuelekea2025 #ServiceDelivery #HudumaZaKijamii #Accountability #Uwajibikaji
#Gambo, kupitia kurasa zake za Mitandao ya Kijamii ameandika “Jana pamoja na Viongozi wa Chama tulitembelea Kivuko cha Mto Rajabu kwenye Kata ya Sakina. Kivuko hiki Awamu ya Kwanza imekamilika na sasa tupo kwenye utaratibu wa kuanza awamu ya pili! Kazi na Utu: Tunasonga Mbele”
Soma https://jamii.app/GamboKivuko
#JamiiAfrica #JamiiForums #Kuelekea2025 #ServiceDelivery #HudumaZaKijamii #Accountability #Uwajibikaji
❤1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Mbunge wa Jimbo la Kisesa, Luhaga Mpina akiongelea mwenendo wa biashara na uwekezaji Nchini amesema taarifa ya 2022/23 kupitia Dirisha la Uwekezaji la Pamoja (One stop facilitation Centre) inaonesha kuwa miradi 240 ilisajiliwa, yenye thamani ya Trilioni 11.4, ambapo miradi 94 ni ya wageni, 89 Watanzania na 57 wabia
Ameeleza kwa mwaka 2023/24 maombi kwenye Tume ya Kugawa Ardhi kwaajili ya Uwekezaji yalikuwa 191 ambapo 130 yalikuwa ya Kampuni za wageni na 61 ya Watanzania hali inayoonesha wageni wanaongoza katika kupewa ardhi ya uwekezaji na uwekezaji kuliko Wazawa
Ameyasema hayo akichangia Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara Bungeni, leo Mei 14, 2025
Zaidi https://jamii.app/MpinaBungeniMei14
#JamiiForums #JamiiAfrica #Biashara #Uwekezaji #Uchumi
Ameeleza kwa mwaka 2023/24 maombi kwenye Tume ya Kugawa Ardhi kwaajili ya Uwekezaji yalikuwa 191 ambapo 130 yalikuwa ya Kampuni za wageni na 61 ya Watanzania hali inayoonesha wageni wanaongoza katika kupewa ardhi ya uwekezaji na uwekezaji kuliko Wazawa
Ameyasema hayo akichangia Bajeti ya Wizara ya Viwanda na Biashara Bungeni, leo Mei 14, 2025
Zaidi https://jamii.app/MpinaBungeniMei14
#JamiiForums #JamiiAfrica #Biashara #Uwekezaji #Uchumi
Raia wa Norway huwa na utaratibu wa kuwaacha Watoto wao nje iwe ni msimu wa joto au wa baridi kali kwa madai kuwa ni njia moja wapo ya Watoto hao wachanga kupata hewa safi na kujenga kinga dhidi ya Magonjwa kama Mafua na kikohozi
Utaratibu huu ukifanyika wakati wa baridi Watoto huvishwa nguo za joto na kuachwa kwenye Magari ya Kutembelea Watoto (Stroller) na mara nyingine hutumia Kipima Joto kufuatilia hali ya hewa
Mdau unaweza kumuacha mwanao nje kwenye baridi ili kuimarisha kinga yake dhidi ya Magonjwa ya Msimu wa Baridi?
#JamiiForums #JamiiAfrica #NordicWeek #ParentHood #Lifestyle
Utaratibu huu ukifanyika wakati wa baridi Watoto huvishwa nguo za joto na kuachwa kwenye Magari ya Kutembelea Watoto (Stroller) na mara nyingine hutumia Kipima Joto kufuatilia hali ya hewa
Mdau unaweza kumuacha mwanao nje kwenye baridi ili kuimarisha kinga yake dhidi ya Magonjwa ya Msimu wa Baridi?
#JamiiForums #JamiiAfrica #NordicWeek #ParentHood #Lifestyle
👍1
MANYARA: Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Joseph Nyamoko na Issa Masoud wamefariki Dunia baada ya kupigwa na radi wakati wakiendelea na majukumu yao ya udhibiti wa usalama
Taarifa ya Jambo TV imeeleza kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP Ahmed Makarani amesema tukio hilo limetokea katika Mji Mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro na kuwa mipango ya kusafirisha miili ya askari hao inaendelea kwa uratibu wa Jeshi la Polisi na Familia za wahusika
Aidha, Nyamoko na Issa kila mmoja ameacha Mke na watoto wawili
Soma https://jamii.app/RadiSimanjiro
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMatukio
Taarifa ya Jambo TV imeeleza kuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP Ahmed Makarani amesema tukio hilo limetokea katika Mji Mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro na kuwa mipango ya kusafirisha miili ya askari hao inaendelea kwa uratibu wa Jeshi la Polisi na Familia za wahusika
Aidha, Nyamoko na Issa kila mmoja ameacha Mke na watoto wawili
Soma https://jamii.app/RadiSimanjiro
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMatukio
😢6👍3
Tuchague kuwa watu wa kutafakari kabla ya kuzungumza. Tuchague kuchukua hatua zinazotokana na ukweli, si hisia, kwa sababu maneno yana nguvu na maamuzi yana athari
Pale kunapokuwa na sintofahamu, epuka kutoa hukumu bila kujiridhisha, kwani hukumu na maamuzi yasiyoangaliwa kwa makini yanaweza kuvunja zaidi kuliko kujenga
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF #GoodMorning #Maisha
Pale kunapokuwa na sintofahamu, epuka kutoa hukumu bila kujiridhisha, kwani hukumu na maamuzi yasiyoangaliwa kwa makini yanaweza kuvunja zaidi kuliko kujenga
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF #GoodMorning #Maisha
👍1
ENGLAND: Mshambuliaji wa Tottenham Hotspur, Son Heung-min (32) amefungua kesi Polisi dhidi ya Mwanamke ambaye alidai ana ujauzito wa staa wake akidai kwamba alifanya hivyo kwa lengo la kupata fedha
Wanasheria wa Son wanadai Mdada huyo alitoa madai hayo Juni 2024 na akataka fedha ili anyamaze, wiki iliyopita Son akaamua kufungua mshtaka kwa kuamini mtu huyo alikuwa na lengo la kumlaghai ili ajipatie fedha
Son hana mke wala Mtoto anayetambulika na aliwahi kunukuliwa akisema “Baba alisema unapooa kipaumbele cha kwanza ni familia, mke na Watoto kisha soka. Nataka kuhakikisha nitaendelea kucheza soka kwa kiwango cha juu, nikistaafu ndio nitaanza kutafuta Watoto.”
Soma https://jamii.app/SonBlackmail
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports
Wanasheria wa Son wanadai Mdada huyo alitoa madai hayo Juni 2024 na akataka fedha ili anyamaze, wiki iliyopita Son akaamua kufungua mshtaka kwa kuamini mtu huyo alikuwa na lengo la kumlaghai ili ajipatie fedha
Son hana mke wala Mtoto anayetambulika na aliwahi kunukuliwa akisema “Baba alisema unapooa kipaumbele cha kwanza ni familia, mke na Watoto kisha soka. Nataka kuhakikisha nitaendelea kucheza soka kwa kiwango cha juu, nikistaafu ndio nitaanza kutafuta Watoto.”
Soma https://jamii.app/SonBlackmail
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Katibu wa Shura ya Maimamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda ametoa wito kwa Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson kurejea kumbukumbu za Bunge kuona taarifa za utekaji zilishawahi kuwasilishwa Bungeni Mwaka 2018 na hazikufanyiwa kazi
Amesema hoja hiyo iliwasilishwa na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe alivyowasilisha hoja kuhusu uwepo wa matukio ya utekaji na mauaji nchini na kuomba Bunge kusimama kwenye nafasi yake katika kuisimamia Serikali ili kuhakikisha matukio hayo yanakoma
Soma https://jamii.app/PondaUtekajiMei14
Video Credits: Jambo TV
#JamiiForums #HumanRights #Governance
Amesema hoja hiyo iliwasilishwa na Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kigoma Mjini, Zitto Kabwe alivyowasilisha hoja kuhusu uwepo wa matukio ya utekaji na mauaji nchini na kuomba Bunge kusimama kwenye nafasi yake katika kuisimamia Serikali ili kuhakikisha matukio hayo yanakoma
Soma https://jamii.app/PondaUtekajiMei14
Video Credits: Jambo TV
#JamiiForums #HumanRights #Governance