JamiiForums
โœ”
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Usikose kujiunga nasi katika mjadala kupitia X Spaces ya JamiiForums kuhusu changamoto za Uchaguzi Mkuu

Tutazungumzia changamoto zilizopo, fursa za maboresho, na njia za kuhakikisha Uchaguzi Huru na wa Haki kwa maendeleo ya Taifa letu

Kushiriki, bofya https://x.com/i/spaces/1gqGvNNlpeeGB

#JamiiForums #UchaguziMkuu25 #MaoniYaDemokrasia #Demokrasia #Governance #Accountability
Siku ya Elimu Duniani huadhimishwa Januari 24 kila Mwaka ikiangazia umuhimu wa Elimu katika kuleta Maendeleo, Usawa na Amani.

Mwaka 2025 dhima inaangazia nafasi ya Akili Mnemba na Elimu katika kudumisha Maendeleo katika Dunia ya Kidigitali. Lengo likiwa ni kuunganisha Elimu na kasi ya #Teknolojia pamoja na kuhakikisha Akili Mnemba inaongeza ubunifu na kuboresha sekta ya Elimu Duniani

Soma https://jamii.app/WorldEducationDay25

#JamiiForums #HumanRights #WorldEducationDay2025 #ServiceDelivery #ArtificialIntelligence
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
RUVUMA: Wananchi wa Kijiji cha Mlalamiwa na Matepwende wamerejesha fulana na Fedha walizopewa na wawakilishi wa Mbunge wao wa Jimbo la #Namtumbo, Vita Rashid Kawawa, wakieleza hawawezi kupokea wakati Huduma za Kijamii ni duni ikiwemo Barabara na Maji

Hayo yametokea kwenye kikao cha Wasaidizi wa Mbunge huyo, Januari 17, 2025 katika Kijiji cha Mlalawima, Kata ya Msisima na kilichohudhuriwa na Watendaji wa Vijiji ambapo wamedai Madarasa ni machache wakitoa mfano Mwaka 2024 kuna Wanafunzi walifanya Mitihani wakiwa chini ya Mti

Jitihada za JamiiForums kuwasiliana na Mbunge Kawawa kuhusu suala hilo zinaendelea

Soma https://jamii.app/Namtumbo

#Governance #Accountability #ServiceDelivery #JamiiForums
๐Ÿ‘3
Shiriki katika Mjadala wa "Uwepo wa Rushwa Katika Uchaguzi: Je, Vijana Wanapata Nafasi ya Kushiriki Kuleta Mabadiliko?" kupitia X Spaces ya JamiiForums uweze kutoa maoni yako

Usikose kujiunga nasi Januari 28, 2025, kuanzia Saa 12 jioni hadi Saa 2 Usiku

Kushiriki, bofya https://x.com/i/spaces/1gqGvNNlpeeGB

#JamiiForums #UchaguziMkuu25 #MaoniYaDemokrasia #Demokrasia #Governance #Accountability
KAGERA: Mtu mmoja ambaye alikuwa anasumbuliwa na maambukizi ya Virusi vya Marburg amefariki Dunia wakati akiendelea kupatiwa matibabu katika Hospital ya Wilaya Biharamulo

Kituo cha Azam TV kimesema Mgonjwa huyo ni kati ya Wawili waliobainika kuwa na ugonjwa huo Wilayani humo, ambapo kimenukuu Mkurugenzi wa Kinga wa Wizara ya Afya, Dkt. Ntuli Kapologwe aliyesema kuwa kifo hicho kilitokea Jumanne ya Januari 21, 2025

Aidha, Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt. Grace Magembe ambaye yupo Biharamulo, amesema elimu inaendelea kutolewa na kusisitiza watu kupunguza migusano isiyokuwa na lazima, pia ametoa wito Wananchi kuripoti katika Kituo cha afya wanapoona dalili za ugonjwa huo

Soma https://jamii.app/MarburgReport

#JamiiForums #Afya #Governance #PublicHealth
Mshiriki wa Shindano la Stories of Change 2024 alipendekeza kuipata "Tanzania Tuitakayo", Serikali ifanye Mabadiliko kwenye Mfumo wa Elimu kwa kuongeza Lugha ya Alama ikiwa Somo la lazima ili kuondoa pengo la Mawasiliano kwenye Jamii

Anasema, kuwepo kwa Somo hilo kutasaidia Wanafunzi wasio na changamoto za Usikivu kuelewa changamoto ambazo wenzao wanazipitia, hivyo kuimarisha hali ya kuheshimiana na kuondoa Ubaguzi wa aina yoyote

Je, unaona Wazo lake linatekelezeka?

Soma https://jamii.app/SOC24LughaAlama

#JamiiForums #SOC2024 #Accountability #Uwajibikaji #HumanRights
๐Ÿ‘2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Shauri lililofunguliwa Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Dar linalomhusu Mwanasiasa, Dkt. Wilbrod Slaa dhidi ya Jamhuri, limeendelea leo Januari 24, 2025, ambapo timu ya Mawakili ya Dkt. Slaa imeiomba Mahakama hiyo kufuta Kesi ya Jinai aliyofunguliwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu

Wakili Peter Madeleka anayeongoza jopo hilo amesema โ€œKatika hali ambayo imetusikitisha sana na kutuweka katika presha ya juu, kulikuwa na jitihada zinazofanywa ili kuhakikisha shauri hili linakwama lakini Timu ya Mawakili wa Utetezi wakafanya kazi kubwa ya utafiti kutafuta vifungu vya Sheria ili kesi isikilizwe.โ€

Soma https://jamii.app/DktSlaaJan24

#JFMatukio #JamiiForums #CivilRights
๐Ÿ‘1
ZANZIBAR: Chama cha #ACTWazalendo kimeitaka Wizara ya Elimu kuacha kuwashirikisha Wanafunzi katika shughuli za Kisiasa muda wa masomo kwani ni kinyume na miongozo ya Elimu na mafunzo ya Amali

Taarifa hiyo iliyotolewa Januari 24, 2025 imesema kuna taarifa za Walimu kulazimisha kuwatoa Wanafunzi Madarasani ili kushiriki katika shughuli za Kisiasa pamoja na mapokezi, Mikutano na Makongamano ya Chama cha Mapinduzi jambo ambalo linawakosesha Haki yao ya Elimu na kuathiri ufaulu wao

Aidha, taarifa hiyo imeitaka Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali kutoa mwongozo mahsusi kwa Wanafunzi kushiriki katika shughuli za Kisiasa ikiwa wanahisi miongozo iliyopo imepitwa na wakati na kama sasa wanaona ipo haja ya kuwatumia Wanafunzi hao katika shughuli za Kisiasa

Soma https://jamii.app/WanafunziKutumikaSiasa

#JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji #ChildrensRights
๐Ÿ‘1
ELIMU: Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (#HESLB) imesema Wanafunzi 80 wa Shahada za Uzamili katika Taasisi ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela (NM-AIST) ambao wamedahiliwa katika Programu za Sayansi na Ubunifu, wamepangiwa ruzuku zenye thamani ya Tsh. Milioni 623.2 kupitia 'Samia Scholarship'

HESLB imesema Wanafunzi walioomba fursa hizo wanashauriwa kuangalia taarifa zao kupitia akaunti walizoombea (SIPA) na wanatakiwa kujisajili kwenye mfumo wa malipo wa Kidigitali (DiDiS), kupitia kwa Maafisa wa HESLB katika Chuo cha NM-AIST

Januari 20, 2025, Wadau wa JamiiForums.com walidai kuwa licha ya Chuo kufunguliwa Januari 13, 2025 na majina yao kupitishwa kwenye listi ya wanufaika, hakukuwa na maelekezo yoyote wala fedha za Ufadhili hazikuwa zimeingia kutoka HESLB na Chuoni hakukuwa na ufafanuzi kuhusu wao

Soma https://jamii.app/UfadhiliSamia25

#JamiiForums #Accountability #ServiceSelivery
Kila hatua kubwa huanza na imani ndogo ndani yako. Kuamini ndoto zako ni hatua ya kwanza ya kuzitimiza.

Kumbuka, ndoto hazina mipaka isipokuwa ile unayojiwekea mwenyewe

Anza kujiamini leo, fanya kazi kwa bidii, na usikubali chochote kikuzuie kufikia kile unachotamani

#JamiiForums #MorningQuote #AmkaNaJF #LifeLessons #LifeTips #Maisha
๐Ÿ‘1
Rushwa inatajwa kuwa miongoni mwa changamoto zinazokwamisha Chaguzi Huru na za Haki, ikiwazuia Vijana kushiriki kikamilifu hususan kugombea nafasi za Uongozi hivyo Wananchi kukosa Uwakilishi sawa wa Makundi ya Kijamii

Ili kujadili changamoto ya Rushwa katika Uchaguzi na nafasi ya Vijana kuleta mabadiliko chanya, usikose kujiunga nasi katika Mjadala kupitia Xspace ya JamiiForums, Januari 28, 2025 kuanzia Saa 12 jioni hadi Saa 2 Usiku

Kushiriki, bofya https://x.com/i/spaces/1gqGvNNlpeeGB

#JamiiForums #UchaguziMkuu25 #MaoniYaDemokrasia #Demokrasia #Governance #Accountability
ZANZIBAR: Imeelezwa hali ya Afya ya Akili kwenye Shule bado ni changamoto kubwa ambapo Wanafunzi wengi wanakabiliwa na matatizo ya Kiakili yanayoathiri uwezo wao wa kujifunza na kufaulu ambapo uelewa mdogo kuhusu hilo umesababisha wengi wao kukosa msaada muhimu

Mkurugenzi Mkuu wa 'Zanzibar Mental Health Support Organization' (ZAMHSO), Zaituni Shabani Salum, amesema wanashirikiana na Serikali kutekeleza Mradi wa kutoa Elimu, ambapo Wakufunzi wa Saikolojia wamepita katika Skuli ya Magufuli na Kwerekwe na kutoa elimu kwa Walimu, Wanafunzi na Wataalamu wa Afya ya Akili

Soma https://jamii.app/MentalHealthUnguja

#MentalHealth #PublicHealth #JamiiForums #ChildRights #JFAfyaAkili
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
RUVUMA: Mbunge wa Jimbo la Namtumbo, Vita Rashid Kawawa, amesema madai yaliyotolewa na baadhi ya Wananchi na Viongozi wa Serikali za Mtaa wa Vijiji vya Mlalamiwa na Matepwende kuwa hajachangia maendeleo ya Vijiji hivyo ni njia ya kumchafua na wanapofanya hivyo wanakichafua Chama Cha Mapinduzi (CCM)

Akizungumza na Wanachama wa #CCM Wanawake jimboni hapo, amesema โ€œTumetengeneza Barabara hadi Matepwende, kuna Mradi wa Maji umejengwa wa Tsh. Bilioni 1.56 na leo tunatandaza mabomba.โ€

Ikumbukwe Januari 17, 2025, baadhi ya Wananchi na Viongozi wa Vijiji hivyo walikataa kupokea fulana na Fedha zilizotolewa na Mbunge huyo kupitia Wasaidizi wake kwa maelezo kuwa Huduma za Kijamii na Miundombinu ni duni hali inayofanya Wananchi wanateseka.

Soma https://jamii.app/VitaKawawa

#JamiiForums #Accountability #Governance
๐Ÿ‘3