KAGERA: Mdau wa JamiiForums.com aliyejitambulisha kuwa Mhitimu wa Igabiro Training Institute of Agriculture ilichopo Muleba amedai Wahitimu wa awamu mbili chuoni hapo hawajapata vyeti licha ya kukamilisha taratibu zote
Akizungumza na JamiiForums, Mkuu wa Chuo, Sadoki Stephano amesema "Wahitimu waliosoma Mifugo Vyeti vyao vinatoka #NACTVET, upande wa Kilimo matokeo yao na Vyeti vinatolewa na Wizara."
Aidha, ameongoza kwa kusema kuwa kuna vyuo zaidi ya 9 ambavyo havijapata vyeti kwani vipo kwenye mchakato na vitapatikana ndani ya mwezi kutoka sasa
Soma https://jamii.app/VyetiChuoIgabiro
#JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji
Akizungumza na JamiiForums, Mkuu wa Chuo, Sadoki Stephano amesema "Wahitimu waliosoma Mifugo Vyeti vyao vinatoka #NACTVET, upande wa Kilimo matokeo yao na Vyeti vinatolewa na Wizara."
Aidha, ameongoza kwa kusema kuwa kuna vyuo zaidi ya 9 ambavyo havijapata vyeti kwani vipo kwenye mchakato na vitapatikana ndani ya mwezi kutoka sasa
Soma https://jamii.app/VyetiChuoIgabiro
#JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji
❤1
MBEYA: Mdau anadai kukosekana kwa Huduma ya Maji maeneo ya Isyesye kumeathiri biashara na huduma za kijamii na kudai kuwa hiyo siyo mara ya kwanza kutokea kwa changamoto ya aina hiyo na wanapofuatilia hawapati majibu sahihi
Akizungumza na JamiiForums, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (MBEYA UWSA), CPA.Gilbert Kayange anasema “Uzalishaji haukidhi mahitaji, kuna maboresho ya mitambo sehemu na mafundi wapo kazini tangu juzi kurekebisha ili huduma irejee.”
Ameongeza “Kumaliza tatizo hilo jumla, tuna Mradi wa Mto Kiwira ukikamilika ndani ya mwaka mmoja na nusu, utazalisha Maji Lita Milioni 117 kwa siku. Kuhusu Isyesye, miaka mitatu nyuma walikuwa na changamoto kubwa ya kukosa maji zaidi ya mwezi lakini sasa ikitokea ni kwa siku kadhaa tu.”
Soma https://jamii.app/IsyesyeMaji
#JFHuduma #JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
Akizungumza na JamiiForums, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Mbeya (MBEYA UWSA), CPA.Gilbert Kayange anasema “Uzalishaji haukidhi mahitaji, kuna maboresho ya mitambo sehemu na mafundi wapo kazini tangu juzi kurekebisha ili huduma irejee.”
Ameongeza “Kumaliza tatizo hilo jumla, tuna Mradi wa Mto Kiwira ukikamilika ndani ya mwaka mmoja na nusu, utazalisha Maji Lita Milioni 117 kwa siku. Kuhusu Isyesye, miaka mitatu nyuma walikuwa na changamoto kubwa ya kukosa maji zaidi ya mwezi lakini sasa ikitokea ni kwa siku kadhaa tu.”
Soma https://jamii.app/IsyesyeMaji
#JFHuduma #JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
MAREKANI: Moja ya masharti waliyowekewa Watu Januari 20, 2025, kabla ya kuingia katika ukumbi wa Capital One Arena, Jijini Washington DC ilikuwa ni kuacha mabegi na mikoba nje ili waweze kushuhudia uapisho wa Rais #DonaldTrump
Soma https://jamii.app/CapitalOneAreaInstructions
#JamiiForums #Democracy
Soma https://jamii.app/CapitalOneAreaInstructions
#JamiiForums #Democracy
❤2
Maisha ni safari yenye changamoto lakini mafanikio huja kwa wale wanaosimama imara na kupambana bila kukata tamaa.
Usikate tamaa, kila hatua unayopiga unakaribia kwenye ushindi wako.
#JamiiForums #LifeLessons #LifeTips #Maisha #MorningQuote #Goodmorning #AmkaNaJF
Usikate tamaa, kila hatua unayopiga unakaribia kwenye ushindi wako.
#JamiiForums #LifeLessons #LifeTips #Maisha #MorningQuote #Goodmorning #AmkaNaJF
👍2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Wagombea wa nafasi ya Umakamu Mwenyekiti Zanzibar katika Uchaguzi wa CHADEMA, Said Mzee Said na Said Issa Mohamed wanapigiwa kura upya baada ya nafasi hiyo kukosa mgombea aliyefikisha zaidi ya Asilimia 50 ya kura zilizopigwa
Hayo yametangazwa na Katibu Mkuu wa #CHADEMA, John Mnyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City
Kutokana na matokeo hayo, Mnyika amesema matokeo ya nafasi nyingine ya Makamu Mwenyekiti Bara na Mwenyekiti Taifa yatachelewa kutangazwa licha ya kukamilika na Wawakilishi wa Wagombea kutangazwa
Soma https://jamii.app/UchaguziCHADEMA
#JamiiForums #Siasa #JFDemocracy #Demokrasia
Hayo yametangazwa na Katibu Mkuu wa #CHADEMA, John Mnyika kwenye Ukumbi wa Mlimani City
Kutokana na matokeo hayo, Mnyika amesema matokeo ya nafasi nyingine ya Makamu Mwenyekiti Bara na Mwenyekiti Taifa yatachelewa kutangazwa licha ya kukamilika na Wawakilishi wa Wagombea kutangazwa
Soma https://jamii.app/UchaguziCHADEMA
#JamiiForums #Siasa #JFDemocracy #Demokrasia
DAR: Kupitia ukurasa wake wa X (Twitter), Mwanasiasa, #FreemanMbowe amempongeza na kumtakia heri #TunduLissu licha ya kuwa matokeo rasmi ya uchaguzi wa #CHADEMA hayajatangazwa
Mbowe ameandika “Nimepokea kwa mikono miwili maamuzi ya uchaguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama chetu CHADEMA uliohitimishwa leo asubuhi 22 Januari 2025. Nampongeza Mhe. Tundu Lissu na wenzake kwa kuaminiwa kutwikwa jukumu la Uongozi wa Chama. Nawatakia kila la kheri katika kukipeleka mbele Chama chetu.”
Baada ya andiko hilo, John Heche akajibu “Asante sana Mwenyekiti, umetujenga na kutulea, umeonesha Demokrasia kwa kuongoza timu kusimamia uchaguzi wa wazi, huru na haki. Historia ya Tanzania itakukumbuka, kama mtu uliejenga Demokrasia na kuleta mageuzi makubwa kwenye Nchi na chama chetu.”
Soma https://jamii.app/MboweAkubali
#JamiiForums #Siasa #JFDemocracy #Demokrasia
Mbowe ameandika “Nimepokea kwa mikono miwili maamuzi ya uchaguzi wa Mkutano Mkuu wa Chama chetu CHADEMA uliohitimishwa leo asubuhi 22 Januari 2025. Nampongeza Mhe. Tundu Lissu na wenzake kwa kuaminiwa kutwikwa jukumu la Uongozi wa Chama. Nawatakia kila la kheri katika kukipeleka mbele Chama chetu.”
Baada ya andiko hilo, John Heche akajibu “Asante sana Mwenyekiti, umetujenga na kutulea, umeonesha Demokrasia kwa kuongoza timu kusimamia uchaguzi wa wazi, huru na haki. Historia ya Tanzania itakukumbuka, kama mtu uliejenga Demokrasia na kuleta mageuzi makubwa kwenye Nchi na chama chetu.”
Soma https://jamii.app/MboweAkubali
#JamiiForums #Siasa #JFDemocracy #Demokrasia
👍2✍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Wakati matokeo ya Uchaguzi Mkuu wa #CHADEMA yakisubiriwa kutangazwa kwenye Ukumbi wa Mlimani City, baadhi ya Wanachama wameonekana wakifurahia muziki wakiongozwa na #TunduLissu ambaye alikuwa mgombea wa nafasi ya Mwenyekiti akishindana na #FreemanMbowe na Odero Odero
Soma https://jamii.app/UchaguziCHADEMA
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Demokrasia
Soma https://jamii.app/UchaguziCHADEMA
#JamiiForums #Siasa #Democracy #Demokrasia
❤2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mgombea wa nafasi ya Makamu Mwenyekiti Zanzibar katika Uchaguzi wa #CHADEMA, Said Issa Mohamed, ametangaza kujiondoa katika kinyang’anyiro hicho na hivyo nafasi kubaki ikiwaniwa na Said Mzee Said
Said Mohamed amesema amefanya maamuzi hayo baada ya kushauriana na mshindani mwenzake na kuwa hana kinyongo kwa kitakachoendelea
Akizungumzia baada ya maamuzi hayo, Katibu wa CHADEMA, John Mnyika, amesema kinachofuata ni upigwaji wa kura wa siri ambapo Wajumbe watatakiwa kuchagua kwa NDIYO au HAPANA
Soma https://jamii.app/UchaguziCHADEMA
#JamiiForums #Siasa #JFDemocracy #Demokrasia
Said Mohamed amesema amefanya maamuzi hayo baada ya kushauriana na mshindani mwenzake na kuwa hana kinyongo kwa kitakachoendelea
Akizungumzia baada ya maamuzi hayo, Katibu wa CHADEMA, John Mnyika, amesema kinachofuata ni upigwaji wa kura wa siri ambapo Wajumbe watatakiwa kuchagua kwa NDIYO au HAPANA
Soma https://jamii.app/UchaguziCHADEMA
#JamiiForums #Siasa #JFDemocracy #Demokrasia
❤1
ZANZIBAR: Mdau wa JamiiForums.com ametoa wito kwa Maktaba ya Vitabu iliyopo Mjini Unguja kushughulikia ukosefu wa huduma ya maji ambayo imekuwa kero kwa Wanachama na Watumishi
Akizungumza na JamiiForums, Mkurugenzi wa Bodi ya Huduma za Maktaba Dkt. Ulfat Abdul-Aziz Ibrahim kuhusu suala hilo amesema anafahamu kuhusu suala hilo na tayari wanalishughulikia
Soma https://jamii.app/MaktabaHakunaChoo
#JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji #ServiceDelivery
Akizungumza na JamiiForums, Mkurugenzi wa Bodi ya Huduma za Maktaba Dkt. Ulfat Abdul-Aziz Ibrahim kuhusu suala hilo amesema anafahamu kuhusu suala hilo na tayari wanalishughulikia
Soma https://jamii.app/MaktabaHakunaChoo
#JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji #ServiceDelivery