JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Andrew Karamagi (Uganda), akiwa kwenye Maadhimisho ya Wiki ya AZAKI, ametambulisha dhana inaitwa 'Techno-Feudalism' yaani Ukabaila wa Kiteknolojia

Anasema Duniani kuna Kampuni kubwa Tano (5) za #Teknolojia yaani Alphabet (inamiliki #Google), #Meta (inamiliki Facebook, #Instagram, #WhatsApp), Amazon, #Apple na Microsoft

Kampuni hizi zinamilikiwa na Watu wachache na tunawapa taarifa nyingi mno ikiwemo alama za vidole, sura zetu n.k. Hatujui zinaenda wapi na Kampuni hizi zina pesa sana kiasi kwamba Bajeti ya kununua vifaa vya Ofisi tu vya #Google ni zaidi ya pato la Taifa la Nchi zetu.

Je, nchi zetu zikitaka kutengeneza #Sheria za kusimamia Kampuni hizi zitaweza?

Kila mara unapoenda Mtandaoni kununua kitu unaamini unanunua bidhaa, ila ukweli mchungu ni kuwa wewe ndio bidhaa. #Taarifa zako zinauzwa kwa Kampuni mbalimbali na zina thamani kweli kweli

#JamiiForums #DigitalWorld #TechnoFeudalism #TechGiants #CSOWeek2023 #WikiYaAZAKI2023 #Technology
👍2