JamiiForums
52.6K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Tume ya Umoja wa Afrika imekuwa muhanga wa Uhalifu wa Mtandaoni baada ya Matapeli kutumia Teknolojia ya Akili Bandia (#AI) kughushi sauti na Taswira ya Mkuu wa Tume hiyo, #MoussaFaki na kisha kupiga video za kuomba mikutano kwenye Miji ya Ulaya

Katika taarifa iliyotolewa na Tume hiyo imesema haijaweza kufahamika rasmi lengo la Matapeli japokuwa dalili zinaonesha walikuwa na nia ya kuiba Vitambulisho vya Kidijitali ili kuweza kufikia taarifa za siri zaidi

'#DeepFake' ni Teknolojia inayotumiwa na Wahalifu wa Mitandao, inazidi kukua na kupata umaarufu na wakati mwingine hutumiwa na Watu kueneza habari za uongo na propaganda

Soma https://jamii.app/DeepFakesAfricanUnion

#CyberCrimes #UlinziWaFaragha #DigitalWorld #DataPrivacy #PersonalDataProtection #JamiiForums
👍5
#Deepfake ni aina ya ubunifu wa Kidijitali unaotumia Teknolojia ya Akili Mnemba (#AI) kubadilisha au kuunda Picha, Sauti na Video ambazo huonekana kama ni za kweli, lakini zimeundwa kwa njia bandia

#Teknolojia hii hutumia Taarifa za Awali kuunda Maudhui mapya yanayofanana na ya awali. Inaweza kubadilisha sura za Watu kwenye Video, kuingiza Watu kwenye matukio ambayo hawakuwepo au hata kutengeneza mazungumzo ya Video na Sauti za Watu ambao hawajasema

Kufahamu mengi kuhusu Teknolojia hii tembelea Jukwaa letu la #JamiiCheck ndani ya JamiiForums.com

Soma https://jamii.app/DeepfakeTechnology

#DigitalWorld #DataPrivacy #JamiiForums
👍4👏1