JamiiForums
βœ”
54K subscribers
34.1K photos
2.26K videos
31K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Ni muhimu kwa anayehitaji kusajili laini yake kuchukua tahadhari kwa kuhakikisha anaweka alama ya kidole mara moja, na ikiwa ipo haja ya zoezi kurudiwa ni muhimu wakala akatoa hakikisho kwamba zoezi halilengi kuchukua alama ya kidole mara mbili

Ikiwa Kitambulisho chako kimetumika na wakala kusajilia laini za Watu wengine bila ridhaa na idhini yako fika katika dawati la Huduma kwa wateja la Mtandao husika ili kutoa taarifa itakayowezesha kufutwa kwa namba ambazo huzitambui

Ni muhimu kuchukua hatua hii ili kulinda Taarifa zako binafsi katika kitambulisho cha NIDA zisitumike vibaya kwenye matukio ya uhalifu

Mjadala zaidi https://jamii.app/UsirudieAlamaZaVidole

#JamiiForums #DataProtection #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DataPrivacy #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako
πŸ‘1
Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya 2022 Kifungu cha 37, inaeleza mhusika wa taarifa ana Haki ya kulipwa fidia kutoka kwa mkusanyaji au mchakataji wa Taarifa iwapo atapata madhara kwa sababu za ukiukwaji wa masharti ya Sheria hiyo

Endapo Tume itajiridhisha na maombi ya mhusika wa taarifa kuwa amepata madhara katika mazingira yanayompatia haki ya kulipwa fidia inaweza kuamuru kurekebishwa, kuzuiwa, kufutwa au kuharibiwa kwa taarifa hizo.

Soma: https://jamii.app/SheriaTaarifaBinafsi2022

#JamiiForums #DataProtection #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DataPrivacy #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako
Kumbuka kulinda taarifa zako na usikubali kuziweka wazi au kumpa mtu mwingine bila kujua lengo na matumizi ya taarifa zako

Usipolinda taarifa zako zinaweza kutumika katika Matukio ya Uhalifu kama vile Uwizi na Utapeli wa Mtandaoni

Mjadala zaidi https://jamii.app/PrivacyIsPower

#JamiiForums #DataProtection #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DataPrivacy #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako
Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi ya 2022 Kifungu cha 61 inaeleza Mtu kuharibu, kufuta, kupotosha, kuficha au kubadilisha Taarifa Binafsi kinyume na Sheria ni kosa

Endapo atakapotiwa hatiani atawajibika kulipa faini isiyopungua Tsh. 100,000 na isiyozidi Tsh. Milioni 10 au kifungo kisichozidi miaka mitano au vyote kwa pamoja

Soma: https://jamii.app/SheriaTaarifaBinafsi2022

#JamiiForums #DataProtection #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DataPrivacy #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako
Kwa mujibu wa Utafiti uliofanywa na Indo-Pacific Center for Civil Society Resilience, jumla ya Nchi 7 katika Bara la Asia na Oceania (Indo - Pacific region) zilipitia changamoto ya kuzimwa kwa mtandao na kuminywa kwa Uhuru wa Kujieleza Mtandaoni

Nchi zilizofanyiwa Utafiti ni Cambodia, Fiji, Malaysia, Pakistan, Sri Lanka, Taiwan na Thailand

Baadhi ya matukio yaliyojitokeza ni pamoja na ukusanyaji wa Taarifa Binafsi za Watu Mitandaoni, Gharama kubwa za Kanuni za Usalama wa Mtandao na kupelekea kuminywa kwa Uhuru wa Utumiaji Mtandao

Soma https://jamii.app/DigitalThreatsIndoPacific

#DigitalThreats #DigitalSecurity #DataPrivacy #DataProtection #IndoPacificRegion
πŸ‘1
MOROGORO: Wateja wa Nyumba za Wageni wamejulishwa kuwa hawatakiwi kuandika taarifa za wanapotoka au wanapoelekea katika Vitabu vya nyumba hizo, kwa kuwa kufanya hivyo ni kukiuka Sheria ya Taarifa Binafsi

Mkurugenzi wa Usajili na Uzingatiaji wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa (#PDPC), Stephen Wangwe amesema Watu wanatakiwa kujua Sheria ya #TaarifaBinafsi ili wasiingie matatizoni, kwa kuwa taarifa hizi hazina uhusiano na wao kufika katika nyumba hizo

Aidha, amesema tangu kuanza kutumika kwa Sheria ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi, mtu anapoona taarifa zake zimetumika bila ridhaa yake anaruhusiwa kulalamika kisha hatua zitachukuliwa dhidi ya wahusika au mhusika

Soma https://jamii.app/PDPCMarch1

#JamiiForums #DataProtection #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DataPrivacy #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako
πŸ‘2
MOROGORO: Washereheshaji wenye tabia ya kusambaza picha za Watu kama hawajapata idhini ya wahusika au mhusika wametakiwa kuwa makini kwa kuwa kufanya hivyo wanavunja Sheria

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC), Dkt. Emmanuel Mkilia akishiriki Warsha kuhusu dhana ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi amesema kuna baadhi ya mambo ambayo yanafanywa na mtu au Watu na hawataki yasambazwe kwa kuwa kufanya hivyo ni kuingilia faragha ya mtu

Anaseme β€œUnakuta umeenda kwenye sherehe, wale MC wanakupiga picha mnato au video baadaye unaonekana Mtandaoni ukiwa umejiachia, ni muhimu kupata ridhaa ya Mtu kabla ya kutumia taarifa zake kama jina, picha, namba za simu, makazi, anuani, taarifa za kifedha na afya.”

Soma https://jamii.app/TaarifaBinafsiSheria

#JamiiForums #DataProtection #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DataPrivacy #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako
πŸ‘3
Ripoti ya Freedom House na Article 19 inaonesha wasiwasi miongoni mwa Wananchi juu ya juhudi za Serikali kudhibiti nafasi ya Kidijitali ambapo ilidhihirishwa na amri ndogo ya awali ya kuanzishwa kwa Lango la Mtandao la Kitaifa (National Internet Gateway - NIG)

Japo utekelezaji wa NIG uliopangwa kuanza Februari 16, 2022, ulizuiwa, Wananchi wanahofia kwani NIG ingekusanya Taarifa za Mtandao, kuwa na mamlaka ya kuzima mtandao, kuhifadhi taarifa kwa mwaka mmoja na kuzitoa kwa mamlaka inapohitajika, na Watoa Huduma wa Mawasiliano wasiotii wangepewa adhabu kali.

Soma https://jamii.app/DigitalThreatsIndoPacific

#DigitalThreats #DigitalSecurity #DataPrivacy #DataProtection #IndoPacificRegion #DigitalThreats
πŸ‘1
Mashirika, Taasisi na Watu Binafsi wametakiwa kuwa makini wanapotumia Taarifa Binafsi za Watu, kwani kufanya hivyo bila idhini ya mhusika au Wahusika ni kinyume cha Sheria na adhabu yake kwa Mchakataji wa Taarifa (Mtu au Taasisi) inaweza kufika hadi Faini ya Tsh. Milioni 100

Mkurugenzi wa Tafiti za Ulinzi wa Taarifa na Teknolojia wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC), Dkt. Noe Nnko amesema faini hiyo ipo Kipengele cha 47 cha Faini za Kiutawala kinachoeleza Tume inaweza kuchukua hatua ya kutoza faini na kiwango cha juu hicho.”

Ameongeza "Taasisi zinapaswa kuwa na Afisa wa Taarifa Binafsi aliyefundishwa kutunza taarifa za Watu kwa usahihi. Mbali na faini pia kuna fidia kwa mwathirika itakayopimwa kulingana na madhara atakayopata ya kifaragha.”

Soma https://jamii.app/FineDataPrivacy

#JamiiForums #DataProtection #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DataPrivacy #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako
πŸ‘2❀1
Ripoti ya Freedom House na Article 19 inaonesha wasiwasi miongoni mwa Wananchi wa Malaysia juu ya juhudi za Serikali kudhibiti nafasi ya Kidigitali na kuzuia Uhuru wa Kujieleza hasa kwa Waandishi wa Habari ilidhihirishwa na Muswada wa Usalama Mtandaoni wa Mwaka 2024

Kupitia mradi wa 'Sinar' ambalo ni shirika lisilo la Kiserikali waligundua madhara yatakayojitokeza na kuchapisha ripoti za kimataifa ambazo zilichochea uhamasishaji nchini humo ambapo Wataalamu wa IT na wajasiriamali waliwasilisha pingamizi juu ya mabadiliko ya Muswada huo kwa Serikali

Soma https://jamii.app/DigitalThreatsIndoPacific

#DigitalThreats #DigitalSecurity #DataPrivacy #DataProtection #IndoPacificRegion #DigitalThreats
Ripoti ya Freedom House na Article 19 inaonesha wasiwasi miongoni mwa Wananchi wa Pakistan juu ya juhudi za Serikali kwenye kudhibiti nafasi ya Kidigitali na kuzuia Uhuru wa Kujieleza Mtandaoni kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa 2024 kupitia Sheria ya Kuzuia Uhalifu wa Kidijitali (PECA) ya 2022

Kupitia jitihada za Shirikisho la Waandishi wa Habari la Pakistan (PFUJ) Mahakama Kuu ya Islamabad ilitangaza kuwa Sheria hiyo ni kinyume na Katiba na kuagiza Serikali ipitie tena Sheria ya Udhalilishaji ya 2002 na kufanya mapendekezo mapya

Soma https://jamii.app/DigitalThreatsIndoPacific

#DigitalThreats #DigitalSecurity #DataPrivacy #DataProtection #IndoPacificRegion #DigitalThreats
Ripoti ya Freedom House na Article 19 imeonesha wasiwasi miongoni mwa Wananchi wa Sri Lanka, juu ya juhudi za Serikali kwenye kuzuia Uhuru wa Kujieleza Mtandaoni kipindi cha Uchaguzi Mkuu wa 2024, kupitia Sheria ya Usalama Mtandaoni (OSA) ya 2023

Sheria hii ilipingwa vikali kutokana na kutoa ruhusa ya Upatikanaji wa mifumo ya kompyuta na taarifa binafsi bila ridhaa ya mhusika

Kupitia jitihada za Vyama kama vile Asia Internet Coalition na Global Network Initiative na mashirika mengine ya ndani na nje ya Sri Lanka, Sheria hiyo ilifanyiwa mabadiliko

Soma https://jamii.app/DigitalThreatsIndoPacific

#DigitalThreats #DigitalSecurity #DataPrivacy #DataProtection #IndoPacificRegion #DigitalThreats
Ripoti ya Freedom House na Article 19 ilionesha wasiwasi miongoni mwa Wananchi wa Taiwan baada ya Wizara ya Mambo ya Ndani kuanzisha mpango wa kubadilisha vitambulisho vya Taifa kuwa vya Kidigitali

Mpango huo ulizua taharuki kutokana na hofu ya uvujaji na matumizi mabaya ya Taarifa Binafsi, pamoja na hatari ya uwezekano wa udukuzi wa Taarifa

Vikundi na Taasisi mbalimbali walishinikiza Serikali kuboresha ulinzi na matumizi ya Taarifa binafsi pamoja na kuanzisha Taasisi huru ya kulinda taarifa binafsi

Soma https://jamii.app/DigitalThreatsIndoPacific

#DigitalThreats #DigitalSecurity #DataPrivacy #DataProtection #IndoPacificRegion #DigitalThreats
MARA: Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Rorya, Abdul Mtaka, ameagiza taasisi za Mikopo zinazoshikilia kadi za benki za Watumishi wa Umma kama dhamana wanapokopa kuacha mara moja vitendo hivyo, kwa kuwa ni kinyume cha Sheria

Amesema β€œWapo Watumishi wanaokopa katika Sekta rasmi zikiwemo Benki kwa kuzingatia utaratibu wa kiasi kinachotakiwa kusalia katika mishahara yao, baada ya hapo wanakwenda kukopa kwenye taasisi zisizo rasmi ambazo huchukua Kadi zao za Benki na namba za Siri na kuchukua fedha zinazoingia ili kurejesha mkopo.”

Ameongeza kuwa, vitendo hivyo vinawafanya Watumishi kutofanya kazi kwa ufanisi kwa kuwa wanajikuta hawana fedha za kukidhi mahitaji yao ya muhimu

Soma https://jamii.app/KaziZaBenki

#DataPrivacy #JamiiForums #Governance #DigitalSecurity #DataProtection
❀1πŸ‘1
Ripoti ya Freedom House na Article 19 imeonesha wasiwasi miongoni mwa Wananchi wa Thailand juu ya juhudi za Serikali kudhibiti Vyombo vya Habari na kuzuia mtandao kupitia Sera ya "Single Gateway"

Sera hii ilipingwa vikali na Asasi za Kiraia na Wadau wa Teknolojia, kutokana na kutoa ruhusa ya kukandamiza Uhuru wa Kujielezea, matumizi ya mtandao n.k, ambapo jitihada zao zilizaa matunda kwa kufanikiwa kuzuia Sera hiyo kupitishwa

Soma https://jamii.app/DigitalThreatsIndoPacific

#DigitalThreats #DigitalSecurity #DataPrivacy #DataProtection #IndoPacificRegion #DigitalThreats
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mtangazaji wa Clouds FM, Samuel Nathaniel Sasali ameeleza hawezi kuweka Picha/Video Mtandao za matukio ya harusi bila ruhusa ya Wahusika, akidai aliwahi kuitwa kuwa shahidi katika kesi iliyotokana na yeye kuposti tukio la Harusi ambapo baadaye ilibainika Bwana Harusi alikuwa na mke mwingine

Ikumbukwe mara kadhaa Wadau wa JamiiForums.com wamekosoa matukio ya Watu kuchapisha picha na Video za Watu wengine Mitandaoni bila ridhaa yao, Washehereshaji (MC) nao walionekana kuwa moja ya kundi linaloongoza kwa kufanya vitendo hivyo

Februari 2025, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC), Dkt. Emmanuel Mkilia alisema β€œNi muhimu kupata ridhaa ya mtu kabla ya kutumia taarifa zake binafsi, Washereheshaji wanaosambaza picha au video bila ridhaa wanakiuka Faragha ya Mtu.”

Soma https://jamii.app/SamSasali

#JamiiForums #DataProtection #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DataPrivacy #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako
πŸ‘1
DAR: Mshereheshaji, Anthony D. Luvanda akihojiwa na Clouds FM Machi 18, 2025, alisema Tasnia hiyo imekuwa ikivamiwa na Watu wengi ambapo wapo wanaofanya vitu kinyume cha Sheria na kukiuka faragha za Watu kwa kuchapisha picha na video ambazo zinadhalilisha Utu

Soma https://jamii.app/NukuuLuvanda

#JamiiForums #DataProtection #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DataPrivacy #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako
Denmark itakuwa Nchi ya kwanza Ulaya kutoa Hakimiliki kwa raia wake juu ya matumizi ya Sura, miili na Sauti zao ili kukabiliana na video na sauti za kughushi "deepfakes" za Akili Unde zenye maudhui ya ngono, utapeli na propaganda za Kisiasa

Pendekezo hilo itamaanisha kuwa Mtu akichakachua au kutumia taarifa zako kutengeneza video, sauti au picha bandia bila ruhusa unaweza kudai ziondolowe na hata kulipwa fidia

Sheria hiyo inatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika rasmi kabla ya mwisho wa Mwaka 2025 na iwapo majukwaa ya #Teknolojia yatashindwa kuondoa maudhui yatakayoripotiwa yatakabiliwa na faini kubwa

Mdau unadhani Sheria kama hii inaweza kutumika kwa Nchi za Afrika?

Mjadala zaidi https://jamii.app/DenmarkFightsDeepfakes

#JamiiAfrica #JamiiForums #DataPrivacy #DataProtection #DigitalRights
πŸ‘2❀1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
ZANZIBAR: Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dkt. Khalid Salumu Mohamed amesema "Zamani taarifa tulikuwa tunatunza kwenye makaratasi hivyo zilikuwa hazisambai kwa kasi lakini sasa hivi kuna ukuaji wa Teknolojia ya kisasa, taarifa zinasambaa haraka sana."

Ameyasema hayo wakati akifungua rasmi mafunzo ya Dhana ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi kwa Maafisa Habari na Wanachama wa Chama cha Waandishi wa Habari Zanzibar, Julai 19, 2025.

Soma https://jamii.app/TuweMakiniUlinziFaragha

#JamiiForums #JamiiAfrica #DataProtection #DataPrivacy #UlinziWaTaarifaBinafsi #UlinziWaFaragha #DigitalRights #TaarifaZakoMaishaYako