Ukivitambua na kuvishinda Vizuizi vya ndani, unafungua mlango wa Mafanikio ya kweli.
Komesha Uvivu kwa kuchukua hatua, tuliza Hasira kwa Busara. Ndani yako kuna nguvu ya kubadilika.
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF #GoodMorning #Maisha
Komesha Uvivu kwa kuchukua hatua, tuliza Hasira kwa Busara. Ndani yako kuna nguvu ya kubadilika.
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF #GoodMorning #Maisha
❤1👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Naibu Spika na Mbunge wa Ilala (CCM), Mussa Zungu akiwaaga Wabunge na Watumishi wa Bunge Juni 20, 2025, amewahimiza kuwa na Ushupavu na kuwajali Wananchi hasa wale wa Kipato cha chini na Yatima kwani wanahitaji kusaidiwa
Soma https://jamii.app/ZunguAdabuHeshima
#JamiiForums #Accountability #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Bungeni
Soma https://jamii.app/ZunguAdabuHeshima
#JamiiForums #Accountability #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Bungeni
DAR: Taarifa ya Kanisa Katoliki imesema Maaskofu wameagiza maboresho ya Maadhimisho yanayohusu Daraja Takatifu, Nadhiri za Kitawa, Ndoa, Jubilei na Maziko ya Kikristo kutokana na kuwepo kwa tabia ya kuingiza matangazo mengi na hotuba nyingi kwenye Maadhimisho mbalimbali ya Kiliturujia
Taarifa imesema kwenye Mkutano Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania-TEC, Kikao cha 109, kilichofanyika Kurasini tarehe 16-19 Juni 2025, Maaskofu wameagiza mwishoni mwa Adhimisho (baada ya sala ya komuniyo), itatolewa mara moja Baraka ya mwisho
Hakutakuwa na hotuba za kupongezana, isipokuwa tu Mwadhimishaji (Paroko/Padri/Askofu/Rais wa TEC) atatambua kwa ufupi uwepo wa Wageni wa Kidini, Kiserikali, Kijamii na Waalikwa wote bila kuwapa nafasi ya kuongea, kutoa hotuba wala kusalimia. Mwadhimishi Mkuu anawajibika kuwaalika wageni kutoa zawadi zao na bila ya wao kutoa Salamu za pongezi.
Soma https://jamii.app/TECBanWanasiasa
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #Uwajibikaji
Taarifa imesema kwenye Mkutano Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania-TEC, Kikao cha 109, kilichofanyika Kurasini tarehe 16-19 Juni 2025, Maaskofu wameagiza mwishoni mwa Adhimisho (baada ya sala ya komuniyo), itatolewa mara moja Baraka ya mwisho
Hakutakuwa na hotuba za kupongezana, isipokuwa tu Mwadhimishaji (Paroko/Padri/Askofu/Rais wa TEC) atatambua kwa ufupi uwepo wa Wageni wa Kidini, Kiserikali, Kijamii na Waalikwa wote bila kuwapa nafasi ya kuongea, kutoa hotuba wala kusalimia. Mwadhimishi Mkuu anawajibika kuwaalika wageni kutoa zawadi zao na bila ya wao kutoa Salamu za pongezi.
Soma https://jamii.app/TECBanWanasiasa
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #Uwajibikaji
❤4👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mbunge wa Viti Maalumu, Thea Ntara, amesisitiza Serikali kuwalipa Watumishi wa Vyuo Vikuu wakiwemo Wahadhiri madeni yao, akieleza wengi wao wanafanya kazi katika Mazingira magumu na hawajitokezi kugoma au kuonesha utovu wa Nidhamu
Ikumbukwe Januari 2025, Mdai wa JamiiForums.com aliandika hoja akisema "Chuo Kikuu Huria Tanzania lipeni Waajiriwa wenu pesa zao za kujikimu, mtawaua njaa na kuwafedhehesha Mtaani"
Mdau huyo alitoa Mfano kuwa Watumishi wanaohamishwa Vituo vya Kazi hukaa hadi zaidi ya Mwaka bila kupewa Fedha zao za kujikimu
Soma https://jamii.app/MbungeMadeniWahadhiri
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance #Bungeni #JFMdau2025
Ikumbukwe Januari 2025, Mdai wa JamiiForums.com aliandika hoja akisema "Chuo Kikuu Huria Tanzania lipeni Waajiriwa wenu pesa zao za kujikimu, mtawaua njaa na kuwafedhehesha Mtaani"
Mdau huyo alitoa Mfano kuwa Watumishi wanaohamishwa Vituo vya Kazi hukaa hadi zaidi ya Mwaka bila kupewa Fedha zao za kujikimu
Soma https://jamii.app/MbungeMadeniWahadhiri
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance #Bungeni #JFMdau2025
👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Uchambuzi wa Bajeti kutoka Chama cha ACT - Wazalendo umesema kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026 Serikali imepanga kutumia Trilioni 56.49, ambapo Mgawanyo wa matumizi ni trilioni 38.99 kwa ajili ya Mishahara, Posho, Magari na Misafara ya Viongozi, Mabango ya Kumsifu Rais, Chai na Deni la Serikali (69.04%)
Wakati Miradi ya Barabara, Mikopo ya Wanafunzi, ujenzi wa vituo vya Afya, Shule, Dawa, Maji, Pembejeo za Kilimo, imetengewa Trilioni 17.49 (30.96%), ikimaanisha katika kila Tsh. 1,000, Tsh. 700 inaenda kwenye Mishahara, Chai, Deni na Posho huku Tsh. 300 tu ndio inaenda kuhudumia Wananchi
ACT imesema Mgawanyo wa Bajeti uliopelekwa kwenye matumizi ya Maendeleo ya Wananchi ni kiwango kidogo zaidi na itategemea zaidi Fedha za nje au Mikopo.
Soma zaidi Uchambuzi huu https://jamii.app/UchambuziBajetiACTWazalendo
#JamiiForums #Uwajibikaji #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025
Wakati Miradi ya Barabara, Mikopo ya Wanafunzi, ujenzi wa vituo vya Afya, Shule, Dawa, Maji, Pembejeo za Kilimo, imetengewa Trilioni 17.49 (30.96%), ikimaanisha katika kila Tsh. 1,000, Tsh. 700 inaenda kwenye Mishahara, Chai, Deni na Posho huku Tsh. 300 tu ndio inaenda kuhudumia Wananchi
ACT imesema Mgawanyo wa Bajeti uliopelekwa kwenye matumizi ya Maendeleo ya Wananchi ni kiwango kidogo zaidi na itategemea zaidi Fedha za nje au Mikopo.
Soma zaidi Uchambuzi huu https://jamii.app/UchambuziBajetiACTWazalendo
#JamiiForums #Uwajibikaji #JamiiAfrica #Accountability #BajetiKuu2025
❤1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Rais mstaafu, Jakaya Mrisho Kikwete amesema licha ya Vyama ya Siasa kuwa na kaulimbiu zake lakini itakapofika Siku ya kupiga kura, Akili za kuambiwa changanya na zako
Ameyasema hayo leo Juni 21, 2025 katika ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Sheria JNICC
Soma https://jamii.app/KikweteAkiliKura
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #UchaguziMkuu2025 #KuelekeaUchaguzi2025
Ameyasema hayo leo Juni 21, 2025 katika ufunguzi wa Kongamano la Kitaifa la Sheria JNICC
Soma https://jamii.app/KikweteAkiliKura
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #UchaguziMkuu2025 #KuelekeaUchaguzi2025
DAR: Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura amesema moja ya changamoto inayosumbua Sekta ya Habari ni suala la Upotoshaji wa Taarifa unaofanyika kwa makusudi ama kwa kutofahamu
Amesema hali hiyo imetokana na maendeleo ya Teknolojia ambayo yanatengeneza fursa kwa usambaaji wa Taarifa Potoshi, ambapo ameeleza hoja za kukabiliana na changamoto hizo ni sehemu ya Mada zitakazojadiliwa katika Mkutano wa Kimataifa wa Mabaraza ya Habari Afrika (Julai 14 - 17, 2025)
Aidha, ameongeza kuwa Mkutano huo utajadili mijadala ya kitalaamu kuhusu changamoto zinazoathiri Tasnia ya Habari na namna Mabaraza ya Habari kote Duniani yanavyokabiliana na changamoto hizo
Soma https://jamii.app/MabarazaYaHabari
#JamiiForums #JamiiAfrica #FactChecking #HakikiTaarifa #VisitJamiiCheck
Amesema hali hiyo imetokana na maendeleo ya Teknolojia ambayo yanatengeneza fursa kwa usambaaji wa Taarifa Potoshi, ambapo ameeleza hoja za kukabiliana na changamoto hizo ni sehemu ya Mada zitakazojadiliwa katika Mkutano wa Kimataifa wa Mabaraza ya Habari Afrika (Julai 14 - 17, 2025)
Aidha, ameongeza kuwa Mkutano huo utajadili mijadala ya kitalaamu kuhusu changamoto zinazoathiri Tasnia ya Habari na namna Mabaraza ya Habari kote Duniani yanavyokabiliana na changamoto hizo
Soma https://jamii.app/MabarazaYaHabari
#JamiiForums #JamiiAfrica #FactChecking #HakikiTaarifa #VisitJamiiCheck
❤1
DAR: Akizungumzia umuhimu wa kuwa na Watu wanaohusika Uhakiki wa Taarifa, Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura amesema “Uwepo wa Wadau kama #JamiiAfrica unahitajika kutumika kusaidia kutoa elimu ya Uhakiki wa Taarifa kama ambavyo wamekuwa wakifanya (kupitia #JamiiCheck).”
Ameongeza “Tunahitaji Wadau aina hiyo waongezeke kusaidia kukabiliana na Taarifa Potoshi hasa wakati huu wa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, kwani kupotosha Sera, Ilani au Taarifa za Watu wakati huu tunapoelekea katika kampeni kunaweza kuwa na madhara makubwa.”
Amesema hayo wakati akizungumzia ujio wa Mkutano wa Kimataifa wa Mabaraza ya Habari Afrika (Julai 14-17, 2025) unaoandaliwa na MCT kwa kushirikiana na Mtandao wa Mabaraza Huru ya Habari Afrika (NIMCA), Umoja wa Mabaraza ya Habari ya Afrika Mashariki (EAPC) na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Soma https://jamii.app/MCTFactChecking
#JamiiForums #JamiiAfrica #FactChecking #HakikiTaarifa #VisitJamiiCheck
Ameongeza “Tunahitaji Wadau aina hiyo waongezeke kusaidia kukabiliana na Taarifa Potoshi hasa wakati huu wa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, kwani kupotosha Sera, Ilani au Taarifa za Watu wakati huu tunapoelekea katika kampeni kunaweza kuwa na madhara makubwa.”
Amesema hayo wakati akizungumzia ujio wa Mkutano wa Kimataifa wa Mabaraza ya Habari Afrika (Julai 14-17, 2025) unaoandaliwa na MCT kwa kushirikiana na Mtandao wa Mabaraza Huru ya Habari Afrika (NIMCA), Umoja wa Mabaraza ya Habari ya Afrika Mashariki (EAPC) na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Soma https://jamii.app/MCTFactChecking
#JamiiForums #JamiiAfrica #FactChecking #HakikiTaarifa #VisitJamiiCheck
DAR: Imeelezwa kuwa nguvu kubwa ya Kiuchumi ya Kampuni na Taasisi za Kidigitali imechangia kuvinyonya Kiuchumi Vyombo vya Habari vinavyotambulika kama "Traditional Media" (ikiwemo Magazeti, Vituo vya Runinga na Redio) kwa kuwa vimeshindwa kuendana na kasi ya ukuaji wa Soko la Digitali
Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura amesema kutokana na hali hiyo Vyombo vya Habari hivyo vinatakiwa kujengewa uwezo na Wadau ili viweze kushindana na Vyombo vya Habari vya Mtandaoni
Amesema kuwa hali hiyo imesababisha Uchumi wa TV, Redio na Magazeti kudorora kiasi kwamba hata taarifa zenye maslahi kwa Umma nazo zimekuwa changamoto kufanyika katika ubora unaotakiwa ikiwemo Habari za Uchunguzi
Soma https://jamii.app/MabarazaYaHabari
#JamiiForums #JamiiAfrica
#PressFreedom #DigitalRights #Accountability
Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Ernest Sungura amesema kutokana na hali hiyo Vyombo vya Habari hivyo vinatakiwa kujengewa uwezo na Wadau ili viweze kushindana na Vyombo vya Habari vya Mtandaoni
Amesema kuwa hali hiyo imesababisha Uchumi wa TV, Redio na Magazeti kudorora kiasi kwamba hata taarifa zenye maslahi kwa Umma nazo zimekuwa changamoto kufanyika katika ubora unaotakiwa ikiwemo Habari za Uchunguzi
Soma https://jamii.app/MabarazaYaHabari
#JamiiForums #JamiiAfrica
#PressFreedom #DigitalRights #Accountability
❤4
Rushwa ni adui mkubwa wa Maendeleo. Kila shilingi inayotolewa kama Rushwa inaongeza pengo la Huduma bora kwa Mwananchi, inadhoofisha Uchumi, na kuharibu Imani ya Wananchi
Tuchague Uadilifu, tusimamie Haki, na tuchague Maendeleo ya kweli
#JamiiForums #JamiiAfrica #UraiaWenyeUelewa #CivicEducation #RestlessDevelopment
Tuchague Uadilifu, tusimamie Haki, na tuchague Maendeleo ya kweli
#JamiiForums #JamiiAfrica #UraiaWenyeUelewa #CivicEducation #RestlessDevelopment
Unaweza kuwa na kipaji, lakini kuna tabia zinaweza kukurudisha nyuma kama vile uvivu, uzembe au kutokuishi kwa mipango
Kipaji pekee hakitoshi, ili uwe na mafanikio achana na tabia hatarishi
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF #GoodMorning #Maisha
Kipaji pekee hakitoshi, ili uwe na mafanikio achana na tabia hatarishi
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJF #GoodMorning #Maisha
DAR: Kiongozi wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania (Kanisa la Ufufuo na Uzima), Askofu Josephat Gwajima, kupitia ukurasa wake wa Instagram Jana Juni 21, 2025, alisema alimtembelea na kumjulia hali Padri Kitima
Aliandika “Leo Tarehe 21 Juni 2025 nimepata nafasi ya kumtembelea na kumjulia hali Padre Dr Charles Kitima, Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).”
Askofu Gwajima ambaye mara ya mwisho alionekana akizungumza hadharani Juni 2, 2025 aliongeza “Namshukuru Mungu afya yake imeendelea kuimarika.”
Soma https://jamii.app/GwajimaNaKitima
#JamiiForums #JFMatukio
Aliandika “Leo Tarehe 21 Juni 2025 nimepata nafasi ya kumtembelea na kumjulia hali Padre Dr Charles Kitima, Katibu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).”
Askofu Gwajima ambaye mara ya mwisho alionekana akizungumza hadharani Juni 2, 2025 aliongeza “Namshukuru Mungu afya yake imeendelea kuimarika.”
Soma https://jamii.app/GwajimaNaKitima
#JamiiForums #JFMatukio
❤3
Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuwa majeshi ya Marekani yamefanikiwa kushambulia vituo Vitatu vya Nyuklia vya Iran vilivyopo Fordow, Natanz na Isfahan, huku akiwaonya Iran kutolipiza kisasi
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, amepongeza hatua hiyo ya Marekani akiiita “uamuzi wa kishujaa” na kusema kuwa Israel na Marekani waliratibu hatua hizo kwa pamoja.
Aidha, Waziri wa mambo ya nje wa Iran, Abbas Araghchi amelaani vikali mashambulizi hayo na kusema ni kitendo cha uhuni, akidai yatakuwa na madhara ya kudumu
Soma https://jamii.app/TrumpShambuliziIran
#JamiiAfrica #JamiiForums #Diplomasia
Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, amepongeza hatua hiyo ya Marekani akiiita “uamuzi wa kishujaa” na kusema kuwa Israel na Marekani waliratibu hatua hizo kwa pamoja.
Aidha, Waziri wa mambo ya nje wa Iran, Abbas Araghchi amelaani vikali mashambulizi hayo na kusema ni kitendo cha uhuni, akidai yatakuwa na madhara ya kudumu
Soma https://jamii.app/TrumpShambuliziIran
#JamiiAfrica #JamiiForums #Diplomasia