JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Mwanafunzi wa Mwaka wa Kwanza wa Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), Emilian J. Duzu (21) anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za mauaji ya Gerald P. Said (22), Mwanafunzi wa Mwaka wa Tatu katika Chuo hicho, tukio ambalo limetokea Alfajiri ya Juni 14, 2025

Polisi imeeleza tukio lilitokea katika maeneo ya Klabu ya Muziki ya Mbeya Pazuri, ikidaiwa Emilian alimjeruhi Gerald kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali tumboni, akakimbizwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya lakini alifariki Saa 7:00 Mchana

Soma https://jamii.app/AmuuaMwanafunziClub

#JamiiForums #JamiiAfrica #JFMatukio
2
Vijana tusibaki kuwa watazamaji wa kinachoendelea kwenye jamii yetu, tujifunze haki na wajibu wetu, tujue sheria na sera zinazotugusa na tushiriki kikamilifu kwenye maamuzi yanayojenga mustakabali wetu

Kila mmoja wetu ana nafasi ya kuwa sehemu ya mabadiliko tunayoyataka, kwa kufanya maamuzi sahihi

Tuchukue hatua kwa kufuatilia taarifa kwa makini, kuhoji kwa hoja, na kutoa maoni yanayojenga. Tuwajibike sasa kwa mabadiliko na maendeleo tunayoyataka katika Jamii zetu

#JamiiAfrica #JamiiForums #RestlessDevelopment #RaiaWajibika #CivicEducation #SautiYaRaia #UraiaWenyeUelewa
KENYA: Polisi wa kutuliza ghasia wamempiga Risasi Kijana mmoja aliyekuwa kwenye #Maandamano ya kudai haki kwenye kifo cha Mwanaharakati Albert Ojwang, ambaye Uchunguzi na Mahojiano ya Polisi vilimebaini alifariki kwa kupigwa na Wafungwa kwa amri ya Mkuu wa Kituo cha Polisi (OCS) na Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi (DIG)

Video inayosambaa Mtandaoni inawaonesha Askari wawili wa kutuliza ghasia wakimfuata Kijana muuza Barakoa, kumpiga na kitako cha Bunduki, kisha kuongea nae kidogo kabla ya Polisi mmoja wao kumnyooshea bunduki na kumfyatulia Risasi, kisha kuondoka

Imeelezwa, Polisi aliyehusika katika tukio hilo tayari anashikiliwa, baada ya Inspekta Jenerali wa Huduma ya Polisi ya Taifa (NPS) kuagiza kukamatwa mara moja na kufikishwa Mahakamani

Soma https://jamii.app/KifoRaiaProtestOjwang

#Democracy #HumanRights #JamiiAfrica #JamiiForums #PoliceBrutarity
1
DIPLOMASIA: Siku kadhaa baada ya Rais wa Marekani, #DonaldTrump kuwaonya raia wa #Iran waliopo Mji wa Tehran kuhama, kwa kile alichoeleza kutakuwa na mashambulizi yanayoweza kufanyika katika eneo hilo, amedai Marekani ina udhibiti wa anga la Iran

Kupitia Mtandao wa Truth Social, Trump ameandika “Marekani sasa inadhibiti kikamilifu anga la Iran. Iran ilikuwa na vifaa vizuri vya kufuatilia anga na ulinzi wa kutosha na vingi lakini haviwezi kulinganishwa na ‘vitu’ vilivyotengenezwa na Wamarekani. Hakuna anayefanya vizuri zaidi ya Marekani.“

Ameongeza “Tunajua kwa uhakika kabisa alipojificha huyo anayeitwa ‘Kiongozi Mkuu’ (akimaanisha Ayatollah Ali Khamenei). Ni mlengwa rahisi, lakini yuko salama pale alipo hatutamwondoa (kumuua!), angalau si kwa sasa. Hatutakubali makombora yaelekezwe kwa raia au kwa Wanajeshi wa Marekani. Subira yetu inaanza kuisha. Asanteni kwa kulipa hili uzito!”

Soma https://jamii.app/MarekaniKumilikiAngaIran

#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio
2
Usikimbilie kufanya mengi bila ubora, fanya kwa kiasi lakini kwa kiwango cha juu na ubora zaidi

Katika maisha au kazi mafanikio si idadi, bali ubora ndio huleta matokeo ya kweli

#JamiiAfrica #JamiiForums #Maisha #GoodMorning #AmkaNaJF
1
Mdau wa JamiiForums.com ametoa wito kwa mamlaka husika kushughulikia kero ya mazingira duni ya vyoo vya Stendi Kuu ya Mkanaledi ya Mtwara, akidai hali hiyo inahatarisha #Afya za Watumiaji na wanavyovizunguka

Soma https://jamii.app/VyooVichafuMkanaledi

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #JFMdau2025
1
Kupitia Televisheni ya Taifa ya Iran, Wananchi wamehimizwa kuondoa programu ya #WhatsApp kwenye Simu zao, ikidaiwa (bila ushahidi wowote wa moja kwa moja) kuwa programu hiyo inakusanya taarifa za Watumiaji na kuzipeleka kwa #Israel

Katika taarifa yake, Kampuni ya #Meta ambayo inamiliki WhatsApp imesema “Tunasikitishwa na ripoti hizi za uongo ambazo huenda zikatumiwa kama kisingizio cha kuzuiwa kwa Huduma zetu wakati Watu wanazihitaji zaidi.”

Serikali ya #Iran imekuwa ikizuia upatikanaji wa Mitandao mbalimbali ya Kijamii kwa Miaka mingi, lakini Watu wengi nchini humo hutumia mbinu za kukwepa vizuizi hivyo kama #proxies na Mitandao Binafsi ya Intaneti (VPNs) ili kuendelea kupata Huduma

Mwaka 2022, Iran ilipiga marufuku WhatsApp na Google Play wakati wa Maandamano makubwa ya kupinga Serikali yaliyotokana na kifo cha Mwanamke aliyekuwa ameshikiliwa na Polisi wa Maadili wa Nchi hiyo. Marufuku hiyo iliondolewa mwishoni mwa Mwaka 2024

Soma https://jamii.app/IranVSWhatsApp

#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Wakati zoezi la uchukuaji fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) likiendelea, aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi wa #TFF, Wakili Aloyce Komba, akizungumza na Clouds FM amesema Kamati ya Uchaguzi haipo huru kutokana na mazingira ya ufanyaji kazi kutokuwa katika msingi ulionyooka

Ikumbukwe Kamati ya Uchaguzi ya TFF imetangaza Uchaguzi huo utafanyika Agosti 16, 2025, Jijini Tanga huku nafasi zinazowaniwa zikiwa ni za Rais (Nafasi 1) na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji (Nafasi 6)

Soma https://jamii.app/UchaguziTFF25

#JamiiForums #JFSports #Accountability
1
DIPLOMASIA: Kufuatia tangazo la Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu kutaka nchi 36 (ikiwemo Tanzania) kufanyia kazi baadhi ya mambo ya kiuhamiaji ambayo yanaweza kusababisha raia kuzuiwa kuingia Marekani, Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema Serikali ya Tanzania imeanza mashauriano

Amesema, Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Mambo ya Nje, imeanza kufanya mashauriano na wenzao upande wa Marekani kujua maeneo ambayo yanatakiwa kufanyiwa maboresho, hususani yanayohusiana na masuala ya kikonselii ili kuharakisha Tanzania isiwe moja ya nchi zitakazozuiwa kuingia Marekani

Tamko la Serikali linakuja baada ya Donald Trump kutaka nchi 36 kufuatilia na kutoa taarifa kabla ya Julai 18, 2025, kuhusu utayari wa nchi zao kuboresha hati za usafiri kwa raia wao, pamoja na kuchukua hatua kuhusu raia wao walioko Marekani kinyume cha sheria

Soma https://jamii.app/TanzaniaMazungumzoMarekani

#JamiiForums #JamiiAfrica #Diplomasia
1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akiuliza swali Bungeni leo, Juni 18, 2025, Mbunge wa Moshi Vijijini, Prof. Patrick Ndakidemi ametaka kujua lini Serikali itatunga Sheria itakayomshurutisha Mtoto kuwatunza Wazazi wake wakizeeka

Amejibiwa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mwanaidi Ali Khamis ambaye amesema suala hilo lipo katika Sera, Maboresho ya Mwaka 2003

Soma https://jamii.app/MatunzoYaWazee

#Maisha #Accountability #Governance #JamiiForums #Malezi
1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mbunge wa Nzega Vijijini, Dkt. Hamisi Kigwangalla, leo Juni 18, 2025 amezungumzia hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2024 pamoja na Mpango wa Maendeleo wa Taifa na Bajeti kuu ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026, akisema bado deni letu ni himilivu, hivyo kama Waziri wa Fedha anakopa ili kuleta maendeleo akope, Bunge litapitisha

Soma https://jamii.app/KigwangallaMikopoMwigulu

#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #JamiiAfrica #Bungeni
Ulitumia mbinu gani ili kufanikisha kujenga Nyumba yako ya kwanza? Ulichukua Mkopo au uliweka Akiba kidogokidogo?

Mjadala zaidi https://jamii.app/NyumbaMaraKwanza

#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats #JFStories #Maisha
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
GEITA: Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (#CCM) Bara, Stephen Wasira amesema tangu kupata uhuru, Tanzania imepata maendeleo makubwa na kwamba anayesema hakuna kilichofanyika anamfanisha na 'Kasuku' kwa kuwa anazungumza mambo kwa kukariri bila kujua maana yake

Amesema hayo Juni 17, 2025 alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara huko Wilayani Katoro

Soma https://jamii.app/WasiraKatoro

#Siasa #Governance #JamiiForums #Kuelekea2025
1