Kupitia Televisheni ya Taifa ya Iran, Wananchi wamehimizwa kuondoa programu ya #WhatsApp kwenye Simu zao, ikidaiwa (bila ushahidi wowote wa moja kwa moja) kuwa programu hiyo inakusanya taarifa za Watumiaji na kuzipeleka kwa #Israel
Katika taarifa yake, Kampuni ya #Meta ambayo inamiliki WhatsApp imesema “Tunasikitishwa na ripoti hizi za uongo ambazo huenda zikatumiwa kama kisingizio cha kuzuiwa kwa Huduma zetu wakati Watu wanazihitaji zaidi.”
Serikali ya #Iran imekuwa ikizuia upatikanaji wa Mitandao mbalimbali ya Kijamii kwa Miaka mingi, lakini Watu wengi nchini humo hutumia mbinu za kukwepa vizuizi hivyo kama #proxies na Mitandao Binafsi ya Intaneti (VPNs) ili kuendelea kupata Huduma
Mwaka 2022, Iran ilipiga marufuku WhatsApp na Google Play wakati wa Maandamano makubwa ya kupinga Serikali yaliyotokana na kifo cha Mwanamke aliyekuwa ameshikiliwa na Polisi wa Maadili wa Nchi hiyo. Marufuku hiyo iliondolewa mwishoni mwa Mwaka 2024
Soma https://jamii.app/IranVSWhatsApp
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
Katika taarifa yake, Kampuni ya #Meta ambayo inamiliki WhatsApp imesema “Tunasikitishwa na ripoti hizi za uongo ambazo huenda zikatumiwa kama kisingizio cha kuzuiwa kwa Huduma zetu wakati Watu wanazihitaji zaidi.”
Serikali ya #Iran imekuwa ikizuia upatikanaji wa Mitandao mbalimbali ya Kijamii kwa Miaka mingi, lakini Watu wengi nchini humo hutumia mbinu za kukwepa vizuizi hivyo kama #proxies na Mitandao Binafsi ya Intaneti (VPNs) ili kuendelea kupata Huduma
Mwaka 2022, Iran ilipiga marufuku WhatsApp na Google Play wakati wa Maandamano makubwa ya kupinga Serikali yaliyotokana na kifo cha Mwanamke aliyekuwa ameshikiliwa na Polisi wa Maadili wa Nchi hiyo. Marufuku hiyo iliondolewa mwishoni mwa Mwaka 2024
Soma https://jamii.app/IranVSWhatsApp
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
❤1