MANYARA: Timu ya Singida Black Stars SC imeingia Fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB Bank, kwa kuichapa Simba SC Magoli 3-1, kwenye Uwanja Tanzanite Kwaraa katika Nusu Fainali
Singida imepata Magoli kipitia kwa Emmanuel Keyeke (35, 48) na Jonathan Sowah (17), huku Jean Ahoua akiifungia Simba goli pekee
Hivyo, mchezo wa Fainali unatarajiwa kuwa kati ya Yanga iliyoingia Fainali kwa kuifunga JKT Tanzania Magoli 2-0 dhidi ya Singida
Soma https://jamii.app/NusuFainali
#JFSports #JamiiForums
Singida imepata Magoli kipitia kwa Emmanuel Keyeke (35, 48) na Jonathan Sowah (17), huku Jean Ahoua akiifungia Simba goli pekee
Hivyo, mchezo wa Fainali unatarajiwa kuwa kati ya Yanga iliyoingia Fainali kwa kuifunga JKT Tanzania Magoli 2-0 dhidi ya Singida
Soma https://jamii.app/NusuFainali
#JFSports #JamiiForums
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Kamanda wa Polisi Kanda Maalum, Jumanne Muliro amesema Jeshi la Polisi linasubiri Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu (TEC), Padri Kitima apate nafuu kiafya kisha ndio watachukua maelezo ya tukio la kushambuliwa na kujeruhiwa lililotokea Aprili 30, 2025
Akizungumzia tukio hilo lililotokea kwenye makazi na Makao Makuu ya Baraza hilo, Kurasini, Muliro amesema ni jukumu la Kisheria kuhakikisha wanapata maelezo ya Padri Kitima ya Kimaandishi, ili yaende Ofisi ya Mashtaka kwa kuwa Askari Polisi walienda mara kadhaa kumuona lakini wakamkuta akiwa katika mazingira magumu ya kuumwa
Ikumbukwe, Padri Kitima inadaiwa alishambuliwa na kuumizwa kichwani ambapo Jeshi la Polisi lilisema linafanya uchunguzi na tayari linawashikilia Watu Wawili wakihusishwa na tukio hilo
Soma https://jamii.app/MuliroKuhusuKitima
#JamiiForums #Uwajibikaji #Accountability #HumanRights
Akizungumzia tukio hilo lililotokea kwenye makazi na Makao Makuu ya Baraza hilo, Kurasini, Muliro amesema ni jukumu la Kisheria kuhakikisha wanapata maelezo ya Padri Kitima ya Kimaandishi, ili yaende Ofisi ya Mashtaka kwa kuwa Askari Polisi walienda mara kadhaa kumuona lakini wakamkuta akiwa katika mazingira magumu ya kuumwa
Ikumbukwe, Padri Kitima inadaiwa alishambuliwa na kuumizwa kichwani ambapo Jeshi la Polisi lilisema linafanya uchunguzi na tayari linawashikilia Watu Wawili wakihusishwa na tukio hilo
Soma https://jamii.app/MuliroKuhusuKitima
#JamiiForums #Uwajibikaji #Accountability #HumanRights
❤3
Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Siasa amehoji kuwa tovuti ya Bunge inaonyesha Wasifu wa Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas kuwa alitumia Miaka Miwili (2010 na 2011) kusoma na kuhitimu masomo katika ngazi ya Shahada (Degree) na Master's Degree katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Anahoji “Hii inawezekanaje, wakati kwa kawaida Shahada pekee si chini ya Miaka mitatu? Ukiachana na hilo hata ngazi nyingine zote amesoma Mwaka mmoja mmoja, ni kwamba tovuti ndio imekosea au ni kweli alisoma hivyo mwaka mmoja mmoja?”
Soma https://jamii.app/MdauTarimba
#JamiiForums #Kuelekea2025 #Democracy
Anahoji “Hii inawezekanaje, wakati kwa kawaida Shahada pekee si chini ya Miaka mitatu? Ukiachana na hilo hata ngazi nyingine zote amesoma Mwaka mmoja mmoja, ni kwamba tovuti ndio imekosea au ni kweli alisoma hivyo mwaka mmoja mmoja?”
Soma https://jamii.app/MdauTarimba
#JamiiForums #Kuelekea2025 #Democracy
Akichangia katika Mjadala unaongazia jukumu la upatikanaji wa Intaneti katika kuvunja Unyanyapaa unaozunguka matatizo ya Afya ya akili, Ajimah Olaghere amesema “Mimi binafsi naamini katika nguvu ya Watu na suluhisho ninalopendekeza linaanzia kwa Watu wenyewe, kwa sababu hapo ndipo palipo na Upatikanaji halisi wa msaada.”
Ameongeza kwa kusema Elimu ya Afya ya Akili ni muhimu sana. Ingawa ana Elimu ya hali ya juu na uzoefu mkubwa, anajua hana maarifa ya kutosha kuhusu Afya ya Akili.
Aidha, amependekeza Mfumo wa "daraja" (bridge framework), ambao unasisitiza kuhusisha Jamii kwa karibu kwenda kwenye Asili, kuelewa jamii na Tamaduni zao na kujenga Madaraja ya mawasiliano na Msaada.
Zaidi https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF
#JamiiAfrica #AfIGF2025 #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
Ameongeza kwa kusema Elimu ya Afya ya Akili ni muhimu sana. Ingawa ana Elimu ya hali ya juu na uzoefu mkubwa, anajua hana maarifa ya kutosha kuhusu Afya ya Akili.
Aidha, amependekeza Mfumo wa "daraja" (bridge framework), ambao unasisitiza kuhusisha Jamii kwa karibu kwenda kwenye Asili, kuelewa jamii na Tamaduni zao na kujenga Madaraja ya mawasiliano na Msaada.
Zaidi https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF
#JamiiAfrica #AfIGF2025 #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
❤1
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Ufaransa ‘Ligue 1’, Paris Saint-Germain (#PSG) wameonesha huu ni mwaka wao, kwa kubeba taji la #UEFAChampionsLeague (Ligi ya Mabingwa Ulaya), pia kushusha kipigo Kizito kwa #InterMilan ya Italia, Magoli 5-0
PSG inayonolewa na Kocha Luis Enrique, imebeba taji hilo kwa magoli ya Achraf Hakimi (12), Désiré Doué (20, 63), Khvicha Kvaratskhelia (73) na Senny Mayulu (86)
Huo unakuwa ubingwa wa kwanza kwa timu ya Ufaransa katika michuano hiyo
Soma https://jamii.app/UEFAFinal25
#JFSports #JamiiForums
PSG inayonolewa na Kocha Luis Enrique, imebeba taji hilo kwa magoli ya Achraf Hakimi (12), Désiré Doué (20, 63), Khvicha Kvaratskhelia (73) na Senny Mayulu (86)
Huo unakuwa ubingwa wa kwanza kwa timu ya Ufaransa katika michuano hiyo
Soma https://jamii.app/UEFAFinal25
#JFSports #JamiiForums
🔥1
Akizungumza katika Siku ya Mwisho ya Mkutano wa Jukwaa la Utawala wa Intaneti Afrika, jana Mei 31, 2025, Daktari John Weilsh alisema tunaweza kutumia Mitandao ya Kijamii, sababu ya uwezo wake wa kuunganisha Watu kupitia intaneti, si tu katika Jamii za Nyumbani bali muhimu zaidi Kimataifa
Alisema eneo mojawapo lenye uwezekano mkubwa wa mafanikio ni kuhimiza ushirikiano kati ya Wataalamu wa tiba hapa Tanzania au Kenya, na Watafiti katika Nchi nyingine wanaojaribu sio tu kushughulikia matatizo ya Afya ya Akili kwa kutumia Teknolojia tulizonazo sasa, bali pia kufikiria Teknolojia za baadaye zitakazokuwa na ufanisi zaidi kupitia mbinu za Akili Mnemba (AI)
Aliongeza "Naamini katika kuunganisha maarifa yetu ya pamoja na ya kipekee ili kujenga jamii ya pamoja ya wataalamu wa Sayansi ya Neva (Neuroscience) na Akili (Neuropsychiatry), kwaajili ya kushughulikia changamoto za Afya ya Akili zinazoathiri jamii katika Mataifa mbalimbali"
Zaidi https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF
#JamiiAfrica #AfIGF2025 #DigitalRights
Alisema eneo mojawapo lenye uwezekano mkubwa wa mafanikio ni kuhimiza ushirikiano kati ya Wataalamu wa tiba hapa Tanzania au Kenya, na Watafiti katika Nchi nyingine wanaojaribu sio tu kushughulikia matatizo ya Afya ya Akili kwa kutumia Teknolojia tulizonazo sasa, bali pia kufikiria Teknolojia za baadaye zitakazokuwa na ufanisi zaidi kupitia mbinu za Akili Mnemba (AI)
Aliongeza "Naamini katika kuunganisha maarifa yetu ya pamoja na ya kipekee ili kujenga jamii ya pamoja ya wataalamu wa Sayansi ya Neva (Neuroscience) na Akili (Neuropsychiatry), kwaajili ya kushughulikia changamoto za Afya ya Akili zinazoathiri jamii katika Mataifa mbalimbali"
Zaidi https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF
#JamiiAfrica #AfIGF2025 #DigitalRights
❤1
Leo hii, tunaishi katika dunia ambayo si kila mmoja anapata haki au fursa sawa. Wapo wanaokumbwa na changamoto kwasababu ya jinsia, ulemavu, hali ya kiuchumi au mazingira waliyozaliwa. Wanaweza wasiwe na jukwaa la kujisemea, lakini wewe unalo. Wanaweza wasisikike, lakini wewe unasikika.
Sauti yako inaweza kuwa faraja, kinga, au dira kwa mwingine. Tuchague kuwa watu wanaojali. Tuchague kuungana kwa ajili ya haki, utu na usawa. Kwasababu, kuijenga jamii salama na yenye haki, ni jukumu letu sote
#JamiiForums #JamiiAfrica #SocialJustice #Demokrasia #Uwajibikaji
Sauti yako inaweza kuwa faraja, kinga, au dira kwa mwingine. Tuchague kuwa watu wanaojali. Tuchague kuungana kwa ajili ya haki, utu na usawa. Kwasababu, kuijenga jamii salama na yenye haki, ni jukumu letu sote
#JamiiForums #JamiiAfrica #SocialJustice #Demokrasia #Uwajibikaji
RUVUMA: Mdau wa JamiiForums.com ametoa wito kwa Mmalaka husika kurekebisha mazingira ya Vyoo vya Shule ya Msingi Miembeni, iliyo Kata ya Msamala, Manispaa ya Songea
Amedai hali ya uchafu wa Vyoo hivyo, inaweza kusababisha mlipuko wa Magonjwa, hivyo kuhatarisha afya za Walimu na Wanafunzi wa Shule hiyo
Soma https://jamii.app/ShuleYaMiembeni
#JamiiForums #PublicHealth #Afya #ServiceDelivery #Accountability #Uwajibikaji
Amedai hali ya uchafu wa Vyoo hivyo, inaweza kusababisha mlipuko wa Magonjwa, hivyo kuhatarisha afya za Walimu na Wanafunzi wa Shule hiyo
Soma https://jamii.app/ShuleYaMiembeni
#JamiiForums #PublicHealth #Afya #ServiceDelivery #Accountability #Uwajibikaji
❤2
Mwongoza Mjadala ulioangazia jukumu la upatikanaji wa Intaneti katika kuvunja Unyanyapaa unaozunguka matatizo ya Afya ya akili, Mary Uduma amesema Kwa upande wa Sera, hatupaswi kuwaangalia Watu walio kwenye Changamoto za Kiakili kama Wahalifu. Tunahitaji sera zinazoweka Watu kwenye Huduma na si kuwaweka Gerezani au kuwafungia.
Amesema "Tunahitaji Haki inayoponya (Restorative Justice), ambayo ni sehemu ya Utamaduni wetu wa Kiafrika, kushirikiana kama Jamii, Kusamehe, na Kuponya.”
Ameongeza "Elimu ya Afya ya Akili ni muhimu. Wengi wetu, hata walioelimika, hatujui Changamoto ya Afya ya Akili inavyoonekana. Tunahitaji kufundishwa jinsi ya kutambua, kupokea, na kuwahudumia wanaopitia. Na haya yote yanaanza na kusikiliza hadithi kama ya Doris, kujifunza kutoka kwenye uzoefu wa kweli.
Zaidi https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF
#JamiiAfrica #AfIGF2025 #MaendeleoYaKidijitali #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
Amesema "Tunahitaji Haki inayoponya (Restorative Justice), ambayo ni sehemu ya Utamaduni wetu wa Kiafrika, kushirikiana kama Jamii, Kusamehe, na Kuponya.”
Ameongeza "Elimu ya Afya ya Akili ni muhimu. Wengi wetu, hata walioelimika, hatujui Changamoto ya Afya ya Akili inavyoonekana. Tunahitaji kufundishwa jinsi ya kutambua, kupokea, na kuwahudumia wanaopitia. Na haya yote yanaanza na kusikiliza hadithi kama ya Doris, kujifunza kutoka kwenye uzoefu wa kweli.
Zaidi https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF
#JamiiAfrica #AfIGF2025 #MaendeleoYaKidijitali #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
DAR: Mdau wa JamiiForums.com anasema licha ya umuhimu wa ujenzi wa Miradi ya Barabara, kujengwa kwa wakati mmoja kumechangia foleni ambayo imekuwa ni usumbufu kwa Watu wengi, akishauri ilitakiwa kuwe na mpango mbadala wa kupunguza au kukwepa changamoto hiyo, katika Jiji ambalo lina purukushani nyingi
Anatoa mfano maeneo ambayo yana changamoto ya foleni kubwa kutokana na ujenzi ni Barabara ya Tegeta - Mwenge, Mwenge - Morocco, Morocco - Posta, Posta Kisutu - Mnazi Mmoja, Ubungo - Mwenge, Kimara - Ubungo, Buguru – Kariakoo, TAZARA - Gongo la Mboto n.k
Mdau anadai sehemu ya kutumia nusu saa au dakika 45 kwa gari sasa hivi inaweza kutumika Dakika 120 hadi 180, anaamini Mamlaka husika zilitakiwa kuwa na mbinu mbadala kabla ya kufanya utekelezaji wa hicho kinachoendelea ambacho kina muhimu pia
Soma https://jamii.app/UjenziBarabaraDar
#JamiiForums
Anatoa mfano maeneo ambayo yana changamoto ya foleni kubwa kutokana na ujenzi ni Barabara ya Tegeta - Mwenge, Mwenge - Morocco, Morocco - Posta, Posta Kisutu - Mnazi Mmoja, Ubungo - Mwenge, Kimara - Ubungo, Buguru – Kariakoo, TAZARA - Gongo la Mboto n.k
Mdau anadai sehemu ya kutumia nusu saa au dakika 45 kwa gari sasa hivi inaweza kutumika Dakika 120 hadi 180, anaamini Mamlaka husika zilitakiwa kuwa na mbinu mbadala kabla ya kufanya utekelezaji wa hicho kinachoendelea ambacho kina muhimu pia
Soma https://jamii.app/UjenziBarabaraDar
#JamiiForums
❤3
Dar: Kesi ya jinai namba CC 32444/24 inayomkabili Saleh Ayoub (39), Mwalimu wa Shule ya Msingi Green Acres iliyopo Mbezi Africana, imeendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni.
Saleh Ayoub anatuhumiwa kumlawiti Mwanafunzi wa Kiume mwenye umri wa Miaka 11, ambapo shauri hilo lilitajwa tena Mahakamani Mei 27, 2025, lakini liliahirishwa hadi Juni 19, 2025 kwaajili ya Mshtakiwa kuanza kujitetea.
Awali, kesi hiyo ilipangwa kuendelea Mei 21, 2025, lakini ilishindikana kusikilizwa katika hatua hiyo, baada ya Wakili wa Mshtakiwa kutoonekana Mahakamani.
Upande wa Jamhuri tayari umefunga ushahidi wake kwa kuwasilisha mashahidi Wanne kati ya 6 waliopangwa na kielelezo kimoja.
Shauri hilo lilifikishwa Mahakamani Novemba 12, 2024, baada ya Mdau wa JamiiForums.com kuchapisha hoja iliyosomeka: “Walimu wa Shule ya Green Acres (Dar) wanaotuhumiwa kulawiti na kuwadhalilisha Wanafunzi, wanalindwa na nani?”
Soma https://jamii.app/KesiMwendelezo
#JFMatukio #JamiiForums #HumanRights #Accountability
Saleh Ayoub anatuhumiwa kumlawiti Mwanafunzi wa Kiume mwenye umri wa Miaka 11, ambapo shauri hilo lilitajwa tena Mahakamani Mei 27, 2025, lakini liliahirishwa hadi Juni 19, 2025 kwaajili ya Mshtakiwa kuanza kujitetea.
Awali, kesi hiyo ilipangwa kuendelea Mei 21, 2025, lakini ilishindikana kusikilizwa katika hatua hiyo, baada ya Wakili wa Mshtakiwa kutoonekana Mahakamani.
Upande wa Jamhuri tayari umefunga ushahidi wake kwa kuwasilisha mashahidi Wanne kati ya 6 waliopangwa na kielelezo kimoja.
Shauri hilo lilifikishwa Mahakamani Novemba 12, 2024, baada ya Mdau wa JamiiForums.com kuchapisha hoja iliyosomeka: “Walimu wa Shule ya Green Acres (Dar) wanaotuhumiwa kulawiti na kuwadhalilisha Wanafunzi, wanalindwa na nani?”
Soma https://jamii.app/KesiMwendelezo
#JFMatukio #JamiiForums #HumanRights #Accountability
❤3
UPDATES: Jana, Mei 31, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alidokeza kuwa tovuti ya Bunge ilikuwa ikionesha Mbunge wa Kinondoni, Tarimba Gulam Abbas alitumia Miaka Miwili (2010 na 2011) kusoma na kuhitimu Shahada (Degree) na Shahada ya Uzamili (Master's Degree) katika Chuo Kikuu cha Dar (UDSM), leo Juni 1, 2025 tovuti hiyo imehariri baadhi ya taarifa
Tovuti ya Bunge imeondoa taarifa za awali za Tarimba kusoma UDSM badala yake sasa inaonyesha alipata Shahada ya Sheria (LLB) katika Chuo Kikuu cha Tumaini (2007 – 2010)
Hata hivyo, taarifa nyingine zilizozua gumzo mtandaoni hazijabadilika, ikiwemo Stashahada aliyoipata Mwaka 1981 katika Chuo cha “Tanzania of Journalism”, pia taarifa za kusoma Diploma nchini Benin (mwaka usiojulikana)
Soma https://jamii.app/TarimbaUpdates
#JamiiForums #Kuelekea2025 #Democracy #Accountability
Tovuti ya Bunge imeondoa taarifa za awali za Tarimba kusoma UDSM badala yake sasa inaonyesha alipata Shahada ya Sheria (LLB) katika Chuo Kikuu cha Tumaini (2007 – 2010)
Hata hivyo, taarifa nyingine zilizozua gumzo mtandaoni hazijabadilika, ikiwemo Stashahada aliyoipata Mwaka 1981 katika Chuo cha “Tanzania of Journalism”, pia taarifa za kusoma Diploma nchini Benin (mwaka usiojulikana)
Soma https://jamii.app/TarimbaUpdates
#JamiiForums #Kuelekea2025 #Democracy #Accountability
❤1
#JFKumbukizi: Aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dkt. Charles Kimei alinukuliwa na Gazeti la Mwananchi, Machi 2018, akieleza kuwa kuanzishwa kwa Tawi la Benki hiyo Wilayani Chato haikuwa kutokana na kujiridhisha kwa Menejimenti, bali shinikizo la Rais John Magufuli kuanzia alipokuwa Waziri
Dkt. Kimei alieleza aliwatuma Wasaidizi wake kwenda Chato kujiridhisha na majibu yakawa Uchumi wa Chato haukushawishi kufungua tawi la benki hiyo, lakini Magufuli aligoma na akamwambia “Vijana wako hawajui kufanya utafiti. Nitafanya utafiti wangu.”
Soma https://jamii.app/CRDBKumbukizi
#JFKumbukizi #JamiiForums
Dkt. Kimei alieleza aliwatuma Wasaidizi wake kwenda Chato kujiridhisha na majibu yakawa Uchumi wa Chato haukushawishi kufungua tawi la benki hiyo, lakini Magufuli aligoma na akamwambia “Vijana wako hawajui kufanya utafiti. Nitafanya utafiti wangu.”
Soma https://jamii.app/CRDBKumbukizi
#JFKumbukizi #JamiiForums
❤3👍1😁1
Pyramids ya Misri imekuwa Bingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika (#CAFChampionsLeague) 2024/25 kwa kuifunga #MamelodiSundowns ya Afrika Kusini Magoli 2-1 katika Fainali ya pili, hivyo kubeba taji kwa jumla ya Magoli 3-2 kwa kuwa Fainali ya kwanza, matokeo yalikuwa sare ya 1-1
Pyramids imepata Magoli yake kupitia kwa #FistonMayele dakika ya 23 na Ahmed Samy (56), wakati Mamelodi ilifunga kupitia kwa Iqraam Rayners (75), Mchezo ukichezwa kwenye Uwanja wa 30 June Jijini #Cairo
Soma https://jamii.app/PyramidsWinner
#JFSports #JFCAFCL25 #JamiiForums
Pyramids imepata Magoli yake kupitia kwa #FistonMayele dakika ya 23 na Ahmed Samy (56), wakati Mamelodi ilifunga kupitia kwa Iqraam Rayners (75), Mchezo ukichezwa kwenye Uwanja wa 30 June Jijini #Cairo
Soma https://jamii.app/PyramidsWinner
#JFSports #JFCAFCL25 #JamiiForums