JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
DAR: Wananchi wamejitokeza kwa wingi leo Mei 19, 2025 katika Mahakama ya Kisutu kufuatilia kesi inayomkabili Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu

Ulinzi umeimarishwa Mahakamani hapo ambapo kuna idadi kubwa ya Askari Polisi na Askari wa Jeshi la Magereza

Awali, kesi hiyo iliendeshwa kwa njia ya Mtandao, Mei 6, 2025 Mahakama iliruhusu Umma kuhudhuria kesi hiyo ambapo Lissu anakabiliwa na tuhuma za Uhaini na Kutoa Taarifa za Uongo

Soma https://jamii.app/KesiYaLissuLeo

#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025 #CitizenParticipation #Transparency
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu alivyowasili ndani ya Mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kuanzia kusikiliza kesi zinazomkabili, leo Mei 19, 2025

Soma https://jamii.app/KinachojiriKesiLissu

#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
🔥2👎1
DAR: Upande wa Jamhuri umeieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa shauri la kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Wakili Tundu Lissu haujakamilika hivyo kuomba kesi hiyo ihairishwe hadi Juni 02, 2025

Aidha, Jopo la Mawakili wa utetezi likiongozwa na Mawakili Mpale Mpoki, Dkt. Rugemeleza Nshala na Peter waliwasilisha maombi Mahakamani ikiwemo kuomba Mahakama 'kulazimisha' upande wa Jamhuri ueleze nini hasa kinachokwamisha upelelezi kwa sababu mwanzo ilidaiwa Mahakamani hapo kuwa ushahidi wote kuhusiana na shauri hilo upo mtandaoni

Mawakili wa Serikali upande wa Jamhuri wamejibu kuwa hakuna sehemu yoyote ya Kisheria na Kikatiba inayowalazimisha kueleza hatua ya upelelezi waliyofikiwa na kwamba mambo ya upelelezi sio ya kuwekwa hadharani

Soma https://jamii.app/KesiLissuKusogezwa

#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
2👏1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Jopo la Mawakili wa utetezi likiongozwa na Mawakili Waandamizi Mpale Mpoki, Dkt. Rugemeleza Nshala na Peter Kibatala wamewasilisha ombi Mahakamani kutoa amri ya kuwaondoa Askari wote 'wanaomlinda' mteja wao, Tundu Lissu ndani ya chumba cha Mahakama

Mawakili hao wamedai kuwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, Mahakama haimtambui mtuhumiwa kama 'mkosaji' na kwamba kitendo cha mteja wao kuzungukwa na Askari wengi hakikubaliki

Aidha, upande wa Jamhuri umeieleza Mahakama kuwa licha ya kwamba Katiba imeeleza hivyo lakini haijatoa maelekezo ya aina gani ya ulinzi unahitajika kwa mtuhumiwa na kwamba ikiwezekana wanaomba ulinzi huo uongezwe kwani suala la ulinzi lina faida kwa mtuhumiwa mwenyewe, Mahakama na Maafisa wa Mahakama kwa ujumla

Soma https://jamii.app/KesiLissuKusogezwa

#JamiiForums #Siasa #Democracy #Kuelekea2025
1
Kitambulisho chako (ID) kinachukuliwa kuwa Taarifa Binafsi kwasababu kina taarifa zako kama Jina, Nambari ya Utambulisho, Picha, Tarehe ya Kuzaliwa, n.k.

Unamshauri Mdau afanye nini hapo?

Mjadala zaidi https://jamii.app/MkopoSimuKitambulisho

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #PersonalDataProtection #DataPrivacy
DAR: Aliyekuwa Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA, John Mrema, Mwenyekiti wa chama hicho Kanda ya Kati, Devotha Minja, aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu Bara, Benson Kigaila, Salum Mwalimu na Makada wengine waliotangaza kujiondoa CHADEMA wameonekana wakishiriki kwenye shughuli za Chama cha Ukombozi wa Umma (#CHAUMMA)

Tukio hilo limefanyika katika Ukumbi wa Golden Tulip, panakofanyika Mkutano Mkuu wa CHAUMMA, leo Mei 19, 2025

Zaidi https://jamii.app/G55WatuaCHAUMMA

#JamiiForums #JamiiAfrica #Kuelekea2025 #Demokrasia #Governance
1👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mwanachama wa JamiiForums.com anasema Magari makubwa ya Mizigo kuruhusiwa kupita katika Barabara za Juu (Flyovers) inaweza kuleta Changamoto pale itakapotokea hitilafu kwenye Gari hilo na Madhara yanaweza kuwa makubwa

Anahoji je, tunasubiri Madhara yatokee ili tuunde Kamati?

Soma https://jamii.app/BarabaraZaJuu

#Accountability #JamiiForums #JamiiAfrica #Uwajibikaji #JFMdau2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Akizungumza leo kwenye Uzinduzi wa Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001, Rais Samia amesema "Nimeona mtiririko wa Wanaharakati katika Ukanda wetu huu kuanza kuvamia na kuingilia mambo yetu. Sasa kama kwao wameshadhibitiwa wasije kutuharibia huku"

Ameyasema hayo leo Mei 19, 2025 katika Ukumbi wa JNICC Jijini Dar Es Salaam.

Soma https://jamii.app/WanaharakatiKudhibitiwa

#JamiiForums #Kuelekea2025 #Diplomasia
DAR: Kufuatia makubaliano yanayoendelea kati ya #CHAUMMA na makada waliotoka #CHADEMA, Hashim Rungwe anaendelea kuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Makamu wake (Bara) anakuwa aliyekuwa Mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Kati, Devotha Minja

Aidha, nafasi ya Katibu Mkuu amepewa Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu Bara amepewa Benson Kigaila, upande wa Zanzibar, Naibu Katibu Mkuu amekuwa Mohamed Masoud

Mgawanyo huo umekuja baada ya waliokuwa Viongozi wa #CHAUMMA kujiuzulu nafasi zao leo Mei 19, 2025 akiwemo aliyekuwa Katibu Mkuu, Mohammed Masoud Rashid, Naibu Katibu Mkuu Bara, Rahman Rungwe na Makamu Mwenyekiti Bara, Kayungo Mohammed

Zaidi https://jamii.app/G55WalambaVyeo

#JamiiForums #KuelekeaUchaguzi2025 #Governance
1
DODOMA: Rais Samia amesema kutokujitokeza kujiandikisha au kuhuisha taarifa zako katika Daftari la Kudumu la Mpiga Kura ni sawa na Mtu kukataa Haki yake ya Kikatiba kwa hiari, jambo ambalo siyo Uzalendo

Akiyasema hayo Mei 17, 2025 ameeleza "Kutokujitokeza kujiandikisha ni kukataa mwenyewe Haki yako ya Kikatiba na unapokataa Haki ya Kikatiba jiulize je, wewe ni Mzalendo? Mzalendo wa aina gani ambaye Katiba imekupa fursa nenda kajiandikishe, piga kura, weka Kiongozi unayehisi atakuja kukuhudumia, wewe unaikataa, ukiikataa wenzio wataenda kuweka wanayemtaka na utakosa fursa ya kushawishi wengine kuweka yule mnayemtaka, kwahiyo unakuwa wewe wa kubabaisha tu na kulalamika."

Soma https://jamii.app/SamiaKajiandikishe

#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #Democracy #UchaguziMkuu2025 #TanzaniaElection2025
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Rais Samia amesema "Nimeona Clip kadhaa za kunisema, mara nina ubaguzi na nini! Ninalofanya ni kulinda Nchi yangu na ndiyo wajibu wangu niliopewa. Kwa hiyo hatutatoa nafasi kwa kiumbe yeyote kutuvuruga awe ndani ama anayetoka nje."

Ameyasema hayo wakati wa Uzinduzi wa Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001, Mei 19, 2025

Soma https://jamii.app/ClipMnanisema

#JamiiForums #Kuelekea2025 #Governance
👍3
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Rais Samia ameelekeza Mamlaka mbalimbali ikiwemo za Usalama na Wizara ziwe zinatoa majibu, ufafanuzi au kuelezea hoja zinazotolewa dhidi ya Nchi au Serikali, ili Jamii iwe na uelewa sahihi wa yanayoendelea

Ametoa maelekezo hayo wakati wa Uzinduzi wa Sera ya Mambo ya Nje ya Mwaka 2001, Mei 19, 2025 katika Ukumbi wa JNICC

Soma https://jamii.app/WanaharakatiKudhibitiwa

#JamiiForums #Kuelekea2025 #Diplomasia #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
KUMBUKIZI: Mwenyekiti wa #CHAUMMA, Hashim Spunda Rungwe alisema haya Aprili 20, 2024, akiwa katika kipindi cha Medani za Siasa kinachoendeshwa na Chief Odemba

Zaidi https://jamii.app/HelaZaCCM

#JamiiForums #Governance #Accountability #KuelekeaUchagua2025 #JFKumbukizi
1👍1
Mwandishi wa Andiko la Shindano la Stories of Change 2021 anasema kuna wizi unaofanywa na Taasisi za Fedha kupitia mikopo inayoitwa Top Up, hii ni Mikopo ambayo Mkopaji anakuwa na Deni lingine analoendelea kulipa, anapewa mkopo mwingine juu ya ule mkopo wa awali

Anadai mpaka sasa hakuna Sera wala Sheria yoyote inayomlazimisha Mwajiri kuboresha maslahi ya Mtumishi wake, bali kilichopo ni kama hiari kwa Mwajiri jambo linalosababisha Watumishi wengi kukimbizana na Mikopo ya hapa na pale inayowaongezea ugumu wa Maisha

Unakubaliana na hoja ya Mdau huyu?

Soma zaidi https://jamii.app/MikopoWatumishiSOC1

#JamiiForums #JamiiAfrica #Maisha #SOC2021
👍1