JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi amemtangaza Rashid Mijuza kuwa Kaimu Meneja wa Uwanja wa Benjamin Mkapa huku aliyekuwa Meneja wa Uwanja huo, Malinde Mahona amepelekwa Makao Makuu ya Wizara hiyo kuwa Msimamizi wa viwanja vyote nchini

Kabudi amesema hayo Mei 10, 2025 alipokagua Uwanja huo na Viwanja vya Mazoezi ya CHAN 2024 ambapo pia amesema nyasi za uwanja huo zipo tayati kwa mchezo wa Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kati ya Simba dhidi ya RS Berkane ya Morocco

Ikumbukwe, Aprili 7, 2025, baadhi ya waliojitambulisha kuwa ni Wazee wa Klabu ya Simba walimlalamikia Mahona kuwa amewazuia kuingia uwanjani wakati timu yao ikijiandaa kucheza dhidi ya Al Masry ya Misri, hivyo wakashinikiza Meneja huyo awapishe hali ambayo ilizua sintofahamu kwa muda

Soma https://jamii.app/MkapaStadiumUpdates

#JFSports #JamiiForums #JamiiAfrics
2
Ukimuuliza Mtanzania kuhusu Nchi za #Nordic, yaani Sweden, Norway, Denmark, Finland au Iceland, wengi watasema: “Aaah zile nchi za maisha bora! Kule hakuna rushwa! Elimu ni bure na watu wao wana furaha kweli kweli”

Lakini, ni hayo tu unayoyajua?

Je, unajua uhusiano wao na Afrika ukoje? Wanavyotumia teknolojia kusaidia jamii? Tamaduni zao za kipekee? Au ushirikiano wao wa kimataifa unaoleta maendeleo ya kijamii?

Ni muda wa kuonesha maarifa yako. Bofya link na uone ni kwa kiasi gani unaelewa kuhusu Nchi za Nordic:

https://jamii.app/NordicDodoso

#JamiiAfrica #JamiiForums #NordicWeek
👍1
DAR: Magoli yaliyofungwa na Steven Mukwala yameiwezesha Timu ya #Simba kupata ushindi wa 2-1 dhidi ya #KMCFC ambayo imepata goli kupitia kwa Rashid Chambo katika Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa KMC

Ushindi huo unaifanya Simba ifikishe alama 69 ikiwa nafasi ya pili kwenye Msimamo wa Ligi nyuma ya Yanga yenye pointi 70, timu zote hizo mbili zikiwa zimecheza michezo 26

Upande wa KMC imesalia katika nafasi ya 11 ikiwa na alama 30 katika michezo 27

Soma https://jamii.app/KMCSimbaDar

#JFSports #JamiiForums #JFLigiKuu25
👍1
HISPANIA: Timu ya #Barcelona imeifunga Real Madrid Magoli 4-3, ushindi unaoifanya ifikishe pointi 82 ikiwa na maana inahitaji alama 2 katika michezo mitatu iliyosalia kutwaa Ubingwa wa Ligi Kuu ya Hispania (#LaLiga), Madrid ikibaki nafasi ya pili kwa kuwa na pointi 75

Licha ya kupoteza #KylianMbappé ameifungia #RealMadrid magoli yote matatu (hat trick) na kushika nafasi ya kwanza ya Wafungaji wa LaLiga akifikisha magoli 27

Matokeo hayo yanaifanya Madrid kuwa imefungwa mara nne mfululizo msimu huu, michezo iliyopita; Barcelona 3-2 Real Madrid (Copa de Rey), Real Madrid 2-5 Barcelona (Super Cup) na Real Madrid 0-4 Barcelona (LaLiga)

Soma https://jamii.app/ElClasico25

#JFSports #JamiiForums #JFLaLiga25
👎1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mdau wa JamiiForums.com anaeleza ili kupunguza changamoto ya foleni katika maeneo mbalimbali ya Jiji, Chama cha Mapinduzi (#CCM) kiliwahi kunukuliwa kuwa kwa kuwa chenyewe kimeshika dola, mpango uliopo kwenye Ilani yao ni kujenga/kukamilisha barabara za juu (flyovers) kwenye makutano kadhaa ya barabara

Anasema baadhi ya maeneo yaliyoanishwa ni makutano ya Changombe, Kamata, Uhasibu, Morocco, Mwenge, Magomeni, Tabata, Fire, Makutano ya Ally Hassan Mwinyi na United Nation, Makutano ya Ally Hassan Mwinyi na Kinondoni

Mdau anakumbushia kuwa aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM, Humphrey Polepole pia alizungumzia mipango hiyo, hivyo anahoji michakato hiyo iliishia wapi?

Soma https://jamii.app/FlyOverDar

#JamiiForums #Accountability #JFHuduma
1👎1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Mabasi ya Mwendokasi (UDART), Waziri Kindamba amekiri kuwa usafiri wa Mwendokasi umekuwa changamoto na kero kwa Watumiani wengi, ndio maana hatua zimechukuliwa ikiwemo kuongeza mabasi mapya ya Kisasa 99

Ameeleza wameelemewa na mabasi chakavu na machache hali iliyosababisha kuagiza Mabaso 100 kutoka China na tayari moja limewasili likitumia gesi asilia, linabeba abiria 155 na linatarajiwa kuanza safari Jumatatu Mei 12, 2025 njia ya Morocco -Kivukoni

Mara kadhaa Wadau wa JamiiForums.com wamekuwa wamelalamikia changamoto mbalimbali za huduma ya usafiri huo, baadhi walisema mradi unazidiwa na wingi wa Wateja kuliko uwezo wa mabasi

Soma https://jamii.app/KindambaMwendokasi

#JamiiForums #ServiceDelivery #JFAccountability
👍4
Kusoma kwa undani habari hizi na nyingine zilizojiri juma lililopita bofya https://jamii.app/YaliyojiriJumaLililopita

#JamiiForums #YaliyojiriJumaLililopita #JFToons
👍1
MWANZA: Mdau anasema Mwanzoni mwa Machi, 2025, kuna Mdau alihoji kuhusu Meli ya New MV Victoria kutofanya kazi na Mamlaka kutotoa muongozo wowote, baadaye Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) ikaeleza kuwa Meli ipo katika ‘service’ ya kawaida na inatarajia kurejea kazini ndani ya wiki tatu hadi Siku 30

Mdau anadai kufikia Mei 11, 2025, miezi miwili imekatika meli haijarejea na hakuna tamko lingine kuhusu kinachoendelea

Anatoa wito kwa TASHICO kujitokeza na kueleza kinachoendelea kwa kuwa ukimya wao unawaumiza wengi

Soma https://jamii.app/MvVictoriaMay

#JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
KILIMANJARO: Mkuu wa Shule ya Polisi Tanzania – Moshi (TPS), SACP Ramadhani A. Mungi amesema “Kundi la Vijana ndilo la uzalishaji, maendeleo ya Taifa hili yanatokana na Vijana kwa kuwa wao ndio wachapakazi, wana nguvu kubwa za mwili na akili, shughuli zote Kiuchumi asilimia kubwa zinaendeshwa na Vijana.”

Amesema hayo alipokuwa TPS wakati wa Ufunguzi wa Mafunzo ya Medani za Kivita kwa Wanafunzi wa mafunzo ya Awali Kambi ya Kamba Pori, Mei 6, 2025.

Soma https://jamii.app/NukuuYaMungi

#JamiiForums #JFNukuu #JFQuote #Governance
👍4
UCHAMBUZI: Mei 10, 2025, Chama cha #ACTWazalendo kilichambua Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (#CAG) Mwaka 2023/24 na kutoa mapendekezo kadhaa na hatua za kuchukuliwa na Serikali

Sehemu ya mapendekezo hayo ni kuwa “Tunasisitiza kwamba Serikali ihakikishe kwamba mfumo wake wa kielektroniki unafanya kazi wakati wote na maeneo yote na kuweka utaratibu wa kutokuruhusu miamala kufanyika nje ya mifumo hiyo.”

Mengine ni “Tunasisitiza Viongozi, Wawakilishi, Vyama vya Siasa, Wadau wa Maendeleo na Wananchi kuhakikisha wanakata mirija ya ubadhirifu ili kuhakikisha kunakuwepo na ustawi wa kweli wa Watu.”

Soma https://jamii.app/CAGUchambuziACT

#JamiiForums #Governance #Accountability #Uwajibikaji #CAGReport2025 #RipotiCAG2025
👍1
Mdau, ni kitu gani kikiboreshwa katika mfumo wa Uchaguzi kitakufanya ujisikie huru na tayari kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025

Kutoa maoni na mapendekezo yako, usikose kujiunga nasi katika Mjadala muhimu kuelekea Uchaguzi Mkuu kupitia #XSpace ya JamiiForums, Mei 12, 2025, Saa 12:00 jioni – 2:00 usiku

Bofya hapa kujiunga: https://jamii.app/ReformsSpace

Tafadhali 'share link' hii na yeyote ambaye hutamani apitwe na Mjadala huu

#ReformsSpace #Uchaguzi2025 #Demokrasia #Uwajibikaji #FreeAndFairElections #Kuelekea2025
1👍1
UCHAMBUZI: Chama cha #ACTWazalendo kikichambua Ripoti ya CAG Mwaka 2023/24, kimesema Deni la Taifa limepanda kufikia Tsh. Trilioni 97.35 kutoka Tsh. Trilioni 82.25 Mwaka uliopita, hilo ni ongezeko la zaidi ya Tsh. Trilioni 15, hali hiyo inaweka hatari mustakabali wa Taifa kwa kuwa baadhi ya viashiria kama “uwiano wa kulipa deni kwa mapato” vinakaribia ukomo wa hatari uliowekwa na taasisi za kimataifa

ACT imesema kuwa ripoti ya #CAG imeonesha uwiano wa kulipa deni kwa mapato ya ndani umefikia 14.5%, ukikaribia kikomo cha tahadhari cha 18%, pia uwiano wa kulipa deni kwa mauzo ya nje ni 11.7%, ukielekea ukomo wa hatari wa 15%

ACT imeongeza "Maana yake, sehemu kubwa ya mapato ya Serikali inaishia kulipa madeni badala ya kuendeleza huduma kwa Wananchi. Mapato ya Serikali kwa Januari 2025, kwa Mfano ilikusanya Tsh. Trilioni 2.63 katika makusanyo hayo Serikali ilitumia Tsh. Trilioni 1.2 kulipia huduma ya deni"

Soma https://jamii.app/CAGUchambuziACT

#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #CAGReport2025
👍2