Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Waziri wa Madini, Anthony Mavunde amesema Kampuni 95 zilizopewa Leseni za Uchimbaji Madini na hazijafanyiwa kazi inavyotakiwa atazifutia Leseni hizo
Amesema hayo, leo Mei 6, 2025 bila kutaja majina ya wawekezaji hao na kwamba Wizara yake imetoa siku 30 kwa wahusika kujieleza na kama hakutakuwa na mrejesho sahihi Leseni zitafutwa hata kama zina majina ya 'Watu wakubwa'
Soma https://jamii.app/MavundeLeseni
#Uwajibikaji #Accountability #JamiiForums
Amesema hayo, leo Mei 6, 2025 bila kutaja majina ya wawekezaji hao na kwamba Wizara yake imetoa siku 30 kwa wahusika kujieleza na kama hakutakuwa na mrejesho sahihi Leseni zitafutwa hata kama zina majina ya 'Watu wakubwa'
Soma https://jamii.app/MavundeLeseni
#Uwajibikaji #Accountability #JamiiForums
😁1
UTEUZI: Rais Samia amemteua Lazaro Jacob Twange kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), akichukua nafasi hiyo baada ya aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji, Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga, kufariki kwa ajali Mkoani Mara usiku wa kuamkia Aprili 13, 2025
Kabla ya uteuzi huo Twange alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, ambapo nafasi hiyo itashikwa na Albert Gasper Msando akitokea Wilaya ya Handeni
Soma https://jamii.app/TwangeEDmpyaTanesco
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
Kabla ya uteuzi huo Twange alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, ambapo nafasi hiyo itashikwa na Albert Gasper Msando akitokea Wilaya ya Handeni
Soma https://jamii.app/TwangeEDmpyaTanesco
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
Leo Mei 6, 2025, IMS, JamiiAfrica na UTPC kwa pamoja wamezindua Mradi wenye lengo la “Kuwawezesha Wanahabari kwaajili ya Jamii yenye taarifa sahihi Tanzania.”
Kupitia ushirikiano huu, Wanahabari watajengewa uwezo wa kuelewa mahitaji ya jamii na kutayarisha maudhui yanayoendana nayo, tafiti zitafanyika kutambua na kujaribu mbinu anuai za kupambana na upotoshaji na Vyombo vya Habari vitawezeshwa kuweza kutekeleza mbinu hizo kwa manufaa ya Umma
Soma https://jamii.app/JamiiAfricaIMSUTPC
#JamiiForums #JamiiAfrica #CitizenEmpowerment #PressFreedom
Kupitia ushirikiano huu, Wanahabari watajengewa uwezo wa kuelewa mahitaji ya jamii na kutayarisha maudhui yanayoendana nayo, tafiti zitafanyika kutambua na kujaribu mbinu anuai za kupambana na upotoshaji na Vyombo vya Habari vitawezeshwa kuweza kutekeleza mbinu hizo kwa manufaa ya Umma
Soma https://jamii.app/JamiiAfricaIMSUTPC
#JamiiForums #JamiiAfrica #CitizenEmpowerment #PressFreedom
Watoto hujifunza kwa kuangalia, si kwa kusikiliza tu. Ikiwa tunataka wawe Wapole, Waadilifu na wenye Heshima, basi nasi tuwe mfano wa hayo. Maneno yana nguvu, lakini matendo yetu ndiyo yanayowalea.
#MaleziBora #JamiiAfrica #JamiiForums #GoodMorning #AmkaNaJF #ParentingInAction
#MaleziBora #JamiiAfrica #JamiiForums #GoodMorning #AmkaNaJF #ParentingInAction
MBEYA: Mimi ni Mkazi wa Isyesye, tunashukuru kwa maboresho ya barabara yanayofanyika lakini anayehusika kutengeneza njia ya michepuko (diversion) hajatengeneza na zilizopo hazipitiki, tunapata shida sana
Mkandarasi anafunga barabara pasipo kuweka alama za kuonesha tunatakiwa kupita wapi matokeo yake tunapita vichochoroni kwenye njia zisizo rasmi, hiyo ni mbaya kwa Vyombo vya Usafiri vinavyotumika
Soma https://jamii.app/MbeyaMkandarasi
#JamiiForums #Uwajibikaji #Accountability
Mkandarasi anafunga barabara pasipo kuweka alama za kuonesha tunatakiwa kupita wapi matokeo yake tunapita vichochoroni kwenye njia zisizo rasmi, hiyo ni mbaya kwa Vyombo vya Usafiri vinavyotumika
Soma https://jamii.app/MbeyaMkandarasi
#JamiiForums #Uwajibikaji #Accountability
👍1
Friedrich Merz (69) amechaguliwa kuwa Kansela wa Ujerumani katika duru la pili la Upigaji Kura katika Bunge la Shirikisho (Bundestag), hiyo ni baada ya kushindwa kwenye duru la kwanza na sasa anachukua nafasi ya Olaf Scholz
Merz ambaye anaongoza muunganiko wa Vyama vya CDU (Christian Democratic Union), Chama ndugu CSU cha Bavaria, na SPDy (Social Democratic Party) unaoshikilia viti 328 Bungeni, amepata kura 325 kati ya 630, akivuka kiwango cha kura 316 kinachohitajika kwa wingi wa moja kwa moja
Hiyo ni mara ya kwanza kwa Kansela kupoteza Kura katika awamu ya kwanza katika Bunge la Bundestag kwa Miaka 76, hali iliyozua maswali kuhusu mshikamano ndani wa muungano wao
Soma https://jamii.app/UchaguziUjerumani
#JamiiForums #Democracy #Governanc
Merz ambaye anaongoza muunganiko wa Vyama vya CDU (Christian Democratic Union), Chama ndugu CSU cha Bavaria, na SPDy (Social Democratic Party) unaoshikilia viti 328 Bungeni, amepata kura 325 kati ya 630, akivuka kiwango cha kura 316 kinachohitajika kwa wingi wa moja kwa moja
Hiyo ni mara ya kwanza kwa Kansela kupoteza Kura katika awamu ya kwanza katika Bunge la Bundestag kwa Miaka 76, hali iliyozua maswali kuhusu mshikamano ndani wa muungano wao
Soma https://jamii.app/UchaguziUjerumani
#JamiiForums #Democracy #Governanc
TABORA: Akiwa katika ziara ya kutembelea vituo vya kuhakiki na kuboresha taarifa zao katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na uwekaji wazi wa Daftari la Awali la Wapiga Kura, Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (#INEC), amesema “Mwananchi atakayeona kuna Mpiga Kura ambaye amekosa sifa, awe huru kutumia Fomu Namba 5B ili kumuondoa huyo ambaye amekosa sifa.”
Soma https://jamii.app/UandikishajiTabora
#JamiiForums #Democracy #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Soma https://jamii.app/UandikishajiTabora
#JamiiForums #Democracy #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Waziri wa Viwanda na Biashara, Selemani Jaffo amefanya ziara katika Soko la Kariakoo na kueleza kuna ukiukwaji wa Sheria za Nchi unaofanywa na Wageni kwa kushirikiana na wazawa, kwa kufanya biashara bila kuwa na vibali vinavyotakiwa
Ametoa maelekezo ya kufanyika kwa msako wa kubaini wanaofanya biashara bila kufuata taratibu za Kisheria kwa muda wa mwezi mmoja kuanzia leo Mei 7, 2025
Ikumbukwe, Aprili 16, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alitoa wito kwa Serikali kuweka mifumo madhubuti ya kudhibiti, kusimamia na kuelekeza uwekezaji wa kigeni ili kuhakikisha kuwa faida za uwekezaji huo zinawanufaisha Watanzania wengi zaidi
Soma https://jamii.app/JaffoKariakoo
#JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
Ametoa maelekezo ya kufanyika kwa msako wa kubaini wanaofanya biashara bila kufuata taratibu za Kisheria kwa muda wa mwezi mmoja kuanzia leo Mei 7, 2025
Ikumbukwe, Aprili 16, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alitoa wito kwa Serikali kuweka mifumo madhubuti ya kudhibiti, kusimamia na kuelekeza uwekezaji wa kigeni ili kuhakikisha kuwa faida za uwekezaji huo zinawanufaisha Watanzania wengi zaidi
Soma https://jamii.app/JaffoKariakoo
#JamiiForums #ServiceDelivery #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu #CHADEMA Bara, Benson Kigaila amesema baada ya Uchaguzi Mkuu wa Chama hicho, Mwenyekiti wao mpya Taifa, #TunduLissu aliendeleza mashambulizi dhidi ya Wanachama waliokuwa wakimuunga mkono #FreemanMbowe hali ambayo anadai iliwaonesha kuwa bado wapo katika kipindi cha Uchaguzi
Aidha, amesema baada ya uchaguzi huo, waliomuunga mkono Mbowe waliendelea kushambuliwa na wafuasi wa Lissu na kwamba suala hilo limeleta ubaguzi, huku akidai baadhi ya wafausi kadhaa ambao walimuunga mkono Mbowe wanavuliwa Uanachama
Soma https://jamii.app/G55Mei7
#JamiiForums #Siasa #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Aidha, amesema baada ya uchaguzi huo, waliomuunga mkono Mbowe waliendelea kushambuliwa na wafuasi wa Lissu na kwamba suala hilo limeleta ubaguzi, huku akidai baadhi ya wafausi kadhaa ambao walimuunga mkono Mbowe wanavuliwa Uanachama
Soma https://jamii.app/G55Mei7
#JamiiForums #Siasa #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Benson Kigaila ambaye alikuwa Naibu Katibu Mkuu CHADEMA - Bara amesema yeye na Wanachama wenzake wamejitoa katika chama hicho kutokana na kutoridhishwa na yanayoendelea
Ametangaza uamuzi huo akiwa pamoja na aliyekuwa Makamu wa CHADEMA Taifa - Zanzibar, Salum Mwalimu, aliyewai kuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake CHADEMA (BAWACHA), Catherine Ruge, John Mrema na Julius Mwita
Soma https://jamii.app/G55Mei7
#JamiiForums #Siasa #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Ametangaza uamuzi huo akiwa pamoja na aliyekuwa Makamu wa CHADEMA Taifa - Zanzibar, Salum Mwalimu, aliyewai kuwa Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake CHADEMA (BAWACHA), Catherine Ruge, John Mrema na Julius Mwita
Soma https://jamii.app/G55Mei7
#JamiiForums #Siasa #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025