JamiiForums
βœ”
52.6K subscribers
34.4K photos
2.46K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
KAGERA: Padri Monsinyori Samwel Muchunguzi ameeleza kuwa suala la Viongozi wa Dini kutozungumzia Siasa ni gumu kwa kuwa sehemu ya Waumini wao ni Wanasiasa, hivyo wao nao ni sehemu ya Waumini wanaostahili kupata darasa wanalolitoa kwa Waumini

Amesema hayo wakati wa Maadhimisho Takatifu ya kuwatengeneza Wanafunzi wa Seminari ndogo ya Mtakatifu Maria Rubya na kuiombea Miito, Jimbo Katoliki Bukoba

Soma https://jamii.app/PadriMuchunguzi

#JamiiForums #Governance #Demokrasia #JamiiAfrica #Kuelekea2025 #Democracy
πŸ‘Ž2❀1πŸ‘1
UGANDA: Mkuu wa Majeshi Muhoozi Kainerugaba ambaye ni Mtoto wa Rais #YoweriMuseveni kupitia machapisho yake katika Mitandao ya Kijamii amekiri kumteka Mlinzi wa Mwanasiasa Bobi Wine (Edward Mutwe) ambaye aliripotiwa kutekwa na Watu wasiojulikana Aprili 27, 2025 na hajulikani alipo hadi sasa

Muhoozi pia amejisifu kuteka na kuwatesa Wapinzani wake huku akitishia kuua hadharani yeyote anayekosoa Serikali iliyopo Madarakani

Edward Mutwe ni Mlinzi Mkuu wa Bobi Wine ambaye ni Kiongozi wa Chama Kikuu cha upinzani Nchini Uganda cha The National Unity Platform (NUP)

Soma https://jamii.app/MuhooziMay2025

#JamiiForums #UgandaPolitics #Governance #HumanRights
πŸ‘1
KENYA: Watu Wanne waliohusika kuandaa Makala ya 'Blood Parliament' iliyoonesha Mauaji yaliyotokea wakati wa Maandamano ya Gen Z kisha kurushwa katika Kituo cha BBC wamekamatwa na kushikiliwa kwa Siku moja na Jeshi la Polisi kabla ya kuachiwa

Taarifa ya Mwenyekiti wa Chama cha Wataalamu wa Filamu na Televisheni Kenya (KFPTA), Ezekiel β€˜Ezy’ Onyango, amesema Vifaa vyao ikiwemo Kompyuta na Vifaa vya kuhifadhi nyaraka (hard drive) vilikamatwa wakati wa operesheni hiyo

Amesema β€œTumejulishwa wanakabiliwa na mashtaka yanayohusiana na kuchapisha taarifa za uongo na #Cyberbullying. Watuhumiwa hao walikamatwa jana Mei 2, 2025 wameachiwa asubuhi ya leo Mei 3, 2025

Soma https://jamii.app/BloodParliamentUpdates

#JamiiForums #KenyanPolitics #HumanRights
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa ameliagiza Jeshi la Polisi kumtafuta na kumhoji Mtu aliyeandika kwenye Mitandao ya Kijamii kuwa "Siku za Kitima zinahesabika"

Mtu huyo anayetambulika kwa jina la Dr. Frey Edward Cosseny akitumia Akaunti yake ya Mtandao wa X, Aprili 28, aliandika β€œMwambieni Kitima iko Siku ataingia kwenye 18 hatokaa asahau Tanzania, Muacheni ajifanye Mwanasiasa. Mfikishieni meseji Siku si nyingi atapata anachokitafuta Dawa yake iko jikoni atakuja kuozea jela.”

Aprili 30, 2025, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima akashambuliwa na kujeruhiwa na Watu wasiojulikana akiwa Makao Mkuu ya TEC, Mei 1, 2025 Jeshi la Polisi likatangaza kumshikilia Mtu mmoja kutokana na tukio hilo

Soma https://jamii.app/BashungwaMaelekezo

#JamiiForums #Accountability #HumanRights #Governance #Uwajibikaji
πŸ‘2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Wakili Peter Kibatala akizungumza na Wanahabari, leo Mei 3, 2025, amesema mteja wao ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Tundu Lissu, ambaye anashikiliwa Gerezani anatarajiwa kuanza kufanya mgomo wa kula Chakula hadi Haki ipatikane

Amesema hiyo ni sehemu ya kusisitiza Haki ipatikane bila kufafanua Haki ipi anayoizungumzia

Soma https://jamii.app/MawakiliMei3

#JamiiForums #Democracy
πŸ‘2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, amesema analaani vikali tukio la kushambuliwa kwa Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima, na ameliagia Jeshi la Polisi kuwasaka wote waliohusika na uhalifu huo ili hatua za Kisheria zichukuliwe

Amesema Serikali inatambua na kuthamini mchango mkubwa wa Viongozi wa dini Nchini katika kudumisha Amani, Mshikamano wa Kijamii, na Maadili ya Taifa

Ameeleza hayo, Mei 02, 2025 wakati wa hafla ya kuwaaga Watumishi wa Umma waliostaafu kutoka Wizara ya Mambo ya Ndani, ambapo alikumbusha kuwa Wizara hiyo ndiyo yenye dhamana ya kuhakikisha Usalama wa Raia na Mali zao kupitia Vyombo vyake vya Usalama

Soma https://jamii.app/BashungwaMaelekezo

#JamiiForums #Accountability #HumanRights #Governance #Uwajibikaji
πŸ‘1
MOROGORO: Askofu wa Kanisa la KKKT Dayosisi ya Morogoro, Jacob Mameo Ole Paulo, alisema ujumbe huo alipokuwa katika Ibada ya Ijumaa Kuu, Aprili 18, 2025 ambapo pia alisisitiza kwa Serikali kuzingatia malalamiko yanayotolewa na Wananchi.

https://jamii.app/AskofuJacobNukuu

#Demokrasia #JamiiForums #HumanRights #JFNukuu #Quote #JamiiAfrica
πŸ‘2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mratibu wa Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), Wakili Onesmo Olengurumwa, amesema Waandishi wa Habari wanao wajibu wa kusaidia umma kubaini Taarifa za ukweli na uongo, na wanaweza kutumia Teknolojia ya Akili Mnemba (AI) kuongeza tija licha ya kuwa nayo inachangia kuzalishwa kwa Taarifa za uongo

Ameyasema hayo Mei 2, 2025 katika mafunzo ya Siku moja ya Wanahabari 150, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, ambayo inaadhimishwa Mei 3, ambapo Kaulimbiu ya Mwaka 2025 ni β€œUhabarishaji kwenye Dunia Mpya: Mchango wa Akili Mnemba/Unde kwenye Uhuru wa Vyombo vya Habari.”

Aidha, ametoa kongole kwa #JamiiAfrica ambayo imekuwa ikishughulikia kubaini Taarifa sahihi na zisizo sahihi kupitia Jukwaa la #JamiiCheck

Soma https://jamii.app/WPFD2025

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #VisitJamiiCheck #FactsCheck #HakikiTaarifa #FactsChecking #MisDis04
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, ameagiza Jeshi la Polisi kuwatafuta waliotengeneza na kusambaza waraka feki uliodaiwa kutolewa na Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC), ambao ulilenga kuchochea mgongano kati ya Kanisa na Serikali

Soma https://jamii.app/BashungwaMaelekezo

#JamiiForums #Accountability #HumanRights #Governance
πŸ‘Ž1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Wakili Jebra Kambole ametoa wito kwa Uongozi wa Mahakama kusimamia suala la Haki ya Wananchi kupata taarifa ya kinachoendelea Mahakamani, akitoa mfano wa Maafisa wa Usalama kuwapiga na kuwazuia Wanahabari kutimiza majukumu yao ya kuwahabarisha Wananchi

Soma https://jamii.app/MawakiliMei3

#JamiiForums #Democracy #WPFD2025 #WorldPressFreedomDay #PressFreedom
πŸ‘1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa, amewahakikishia Watanzania kuwa Nchi iko salama na kwamba waendelee kutii Sheria bila Shuruti na kulitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha uchunguzi wa kina unafanyika na kuchukua hatua zinazostahili dhidi ya Wahalifu wanaotaka kuvuruga Amani ya Nchi

Soma https://jamii.app/BashungwaMaelekezo

#JamiiForums #Accountability #HumanRights #Governance
πŸ‘Ž1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
SHINYANGA: Serikali imesema Vitambulisho vya Kidigitali kwa Waandishi wa Habari vinatarajiwa kuanza kutolea wiki moja kutoka leo Mei 3, 2025

Hayo yamesemwa na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, ambaye ameongeza kuwa Bodi ya Ithibati ya Wanahabari haitasita kuwafutia usajili Wanahabari watakaokwenda kinyume cha Kanuni na Maadili ya kazi zao

Soma https://jamii.app/KitambulishoMwandishi

#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #JamiiForums #JamiiAfrica
πŸ‘3
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Jaji Warioba amesema Viongozi wa Dini wanaweza kusaidia kufanya mazungumzo ya kutafuta muafaka wa Kisiasa nchini, ambapo watakuwa wanazungumza na kushauri nini kifanyike

Akizungumza katika Kongamano la Uchaguzi Mkuu wa Tanzania lililoandaliwa na Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), amesema wanaamini kama Viongozi wa Kisiasa wakikubali kukutana, wakawa na Watu wa kuwashauri inawezekana kufikia muafaka tukaenda kwenye Uchaguzi vyama vyote vikishiriki, Wananchi wakashiriki na tukatoka salama

Soma https://jamii.app/JajiWariobaMei3

#JamiiForums #Governance #Demokracy #Kuelekea2025
πŸ‘4
KENYA: Ripoti ya Wizara ya Afya kwa ushirikiano wa African Population and Health Research Centre (APHRC) na Taasisi ya Guttmacher imeeleza kuwa kati ya Aprili 2023 na Mei 2024, zaidi ya visa 792,000 vya utoaji mimba vimeripotiwa Nchini #Kenya

Ripoti imeeleza namba hiyo ni sawa na wastani wa visa 57.3 kati ya Wanawake 1,000 wenye umri wa miaka 15 – 49, na Asilimia 80 ya wanaofanya hivyo wapo kwenye ndoa

Mtafiti Mkuu wa Guttmacher, Margaret Giorgio amesema β€œWanaotoa wanafanya hivyo kwa kuwa hawajajiandaa kuwa wazazi, pia wengine ambao tayari wameshakuwa na Watoto wanachukua hatua hiyo kutokana na kuhofia gharama za maisha kuwa kubwa.”

Soma https://jamii.app/AbortionsKenya

#PublicHealth #JamiiForums #PublicHealth
πŸ‘1πŸ‘Ž1
Muda mfupi baada ya Rais Donald Trump kupost picha yake iliyotengenezwa kwa AI yenye Mwonekano wa Mavazi Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki Duniani (Papa) na kukosolewa na wengi Mtandaoni, Uongozi wa Kanisa Katoliki New York umemwambia Trump asiwakejeli

Kupitia ukurasa wao wa X (zamani Twitter), Uongozi wa Kanisa Katoliki New York ulisema kuwa hakuna cha kufurahisha kuhusu alichokifanya Trump, hasa ikizingatiwa kuwa Kanisa bado linaomboleza kifo cha Papa Francis aliyezikwa Aprili 26, 2025 na lipo kwenye mchakato wa kumpata kiongozi mpya, hivyo kumtaka Trump kutochukulia jambo hilo kwa mzaha

Zaidi https://jamii.app/TrumpPapa

#JamiiForums #JamiiAfrica
😁3πŸ‘1
Mdau wa JamiiForums.com anasema Vijana msikubali kubanwa na Visingizio. Kama huwezi kuwa Mwanafunzi bora, basi kuwa Mfanyabiashara hodari. Kama huwezi kuwa Mfanyabiashara mkubwa, basi anza na vibanda. Kama huwezi kuwa na Duka, tafuta bidhaa na utembeze. Vyovyote iwavyo hakikisha unapiga hatua

Anasema kuwa na Mtaji mdogo sio shida, unachohitaji ni Wazo bora, Akili za Mtaani na Darasani huku akitaja Biashara unazoweza kuzifanya kwa Mtaji wa kuanzia Tsh. 20,000–100,000.

Fungua hapa kufahamu Mawazo ya Biashara aliyoyataja https://jamii.app/PambanaKiakili

#JamiiForums #JamiiAfrica #Biashara #Uchumi #Ujasiriamali
πŸ‘2