UGANDA: Sehemu ya Wabunge kutoka Chama Tawala cha National Resistance Movement (NRM), Wabunge huru, na wa Upinzani wanaripotiwa kupokea kiasi cha Shilingi ya Uganda Milioni 100 (takriban Tsh. Milioni 70) kila mmoja kutoka kwa Rais Yoweri Museveni kama 'zawadi'
Gazeti la Monitor limeeleza kuwa Wabunge wa NRM walipokea pesa hizo kutoka Ofisi ya Katibu Mkuu wa Serikali Bungeni kati ya Saa mbili na Saa tatu Usiku Aprili 7, 2025 huku wengine wakiripotiwa kupokea kutoka katika makazi ya Spika, Anita Among, yaliyoko Nakasero
Inadaiwa Pesa hizo zilitolewa kama ishara ya shukrani kutoka kwa Rais kwa ajili ya "tabia njema" ya Wabunge hao, na pia kama mwitikio wa maombi yaliyotolewa na baadhi ya Wabunge waliokuwa wakikabiliwa na matatizo ya kifedha.
Soma https://jamii.app/MuseveniGifts100milion
#JamiiForums #AfricanPolitics
Gazeti la Monitor limeeleza kuwa Wabunge wa NRM walipokea pesa hizo kutoka Ofisi ya Katibu Mkuu wa Serikali Bungeni kati ya Saa mbili na Saa tatu Usiku Aprili 7, 2025 huku wengine wakiripotiwa kupokea kutoka katika makazi ya Spika, Anita Among, yaliyoko Nakasero
Inadaiwa Pesa hizo zilitolewa kama ishara ya shukrani kutoka kwa Rais kwa ajili ya "tabia njema" ya Wabunge hao, na pia kama mwitikio wa maombi yaliyotolewa na baadhi ya Wabunge waliokuwa wakikabiliwa na matatizo ya kifedha.
Soma https://jamii.app/MuseveniGifts100milion
#JamiiForums #AfricanPolitics
KILIMANJARO: Aliyekuwa Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Godfrey Malisa amewasilisha maombi Mahakamani akiomba uanachama wake ulindwe, ili afungue maombi ya kupinga mchakato wa kumteua Rais Samia kuwa mgombea Urais
Dkt. Malisa amewasilisha ombi hilo akiomba Mahakama itoe zuio la muda kwa lengo la kulinda hadhi ya Uanachama wake, wakati maombi yake ya kupinga uteuzi huo wa Rais yakiwa bado hayajafunguliwa
Katika maombi hayo, Dkt. Malisa ameishtaki Bodi ya Wadhamini ya #CCM na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kilimanjaro, ambayo ilitangaza kumfuta Uanachama, huku akidai anaweza kuthibitisha kuwa Katiba ya CCM na Utaratibu wa kumpata mgombea, Rais Samia katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 ulikiukwa na chama hicho.
Soma https://jamii.app/KupingaMgombeaUrais25
#JamiiForums #Governance #UchaguziMkuu2025
Dkt. Malisa amewasilisha ombi hilo akiomba Mahakama itoe zuio la muda kwa lengo la kulinda hadhi ya Uanachama wake, wakati maombi yake ya kupinga uteuzi huo wa Rais yakiwa bado hayajafunguliwa
Katika maombi hayo, Dkt. Malisa ameishtaki Bodi ya Wadhamini ya #CCM na Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Kilimanjaro, ambayo ilitangaza kumfuta Uanachama, huku akidai anaweza kuthibitisha kuwa Katiba ya CCM na Utaratibu wa kumpata mgombea, Rais Samia katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 ulikiukwa na chama hicho.
Soma https://jamii.app/KupingaMgombeaUrais25
#JamiiForums #Governance #UchaguziMkuu2025
π2
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akijibu hoja ya Mbunge Zahor Mohamed Haji aliyedai kuna dalili za Uvunjifu wa Amani kwa lugha za kejeli kuelekea kwenye Uchaguzi wa Mwaka 2025, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Boniface Simbachawene amesema Serikali imejipanga na haipumziki
Amesema βTumefanya Uchaguzi takriban mara Saba, kwa uzoefu huo Nchi yetu ni Mwalimu wa Demokrasia katika Kanda yetu, waliojiandaa kuleta fujo watambue Serikali haipumziki na imejipanga kusimamia Uchaguzi wa 2025.β
Soma https://jamii.app/BungeAprili9
#JamiiForums #Governance #Demokrasia #Kuelekea2025
Amesema βTumefanya Uchaguzi takriban mara Saba, kwa uzoefu huo Nchi yetu ni Mwalimu wa Demokrasia katika Kanda yetu, waliojiandaa kuleta fujo watambue Serikali haipumziki na imejipanga kusimamia Uchaguzi wa 2025.β
Soma https://jamii.app/BungeAprili9
#JamiiForums #Governance #Demokrasia #Kuelekea2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Taifa, Othman Masoud Othman amesema kuwepo kwa mazingira magumu yaliyogubikwa na nguvu kubwa za Vyombo vya Dola katika zoezi la Uandikishaji Wapigakura wapya Zanzibar ni kielelezo tosha kuwa Watawala hawapo tayari kutenda Haki licha ya kuwa ni mahodari wa kuhubiri Amani
Amesema hayo wakati alipokuwa akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Chama Mkoa wa Kichama wa Micheweni katika Ukumbi wa Jimbo la Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba, Aprili 8, 2025
Soma https://jamii.app/NukuuOthman
#JamiiForums #Siasa #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
Amesema hayo wakati alipokuwa akizungumza na Viongozi mbalimbali wa Chama Mkoa wa Kichama wa Micheweni katika Ukumbi wa Jimbo la Konde Mkoa wa Kaskazini Pemba, Aprili 8, 2025
Soma https://jamii.app/NukuuOthman
#JamiiForums #Siasa #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
DAR: Timu ya #Simba inaongoza kwa Magoli 2-0 dhidi ya Al Masry ya Misri katika dakika 45 za kipindi cha kwanza kwenye mchezo wa Pili wa Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika unaopigwa kwenye Uwanja wa Mkapa, magoli yakiwekwa wavuni na Elie Mpanzu na Steven Mukwala
Matokeo ya jumla mpaka sasa ni 2-2 kwa kuwa katika mchezo wa kwanza Simba ilipoteza kwa Magoli 2-0 Nchini Misri
Soma https://jamii.app/SimbaAlMasry
#JFSports #JamiiForums #CAFCC
Matokeo ya jumla mpaka sasa ni 2-2 kwa kuwa katika mchezo wa kwanza Simba ilipoteza kwa Magoli 2-0 Nchini Misri
Soma https://jamii.app/SimbaAlMasry
#JFSports #JamiiForums #CAFCC
β€3
DAR: Timu ya #Simba imeendeleza rekodi yake ya kufanya kweli katika michuano ya kimataifa, hiyo ni baada ya kuingia Nusu Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika kwa penati 4-1 dhidi ya Al Masry ya Misri kwenye Uwanja wa Mkapa
Dakika 90 zilikamilika kwa Simba kushinda Magoli 2-0 wafungaji wakiwa ni Elie Mpanzu na Steven Mukwala, hivyo kufanya matokeo ya jumla kuwa 2-2 kwa kuwa Robo Fainali ya kwanza Al Masry ilishinda 2-0
Hatua ya Nusu Fainali, Simba inatarajiwa kukutana na mshindi kati ya Zamalek (Misri) dhidi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini
Soma https://jamii.app/SimbaAlMasry
#JFSports #JamiiForums #CAFCC
Dakika 90 zilikamilika kwa Simba kushinda Magoli 2-0 wafungaji wakiwa ni Elie Mpanzu na Steven Mukwala, hivyo kufanya matokeo ya jumla kuwa 2-2 kwa kuwa Robo Fainali ya kwanza Al Masry ilishinda 2-0
Hatua ya Nusu Fainali, Simba inatarajiwa kukutana na mshindi kati ya Zamalek (Misri) dhidi ya Stellenbosch ya Afrika Kusini
Soma https://jamii.app/SimbaAlMasry
#JFSports #JamiiForums #CAFCC
β€3π2
RUVUMA: Kwa mujibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA) kupitia Ukurasa wao wa Mtandao wa X, Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa, #TunduLissu amekamatwa na Jeshi la Polisi Wilayani Mbinga
Taarifa hiyo imeeleza Lissu amekamatwa wakati alipomaliza mkutano wa hadhara uliofanyika leo Aprili 9, 2025 pamoja na Wanachama wengine kadhaa na kwamba bado hawajafahamu wamepelekwa Kituo gani cha Polisi
Soma https://jamii.app/LissuAkamatwaRuvuma
#JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Kuelekea2025 #Siasa
Taarifa hiyo imeeleza Lissu amekamatwa wakati alipomaliza mkutano wa hadhara uliofanyika leo Aprili 9, 2025 pamoja na Wanachama wengine kadhaa na kwamba bado hawajafahamu wamepelekwa Kituo gani cha Polisi
Soma https://jamii.app/LissuAkamatwaRuvuma
#JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Kuelekea2025 #Siasa
β€1
Mifumo ya udhibiti inayotumika kudhibiti taarifa Mtandaoni inaweza kutumiwa kuzuia taarifa muhimu, kupunguza upatikanaji wa taarifa huru, na kuzuia sauti za Wananchi kutoka kwenye majukwaa ya Kidijitali.
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
TABORA: Mdau wa JamiiForums.com anasema akiwa katika safari zake alipita Urambo katika Stendi ya Wilaya ambapo alishangazwa na mwonekano wa Kituo hicho, Mazingira yake sio mazuri na kudai kimekaa 'local'
Anaeleza "Tuliposhuka kupata Huduma ya Vyoo kwa Wanaume, tulilipa ila nako tukakuta hali siyo nzuri, usafi hauzingatiwi na inavyoonekana hapafanyiwi usafi vizuri jambo ambalo ni hatari kwa Afya. Natoa wito Mamlaka husika kuchukua hatua kuweka Mazingira vizuri."
Soma https://jamii.app/UduniStendiUrambo
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #HudumaZaKijamii #ServiceDelivery
Anaeleza "Tuliposhuka kupata Huduma ya Vyoo kwa Wanaume, tulilipa ila nako tukakuta hali siyo nzuri, usafi hauzingatiwi na inavyoonekana hapafanyiwi usafi vizuri jambo ambalo ni hatari kwa Afya. Natoa wito Mamlaka husika kuchukua hatua kuweka Mazingira vizuri."
Soma https://jamii.app/UduniStendiUrambo
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #HudumaZaKijamii #ServiceDelivery
π1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
RUVUMA: Mjumbe wa Kamati Kuu ya #CHADEMA, Godbless Lema kupitia Akaunti yake kwenye Mtandao wa X ameandika kuwa wameshambuliwa kwa mabomu ya machozi walipokuwa katika ofisi za chama hicho, Songea, eneo ambalo walitarajiwa kufanya mkutano wao leo Aprili 10, 2025
Upande wa Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Brenda Rupia kuhusu tukio hilo amezungumza na JamiiForums na kusema "Polisi wamevamia mkutano wetu na Wanahabari, wameondoka na Viongozi wetu kadhaa wakiwemo Makamu Mwenyekiti, John Heche na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema.β
Amesema Polisi imewachukua kwa ajili ya mahojiano, alipoulizwa sababu za wao kuzuiwa kufanya mkutano na Wanahabari ambao ulipangwa kufanyika asubuji ya leo, amesema Polisi hawajatoa sababu yoyote
Jitihada za JamiiForums kutafuta upande wa Jeshi la Polisi Mkoa zinaendelea
Soma https://jamii.app/CHADEMAKuvamiwaSongea
#JamiiForums #Demokrasia #KuelekeaUchaguzi2025 #HumanRights
Upande wa Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi wa CHADEMA, Brenda Rupia kuhusu tukio hilo amezungumza na JamiiForums na kusema "Polisi wamevamia mkutano wetu na Wanahabari, wameondoka na Viongozi wetu kadhaa wakiwemo Makamu Mwenyekiti, John Heche na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Godbless Lema.β
Amesema Polisi imewachukua kwa ajili ya mahojiano, alipoulizwa sababu za wao kuzuiwa kufanya mkutano na Wanahabari ambao ulipangwa kufanyika asubuji ya leo, amesema Polisi hawajatoa sababu yoyote
Jitihada za JamiiForums kutafuta upande wa Jeshi la Polisi Mkoa zinaendelea
Soma https://jamii.app/CHADEMAKuvamiwaSongea
#JamiiForums #Demokrasia #KuelekeaUchaguzi2025 #HumanRights
π1
DAR: Aprili 8, 2025, Mdau wa JamiiForums alieleza kuwa eneo la Posta Barabara ya Kanisa la KKKT kuelekea Karimjee kuna chemba zimepasuka na kutiririsha majitaka, Mamlaka zimechukua hatua kwa kushughulikia utengenezaji wa miundombinu hiyo ambapo kwa sasa majitaka hayo hayatiririki
Soma https://jamii.app/ChembaKurekebishwa
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
Soma https://jamii.app/ChembaKurekebishwa
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
MAREKANI: Rais #DonaldTrump, siku ya Jumatano Aprili 9, 2025 alisitisha ghafla ushuru wa Forodha kwa Nchi nyingi kwa kipindi cha Siku 90, na kuongeza zaidi kiwango cha ushuru kwa Bidhaa kutoka China hadi kufikia 125%
Hatua hiyo imeonekana kuwa jaribio la kupunguza Mvutano wa Vita ya Kibiashara ambayo haijawahi kushuhudiwa kati ya Marekani na Mataifa mengi Duniani, na kulenga zaidi mzozo kati ya Marekani na China
Wakati Hisa na Dhamana za Serikali zikiuzwa kwa wingi, Wananchi wanashuhudia Akiba zao za kustaafu zikipungua, huku Biashara zikiashiria mauzo duni kuliko matarajio na kupanda kwa bei.
Soma https://jamii.app/TrumpTariffs90Days
#JamiiForums #Governance #TariffWar #TrumpTarrifs
Hatua hiyo imeonekana kuwa jaribio la kupunguza Mvutano wa Vita ya Kibiashara ambayo haijawahi kushuhudiwa kati ya Marekani na Mataifa mengi Duniani, na kulenga zaidi mzozo kati ya Marekani na China
Wakati Hisa na Dhamana za Serikali zikiuzwa kwa wingi, Wananchi wanashuhudia Akiba zao za kustaafu zikipungua, huku Biashara zikiashiria mauzo duni kuliko matarajio na kupanda kwa bei.
Soma https://jamii.app/TrumpTariffs90Days
#JamiiForums #Governance #TariffWar #TrumpTarrifs
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
GEITA: Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (SACP), Safia Jongo ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa amesema hakuna raia yeyote akiwemo Askari Polisi anayeruhusiwa kumpiga Mtu bali anatakiwa amueleze kosa lake kisha amfikishe Kituo cha Polisi
Ametoa kauli hiyo wakati wa Mafunzo ya Ulinzi Shirikishi na Polisi Jamii yaliyotolewa kwa Watendaji wa Kata, Vijiji, Mitaa wenye viti na Maafisa Tarafa, yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Mgodi wa Dhahabu wa Geita(GGML) kwa lengo la kuimarisha usalama wa Wananchi kupitia ushirikiano wa karibu.
Soma https://jamii.app/AskariKumpigaMtu
Video Credits: Star TV
#Accountability #Uwajibikaji #HumanRights #JamiiForums
Ametoa kauli hiyo wakati wa Mafunzo ya Ulinzi Shirikishi na Polisi Jamii yaliyotolewa kwa Watendaji wa Kata, Vijiji, Mitaa wenye viti na Maafisa Tarafa, yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Mgodi wa Dhahabu wa Geita(GGML) kwa lengo la kuimarisha usalama wa Wananchi kupitia ushirikiano wa karibu.
Soma https://jamii.app/AskariKumpigaMtu
Video Credits: Star TV
#Accountability #Uwajibikaji #HumanRights #JamiiForums
β€1π1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
UWAJIBIKAJI: Mbunge wa Nkasi Kaskazini, Aida Kenani amehoji hatua ya Serikali kumkamata Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu na kuitaka itoe maelezo kuhusu sababu za kukamatwa kwake
Amesema hayo leo Aprili 10, 2025 akiwa Bungeni Dodoma
Soma https://jamii.app/KukamatwaTunduLissu
#JamiiForums #Governance #Uwajibikaji #Accountability
Amesema hayo leo Aprili 10, 2025 akiwa Bungeni Dodoma
Soma https://jamii.app/KukamatwaTunduLissu
#JamiiForums #Governance #Uwajibikaji #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mkurugenzi wa Sheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wakili Gaston Garubindi amesema Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa, Tundu Lissu amefikishwa Kituo cha Polisi kati (Central) na tayari amehojiwa na Ofisi ya Upelelezi ya Kanda Maalumu
Amesema Lissu amehojiwa kwa tuhuma mbili ambazo ni Uhaini na kutoa taarifa za uongo huku ikielezwa atafikishwa Mahakamani ndani ya Saa 48
Lissu alikamatwa Aprili 9, 2024 Wilayani Mbinga wakati alipomaliza mkutano wa hadhara pamoja na Wanachama wengine kadhaa
Soma https://jamii.app/LissuUhainiCentral
#JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Kuelekea2025 #Siasa
Amesema Lissu amehojiwa kwa tuhuma mbili ambazo ni Uhaini na kutoa taarifa za uongo huku ikielezwa atafikishwa Mahakamani ndani ya Saa 48
Lissu alikamatwa Aprili 9, 2024 Wilayani Mbinga wakati alipomaliza mkutano wa hadhara pamoja na Wanachama wengine kadhaa
Soma https://jamii.app/LissuUhainiCentral
#JamiiForums #UchaguziMkuu2025 #Kuelekea2025 #Siasa
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
RUVUMA: Jeshi la Polisi limetoa taarifa ya kukamatwa kwa Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu mnamo Aprili 9, 2025 katika Mtaa wa Soko Kuu, Wilaya ya Mbinga kwa kosa la kufanya uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025
Taarifa imetoa onyo kwa Vyama vya Siasa kutoa maneno ya uchochezi na Kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu
Aidha, taarifa ya Mkurugenzi wa Sheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wakili Gaston Garubindi imesema Tundu Lissu amefikishwa Kituo cha Polisi Kati (Central) na tayari amehojiwa na Ofisi ya Upelelezi ya Kanda Maalumu kwa tuhuma mbili ambazo ni Uhaini na Kutoa Taarifa zilizokuwa zinapelelezwa za kufanya Uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025
Soma https://jamii.app/LissuKukamatwaUchochezi
#JamiiForums #Governance #Uwajibikaji #Demokrasia #Accountability #KuelekeaUchaguzi2025
Taarifa imetoa onyo kwa Vyama vya Siasa kutoa maneno ya uchochezi na Kashfa kwa Polisi na Serikali au viashiria vyovyote vya uvunjifu wa amani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu
Aidha, taarifa ya Mkurugenzi wa Sheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Wakili Gaston Garubindi imesema Tundu Lissu amefikishwa Kituo cha Polisi Kati (Central) na tayari amehojiwa na Ofisi ya Upelelezi ya Kanda Maalumu kwa tuhuma mbili ambazo ni Uhaini na Kutoa Taarifa zilizokuwa zinapelelezwa za kufanya Uchochezi wa kutofanyika Uchaguzi Mkuu 2025
Soma https://jamii.app/LissuKukamatwaUchochezi
#JamiiForums #Governance #Uwajibikaji #Demokrasia #Accountability #KuelekeaUchaguzi2025