DAR: Mdau anadai tangu kuanza kwa Mwaka 2025, hajaona gari la taka katika Mtaa anaoishi (Mbezi Beach), ambapo Wananchi hulazimika kuwakodi Vijana wenye mikokoteni ili kuzoa taka na kuondoka nazo, bila kujua zinaenda kutupwa wapi
Mdau anadai Mamlaka inayosimamia mazingira (NEMC) imekuwa kimya katika suala hilo, akihoji au inasubiri mlipuko wa Magonjwa utokee ndio watoe tamko na kuchukua hatua, halafu ukiisha 'wapige kimya' tena?
Soma https://jamii.app/UzoajiTaka
#Accountability #JamiiForums
Mdau anadai Mamlaka inayosimamia mazingira (NEMC) imekuwa kimya katika suala hilo, akihoji au inasubiri mlipuko wa Magonjwa utokee ndio watoe tamko na kuchukua hatua, halafu ukiisha 'wapige kimya' tena?
Soma https://jamii.app/UzoajiTaka
#Accountability #JamiiForums
Siku ya Mtoto wa Afrika huadhimishwa kila Mwaka tarehe 16 Juni, ikiwa ni kumbukumbu ya Maandamano ya Wanafunzi huko Soweto, Afrika Kusini Mwaka 1976, ambapo walidai Haki yao ya kupata Elimu bora
Ulimwenguni kote, Watoto wanaendelea kukabiliwa na vitisho vinavyoingiliana, kutoka Umasikini na njaa hadi upatikanaji mdogo wa Elimu bora na Huduma za Afya. Kwa mujibu wa Shirika la #UNICEF (2023), zaidi ya Watoto Bilioni moja Duniani kote wanakabiliwa na angalau aina moja ya kunyimwa mahitaji muhimu
Hili ni suala la dharura hasa Barani Afrika, ambalo lina idadi ya Watoto inayokua kwa kasi zaidi Duniani, kukiwa na zaidi ya Watoto Milioni 540, karibu 50% ya idadi ya Watu Barani kote. Ifikapo Mwaka 2055, Afrika itakuwa na idadi kubwa zaidi ya Watoto Duniani
Soma https://jamii.app/DAC2025
#AfricanChildDay #InvestInChildren #DAC2025 #DayOfTheAfricanChild #JamiiForums #JamiiAfrica
Ulimwenguni kote, Watoto wanaendelea kukabiliwa na vitisho vinavyoingiliana, kutoka Umasikini na njaa hadi upatikanaji mdogo wa Elimu bora na Huduma za Afya. Kwa mujibu wa Shirika la #UNICEF (2023), zaidi ya Watoto Bilioni moja Duniani kote wanakabiliwa na angalau aina moja ya kunyimwa mahitaji muhimu
Hili ni suala la dharura hasa Barani Afrika, ambalo lina idadi ya Watoto inayokua kwa kasi zaidi Duniani, kukiwa na zaidi ya Watoto Milioni 540, karibu 50% ya idadi ya Watu Barani kote. Ifikapo Mwaka 2055, Afrika itakuwa na idadi kubwa zaidi ya Watoto Duniani
Soma https://jamii.app/DAC2025
#AfricanChildDay #InvestInChildren #DAC2025 #DayOfTheAfricanChild #JamiiForums #JamiiAfrica
❤1
KENYA: Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi (DIG), Eliud Kipkoech Lagat, ametangaza kujiondoa kwa muda kazini wakati uchunguzi ukiendelea kuhusu kifo cha Mwanaharakati Albert Ojwang’, ambaye alikamatwa kufuatia malalamiko ya kashfa yanayodaiwa kuwasilishwa na Afisa huyo
Katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumatatu, Lagat amesema “Leo nimeamua kujiondoa kwa muda kutoka katika Wadhifa wa Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi Kenya hadi uchunguzi utakapokamilika. Majukumu ya Ofisi yataendelea kutekelezwa na Naibu wangu hadi uchunguzi utakapokamilika.”
Ojwang’ alikamatwa muda mfupi baada ya kuchapisha madai ya Ufisadi yaliyomhusisha Lagat, hasa kuhusu upangaji wa kimkakati wa Maafisa ndani ya Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) na vitengo vya trafiki, nafasi zinazodaiwa kuwa na uhusiano na udhibiti wa mapato na taarifa za Kijasusi
Soma https://jamii.app/DIGResignsKE
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji
Katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumatatu, Lagat amesema “Leo nimeamua kujiondoa kwa muda kutoka katika Wadhifa wa Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi Kenya hadi uchunguzi utakapokamilika. Majukumu ya Ofisi yataendelea kutekelezwa na Naibu wangu hadi uchunguzi utakapokamilika.”
Ojwang’ alikamatwa muda mfupi baada ya kuchapisha madai ya Ufisadi yaliyomhusisha Lagat, hasa kuhusu upangaji wa kimkakati wa Maafisa ndani ya Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) na vitengo vya trafiki, nafasi zinazodaiwa kuwa na uhusiano na udhibiti wa mapato na taarifa za Kijasusi
Soma https://jamii.app/DIGResignsKE
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji
❤2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akiongea Mahakamani leo Juni 16, 2025, Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu amesema kuwa licha ya kuwa hajahukumiwa, anakaa upande wa Watu waliohukumiwa kifo katika Gereza la Ukonga
Zaidi https://jamii.app/LissuKuhusuGerezani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights
Zaidi https://jamii.app/LissuKuhusuGerezani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
SIMIYU: Rais Samia Suluhu ametoa wito kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kukusanya mapato kwa njia rafiki, lakini sio kubembelezana anayekataa asilipe. Amesema kila anayepaswa kulipa kodi, alipe
Amesema hayo baada ya kufungua Jengo la Ofisi ya TRA Mkoani humo, leo Juni 16, 2025
Soma https://jamii.app/MikopoYaNje
#JamiiForums #Governance #Accountability
Amesema hayo baada ya kufungua Jengo la Ofisi ya TRA Mkoani humo, leo Juni 16, 2025
Soma https://jamii.app/MikopoYaNje
#JamiiForums #Governance #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
SIMIYU: Rais Samia akifungua Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Mapato TRA Mkoa wa Simiyu, leo Juni 16, 2025 amesema "Ulaya na Marekani sasa hivi hawafanyi vizuri Kiuchumi kama tunavyofanya Sisi huku, hata ndani ya kanda yetu hii ya Afrika Mashariki, Tanzania tunafanya vizuri”
Soma https://jamii.app/SamiaUlayaMarekani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
Soma https://jamii.app/SamiaUlayaMarekani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
❤1👎1
#MALEZI: Vipi kwa upande wako, Mzazi/Mlezi wako aliwahi kukuhusia jambo gani ambalo bado unalizingatia mpaka sasa?
Mjadala zaidi https://jamii.app/MausiaMzazi
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFStories #JFChitChats #Maisha
Mjadala zaidi https://jamii.app/MausiaMzazi
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFStories #JFChitChats #Maisha
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
SIMIYU: Rais Samia Suluhu Hassan akifungua Jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Mapato TRA, leo Juni 16, 2025, amezungumzia umuhimu wa Wananchi kulipa Kodi ili Nchi ianze kutegemea mikopo na misaada kutoka nje
Soma https://jamii.app/MikopoYaNje
#JamiiForums #Governance #Accountability
Soma https://jamii.app/MikopoYaNje
#JamiiForums #Governance #Accountability
❤1
MARA: Kesi ya madai iliyokuwa inawakabili Mbunge wa Jimbo la Tarime Vijijini Mwita Waitara ambaye ni Mdaiwa namba 1, Karoli Jacob (Mdaiwa namba 2) na Mara TV (Mdaiwa namba 3), imetolewa hukumu leo Juni, 16, 2025 katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Musoma
Wadaiwa walikuwa wakikabiliwa na kesi ya madai shauri namba 23, ya Mwaka 2023 iliyofunguliwa na Eliakim Chacha Maswi, aliyewahi kuwa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma ( PPRA) , ambaye kwasasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria
Eliakim Maswi alifungua kesi kutaka wadaiwa kumlipa Tsh. Bilioni 12 kama fidia ya madhara ya jumla pamoja na Tsh. Bilioni 1 kama fidia ya adhabu, kwa madai ya kumkashfu na kutoa tuhuma za uongo dhidi yake kuhusu Wizi wa Fedha, ambapo Mahakama imeamua Waitara na wenzake wamlipe Maswi Tsh. Bilioni 6, pia waite Vyombo vya habari na kumsafisha dhidi ya tuhuma walizotoa dhidi yake na walipia alipie gharama za kesi
Soma https://jamii.app/WaitaraBili6Udhalilishaji
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
Wadaiwa walikuwa wakikabiliwa na kesi ya madai shauri namba 23, ya Mwaka 2023 iliyofunguliwa na Eliakim Chacha Maswi, aliyewahi kuwa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Kudhibiti Ununuzi wa Umma ( PPRA) , ambaye kwasasa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria
Eliakim Maswi alifungua kesi kutaka wadaiwa kumlipa Tsh. Bilioni 12 kama fidia ya madhara ya jumla pamoja na Tsh. Bilioni 1 kama fidia ya adhabu, kwa madai ya kumkashfu na kutoa tuhuma za uongo dhidi yake kuhusu Wizi wa Fedha, ambapo Mahakama imeamua Waitara na wenzake wamlipe Maswi Tsh. Bilioni 6, pia waite Vyombo vya habari na kumsafisha dhidi ya tuhuma walizotoa dhidi yake na walipia alipie gharama za kesi
Soma https://jamii.app/WaitaraBili6Udhalilishaji
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
❤2
UGANDA: Rais, #YoweriMuseveni, amesaini Sheria mpya inayoruhusu Mahakama za Kijeshi kuwahukumu raia, hatua ambayo Viongozi wa upinzani wamesema inakiuka uamuzi wa Mahakama ya Juu
Wanaharakati wa Haki za Binadamu kwa muda mrefu wamekuwa wakilalamika kuwa Serikali imekuwa ikitumia Mahakama za Kijeshi kuwatesa Wapinzani wa Kisiasa wa Museveni, ambaye amekuwa Madarakani kwa takribani Miaka 40. Wasimamizi wake wamekanusha madai hayo, wakisema kuwa ni raia wanaotumia silaha kwa vurugu za kisiasa tu ndio wanaofikishwa katika mahakama hizo.
Katika uamuzi wake mapema Mwaka huu, Mahakama ya Juu ya #Uganda ilipiga marufuku utaratibu huo, ikisema kuwa ni kinyume cha #Katiba. Serikali ya Museveni iliwasilisha Muswada mpya wa Sheria uliolenga kurejesha utaratibu huo, na Bunge liliupitisha Mwezi uliopita
Soma https://jamii.app/MuseveniMilitaryCourt
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #Democracy
Wanaharakati wa Haki za Binadamu kwa muda mrefu wamekuwa wakilalamika kuwa Serikali imekuwa ikitumia Mahakama za Kijeshi kuwatesa Wapinzani wa Kisiasa wa Museveni, ambaye amekuwa Madarakani kwa takribani Miaka 40. Wasimamizi wake wamekanusha madai hayo, wakisema kuwa ni raia wanaotumia silaha kwa vurugu za kisiasa tu ndio wanaofikishwa katika mahakama hizo.
Katika uamuzi wake mapema Mwaka huu, Mahakama ya Juu ya #Uganda ilipiga marufuku utaratibu huo, ikisema kuwa ni kinyume cha #Katiba. Serikali ya Museveni iliwasilisha Muswada mpya wa Sheria uliolenga kurejesha utaratibu huo, na Bunge liliupitisha Mwezi uliopita
Soma https://jamii.app/MuseveniMilitaryCourt
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #Democracy
Je, Wajua Asilimia 34.4 ya Watu wote Tanzania Bara ni Vijana?
Kwa mujibu wa Takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 (SWM 2022), Tanzania Bara ina Watu 59,851,347, kati ya hao, Vijana ni 20,612,566 sawa na 34.4%
Ni ukweli usiopingika kwamba Vijana ni kundi kubwa na ndilo lenye nguvu za kufanya kazi, ndio watu wenye ubunifu, wenye uthubutu na ujasiri na ndio waliobeba maono ya Taifa, hivyo Mapinduzi makubwa kwenye uchumi, jamii na teknolojia yatafikiwa endapo kila Kijana atashiriki na kujitoa kikamilifu kuleta mawazo mapya, ubunifu na mikakati mipya ya kuchangia maendeleo kwenye jamii yake
Soma https://jamii.app/UwajibikajiWaVijana
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFVijana #RestlessDevelopment #UshirikiWaVijana
Kwa mujibu wa Takwimu za Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 (SWM 2022), Tanzania Bara ina Watu 59,851,347, kati ya hao, Vijana ni 20,612,566 sawa na 34.4%
Ni ukweli usiopingika kwamba Vijana ni kundi kubwa na ndilo lenye nguvu za kufanya kazi, ndio watu wenye ubunifu, wenye uthubutu na ujasiri na ndio waliobeba maono ya Taifa, hivyo Mapinduzi makubwa kwenye uchumi, jamii na teknolojia yatafikiwa endapo kila Kijana atashiriki na kujitoa kikamilifu kuleta mawazo mapya, ubunifu na mikakati mipya ya kuchangia maendeleo kwenye jamii yake
Soma https://jamii.app/UwajibikajiWaVijana
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFVijana #RestlessDevelopment #UshirikiWaVijana
Hakuna mafanikio ya haraka. Unahitaji kuwaza, kupanga na kuendelea kujaribu bila kuchoka. Hii ndo njia ya kuona ndoto yako ikigeuka kuwa kweli
#JamiiAfrica #JamiiForums #Maisha #GoodMorning #AmkaNaJF
#JamiiAfrica #JamiiForums #Maisha #GoodMorning #AmkaNaJF
👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Wakili Peter Kibatala, mmoja wa Mawakili wanaomtetea Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, Tundu Lissu katika shtaka linalomkabili la 'kuchapisha taarifa za uwongo Mtandaoni', amesema walikuwa wamejipanga kumtetea mteja wao kwa kumuuliza maswali shahidi ambaye alianza kutoa Ushahidi wake jana Juni 16, 2025
Kibatala amesema shahidi huyo aliyejitambulisha kwa jina la PF. 22863 Inspekta John, wanamfahamu vizuri na siku atakaporejea Mahakamani wataonesha kitu tofauti
Shahidi huyo akitoa ushahidi Mahakamani, amesema alikutana na picha mjongeo (video) kupitia Akaunti ya YouTube ya Jambo TV, ambayo ilichapishwa Aprili 3, 2025 na kudai alibaini maudhui yenye jinai kupitia matamshi yaliyotolewa na Lissu
Soma https://jamii.app/KibatalaNaShahidi
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights
Kibatala amesema shahidi huyo aliyejitambulisha kwa jina la PF. 22863 Inspekta John, wanamfahamu vizuri na siku atakaporejea Mahakamani wataonesha kitu tofauti
Shahidi huyo akitoa ushahidi Mahakamani, amesema alikutana na picha mjongeo (video) kupitia Akaunti ya YouTube ya Jambo TV, ambayo ilichapishwa Aprili 3, 2025 na kudai alibaini maudhui yenye jinai kupitia matamshi yaliyotolewa na Lissu
Soma https://jamii.app/KibatalaNaShahidi
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights
❤1
Wimbo wa 'My Heart Will Go On' ni kati ya kazi zilizomuongezea umaarufu #CelineDion, ambayo alirekodi akiwa na umri wa Miaka 29, ukiwa maalum kwaajili ya ‘soundtrack’ ya Filamu ya #Titanic iliyotoka Mwaka 1997
Celine aliwahi kuhojiwa na kusema alipofuatwa kwaajili ya kurekodi wimbo huo hakuona kama inamfaa. Alisema“Sikuona kama inanifaa, nilichoka sana siku hiyo. Nilifikiria nimeshafanya ‘soundtrack’ kadhaa, sikutaka kuonekana kazi yangu ni hiyo tu, mume wangu (René Angélil) akanishawishi niimbe demo (wimbo wa awali kabla ya wimbo wenyewe).”
Alieleza kuwa baada ya demo aliondoka studio, hawakurudi tena kwaajili ya kuimba wimbo wenyewe, na hiyo ndiyo ikatengenezwa na kutumika kuwa wimbo rasmi wa Filamu
Soma https://jamii.app/MyHeartWillGoOn
#JFEntertainment #JamiiForums #JamiiAfrica
Celine aliwahi kuhojiwa na kusema alipofuatwa kwaajili ya kurekodi wimbo huo hakuona kama inamfaa. Alisema“Sikuona kama inanifaa, nilichoka sana siku hiyo. Nilifikiria nimeshafanya ‘soundtrack’ kadhaa, sikutaka kuonekana kazi yangu ni hiyo tu, mume wangu (René Angélil) akanishawishi niimbe demo (wimbo wa awali kabla ya wimbo wenyewe).”
Alieleza kuwa baada ya demo aliondoka studio, hawakurudi tena kwaajili ya kuimba wimbo wenyewe, na hiyo ndiyo ikatengenezwa na kutumika kuwa wimbo rasmi wa Filamu
Soma https://jamii.app/MyHeartWillGoOn
#JFEntertainment #JamiiForums #JamiiAfrica
❤1
Israel na Iran wamekuwa wakishambuliana kwa Makombora kwa Siku ya tano mfululizo, baada ya #Israel kufanya mashambulizi ya anga Juni 13, 2025 dhidi ya maeneo ya #Iran, ikiwemo Shirika la Utangazaji la Taifa huko Tehran na vituo vya kurutubisha Urani
Iran ilijibu kwa kurusha Makombora na Ndege zisizo na Rubani (Drones) kuelekea Miji ya Israel, na kusababisha vifo vya raia zaidi ya 220 Nchini Iran na takriban 24 Nchini Israel
Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Pete Hegseth amesisitiza kuwa Marekani iko katika msimamo wa kujilinda, ikiwa tayari kusaidia kufanikisha makubaliano ya amani na kulinda majeshi yake katika eneo hilo lakini si kwa ajili ya kushambulia.
Soma https://jamii.app/IsraelIranMissileTrade
#JamiiForums #JamiiAfrica #Diplomacy #HumanRights #IsraelIranConflict #Diplomacy
Iran ilijibu kwa kurusha Makombora na Ndege zisizo na Rubani (Drones) kuelekea Miji ya Israel, na kusababisha vifo vya raia zaidi ya 220 Nchini Iran na takriban 24 Nchini Israel
Waziri wa Ulinzi wa Marekani, Pete Hegseth amesisitiza kuwa Marekani iko katika msimamo wa kujilinda, ikiwa tayari kusaidia kufanikisha makubaliano ya amani na kulinda majeshi yake katika eneo hilo lakini si kwa ajili ya kushambulia.
Soma https://jamii.app/IsraelIranMissileTrade
#JamiiForums #JamiiAfrica #Diplomacy #HumanRights #IsraelIranConflict #Diplomacy
KENYA: Inaelezwa Askari James Mukhwana ambaye kwa sasa anashikiliwa kwa tuhuma za mauaji ya Mwanaharakati Albert Ojwang’, amesema (OCS), Samson Talaam alitoa amri ya “kumuadhibu” Ojwang, amri ambayo Mukhwana anadai ilitoka kwa Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi, Eliud Lagat
Maelezo hayo, ambayo Citizen TV imeyapata yanadai Mukhwana amesimulia jinsi alivyoitwa Ofisini kwa OCS usiku huo akiwa kazini, na kuelezwa “Kuna agizo kutoka kwa DIG Lagat. Unamfahamu? Kuna Maafisa kutoka Makao Makuu ya DCI wanamleta mtuhumiwa hapa saa mbili Usiku. Waambie wale wafungwa wamuonyeshe adabu kidogo.”
Ojwang alifungiwa ndani Saa tatu na dakika 20 Usiku, muda mfupi baada ya hapo mateso yakaanza kwenye selo ya mwisho karibu na Vyoo. Mukhwana anasema wafungwa wanne, Collins Ireri, Gil Ammiton, Brian Mwaniki na Erick Ndambuki waliagizwa kumshambulia.
Soma zaidi Ushahidi huu https://jamii.app/KonsteboMukhwanaTalks
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #HumanRights #HakiZaBinadamu #Transparency
Maelezo hayo, ambayo Citizen TV imeyapata yanadai Mukhwana amesimulia jinsi alivyoitwa Ofisini kwa OCS usiku huo akiwa kazini, na kuelezwa “Kuna agizo kutoka kwa DIG Lagat. Unamfahamu? Kuna Maafisa kutoka Makao Makuu ya DCI wanamleta mtuhumiwa hapa saa mbili Usiku. Waambie wale wafungwa wamuonyeshe adabu kidogo.”
Ojwang alifungiwa ndani Saa tatu na dakika 20 Usiku, muda mfupi baada ya hapo mateso yakaanza kwenye selo ya mwisho karibu na Vyoo. Mukhwana anasema wafungwa wanne, Collins Ireri, Gil Ammiton, Brian Mwaniki na Erick Ndambuki waliagizwa kumshambulia.
Soma zaidi Ushahidi huu https://jamii.app/KonsteboMukhwanaTalks
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #HumanRights #HakiZaBinadamu #Transparency
❤2🤔1