JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Moses Kunkuyu, Waziri Habari na Digitali wa Malawi amesema Kama Bara la Afrika, hebu tuanze mazungumzo kwa ajili ya Afrika nzima, mazungumzo ya kuhakikisha kwamba Bara letu lote linaunganishwa Kimtandao.

Ameeleza kuwa "Kwa sababu, tukikumbuka yaliyopita: wakati janga la COVID-19 lilipotokea, Watoto wa Nchi zilizoendelea waliendelea na masomo yao kupitia mtandao. Lakini Watoto wa Afrika? Walibaki nyumbani, bila shule, bila intaneti. Tusiruhusu hilo litokee tena"

Ameongeza kuwa "Ikiwa tukio jingine kama hilo litakuja, Kila Mtoto wa Kiafrika lazima aendelee na masomo yake. Kila raia wa Afrika apate Huduma za Afya kwa njia ya mtandao. Ni hapo ndipo tutaweza kusema kwa dhati kuwa: Ajenda ya mabadiliko ya Kidijitali Barani Afrika ni ajenda ya kila Nchi ya Afrika.

Soma https://jamii.app/AfIGF2025Day2

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
1
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa amesema Serikali imeendelea kuweka mazingira wezeshi katika kuwezesha huduma za Mtandao wa simu nchini ambapo ameeleza kwamba kwa sasa Wananchi wanaotumia Mtandao wa 5G ni Asilimia 23.

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Jukwaa la Utawala wa Mtandao (IGF) Mei 30, 2025 amesema "Tumeweka mazingira wezeshi ya uwekezaji, jambo lililowezesha huduma za mtandao wa simu kufikia 92% (3G), 91% (4G), 23% (5G) ya Wananchi."

Ameongeza "Lengo letu ni kuongeza matumizi ya TEHAMA ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa Kidijitali na kuboresha maisha ya Wananchi katika maeneo ya mijini na vijijini.”

Soma https://jamii.app/AfIGF2025Day2

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
Akizungumza katika Mkutano wa Jukwaa la 14 la Utawala wa Mtandao Afrika, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa, amesema pochi ya Kidijitali, ni kama ile Pochi ya kawaida tu ambapo Mtu huhifadhi pesa zake, kadi za Benki, na Vitambulisho. Ni programu salama iliyounganishwa na inayomruhusu Mtu kuhifadhi, kutuma, kupokea, na kusimamia Fedha zake katika Mfumo wa Kidijitali.

Ameeleza hii inawasaidia sana Wajasiriamali kwa kurahisisha njia ya kufanya Biashara, na pia kurahisisha upatikanaji wa Mitaji.

Amesema "Kama unavyojua, ukienda Benki za kawaida kuomba mkopo, unalazimika kujaza fomu, kuandaa ripoti – na mara nyingine ripoti hizo zinaweza kuwa za kughushi. Lakini sasa, kupitia pochi ya Kidijitali iliyounganishwa, ni rahisi kupata Huduma za Kifedha kwa njia ya Mtandao, na kwa haraka.

Fuatilia https://jamii.app/AfIGF2025Day2

#JamiiAfrica #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Rais Samia Suluhu ameagiza mchakato wa kuchuja Wagombea ndani ya Chama Cha Mapinduzi (#CCM) ufanyike kwa haki ili kuzuia chama hicho kisiwe ‘Gwajiminized’

Amesema hayo Mei 30, 2025 wakati wa Mkutano Maalum wa CCM, katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete

Soma https://jamii.app/RaisSamiaGwajima

#JamiiForums #Siasa #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025
1
Lamin Jabbi, Waziri wa Mawasiliano na Uchumi wa Kidigitali Nchini Gambia, amesema ni muhimu sana kutambua Teknolojia zinazobadilisha Mifumo (disruptive technologies) ambazo tayari zipo na zinakuja Afrika

Ameeleza kuwa "ni muhimu kuwa na msimamo wa pamoja kama Nchi za Afrika katika kukabiliana na changamoto hizi. Hatupaswi kukabiliana na changamoto hizo kama nchi moja-moja, bali kwa mtazamo wa pamoja wa Afrika."

Amesisitiza kuwa "Tunahitaji kuelewa kwamba kuendeleza Miundombinu ya Kidijitali si jambo la mara moja au la mwisho, ni mchakato unaoendelea, kwani Teknolojia hubadilika mara kwa mara. Ni muhimu sana kutambua mabadiliko hayo na tuyakabili kwa mtazamo wa Kiafrika. Hili haliwezi kufanywa na Nchi moja au mbili – lazima tufanye kama Bara moja lenye msimamo mmoja.

Soma https://jamii.app/AfIGF2025Day2

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mwenyekiti wa Kamati Ndogo ya Kamati Kuu ya Kuandaa Ilani ya CCM ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025, Prof. Kitila Mkumbo, akiwasilisha Ilani hiyo ya Uchaguzi Mkuu wa 2025 amesema sehemu kubwa ya maudhui yametokana na maoni ya Wanachama wa CCM, Wananchi na wadau mbalimbali

Amesema Chama kitaelekeza Serikali kuimarisha Demokrasia na Utawala Bora ikiwemo kuuhisha na kukamilisha mchakato wa Katiba Mpya

Soma https://jamii.app/KatibaMpyaCCM

#JamiiForums #Siasa #Kuelekea2025 #JamiiAfrica #UchaguziMkuu2025
1
Mdau wa masuala ya Usalama Kidigitali, Ihueze Nwobilor amesema “Usalama wa Kidijitali ni muhimu sana na tunapaswa kuhakikisha kuwa hata wale wasiojua kusoma na kuandika wanaweza kutumia kwa urahisi.”

Ameongeza kuwa ni muhimu kutengeneza Mifumo na Vifaa ambavyo hata Watu wa Kijijini wasiojua Kusoma na Kuandika ila wana Vifaa vya Kieletroniki wanaweza kutumia humu wakizingatia Usalama wa Kimtandao wa taarifa zao

Ameeleza “Nchini kwangu tunatoa Elimu kuhusu Usalama Mtandaoni lakini ukimwambia Mtu wa Kijijini kuhusu “Two factor authentication” hawezi kukuelewa”

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
3
Naibu Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia za Digitali Afrika Kusini, Mondli Gungubele akielezea Mafanikio ya Nchi hiyo katika Mifumo ya Kidigitali amesema, Mabadiliko ya Kidijitali ya Afrika Kusini yanaendelea kwa kasi na yana Mafanikio

Ameeleza Mafanikio ya Kidijitali ya Afrika Kusini yanajumuisha: Upatikanaji wa Kitaifa wa Usafiri wa Kidijitali, unaosaidia Mamlaka kufuatilia taarifa za Trafiki (foleni ya barabarani) kwa wakati halisi, pia kuna Mfumo wa malipo wa kisasa, unaowezesha Miamala kufanyika papo kwa papo (instant to instant transactions)

Ameongeza kuwa Mashirika kama Interpol na wadau wengine yanatumia Huduma za Kidijitali kufuatilia na kudhibiti taarifa za Kijasusi za kuvuka mipaka

Soma https://jamii.app/AfIGF2025Day2

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
1
Leo ni Siku ya Mwisho ya Mkutano wa Jukwaa la Utawala wa Intaneti Afrika (AfIGF) 2025, unaofanyika katika Ukumbi wa JNICC, Dar es Salaam

Kwa siku 3, wadau mbalimbali kutoka barani Afrika wamekutana kujadili mustakabali wa usimamizi wa intaneti kuanzia haki za kidijitali, usalama mtandaoni, sera, hadi ushirikishwaji wa vijana na makundi maalum.

JamiiAfrica inajivunia kuwa sehemu ya mijadala yenye tija, kubadilishana uzoefu, na kujifunza namna bora ya kuhakikisha intaneti salama, jumuishi na endelevu kwa wote

Kufuatilia bofya https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
👍1
Leo Mei 31, 2025, JamiiAfrica inashiriki kwenye Majadiliano yanayogusia Upatikanaji wa Mtandao kwa Wote pamoja na AI na Teknolojia zinazoibuka, kwa kusisitiza jukumu muhimu la upatikanaji wa Intaneti katika kuvunja Unyanyapaa unaozunguka matatizo ya Afya ya akili na kujenga jamii zenye uthabiti na usaidizi wa kweli

Wadau watajadili unyanyapaa unaohusiana na Afya ya Akili na kutoa Elimu kwa washiriki kuhusu asili yake ikiwa ni pamoja na mitazamo ya kitabibu, kiroho na kisaikolojia.

Teknolojia kama vile Akili Mnemba (AI) inaweza kutumika kuongeza uelewa, kutoa msaada wa mapema na kujenga mifumo rafiki ya Kidijitali inayosaidia Watu wanaokumbwa na changamoto za Afya ya Akili bila kuhukumiwa

Kufuatilia bofya https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
Imeelezwa #Tanzania imepiga hatua katika ujenzi wa Miundombinu ya TEHAMA, ikiwa ni pamoja na Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano wenye urefu wa Kilomita 13,820 (NICTBB) unaounganisha Mikoa na Wilaya zote, pamoja na kuunganisha Nchi za #Kenya, #Uganda, Rwanda, #Burundi, Zambia, #Malawi, na Msumbiji, ambapo sasa inajiandaa kuunganisha DR Congo kupitia Ziwa Tanganyika

Takwimu hizo ni kwa mujibu wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, ambayo imesema Tanzania ni miongoni mwa Nchi zinazoongoza katika Ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuwa na Mtandao mkubwa wa nyaya za nyuzi za Mawasiliano (Fiber optic)

Hayo yameelezwa katika ufunguzi wa Mkutano wa Jukwaa la 14 la Utawala wa Mtandao Afrika (AfIGF 2025), Mei 30, 2025, unaoendelea katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC)

Soma https://jamii.app/AfIGF2025Day2

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
2
Akizungumza katika Mkutano wa Jukwaa la 14 la Utawala wa Mtandao Afrika, Seneta wa Kenya amesema mara nyingine Watawala au Mamlaka hazina hisia, hawajui changamoto au hali halisi ya Kijinsia, na wanapobuni Sera au zana, mara nyingi ni mzigo unaobebwa na Wanawake

Ameongeza kuwa Idara za Kijinsia zinapaswa kuwa bora zaidi, zinapaswa kuelewa kuwa hazipaswi kutengwa kama idara za pembeni, bali ni Wataalamu wa Sekta mbalimbali wanaopaswa kutoa mwongozo kwa Wizara ya Afya, Wizara ya Maji, Wizara ya Kilimo, n.k.

Ameongeza kwa kusema “Kila Nchi inakuwa na muundo wake wa kukabiliana na changamoto za mambo ya Kijinsia, katika Dunia ya Kiditali, nafikiri kuna mambo yanatakiwa kufanyiwa zaidi”

Zaidi https://jamii.app/AfIGF2025Day2

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
1
Seneta wa Kenya, Catherine Mumma amesema suala la jinsia katika mifumo limekuwa likibaki nyuma, kwa sababu ukiangalia mgawanyo wa masuala mbalimbali kama miundombinu, ushirikishwaji wa Wanawake nakadhalika utagundua kuwa Wanawake bado hawajajumuishwa ipasavyo.

Amesema kuwa Wanawake wanabaki nyuma katika jamii zetu iwe ni katika masomo na hata sasa katika ushiriki wa Teknolojia ya Kidijitali, au Uchumi na biashara za Kidijitali na hata katika tasnia wanazoendesha na kumiliki

Amesema kwa mtazamo wake jambo jema kufanya mazungumzo kuhusu Wanawake kwa sababu yanaweza kuwa na msaada katika kubadilisha Jamii kama yataungizwa kwenye mifumo na kufanyiwa kazi

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
1
Akizungumza katika Mkutano wa Jukwaa la 14 la Utawala wa Mtandao, Dkt Sabra Hussein kutoka Tanzania AI Community amesema “Unakuta Wanawake wa Vijijini labda Mkoani Kilimanjaro, wanatumia programu za Simu kujua wanapoweza kupata msaada lakini wanakutana na changamoto kwasababu vifaa vingi vya AI vipo kwa Kiingereza na hazijabadilishwa kuendana na Mazingira wa kienyeji.”

Amesema kuwa, Kuna baadhi ya Mifumo ya kuomba Ajira, Mwanamke anapojaribu kutumia programu hizo kutafuta kazi, hazitamtambua kwa usawa na inaweza kumuathiri

Hali hiyo Matokeo yake ni Wanawake kutopata nafasi sawa za Ajira kama Wanaume, na hivyo kuongeza pengo la Kiuchumi na Ajira kati ya Jinsia

Zaidi https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
Dorris Magiri (Kijiji Link) amesema “Siku hizi wengi wetu tunaona ni bora kuzungumza na Simu zetu badala ya kuzungumza na Watu. Mtu akiwa na jambo anaamini sana kwenda kuiambia ChatGPT badala ya kumwambia Rafiki yake”

Amesema "tunatakiwa kujiuliza kwamba Je, tunaweza kuiamini AI? Jibu ni kwamba Binadamu tayari anaiamini AI. Nadhani tunatakiwa kurejesha ule Muunganiko wa Kibinadamu, tuzungumze na Watu wetu wa karibu kuhusu yale tunayoyapitia Kihisia"

"Tujenge Mfumo wa kweli wa kusaidia Afya ya Akili kwa kutumia AI kwa Uangalifu, kwa kushirikiana na Watu wenye uzoefu, na tukikumbuka Hekima ya Kiafrika"

Zaidi https://jamii.app/SikuYaMwishoIGF

#JamiiAfrica #AfIGF2025 #UadilifuWaTaarifa #MaendeleoYaKidijitali #HakiZaKidijitali #UsalamaMtandaoni #UpotoshajiWaTaarifa #UtawalaWaMtandao #Uwajibikaji #DigitalRights
1
Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Mary Gervas Matogolo (22), amewekwa mahabusu baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana kufuatia kesi ya Jinai inayomkabili yeye na Wanafunzi wenzake wawili, wakidaiwa kumshambulia mwenzao kwa kumgombania Msanii na Mtangazaji wa Redio, Burton Mwemba maarufu Mwijaku

Mary na wenzake, Ryner Ponci Mkwawili wa Chuo Kikuu Ardhi na Asha Suleiman Juma wa Chuo cha Uhasibu Tanzania (TIA), walisomewa mashtaka 8 yakiwemo kusababisha madhara ya Mwilini, kutishia kuua, kusambaza taarifa za uongo kupitia Mitandao ya Kijamii na Uharibifu wa Mali

Ryner na Asha walitimiza masharti hayo na kuachiwa kwa dhamana, Mary alishindwa kutimiza vigezo na hivyo kupelekwa mahabusu hadi Juni 13, 2025, kesi hiyo itakapotajwa tena

Soma https://jamii.app/MaryDhamana

#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #HumanRights #JFWomen #SocialJustice
1