MWANZA: Kampuni ya Meli Tanzania (TASHICO) imesema Meli ya New MV Victoria inatarajiwa kuanza safari zake rasmi leo Alhamisi Mei 22, 2025 ikitokea Bandari ya Mwanza Kaskazini kuelekea Bandari ya Bukoba kupitia Bandari ya Kemondo
Itakuwa mara ya kwanza meli hiyo kufanya safari baada ya kusimamisha huduma kwa miezi miwili ambapo TASHICO imewataka abiria kufika bandarini Saa 1:30 Jioni au kabla ya muda huo kwa kuwa meli inatarajiwa kuanza safari Saa 3:00 Usiku
Ikumbukwe Machi 10, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alihoji ukimya wa Mamlaka kuhusu meli hiyo kusitisha huduma, TASHICO ikajitokeza na kueleza ipo katika matengenezo ya mwezi mmoja, baadaye ikaeleza maboresho yanaenda.
Soma https://jamii.app/MvVictoriaReturn
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #ServiceDelivery
Itakuwa mara ya kwanza meli hiyo kufanya safari baada ya kusimamisha huduma kwa miezi miwili ambapo TASHICO imewataka abiria kufika bandarini Saa 1:30 Jioni au kabla ya muda huo kwa kuwa meli inatarajiwa kuanza safari Saa 3:00 Usiku
Ikumbukwe Machi 10, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alihoji ukimya wa Mamlaka kuhusu meli hiyo kusitisha huduma, TASHICO ikajitokeza na kueleza ipo katika matengenezo ya mwezi mmoja, baadaye ikaeleza maboresho yanaenda.
Soma https://jamii.app/MvVictoriaReturn
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #ServiceDelivery
PWANI: Mdau wa JamiiForums.com anahoji ni kwa nini Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) halichukui hatua au kukagua uharibifu wa mazingira unaofanywa na Kiwanda cha Pombe kilichopo Misugusugu Kibaha ikiwa Wananchi wameshalalamika mara kadhaa kwa Mamlaka hiyo?
Anadai maji hayo machafu yamekuwa na athari kwa viumbe wanaoishi au kutumia mabwawa madogo yaliyopo jirani
Soma https://jamii.app/MazingiraKibaha
#JamiiForums #ClimateChange #Accountability
Anadai maji hayo machafu yamekuwa na athari kwa viumbe wanaoishi au kutumia mabwawa madogo yaliyopo jirani
Soma https://jamii.app/MazingiraKibaha
#JamiiForums #ClimateChange #Accountability
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
UCHUMI: Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Emmanuel Akaro amesema "Kwa Mwaka huu fedha za kigeni zilizopo kwenye soko zimeongezeka ukilinganisha na Mwaka uliopita (2024), tulikuwa na Dola Milioni 30 kwa siku, sasa hivi tuna Dola Milioni 70 kwa siku."
Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza katika Semina ya Waandishi wa Habari iliyofanyika Mei 20, 2025 katika ofisi za Benki Kuu, Dar es Salaam
Soma https://jamii.app/MarufukuFedhaKigeniManunuzi
#JamiiForums #JFUchumi
Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza katika Semina ya Waandishi wa Habari iliyofanyika Mei 20, 2025 katika ofisi za Benki Kuu, Dar es Salaam
Soma https://jamii.app/MarufukuFedhaKigeniManunuzi
#JamiiForums #JFUchumi
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
KAGERA: Baada ya ujenzi wa Daraja la Mto Kanoni kuonekana unasuasua kwa madai ya ujenzi holela kando ya Mto huo, Mkuu wa Mkoa, Fatma Mwassa ameelekeza TANROADS na Manispaa ya Bukoba kufanya vipimo kubaini usahihi wa kingo za Mto huo
Ikumbukwe Januari 6, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alieleza ujenzi holela maeneo hayo mfano jengo la 'Night Club & Bar' limejengwa katika eneo la Hifadhi ya Mto Kanoni, akahoji Mamlaka zinatoaje kibali cha ujenzi wakati sehemu hiyo sio salama kwa Watu
Soma https://jamii.app/DarajaMtoKanoni
#JamiiForums #Accountability
Ikumbukwe Januari 6, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alieleza ujenzi holela maeneo hayo mfano jengo la 'Night Club & Bar' limejengwa katika eneo la Hifadhi ya Mto Kanoni, akahoji Mamlaka zinatoaje kibali cha ujenzi wakati sehemu hiyo sio salama kwa Watu
Soma https://jamii.app/DarajaMtoKanoni
#JamiiForums #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Kaulimbiu ya Mwaka 2025 ikiwa ni "Kuimarisha Mustakabali wa Kidijitali wa Afrika" mada mbalimbali zitajadiliwa ikiwemo Miundombinu ya Umma ya Kidijitali na Utawala wa Taarifa, Usalama Mtandaoni, Uhimilivu na Uaminifu pamoja na Akili Mnemba (AI) na Teknolojia Zinazoibuka katika Jukwaa la 14 la Utawala wa Mtandao Afrika utakaofanyika kuanzia Mei 29 hadi Mei 31, 2025 Jijini Dar es Salaam.
#AfIGF2025 #AfricalGF #KuimarishaKidijitaliAfrika #JamiiForums
#AfIGF2025 #AfricalGF #KuimarishaKidijitaliAfrika #JamiiForums
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mdau wa JamiiForums.com anasema Barabara ya Tabata - Kimanga kutokea Tabata Bima imeharibika sana hasa kutokea Chama mpaka Mawenzi
Anaeleza kuwa Gari nyingi zinaharibika kila Siku na kipindi cha Mvua baadhi ya Daladala zinashusha Abiria au kukatisha ruti kwasababu hakupitiki, hivyo Mamlaka husika iangalie namna ya kurekebisha changamoto hiyo
Soma https://jamii.app/RoadTabataBimaKimanga
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #ServiceDelivery #HudumaZaKijamii
Anaeleza kuwa Gari nyingi zinaharibika kila Siku na kipindi cha Mvua baadhi ya Daladala zinashusha Abiria au kukatisha ruti kwasababu hakupitiki, hivyo Mamlaka husika iangalie namna ya kurekebisha changamoto hiyo
Soma https://jamii.app/RoadTabataBimaKimanga
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #ServiceDelivery #HudumaZaKijamii
❤1
Kwenye Elimu kidogo umetupa ahueni japo Mazingira ya Shuleni magumu ila kwenye Afya unanikamua haswa, Umeme nako mpaka nimeshindwa kuunganisha Nyumbani, Maji siyaoni. Kwani unafanya Biashara kwamba unahitaji faida? Nakuchangia kwa kila ninachopata kwani unazipeleka wapi mbona sioni matumizi yake
Ila niliambiwa waliopo kwenye ‘System’ wanazifaidi, hivi ni kweli? Maana wakipoteza Mabilioni wanaambiwa walipe faini Milioni, inashangaza.
Hili ni Andiko liliwasilishwa kwenye Shindano la Stories of Change 2023 na unaweza kulisoma zaidi kwa kubofya hapa https://jamii.app/TabasamuTZSOC03
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #SOC2023
Ila niliambiwa waliopo kwenye ‘System’ wanazifaidi, hivi ni kweli? Maana wakipoteza Mabilioni wanaambiwa walipe faini Milioni, inashangaza.
Hili ni Andiko liliwasilishwa kwenye Shindano la Stories of Change 2023 na unaweza kulisoma zaidi kwa kubofya hapa https://jamii.app/TabasamuTZSOC03
#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #SOC2023
👍2
Mdau wa Jukwaa la Biashara, Uchumi na Ujasiriamali ndani ya JamiiForums.com amesema Watu wachache wako tayari kuingia kwenye gharama ya kujifunza kidogo na kuwa na moyo usiokata tamaa ndiyo maana matajiri ni wachache kwa kisingizio cha kauli ya "Sina Mtaji wa Biashara"
Je, unakubaliana na Mdau huyu?
Mjadala zaidi https://jamii.app/MtajiSioMafanikio
#JamiiForums #Lifestyle #Biashara
Je, unakubaliana na Mdau huyu?
Mjadala zaidi https://jamii.app/MtajiSioMafanikio
#JamiiForums #Lifestyle #Biashara
UGANDA: Kituo cha Utafiti cha Agora kimethibitisha kuwa Mkurugenzi wao, Agather Atuhaire amepatikana katika Mpaka wa Uganda na Tanzania (Mutukula) leo asubuhi Mei 23, 2025 akiwa hai
Taarifa ya Agora kupitia Mtandao wa X imesema kuwa "Tunafarijika kuufahamisha Umma kuwa amepatikana. Alitelekezwa mpakani na Mamlaka ya Tanzania. Maelezo zaidi yatatolewa baadaye leo. Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mtu ambaye alisimama kwa mshikamano wakati huu. Juhudi zako zilifanya mabadiliko."
Ikumbukwe kuwa wanaharakati Agather Atuhaire na Boniface Mwangi kutoka Kenya walishikiliwa Jijini Dar es Salaam ambapo walienda fuatilia kesi inayomkabili Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu
Soma https://jamii.app/AgatherAkutwaMpakani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Diplomacy #HumanRights
Taarifa ya Agora kupitia Mtandao wa X imesema kuwa "Tunafarijika kuufahamisha Umma kuwa amepatikana. Alitelekezwa mpakani na Mamlaka ya Tanzania. Maelezo zaidi yatatolewa baadaye leo. Tunatoa shukrani zetu za dhati kwa kila mtu ambaye alisimama kwa mshikamano wakati huu. Juhudi zako zilifanya mabadiliko."
Ikumbukwe kuwa wanaharakati Agather Atuhaire na Boniface Mwangi kutoka Kenya walishikiliwa Jijini Dar es Salaam ambapo walienda fuatilia kesi inayomkabili Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu
Soma https://jamii.app/AgatherAkutwaMpakani
#JamiiForums #JamiiAfrica #Diplomacy #HumanRights
DAR: Makamu Mwenyekiti wa Chama cha #ACTWazalendo, Isihaka Mchinjita amekamatwa na Jeshi la Polisi, leo Mei 23, 2025 baada ya kuingia kwenye Kituo cha Mwendokasi cha Kimara Mwisho kwa lengo la kujionea adha ya usafiri huo
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Naibu Katibu wa Habari na Uenezi wa ACT, Shangwe Ayo amesema “ACT tumekuwa tukipata malalamiko mara nyingi ya malalamiko ya Usafiri wa Mwendokasi kutoka kwa Wananchi hasa wa Kimara, hivyo Baraza Kivuli la Mawaziri tulikwenda kujionea, kukagua na kufichua madudu yanayoendelea katika huduma hiyo, ndipo Askari Polisi wakafika na kumkamata."
Ameongeza "Amekamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi Kimara, aliongozana na Mlinzi wake na Mwandishi wa Habari, tunafuatilia kujua kinachoendelea, tutatoa taarifa kamili baadaye.”
Zaidi https://jamii.app/MchinjitaAkatwaKimara
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Naibu Katibu wa Habari na Uenezi wa ACT, Shangwe Ayo amesema “ACT tumekuwa tukipata malalamiko mara nyingi ya malalamiko ya Usafiri wa Mwendokasi kutoka kwa Wananchi hasa wa Kimara, hivyo Baraza Kivuli la Mawaziri tulikwenda kujionea, kukagua na kufichua madudu yanayoendelea katika huduma hiyo, ndipo Askari Polisi wakafika na kumkamata."
Ameongeza "Amekamatwa na kupelekwa Kituo cha Polisi Kimara, aliongozana na Mlinzi wake na Mwandishi wa Habari, tunafuatilia kujua kinachoendelea, tutatoa taarifa kamili baadaye.”
Zaidi https://jamii.app/MchinjitaAkatwaKimara
#JamiiForums #JamiiAfrica #Governance
👍1
ZANZIBAR: Mdau wa JamiiForums.com anasema Mamlaka zimekuwa zikifungia Watu Nyumba kwasababu ya uchafu katika maeneo ya Kilimahewa na Jang'ombe lakini kwanini Wakazi wa Nyumba za Michenzani zinazoweka Afya za Watu hatarini zimekuwa hazichukuliwi hatua?
Soma https://jamii.app/MajitakaMichenzani
#JamiiForums #Accountability #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Governance
Soma https://jamii.app/MajitakaMichenzani
#JamiiForums #Accountability #JamiiAfrica #Uwajibikaji #Governance
Tembelea Mjadala huu kuona majibu ya Wadau wa JamiiForums.com kuhusu maana ya Ndwele https://jamii.app/NdweleNinini
#JamiiForums #JamiiAfrica #Maisha #QuestionOftheDay #JFChitChats #JFStories
#JamiiForums #JamiiAfrica #Maisha #QuestionOftheDay #JFChitChats #JFStories
MAREKANI: Serikali ya Rais #DonaldTrump imekizuia Chuo Kikuu cha Harvard kuandikisha Wanafunzi wa Kigeni ambapo inaelezwa imechukua hatua hiyo kwa kuwa #Harvard inaiunga Mkono Palestina pamoja na kushirikiana na Chama cha Kikomunisti cha China
Barua iliyoelekezwa kwa Uongozi wa Chuo hicho inaeleza kuwa Cheti cha Usajili cha Mpango wa Kubadilishana Wageni (Student Exchange Visitor Program – SEVP) cha Chuo hicho kimefutwa rasmi
Chuo cha Harvard kina jumla ya Watu 9,970 katika kundi lake la Taaluma ya Kimataifa na takwimu zinaonesha Wanafunzi wa Kimataifa 6,793 wanachangia 27.2% ya Usajili wake kwa Mwaka wa Masomo wa 2024–2025
Soma https://jamii.app/HarvardBannedOutsiders
#JamiiForums #Governance #Diplomacy #JamiiAfrica
Barua iliyoelekezwa kwa Uongozi wa Chuo hicho inaeleza kuwa Cheti cha Usajili cha Mpango wa Kubadilishana Wageni (Student Exchange Visitor Program – SEVP) cha Chuo hicho kimefutwa rasmi
Chuo cha Harvard kina jumla ya Watu 9,970 katika kundi lake la Taaluma ya Kimataifa na takwimu zinaonesha Wanafunzi wa Kimataifa 6,793 wanachangia 27.2% ya Usajili wake kwa Mwaka wa Masomo wa 2024–2025
Soma https://jamii.app/HarvardBannedOutsiders
#JamiiForums #Governance #Diplomacy #JamiiAfrica
👍1👎1