JamiiForums
52.6K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Jukwaa la 14 la Afrika kuhusu Utawala wa Mtandao (AfIGF) linalotarajiwa kufanyika kuanzia Mei 29 hadi 31 Mei 2025 Jijini Dar es Salaam litawakutanisha Wadau kutoka Sekta mbalimbali ikiwemo Serikali, Sekta Binafsi, Asasi za Kiraia, Watafiti na Vijana kwa lengo la kujadili kwa kina masuala ya maendeleo ya Kidijitali Barani Afrika

#AfIGF2025 #AfricalGF #KuimarishaKidijitaliAfrika #JamiiForums
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Serikali imetoa fedha Tsh. Bilioni 6 kwa ajili ya kujenga ofisi mpya ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, ambayo itajengwa eneo la Magomeni

Pia, imetoa magari mawili mapya kwa Katibu Tawala Mkoa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala yenye thamani ya Tsh. Milioni 639 huku Mkuu wa Mkoa wa Dar, Albert Chalamila akisema bado wanahitaji magari mengine zaidi.

Soma https://jamii.app/OfisiMpyaDar

#JamiiForums #Governance #Transparency
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
UCHUMI: Mkurugenzi wa Masoko ya Fedha Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Emmanuel Akaro amesema kwa mujibu wa kanuni za Matumizi ya Fedha za Kigeni za Mwaka 2025 bei na malipo ya bidhaa na huduma zote ndani ya nchi yanapaswa kufanyika kwa Shilingi ya Tanzania

Ameongeza kwa kusema ni kosa la Kisheria kunukuu, kutangaza au kubainisha bei kwa kutumia fedha za kigeni; kulazimisha, kuwezesha au kupokea malipo kwa fedha za kigeni; au kukataa malipo yanayofanyika kwa Shilingi ya Tanzania

Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza katika semina ya Waandishi wa Habari iliyofanyika Mei 20, 2025 katika Ofisi za Benki Kuu, Dar es Salaam

Soma https://jamii.app/MarufukuFedhaKigeniManunuzi

#JamiiForums #JamiiAfrica #JFUchumi
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Jerry Silaa amesema kilichoingiliwa ni akaunti za Mitandao ya Taasisi na sio Mifumo ya Serikali, akilihakikishia Bunge kuwa Mifumo ya #TEHAMA ipo salama na akaunti tayari zimerejeshwa

Akizungumza #Bungeni, leo Mei 21, 2025, Waziri Silaa ametoa kauli hiyo wakati akijibu swali la Mbunge wa Makete, Festo Sanga, ambapo amesema akaunti hizo ziliingiliwa kutokana na udhaifu wa taratibu za kiusalama katika usimamizi wa akaunti.

Soma https://jamii.app/KudukuliwaAkauntiJerry

#JamiiForums #JamiiAfrica #OnlineSafety #CyberSecurity #CyberAttacks
Ajali ya MV Bukoba ilitokea Mei 21, 1996 katika Ziwa Victoria ambapo taarifa za vyanzo mbalimbali zilionesha Meli hiyo ilitengenezwa na Kampuni ya Kibelgiji na ikazinduliwa Julai 27, 1979. Siku ya uzinduzi, ilibainika haikuwa thabiti na ilikosa uwiano.

Ili kupunguza Majanga ya Ajali Nchini, tunajifunza kutokana na makosa au tunaendelea kuyapuuza?

Soma https://jamii.app/MVBukobaMei21

#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHistoria #MVBukoba
👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Serikali kupitia Waziri ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Innocent Bashungwa imeonya wanaopanga au wanaotarajia kuvuruga Amani wakati wa Uchaguzi Mkuu 2025 na kwamba Vyombo vya Dola vimejipanga kuhakikisha Uchaguzi unafanyika katika mazingira ya Amani na Utulivu

Akijibu swali la Mbunge wa Malinyi, Antipas Mgungusi aliyeomba kuongezewa Gari la Polisi ili kuimarisha Ulinzi katika Jimbo lake, #Bungeni, leo Mei 20, 2025, Waziri Bashungwa amesema Serikali haitasita kuchukua hatua kali za kisheria kwa yeyote atakayebainika kupanga au kuchochea vurugu wakati wa Uchaguzi.

Soma https://jamii.app/BashungwaPolisiUchaguzi

#JamiiForums #JamiiAfrica #Democracy #UchaguziMkuu2025 #Governance
👍1
Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC) umeeleza Mwanaharakati kutoka Kenya Boniface Mwangi, pamoja na Mwanasheria kutoka Uganda, Agather Atuhaire bado hawajapata taarifa kamili wako wapi baada ya kushikiliwa na Jeshi la Polisi

Mratibu wa #THRDC Kitaifa, Wakili Onesmo Olengurumwa amesema Mawakili walipewa taarifa jana, Mei 20, 2025 na Jeshi la Polisi kwamba taratibu za kuwarudisha wawili hao kwenye Nchi zao zimekamilika lakini hawaelewi kwanini bado wameendelea kubaki nao mpaka sasa

Mwangi na Atuhaire walikuja Tanzania kufuatilia kesi inayomkabili Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu, iliyosikilizwa Mei 19, 2025 katika Mahakama ya Kisutu.

Soma https://jamii.app/MwangiAtuhaireTHRDC

#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #Diplomacy
Mei 21 kila mwaka Maadhimisho ya Siku ya Chai Duniani.

Mdau unazifahamu aina ngapi za chai?

Mjadala zaidi https://jamii.app/AinaNgapiChai

#JamiiForums #InternationalTeaDay #JFChitChats
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Lawrence Tax akiwasilisha makadirio ya Bajeti ya Wizara yake, jana Mei 20, 2025 amewataka Watanzania kuendelea kuliamini Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kulipa uhuru na kuliwezesha kutekeleza majukumu yake bila kuingiliwa

Soma https://jamii.app/WaziriTaxNukuu

#Governance #JamiiForums #Accountability #Transparency #JFNukuu #JFQuote
Vipi Mdau, ulizingatia nini kwenye kumpa Mtoto wako Jina?

Jina ulilopewa na Wazazi/Walezi wako limewahi kukuletea usumbufu wowote Maishani mwako?

Mjadala zaidi https://jamii.app/JinaMtotoKitaa

#JamiiForums #JamiiAfrica #Maisha #JFChitChats #JFStories #Malezi #Parenting
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mbeya Kusini kimetangaza kuvunja rasmi kambi iliyokuwa imewekwa kushinikiza kupatikana kwa Kada wao, Mpaluka Said Nyagali (Mdude) aliyetoweka tangu Mei 02, 2025

Ikumbukwe Mdude anadaiwa kuvamiwa na kupigwa nyumbani kwake, Mtaa wa Iwambi Jijini hapo, hajapatikana huku CHADEMA ikitumia njia tofauti kumtafuta Mwanaharakati huyo bila mafanikio

Akizungumza na Gazeti la Mwananchi, Mei 21, 2025, Mwenyekiti wa Chama hicho Mkoa wa Mbeya, Masaga Kaloli amesema baada ya kupata vitisho ikiwamo kumwagiwa vitu vinavyodhaniwa kuwa ni sumu, wameona harakati za kumpigania Mdude zihamie nyumbani ili kuokoa maisha ya wengine.

Soma https://jamii.app/KambiMdudeKuvunjwa

#JamiiForums #HumanRights #Governance #KuelekeaUchagua2025
👍2
Mwandishi wa Andiko hili la Stories of Change 2022 anasema Watu wanaoingia Madarakani wanapaswa kutunza Amani ya Nchi, Kuhamasisha Uzalendo, kuleta Mabadiliko bora, Fursa kwa Haki na Usawa, Haki za Binadamu kuzingatiwa na Utawala bora kutekelezwa kwa misingi thabiti

Soma zaidi https://jamii.app/KigodaUzalendo

#JamiiForums #JamiiAfrica #SOC2022 #Democracy #Governance
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Mkurugenzi wa Uchaguzi, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Ramadhani Kailima amewataka Watanzania kuitumia siku ya leo Mei 22, 2025 ambayo ni ya mwisho kujiandikisha katika Vituo vya Wapiga Kura ili waweze kupata haki zao za kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 2025

Amesema hayo alipotembelea Vituo katika Jimbo la Dodoma Mjini na Mtumba kukagua zoezi la uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili

Soma https://jamii.app/KujiandikishaMwisho

#JamiiForums #Kuelekea2025 #UchaguziMkuu2025 #Democracy
Mdau wa JamiiForums.com anasema Mfundishe Mwanao awe anasalimia Watu wadogo kwa wakubwa pamoja na Kuwaheshimu Wageni au Jamaa mnaokaa nao hapo Nyumbani. Asiwadharau kwa namna yoyote hasa watakapomkanya jambo kwa namna ya kumfunza

Jifunze mengi zaidi ya kumfundisha Mwanao hapa https://jamii.app/MfundisheMwanaoYafaida

#JamiiForums #JamiiAfrica #Malezi #Maisha #JFStories #JFChitChats
2