#MAISHA: Mdau wa JamiiForums.com anasema licha ya kuwa ana Marafiki wengi ila anaye Rafiki mmoja ambaye walijuana tangu Shule ya Msingi, na huwa wanakwaruzana na kupotezeana kwa muda ila baadaye wanasameheana na Maisha yanaendelea
Vipi Mdau, nawe unaye Rafiki ambaye hata mkigombana bado Urafiki wenu huwa unaendelea?
Shiriki Mjadala huu zaidi https://jamii.app/UrafikiUsiokwisha
#JamiiForums #JFChitChats #JFStories #JamiiAfrica #LongtimeFriendship
Vipi Mdau, nawe unaye Rafiki ambaye hata mkigombana bado Urafiki wenu huwa unaendelea?
Shiriki Mjadala huu zaidi https://jamii.app/UrafikiUsiokwisha
#JamiiForums #JFChitChats #JFStories #JamiiAfrica #LongtimeFriendship
❤1👍1
Maisha yanaendeshwa na Imani na Matumaini, hata kama hauna hakika ya kesho. Ishi bila woga huku ukiamini kesho itakuja na utakuwa tayari kuikabili.
Tunakutakia Mapumziko mema ya mwisho wa Wiki
#JamiiForums #JamiiAfrica #GoodMorning #AmkaNaJF #Maisha
Tunakutakia Mapumziko mema ya mwisho wa Wiki
#JamiiForums #JamiiAfrica #GoodMorning #AmkaNaJF #Maisha
🙏1
Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025, mjadala kuhusu Marekebisho ya Mfumo wa Uchaguzi (Reforms) haukwepeki. Kuna wanaosema reforms tayari zimefanyika, huku wengine vikisema bado kuna kasoro na wengine wakisema hawatashiriki Uchaguzi hadi kasoro hizo zishughulikiwe
Maswali muhimu ni je, ‘Reforms’ zilizofanyika zinatosha? Kwanini sauti ya pamoja ya Vyama haijasikika? Vyama vingine vinaona umuhimu wa ‘reforms’? Je, Wananchi wanafahamu mabadiliko yaliyofanywa na kuyaridhia?
Kufahamu haya na mengine, jiunge nasi katika Mjadala, kupitia Xspaces ya JamiiForums, Mei 12, 2025 kuanzia Saa 12:00 jioni hadi 2:00 usiku
Kujiunga bofya https://jamii.app/ReformsSpace
#ElectionReforms #Kuelekea2025 #ReformsSpace #Accountability #Democracy #FreeAndFairElections
Maswali muhimu ni je, ‘Reforms’ zilizofanyika zinatosha? Kwanini sauti ya pamoja ya Vyama haijasikika? Vyama vingine vinaona umuhimu wa ‘reforms’? Je, Wananchi wanafahamu mabadiliko yaliyofanywa na kuyaridhia?
Kufahamu haya na mengine, jiunge nasi katika Mjadala, kupitia Xspaces ya JamiiForums, Mei 12, 2025 kuanzia Saa 12:00 jioni hadi 2:00 usiku
Kujiunga bofya https://jamii.app/ReformsSpace
#ElectionReforms #Kuelekea2025 #ReformsSpace #Accountability #Democracy #FreeAndFairElections
👍3
Tanzania inajiandaa kwa Uchaguzi Mkuu 2025, lakini je, tuko tayari?
Mabadiliko ya Mfumo wa Uchaguzi yamejadiliwa, huku baadhi yakitajwa yamefanyika, lakini yamegusa kiini cha matatizo yanayolalamikiwa?
Kufahamu haya na mengine usikose kujiunga nasi katika Mjadala wa “‘Reforms’ za Uchaguzi; Je, Tume, Vyama na Wananchi wanaongea Lugha moja?” kupitia #XSpaces ya JamiiForums, Mei 12, 2025, Saa 12:00 jioni – 2:00 usiku
Kujiunga bofya https://jamii.app/ReformsSpace
#ElectionReforms #ReformsSpace #Kuelekea2025 #Uwajibikaji #Demokrasia #FreeAndFairElections
Mabadiliko ya Mfumo wa Uchaguzi yamejadiliwa, huku baadhi yakitajwa yamefanyika, lakini yamegusa kiini cha matatizo yanayolalamikiwa?
Kufahamu haya na mengine usikose kujiunga nasi katika Mjadala wa “‘Reforms’ za Uchaguzi; Je, Tume, Vyama na Wananchi wanaongea Lugha moja?” kupitia #XSpaces ya JamiiForums, Mei 12, 2025, Saa 12:00 jioni – 2:00 usiku
Kujiunga bofya https://jamii.app/ReformsSpace
#ElectionReforms #ReformsSpace #Kuelekea2025 #Uwajibikaji #Demokrasia #FreeAndFairElections
👍1
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Afya ya Uzazi na Jinsia (UNFPA) limetangaza kuwa Serikali ya Marekani imeamua kukata ufadhili wake wa baadaye kwa shirika hilo, hatua inayotajwa kusitisha msaada muhimu kwa Mamilioni ya Watu walio katika Mazingira ya Migogoro na kwa Wakunga wanaookoa Maisha ya akina Mama wakati wa kujifungua
Imeelezwa Marekani imefikia hatua hiyo ikidai UNFPA inahusishwa na utoaji wa Mimba wa kulazimishwa na upasuaji wa Uzazi wa hiari Nchini China, madai ambayo yamekanushwa mara kadhaa na tathmini huru, ikiwemo zile zilizofanywa na Serikali ya Marekani yenyewe
Uamuzi huu unakuja huku zaidi ya ruzuku 40 za kibinadamu zikiwa tayari zimesitishwa, zenye thamani ya takriban Dola Milioni 335. #UNFPA ilikuwa ikitegemea wastani wa Dola Milioni 180 kutoka Marekani kwa Mwaka
Soma https://jamii.app/USCutsUNFPA
#UNFPA #AfyaYaUzazi #HakiZaWanawake #JamiiAfrica #JamiiForums #HumanitarianAids
Imeelezwa Marekani imefikia hatua hiyo ikidai UNFPA inahusishwa na utoaji wa Mimba wa kulazimishwa na upasuaji wa Uzazi wa hiari Nchini China, madai ambayo yamekanushwa mara kadhaa na tathmini huru, ikiwemo zile zilizofanywa na Serikali ya Marekani yenyewe
Uamuzi huu unakuja huku zaidi ya ruzuku 40 za kibinadamu zikiwa tayari zimesitishwa, zenye thamani ya takriban Dola Milioni 335. #UNFPA ilikuwa ikitegemea wastani wa Dola Milioni 180 kutoka Marekani kwa Mwaka
Soma https://jamii.app/USCutsUNFPA
#UNFPA #AfyaYaUzazi #HakiZaWanawake #JamiiAfrica #JamiiForums #HumanitarianAids
👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Bara, Amani Golugwa, amesema Chama hicho kimetenga Tsh. Milioni 10, kwa yeyote atakayesaidia kutoa taarifa za mahali alipo Mdude Nyagali ambaye hajulikani alipo, tangu alipochukuliwa na Watu waliodaiwa kuwa Polisi usiku wa kuamkia Mei 02, 2025
Soma https://jamii.app/Mil10CDMMdude
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #Democracy
Soma https://jamii.app/Mil10CDMMdude
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #Democracy
👍1👎1
Unamshauri Mdau huyu afanye nini?
Mjadala zaidi https://jamii.app/MkeAnanikwamisha
#JamiiForums #JamiiAfrica #Maisha #JFStories #JFChitChats
Mjadala zaidi https://jamii.app/MkeAnanikwamisha
#JamiiForums #JamiiAfrica #Maisha #JFStories #JFChitChats
DAR: Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU) imemkamata Diwani wa Kata ya Buguruni, Busoro Pazi (CCM), kwa tuhuma za #Rushwa na wizi wa Mali za Umma
Tuhuma za wizi zinahusu vifaa vya majengo ya Halmashauri ya Wilaya ya Ilala, yaliyobomolewa na vifaa vyake kutoweka, ikidaiwa kuwa yeye na wafuasi wake walihusika
Kwa mujibu wa gazeti la Raia Mwema, TAKUKURU ilimkamata Pazi Aprili 9, 2025 na baadaye akaachiwa kwa dhamana. Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Ilala, Sosthenes Kibwengo, alithibitisha kukamatwa na kuachiwa kwa dhamana Diwani Pazi, lakini akasisitiza kuwa suala hilo liko katika uchunguzi
Soma https://jamii.app/DiwaniBuguruniRushwa
#JamiiAfrica #JamiiForums #KemeaRushwa #UchaguziMkuu2025
Tuhuma za wizi zinahusu vifaa vya majengo ya Halmashauri ya Wilaya ya Ilala, yaliyobomolewa na vifaa vyake kutoweka, ikidaiwa kuwa yeye na wafuasi wake walihusika
Kwa mujibu wa gazeti la Raia Mwema, TAKUKURU ilimkamata Pazi Aprili 9, 2025 na baadaye akaachiwa kwa dhamana. Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Ilala, Sosthenes Kibwengo, alithibitisha kukamatwa na kuachiwa kwa dhamana Diwani Pazi, lakini akasisitiza kuwa suala hilo liko katika uchunguzi
Soma https://jamii.app/DiwaniBuguruniRushwa
#JamiiAfrica #JamiiForums #KemeaRushwa #UchaguziMkuu2025
SHINYANGA: Chama cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kahama kimesema, Watia nia 9 wa nafasi za Ubunge na Udiwani Wilayani humo, wamebainika kujihusisha na vitendo vya kugawa Fedha kwa Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM nyakati za usiku, kinyume na Maadili ya Chama
Katibu wa CCM Wilaya ya Kahama, Andrew Chatwanga, amesema Wagombea hao wanatoka kwenye Majimbo yote matatu ya Wilaya hiyo: Kahama Mjini (5), Ushetu (2) na Msalala (2)
Ameeleza “Tumebaini baadhi ya watia nia wanazunguka usiku kwenye Kata mbalimbali kuwapa Wajumbe Fedha, wengine hadi Tsh. 10,000 ili wawapitishe kwenye mchakato wa ndani. Hii ni aibu, ni udhalilishaji na ni kinyume cha Maadili ya CCM. Chama hakiwezi kumvumilia Mgombea wa aina hiyo."
Soma https://jamii.app/RushwaWatianiaUdiwani
#UchaguziMkuu2025 #KemeaRushwa #JamiiForums #JamiiAfrica #Democracy #Siasa
Katibu wa CCM Wilaya ya Kahama, Andrew Chatwanga, amesema Wagombea hao wanatoka kwenye Majimbo yote matatu ya Wilaya hiyo: Kahama Mjini (5), Ushetu (2) na Msalala (2)
Ameeleza “Tumebaini baadhi ya watia nia wanazunguka usiku kwenye Kata mbalimbali kuwapa Wajumbe Fedha, wengine hadi Tsh. 10,000 ili wawapitishe kwenye mchakato wa ndani. Hii ni aibu, ni udhalilishaji na ni kinyume cha Maadili ya CCM. Chama hakiwezi kumvumilia Mgombea wa aina hiyo."
Soma https://jamii.app/RushwaWatianiaUdiwani
#UchaguziMkuu2025 #KemeaRushwa #JamiiForums #JamiiAfrica #Democracy #Siasa
Mkurugenzi wa ldara ya Mawasiliano Ikulu ya Zanzibar na Msemaji Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Charles Hillary (66) amefariki dunia alfajiri ya leo Mei 11, 2025
Inaelezwa kuwa Hillary amefariki baada ya kuugua ghafla na mauti yamemkuta akiwa njiani kupelekwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili tawi la Mloganzila.
Amefanya kazi Redio Tanzania mwaka 1981 hadi 1994 alipojiunga na Radio One Stereo. Mwaka 2003 alijiunga na Radio Deusch Welle (DW) nchini Ujerumani, na miaka mitatu baadaye alijiunga na BBC akiwa Idhaa ya Kiswahili. Mwaka 2015 aliamua kurejea nchini na kujiunga Azam Media. Desemba 30, 2021 aliteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano – Ikulu Zanzibar
Zaidi, Soma https://jamii.app/CharlesHilaryAfariki
#RIPCharlesHilary #JamiiAfrica #JamiiForums
Inaelezwa kuwa Hillary amefariki baada ya kuugua ghafla na mauti yamemkuta akiwa njiani kupelekwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili tawi la Mloganzila.
Amefanya kazi Redio Tanzania mwaka 1981 hadi 1994 alipojiunga na Radio One Stereo. Mwaka 2003 alijiunga na Radio Deusch Welle (DW) nchini Ujerumani, na miaka mitatu baadaye alijiunga na BBC akiwa Idhaa ya Kiswahili. Mwaka 2015 aliamua kurejea nchini na kujiunga Azam Media. Desemba 30, 2021 aliteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano – Ikulu Zanzibar
Zaidi, Soma https://jamii.app/CharlesHilaryAfariki
#RIPCharlesHilary #JamiiAfrica #JamiiForums
👍1😭1
Katika kusherekea Siku hii ya Mama Duniani, tunawatakia kina mama wote heri, afya njema na upendo usio na kifani
Asanteni kwa upendo, nguvu na kujitolea kwenu kila siku, ninyi ni nguzo ya familia na jamii
#JamiiAfrica #JamiiForums #MothersDay #Mother
Asanteni kwa upendo, nguvu na kujitolea kwenu kila siku, ninyi ni nguzo ya familia na jamii
#JamiiAfrica #JamiiForums #MothersDay #Mother
👏3👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Spika na Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Tulia Ackson akifafanua hoja ya Bunge kutojadili kuhusu uwepo wa matukio ya Watu kudaiwa kutekwa na wengine kupotea Nchini, amesema suala hilo linahitaji ushahidi na isiwe suala la kusikia
Amezungumza hayo wakati akihojiwa na Wasafi FM, Mei 9, 2025, ambapo Mtangazaji Charles Williams alimuuliza “Kumekuwa na vitendo vinavyoitwa vya Utekaji, hata Ripoti ya LHRC imeeleza hilo, hapa Mbeya amepotea Mdude (Nyangali), CHADEMA na Serikali wametangaza dau kwa atakayefanikisha kupatikana kwake.”
Akaongeza “Je, vitendo vya Watu kupotea au kutekwa vinaonekana vimeshamiri au vimerejea kwa kasi, Watu wanadhani Bunge lina sababu ya kusimamisha shughuli zake na kulijadili kwa kina suala hilo, wewe unasemaje?"
Soma https://jamii.app/TuliaNaWasafi
#JamiiForums #Governance
Amezungumza hayo wakati akihojiwa na Wasafi FM, Mei 9, 2025, ambapo Mtangazaji Charles Williams alimuuliza “Kumekuwa na vitendo vinavyoitwa vya Utekaji, hata Ripoti ya LHRC imeeleza hilo, hapa Mbeya amepotea Mdude (Nyangali), CHADEMA na Serikali wametangaza dau kwa atakayefanikisha kupatikana kwake.”
Akaongeza “Je, vitendo vya Watu kupotea au kutekwa vinaonekana vimeshamiri au vimerejea kwa kasi, Watu wanadhani Bunge lina sababu ya kusimamisha shughuli zake na kulijadili kwa kina suala hilo, wewe unasemaje?"
Soma https://jamii.app/TuliaNaWasafi
#JamiiForums #Governance
🤬2👍1😭1
Marekebisho ya Mfumo wa Uchaguzi (Reforms) ni msingi wa Uchaguzi Huru na wa Haki, lakini Je, maboresho “yanayotajwa” kufanyika tayari yanatosha? Wananchi na Wapigakura wanayafahamu na kuyaunga mkono? Msimamo wa Vyama vya Siasa ni upi? Vimeridhika?
Usikose Mjadala wa “Reforms’ za Uchaguzi; Je, Tume, Vyama na Wananchi wanaongea lugha moja?” kupitia Xspaces ya JamiiForums, Mei 12, 2025 kuanzia saa 12:00 jioni hadi 2:00 usiku, tuchambue hali halisi ya ‘reforms’, changamoto na njia ya kuelekea Uchaguzi Mkuu Huru, wa Haki na wenye uwazi
Kujiunga bofya https://jamii.app/ReformsSpace
#ReformsSpace #Uchaguzi2025 #Demokrasia #Uwajibikaji #FreeAndFairElections #Kuelekea2025
Usikose Mjadala wa “Reforms’ za Uchaguzi; Je, Tume, Vyama na Wananchi wanaongea lugha moja?” kupitia Xspaces ya JamiiForums, Mei 12, 2025 kuanzia saa 12:00 jioni hadi 2:00 usiku, tuchambue hali halisi ya ‘reforms’, changamoto na njia ya kuelekea Uchaguzi Mkuu Huru, wa Haki na wenye uwazi
Kujiunga bofya https://jamii.app/ReformsSpace
#ReformsSpace #Uchaguzi2025 #Demokrasia #Uwajibikaji #FreeAndFairElections #Kuelekea2025
👍2👏1
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya limesema kuna baadhi ya Watu na Viongozi wa #CHADEMA wanatoa matamko ikiwemo ya kutaja majina ya Askari wakiwatuhumu kuhusika na tukio la kupotea kwa Mwanachama wa Chama hicho, Mpaluka Said Nyagali (Mdude) bila kuwasilisha ushahidi wowote
Taarifa ya Polisi inaeleza “Jeshi linatoa onyo kali kwa Mtu au kikundi chochote cha Watu wenye nia ovu kujaribu wala kuthubutu kujihusisha na uhalifu wa aina yoyote ikiwemo kudhuru Askari ama familia za Askari, pia wajionye sana na wasifikiri kufanya kitendo hicho ni rahisi kwao.”
Imeendelea “Jeshi la Polisi halitasita kumchukulia hatua za Kisheria na kumshughulikia Mtu au kikundi chochote cha Watu watakaojaribu kufanya uhalifu kutokana na matamko au kauli hizo zinazotolewa.”
Soma https://jamii.app/PolisiTamkoMbeya
#JFMatukio #JamiiForums #Governance
Taarifa ya Polisi inaeleza “Jeshi linatoa onyo kali kwa Mtu au kikundi chochote cha Watu wenye nia ovu kujaribu wala kuthubutu kujihusisha na uhalifu wa aina yoyote ikiwemo kudhuru Askari ama familia za Askari, pia wajionye sana na wasifikiri kufanya kitendo hicho ni rahisi kwao.”
Imeendelea “Jeshi la Polisi halitasita kumchukulia hatua za Kisheria na kumshughulikia Mtu au kikundi chochote cha Watu watakaojaribu kufanya uhalifu kutokana na matamko au kauli hizo zinazotolewa.”
Soma https://jamii.app/PolisiTamkoMbeya
#JFMatukio #JamiiForums #Governance
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Ndugu wa marehemu, Kurwa Igembe wamekataa kuuchukua mwili katika Hospitali ya Misheni Chimala wakitaka uchunguzi ufanyike kuhusu kifo cha Kurwa ambaye inadaiwa alipigwa risasi na Askari wa Hifadhi ya Taifa (TANAPA), Mei 7, 2025
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Kanal Maurid Surumbu ameiambia Azam TV kuwa Askari Wanne wa TANAPA wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma hizo ikidaiwa kulitokea majibizano kati ya Askari hao waliowatuhumu Wafugaji kuingiza mifugo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, Wilayani Mbarali
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Misheni Chimala, Nursheed Mridi amekiri mwili huo kuwa na jeraha la risasi lakini bado uchunguzi haujafanyika
Soma https://jamii.app/AskariWaTANAPA
#JamiiForums #Accountability
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Kanal Maurid Surumbu ameiambia Azam TV kuwa Askari Wanne wa TANAPA wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma hizo ikidaiwa kulitokea majibizano kati ya Askari hao waliowatuhumu Wafugaji kuingiza mifugo ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, Wilayani Mbarali
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Misheni Chimala, Nursheed Mridi amekiri mwili huo kuwa na jeraha la risasi lakini bado uchunguzi haujafanyika
Soma https://jamii.app/AskariWaTANAPA
#JamiiForums #Accountability