ARUSHA: Akifungua Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2025, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiAfrica, Maxence Melo amesema kwenye Dunia ya sasa, Vyombo vya Habari havihusishi tena Magazeti, Redio na Televisheni pekee
Amesema “Kuna ongezeko la Watengeneza Maudhui wa Kidigitali ikijumuisha Wanablogu, Wapigapicha huru, Vloggers, Podcasters na wengine wengi ambao kwa ubunifu wao, wamepanua mipaka ya Uhuru wa Kujieleza.”
Maxence ameongeza “Tunatambua mchango wao mkubwa katika kuweka Jamii zetu hai kwa taarifa, fikra na mazungumzo muhimu. Tunasisitiza kuwa Uhuru wa Habari lazima uwe shirikishi, ukilinda na kuenzi Haki za makundi yote yanayochangia katika mnyororo wa Mawasiliano ya kisasa.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Amesema “Kuna ongezeko la Watengeneza Maudhui wa Kidigitali ikijumuisha Wanablogu, Wapigapicha huru, Vloggers, Podcasters na wengine wengi ambao kwa ubunifu wao, wamepanua mipaka ya Uhuru wa Kujieleza.”
Maxence ameongeza “Tunatambua mchango wao mkubwa katika kuweka Jamii zetu hai kwa taarifa, fikra na mazungumzo muhimu. Tunasisitiza kuwa Uhuru wa Habari lazima uwe shirikishi, ukilinda na kuenzi Haki za makundi yote yanayochangia katika mnyororo wa Mawasiliano ya kisasa.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
👍1
ARUSHA: Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiAfrica, Maxence Melo amesema “Kuelekea Uchaguzi Mkuu, tunatoa wito kwa Mamlaka, Taasisi, Vyama vya Siasa na Jamii kwa ujumla kuheshimu na kulinda Uhuru wa Vyombo vya Habari, kuhakikisha hakuna vitisho, mashinikizo wala vizingiti vinavyowekwa kwa wanaohakikisha Wananchi wanapata taarifa sahihi, za kina na kwa wakati.”
Ameongeza “Leo tunapenda kukumbushana kuwa Uhuru wa Vyombo vya Habari sio Hisani, bali ni Haki ya Msingi inayodaiwa na kulindwa kila Siku na ni jukumu letu sote – Wanahabari, Watengeneza Maudhui, Wanateknolojia, Watunga Sera na Raia.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Ameongeza “Leo tunapenda kukumbushana kuwa Uhuru wa Vyombo vya Habari sio Hisani, bali ni Haki ya Msingi inayodaiwa na kulindwa kila Siku na ni jukumu letu sote – Wanahabari, Watengeneza Maudhui, Wanateknolojia, Watunga Sera na Raia.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
ARUSHA: Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiAfrica, Maxence Melo amesema “Ripoti ya UNESCO ya Mwaka 2023 kuhusu Uhuru wa Vyombo vya Habari inaeleza kuwa Uwezo wa kupima ubora wa taarifa ni ujuzi muhimu kwa kila Mtu katika karne ya ishirini na moja"
Amesema kuwa katika nyakati hizi, kuimarisha Akili Mnemba si tu hitaji la Mtu binafsi, bali ni jukumu la pamoja kwa tasnia ya Habari na Jamii nzima. Pia, Uhuru wa Vyombo vya Habari unapata maana kamili pale unapochanganyika na Uwajibikaji, Uchambuzi wa kina na uelewa sahihi wa taarifa zinazochakatwa
Maxence ameongeza “Hii inaonesha si Vyombo vya Habari pekee vinavyopaswa kuwa na viwango vya juu vya weledi, bali Jamii inapaswa kujifunza jinsi ya kuwa Wasomaji, Watazamaji na Wasikilizaji makini.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Amesema kuwa katika nyakati hizi, kuimarisha Akili Mnemba si tu hitaji la Mtu binafsi, bali ni jukumu la pamoja kwa tasnia ya Habari na Jamii nzima. Pia, Uhuru wa Vyombo vya Habari unapata maana kamili pale unapochanganyika na Uwajibikaji, Uchambuzi wa kina na uelewa sahihi wa taarifa zinazochakatwa
Maxence ameongeza “Hii inaonesha si Vyombo vya Habari pekee vinavyopaswa kuwa na viwango vya juu vya weledi, bali Jamii inapaswa kujifunza jinsi ya kuwa Wasomaji, Watazamaji na Wasikilizaji makini.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
ARUSHA: Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiAfrica, Maxence Melo amesema Kaulimbiu ya Mwaka 2025 katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2025 ni “Uhabarishaji katika Dunia Mpya: Mchango wa Akili Mnemba kwenye Uhuru wa Vyombo vya Habari.”
Ameeleza kuwa Kaulimbiu hiyo inakumbusha katika nyakati hizi za taarifa nyingi na Teknolojia za Kisasa, kunahitajika uwezo wa ziada kuchuja, kuchambua na kuelewa taarifa kwa umakini wa hali ya juu ili kulinda Uhuru wa Habari na kuhakikisha Uwajibikaji wa wanaohabarisha na wanaohabarishwa
Maxence amesema “Katika Mazingira haya mapya, Akili Mnemba (AI) imekuwa nyenzo isiyokwepeka katika Tasnia ya Habari na Uchakataji Taarifa. Wanahabari na jamii kwa ujumla wanahimizwa kuwa na uwezo wa kuchambua chanzo cha taarifa na kutambua upendeleo au propaganda zinazoweza kuathiri maudhui.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Ameeleza kuwa Kaulimbiu hiyo inakumbusha katika nyakati hizi za taarifa nyingi na Teknolojia za Kisasa, kunahitajika uwezo wa ziada kuchuja, kuchambua na kuelewa taarifa kwa umakini wa hali ya juu ili kulinda Uhuru wa Habari na kuhakikisha Uwajibikaji wa wanaohabarisha na wanaohabarishwa
Maxence amesema “Katika Mazingira haya mapya, Akili Mnemba (AI) imekuwa nyenzo isiyokwepeka katika Tasnia ya Habari na Uchakataji Taarifa. Wanahabari na jamii kwa ujumla wanahimizwa kuwa na uwezo wa kuchambua chanzo cha taarifa na kutambua upendeleo au propaganda zinazoweza kuathiri maudhui.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
ARUSHA: Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2025, Balozi wa Sweden-Tanzania, Charlotta Ozaki Macias amesema Dunia inabadilishwa na Akili Mnemba (AI) ambayo ina faida nyingi lakini pia ina changamoto zake ikiwemo upotoshaji wa taarifa na kupungua kwa nafasi ya kiraia
Balozi Charlotta amesema AI zinasisimua na zinatisha pia, zinaweza kuwasaidia Wanahabari kwa kurahisisha kazi na kuchakata kiasi kikubwa cha taarifa n.k hiyo inasaidia kutengeneza habari za ubora wa juu na zenye ushahidi wa kutosha
Anaongeza “AI inaweza pia kutumiwa kufanya upotoshaji wa taarifa, Picha, Video na Maandishi bandia, inazidi kuwa vigumu kujua ukweli ni upi. Hili si tatizo la Kiteknolojia tu, ni tatizo la Uaminifu."
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
Balozi Charlotta amesema AI zinasisimua na zinatisha pia, zinaweza kuwasaidia Wanahabari kwa kurahisisha kazi na kuchakata kiasi kikubwa cha taarifa n.k hiyo inasaidia kutengeneza habari za ubora wa juu na zenye ushahidi wa kutosha
Anaongeza “AI inaweza pia kutumiwa kufanya upotoshaji wa taarifa, Picha, Video na Maandishi bandia, inazidi kuwa vigumu kujua ukweli ni upi. Hili si tatizo la Kiteknolojia tu, ni tatizo la Uaminifu."
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
ARUSHA: Balozi wa Sweden-Tanzania, Charlotta Ozaki Macias anasema “Nchini Sweden, tumejaribu kuelekeza Maendeleo ya Akili Mnemba (AI) kwa njia ya kimaadili. Mkakati wetu wa kitaifa kuhusu AI unalenga mambo matatu kwa kuwa AI inapaswa kufanya kazi kwa ajili ya Watu, si dhidi yao.”
Ameyataja mambo hayo kuwa ni Kulinda faragha na kuhakikisha usalama wa taarifa za Watu, Kufanya AI iwe wazi, ili Watu waelewe jinsi maamuzi yanavyofanyika na Kupambana na upendeleo ili kuhakikisha AI haisaidii kuendeleza Ubaguzi.
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
Ameyataja mambo hayo kuwa ni Kulinda faragha na kuhakikisha usalama wa taarifa za Watu, Kufanya AI iwe wazi, ili Watu waelewe jinsi maamuzi yanavyofanyika na Kupambana na upendeleo ili kuhakikisha AI haisaidii kuendeleza Ubaguzi.
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
ARUSHA: Balozi wa Sweden-Tanzania, Charlotta Ozaki Macias anasema “Nimeona ujasiri wa ajabu miongoni mwa Waandishi wa Habari hapa Tanzania na Afrika kwa ujumla, licha ya Rasilimali chache, udhibiti wa Habari na wakati mwingine hata vitisho kwa Maisha yao lakini wanaendelea mbele.”
Ameeleza hivi karibuni alitembelea Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) akaona changamoto wanazokabiliana nazo, akitoa Mfano Mkoani Manyara, Wanahabari Vijana walivamiwa walipokuwa wakiripoti kuhusu Ukatili wa Kijinsia
Ameongeza “Njombe, Waandishi walieleza Hadithi ya Watoto wenye Ulemavu wanaofichwa na walifanya hivyo kwa kuhatarisha usalama wao binafsi. Hadithi hizi zilinigusa sana na zilinikumbusha kwanini kazi hii ina umuhimu mkubwa.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Ameeleza hivi karibuni alitembelea Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC) akaona changamoto wanazokabiliana nazo, akitoa Mfano Mkoani Manyara, Wanahabari Vijana walivamiwa walipokuwa wakiripoti kuhusu Ukatili wa Kijinsia
Ameongeza “Njombe, Waandishi walieleza Hadithi ya Watoto wenye Ulemavu wanaofichwa na walifanya hivyo kwa kuhatarisha usalama wao binafsi. Hadithi hizi zilinigusa sana na zilinikumbusha kwanini kazi hii ina umuhimu mkubwa.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
ARUSHA: Mwakilishi wa UNESCO Nchini Tanzania, Michel Toto katika uzinduzi wa Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, ametoa wito kwa wadau wa Tasnia ya Habari kuwekeza zaidi katika kulinda Ukweli, Uhuru wa Maoni na mustakabali wa Uandishi wa Habari Duniani, akisema Uandishi wa Habari ni nguzo ya Demokrasia, Uwajibikaji na Amani
Amesisitiza kusema ukweli sio kosa, huku akieleza kwa Mwaka 2025 pekee, UNESCO imetoa zaidi ya matamko 90 kulaani mauaji ya Waandishi wa Habari Duniani kote, ambapo Waandishi wengi wamepoteza maisha kwa kuleta ukweli mbele ya Jamii
Aidha, ametoa tahadhari kuhusu changamoto mpya zinazochangiwa na kuibuka kwa Teknolojia ya Akili Mnemba (AI), akieleza kuwa pamoja na fursa, AI inaleta hatari kubwa kwa Haki na Uhuru wa Vyombo vya Habari
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Amesisitiza kusema ukweli sio kosa, huku akieleza kwa Mwaka 2025 pekee, UNESCO imetoa zaidi ya matamko 90 kulaani mauaji ya Waandishi wa Habari Duniani kote, ambapo Waandishi wengi wamepoteza maisha kwa kuleta ukweli mbele ya Jamii
Aidha, ametoa tahadhari kuhusu changamoto mpya zinazochangiwa na kuibuka kwa Teknolojia ya Akili Mnemba (AI), akieleza kuwa pamoja na fursa, AI inaleta hatari kubwa kwa Haki na Uhuru wa Vyombo vya Habari
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
ARUSHA: Balozi wa Sweden-Tanzania, Charlotta Ozaki Macias amesema “Kwanini Uhuru wa Kujieleza ni muhimu sana? Na kwanini Nchi kama yangu zinasimama imara kuutetea? Kwasababu tunaamini Watu wanapokuwa huru kusema, kushiriki na kutofautiana, Jamii huwa imara zaidi. Hakuna Mtu au Chama cha Siasa kilicho na majibu yote, ndiyo maana tunahitaji nafasi ya mawazo tofauti kushirikishwa, kupingwa na kuboreshwa.”
Ameongeza “Katika Demokrasia ya Vyama vingi, Uhuru wa Kujieleza unahakikisha Watu wanapata taarifa. Unawasaidia Wapigakura kufanya maamuzi sahihi. Unawafanya Viongozi wawajibike na unaipa nguvu Jamii ya Kiraia kushinikiza Mabadiliko."
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Ameongeza “Katika Demokrasia ya Vyama vingi, Uhuru wa Kujieleza unahakikisha Watu wanapata taarifa. Unawasaidia Wapigakura kufanya maamuzi sahihi. Unawafanya Viongozi wawajibike na unaipa nguvu Jamii ya Kiraia kushinikiza Mabadiliko."
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
ARUSHA: Akizungumza katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari 2025, Balozi wa Sweden-Tanzania, Charlotta Ozaki Macias amesema “Tunapoingia kwenye enzi hii ya Kidijitali, Waandishi wa Habari lazima wakabiliane na mashambulizi Mtandaoni, ufuatiliaji wa Kidijitali na taarifa za uongo. Pia, wanapaswa kutafuta njia za kutumia Teknolojia ili kuelimisha na kuhamasisha.”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
DEMOKRASIA: Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimedai nyumba ya Mwenyekiti wa Chama hicho - Taifa, Tundu Antipas Lissu imezingirwa na Polisi huku Mkurugenzi wa Uenezi na Mawasiliano wa CHADEMA, Brenda Rupia akidai Polisi hao wanataka kufanya upekuzi
Akielezea hali ilivyo, Msaidizi wa Lissu, David Djumbe amesema awali Polisi walifika alfajiri wakiwa na Magari manne na kuanza kugonga geti lakini hawakufunguliwa. Baadaye walikwenda kwa Mjumbe wa shina, ambaye aliwapigia simu Wanafamilia akisema Polisi hao wamekuja hapo kufanya upekuzi, ndipo akaambiwa mwenye nyumba (Lissu) hayupo hawawezi kuwafungulia”
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro alipoulizwa sababu ya askari hao kufika mahali hapo, amesema ni ulinzi wa kawaida
Zaidi https://jamii.app/NyumbaKuzingirwa
#JamiiForums #Accountability #Governance
Akielezea hali ilivyo, Msaidizi wa Lissu, David Djumbe amesema awali Polisi walifika alfajiri wakiwa na Magari manne na kuanza kugonga geti lakini hawakufunguliwa. Baadaye walikwenda kwa Mjumbe wa shina, ambaye aliwapigia simu Wanafamilia akisema Polisi hao wamekuja hapo kufanya upekuzi, ndipo akaambiwa mwenye nyumba (Lissu) hayupo hawawezi kuwafungulia”
Hata hivyo, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro alipoulizwa sababu ya askari hao kufika mahali hapo, amesema ni ulinzi wa kawaida
Zaidi https://jamii.app/NyumbaKuzingirwa
#JamiiForums #Accountability #Governance
👍1
Mtaalamu wa Mawasiliano na Vyombo vya Habari wa EAC, Lilian Kiarie akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) katika Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani 2025 amesema Teknolojia imeimarisha Uandishi wa kiraia huku Watu wa kawaida wakipewa uwezo wa kuripoti matukio kwa wakati halisi, jambo ambalo limepanua Demokrasia ya upatikanaji wa habari
Ametoa wito kwa Waandishi wa Habari kuendelea kushikilia misingi ya ukweli, uadilifu na uwazi, pamoja na Serikali na wadau kulinda Uhuru wa Kujieleza na kukuza ubunifu, ili kuhakikisha Uandishi wa habari unabaki kuwa nguzo ya Demokrasia hata katika enzi za Akili Mnemba
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
Ametoa wito kwa Waandishi wa Habari kuendelea kushikilia misingi ya ukweli, uadilifu na uwazi, pamoja na Serikali na wadau kulinda Uhuru wa Kujieleza na kukuza ubunifu, ili kuhakikisha Uandishi wa habari unabaki kuwa nguzo ya Demokrasia hata katika enzi za Akili Mnemba
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania Media Foundation, Dastan Kamanzi akizungumza katika Siku ya Kwanza ya Maadhimisho ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani ameyataja mambo matatu muhimu wanayohitaji Waandishi wa Habari ili kuboresha kazi zao
Amesema “Waandishi wanahitaji mambo matatu muhimu ili kuboresha kazi zao, kwanza ni Shauku inayohusisha kubadilika na kukua. Pili, ni Utayari unaohusisha Uwekezaji wa maarifa na Uwekezaji wa muda, tatu wanahitaji kudhamiria na kujikita kwenye Majukumu yao”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
Amesema “Waandishi wanahitaji mambo matatu muhimu ili kuboresha kazi zao, kwanza ni Shauku inayohusisha kubadilika na kukua. Pili, ni Utayari unaohusisha Uwekezaji wa maarifa na Uwekezaji wa muda, tatu wanahitaji kudhamiria na kujikita kwenye Majukumu yao”
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia #AIandMedia #HakikiTaarifa #FactsChecking
❤1
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salam, Jumanne Muliro akizungumza na JamiiForums amesema Makada wa CHADEMA waliokamatwa Aprili 24, 2025 ni Makamu Mwenyekiti, John Heche na Katibu Mkuu, John Mnyika na walirudi wakiwa salama
Akielezea sababu ya kuwafukuza Wanachama wa CHADEMA eneo la Mahakama siku hiyo alisema “Sisi tuliweka mazingira mazuri kwa Mahakama kufanya kazi. Kwani hao CHADEMA peke yao ndio wenye kesi? Pale Kisutu kuna Mahakimu wangapi? Kama Mahakimu wapo 20, kesi moja ya Lissu ndio isimamishe kesi nyingine 19? Hao wanyonge wengine wasisikilize kesi zao? Iweje Watu kama 3,000 waje pale Mahakamani wapige kelele Dunia yote ijue?”
Ameongeza “Walisema tunataka Mahakama imwachilie Lissu la sivyo tutachukua hatua, kwa hiyo ulitaka tusubiri hiyo hatua? Ulitaka tusubiri ushahidi? Sisi kazi yetu ni kuzuia uhalifu usifanyike”
Zaidi https://jamii.app/WaliokamatwaAprili24
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #Governance
Akielezea sababu ya kuwafukuza Wanachama wa CHADEMA eneo la Mahakama siku hiyo alisema “Sisi tuliweka mazingira mazuri kwa Mahakama kufanya kazi. Kwani hao CHADEMA peke yao ndio wenye kesi? Pale Kisutu kuna Mahakimu wangapi? Kama Mahakimu wapo 20, kesi moja ya Lissu ndio isimamishe kesi nyingine 19? Hao wanyonge wengine wasisikilize kesi zao? Iweje Watu kama 3,000 waje pale Mahakamani wapige kelele Dunia yote ijue?”
Ameongeza “Walisema tunataka Mahakama imwachilie Lissu la sivyo tutachukua hatua, kwa hiyo ulitaka tusubiri hiyo hatua? Ulitaka tusubiri ushahidi? Sisi kazi yetu ni kuzuia uhalifu usifanyike”
Zaidi https://jamii.app/WaliokamatwaAprili24
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #Governance
ARUSHA: Akishiriki Majadiliano katika Siku ya kwanza ya Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani, Mercy Ndegwa, Mwakilishi wa Kampuni ya Meta amesema Kampuni hiyo imekuwa ikishirikiana kwa karibu na wadau pamoja na Serikali kuboresha Mazingira ya Kidigitali ikiwemo watumiaji wa majukwaa hayo kuingiza kipato
Amesema "Tumeona platforms zetu za WhatsApp na Instagram zimekuwa zikifanya vizuri na kupiganiwa na Watu wengi, tunaona namna gani ya kuweka njia ya kuingiza Fedha (Monetization), tunafanya hivyo kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali kwa ukaribu wakiwemo JamiiAfrica"
Ndegwa ameongeza "Tumepitisha mambo kadhaa ikiwemo masuala ya Kodi, ambayo kabla ya kuchukua Maamuzi tunashirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutimiza hilo, ili lifanyike kwa njia sahihi, pamoja na hivyo tunazidi kufikiria vitu kwa ajili ya kuboresha ‘tools’ zetu"
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Amesema "Tumeona platforms zetu za WhatsApp na Instagram zimekuwa zikifanya vizuri na kupiganiwa na Watu wengi, tunaona namna gani ya kuweka njia ya kuingiza Fedha (Monetization), tunafanya hivyo kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali kwa ukaribu wakiwemo JamiiAfrica"
Ndegwa ameongeza "Tumepitisha mambo kadhaa ikiwemo masuala ya Kodi, ambayo kabla ya kuchukua Maamuzi tunashirikiana na Serikali ya Tanzania katika kutimiza hilo, ili lifanyike kwa njia sahihi, pamoja na hivyo tunazidi kufikiria vitu kwa ajili ya kuboresha ‘tools’ zetu"
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
❤1
Akizungumzia suala la Waandaa Maudhui kunufaika kupitia Majukwaa ya Kidigitali, Maxence Melo, Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiAfrica amesema "Tumezungumza na wenzetu #Meta, tunashirikiana nao na baadhi ya vikao kati yetu na wao tutafanya kwa njia ya Digitali ili Wadau wengine washiriki na waweze kutoa maoni yafanyiwe kazi. Mikutano hiyo itashirikisha Wadau mbalimbali wakiwemo wa Serikalini na Sekta Binafsi"
Awali Mwakilishi wa Meta, Mercy Ndegwa alisema wameona Majukwaa yao ya Whatsapp na Instagram yamekuwa yakifanya vizuri, hivyo kwa kushirikiana na Wadau wanatafuta namna ya kuweka njia ya kuwawezesha Watumiaji wa majukwaa hayo kujipatia Fedha (Monetization)
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
Awali Mwakilishi wa Meta, Mercy Ndegwa alisema wameona Majukwaa yao ya Whatsapp na Instagram yamekuwa yakifanya vizuri, hivyo kwa kushirikiana na Wadau wanatafuta namna ya kuweka njia ya kuwawezesha Watumiaji wa majukwaa hayo kujipatia Fedha (Monetization)
Soma https://jamii.app/WPFD2025DayOne
#WorldPressFreedomDay #WPFD2025 #PressFreedom #MediaAndAI #AIForMedia
👍2