JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
RAIS SAMIA: MFUMO WA TAASISI ZA HAKI JAMII KUFANYIWA MAGEUZI

Amesema miundo ya Taasisi hizo zinazojumuisha Jeshi la Polisi, Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Jeshi la Magereza na nyinginezo itatazamwa ili kuona kama inaleta ufanisi

Ameeleza, "Tutatizama wale tuliowaamini kwenye maeneo hayo, mifumo yao ya ajira, mafunzo, maadili na nidhamu zipoje"

Soma - https://jamii.app/UapishoIkuluLeo

#Governance
👍11
RAIS SAMIA: UPANDISHWAJI VYEO JESHINI KUANGALIWA

Akizungumza baada ya uapisho wa Viongozi Rais Samia amesema, "Nimetizama kila ninapokwenda, Mtu anakaribia kustaafu lakini bega lipo tupu. Nikawa nasema upandishwaji vyeo upoje kwenye haya Majeshi?"

Aidha, amesema uhusiano kati ya Raia na Taasisi za Haki Jamii utaangaliwa kwani malalamiko yamekuwa mengi

Soma - https://jamii.app/UapishoIkuluLeo

#Governance
👍14😢1
RAIS SAMIA: TUTACHUJANA KUJENGA MAJESHI YENYE SIFA

Amesema upatikanaji wa Watenda kazi kwa Majeshi yote utatazamwa ili kujenga majeshi yenye sifa na hadhi ya kusimamia Nchi

Amesisitiza, "Kama yalishapita, huko mbele tutachujana vizuri"

Pia, amegusia vitendo vinavyofanywa na baadhi ya Polisi barabarani akisema, "Hudhani kama ni Mhitimu wa Chuo"

Soma - https://jamii.app/UapishoIkuluLeo

#JFUwajibikaji
👏13👍5🤮1
KUONGEA MWENYEWE NI HALI YA KAWAIDA?

Kwa mujibu wa Jariba la Medical News Today, ni kuwa mara nyingi mtu kuongea peke yake ni tabia ya kawaida yenye manufaa mbalimbali ikiwemo kukusaidia kutafakari

Hata hivyo, baadhi ya Watu wanaweza kuona kuongea mwenyewe kunaathiri #AfyaYaAkili ikiwa kauli ni hasi na za kujikosoa wakati wote

Fahamu zaidi > https://jamii.app/SelfTalkJF

#JFAfya #PublicHealth
👍18
Mdau wa Jukwaa letu la Ajira ametoa ushauri kuhusu Lugha za Mwili (Body Language) ambazo ni vizuri kuzikwepa au kutozionesha wakati wa Usaili wa Kazi kwa kuwa zinaweza kutoa tafsiri hasi kwa wanaokusaili

Msome hapa - https://jamii.app/ElimuYaAjira

#JFMdau #Ajira
👍18
NIGERIA: Padri John Mark Cheitnum amekutwa amefariki ktk Jimbo la Kaduna ikiwa ni siku chache tangu iliporipotiwa kuwa ametekwa Julai 15, 2022

> Padri mwenzake ambaye walitekwa pamoja, Donatus Cleophas akifanikiwa kutoroka

Soma https://jamii.app/PadriAuawaNigeria
😢12👍8🥰1😁1😱1
UCHAGUZI KENYA: Mgombea Mwenza wa Urais wa Kenya Kwanza, Rigathi Gachagua amesema Rais Kenyatta alijaribu kumtisha kuhusu kumuunga mkono Ruto

> Amesema Kenyatta anatumia Mfumo wa Sheria ya Jinai kukabiliana na wale ambao hawakubaliani naye

Soma https://jamii.app/GachaguaKenyattaSaga

#Democracy
😁4👍2🤔1
TETESI: DE JONG HAUPENDI MJI WA MANCHESTER

Frenkie de Jong wa Barcelona hana mpango wa kujiunga na Manchester United, inadaiwa haupendi Mji wa Manchester na anaamini klabu hiyo haiendeshwi vizuri

> Inadaiwa anaona bora aende Chelsea au Bayern Munich

Soma https://jamii.app/DeJongUpdates

#JFSports
😁16👍6👎2🤔1
Mamlaka katika eneo lililojitenga la Somalia liitwalo Somaliland, zimesitisha shughuli za #BBC zikiishutumu kwa kudhoofisha uaminifu wa Taifa hilo

#Somaliland ilitangaza uhuru kutoka kwa Somalia ktk ya Vita ya Wenyewe kwa Wenyewe mwaka 1991

Soma https://jamii.app/BBCSomaliland

#PressFreedom
👍8🤔5😁1
URENO: JOTO LASABABISHA VIFO VYA WATU 1,063

Wizara ya Afya imesema kiwango cha juu cha Joto kimefikia Nyuzi Joto 47 kikiwa ni cha juu zaidi kuwahi kutokea Nchini humo

> Pia, Joto kali lilichochea moto wa nyika ambao uliteketeza hekta 45,467 za ardhi

Soma https://jamii.app/JotoKaliUreno

#ClimateChange
👍8🤔4😢2😁1
MALAWI: Watu 76 wamekamatwa katika maandamano ya kupinga Mfumo wa Uendeshaji kesi Mahakamani, wakidai utendaji kazi ni wa taratibu, kuna rushwa na kupanda kwa gharama za maisha

> Pia, Waandamanaji hao walimtaka Rais Chakwera kuchukua hatua

Soma https://jamii.app/MahakamaMalawi

#Accountablity
👍10👎1
MUSEVENI: SIKUSEMA UGANDA IMEINGIA UCHUMI WA KATI

Kufuatia wiki kadhaa za taarifa kinzani zilizohusisha Benki ya Dunia (WB) na Ofisi ya Takwimu ya Uganda (Ubos), Rais Yoweri Museveni amesema kauli aliyotoa awali haikumaanisha Uganda tayari imeshaingia Uchumi wa Kati, bali Taifa hilo linaingia katika ngazi hiyo

Soma - https://jamii.app/MuseveniUG-MI
😁16👍4🤯3😱3
TFF YAMFUNGIA HAJI MANARA MIAKA MIWILI

Kamati ya Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imemfungia Msemaji Klabu ya Yanga, Haji Manara kujihusisha na Mpira wa Miguu ndani na nje ya nchi kwa muda wa miaka 2 na kupigwa faini ya Tsh. milioni 20

Amekutwa na hatia kwa makosa ya kumvunjia heshima Rais wa TFF, Wallace Karia kwenye Fainali ya ASFC kati ya Yanga na Coastal, Jijini Arusha

#JamiiForums #JFSports
👍33👎14😁6🤔4😱2🤬1😢1
TANZIA: Msanii wa Filamu nchini, Farida Sabu maarufu kwa jina la 'Bi Sonia' amefariki dunia leo Julai 21, 2022 akiwa Zanzibar

> Muigizaji huyo alijulikana kupitia Kikundi cha Kaole Sanaa Group

Soma https://jamii.app/BiSoniaAfariki

#JFMatukio
😢15
WAZIRI MKUU WA ITALIA AJIUZULU

Mario Draghi amewasilisha barua ya kujiuzulu kwa Rais Sergio Mattarella baada ya Serikali yake ya Muungano kuvunjika

Hali hiyo imeleta sintofahamu kwa Siasa za Italia, na kuathiri Soko la Fedha. Rais Mattarella amemtaka Draghi kubaki katika nafasi ya usimamizi

Soma - https://jamii.app/ItalyPMResigns

#Governance
👍12🤔1
CHAD: Serikali imepiga marufuku mabinti wadogo kusafiri nje ya Nchi bila Wazazi au Kibali cha Wazazi

> Hatua hiyo ni katika kupambana Biashara Haramu ya Usafirishaji Watu na wimbi la Wasichana wadogo kutumikishwa kingono katika Nchi jirani

Soma https://jamii.app/MabintiChad

#HumanTrafficking
👍15👏2
Umoja wa Ulaya umeidhinisha vikwazo vipya dhidi ya #Russia ikiwa ni pamoja na kupiga marufuku kuagiza dhahabu kutoka nchini humo na kuzuia mali za #Sberbank

> Usafirishaji wa dhahabu ndio chanzo kikuu cha mapato ya Urusi

Soma https://jamii.app/NewEuSanctions

#JFDiplomasia
👍8👎7🥰3😁1
KENYA: FACEBOOK YAFUTA MAELFU YA MAUDHUI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Facebook imeondoa machapisho zaidi ya 37,000 yaliyohamasisha chuki na 42,000 kwa kukiuka Sera yake ya ghasia

Pia, imekataa matangazo 36,000 ya kisiasa kwa kutofuata Sheria zake

Soma - https://jamii.app/FacebookKenya

#Kenya2022
👍7
Elimu ya Digitali ni hitaji muhimu la Mafanikio katika mazingira ya sasa

Hata hivyo, Mafunzo na Vifaa katika Shule na Vyuo vingi barani Afrika bado haviendani na kasi ya ukuaji wa Teknolojia

Wanafunzi wengi wanaotaka Ujuzi wa TEHAMA hawana njia nyingine na hulazimika kulipia mafunzo, hali hii ni kikwazo kwa wasioweza kujikimu kimaisha

Soma zaidi > https://jamii.app/UjuziTEHAMA
👍9
SIHA: Madiwani na Mbunge wamekataa kupokea Mradi wa Maji wa Gararagua uliojengwa kwa zaidi ya Tsh. Bilioni 1.7 kwa madai umejengwa chini ya kiwango

> Meneja wa RUWASA-SIHA amesema hakuna tatizo lolote katika mradi huo na yaliyopo ni ya kawaida

Soma https://jamii.app/MradiSiha

#JFUwajibikaji
👏8👍4🔥2😁1