JamiiForums
βœ”
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Ili kuweza kutuma Maombi ya nafasi hizi tembelea - https://jamii.app/NafasiAjira
#JamiiForums
URUSI: Waziri Mkuu wa Canada, Justin Trudeau pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa #Canada, Melanie Joly na Waziri wa Ulinzi wa Canada, Anita Ananda hawataruhusiwa kuingia #Urusi

> Katazo limeandikwa na Waziri wa Mambo ya Nje ya Urusi

Soma https://jamii.app/MawaziriCanada
#KENYA: Wajumbe wa Chama cha UDA wamemuidhinisha Naibu Rais, William Ruto kuwania kiti cha Urais ktk Uchaguzi Mkuu Agosti 2022

Ruto atamenyana na Kiongozi wa Muungano wa Azimio la Umoja, Raila Odinga anayeungwa Mkono na Rais Uhuru Kenyatta

Soma - https://jamii.app/RutoUrais
#JFLeo
Mwaka 2019/20, CAG alikagua Taasisi 263 ambazo ni Wizara, Idara na Wakala wa Serikali Kuu na kutoa Hati za Ukaguzi 260 ikilinganishwa na 294 kwa Mwaka 2018/19

Kupungua kwa Hati za Ukaguzi ni kutokana na CAG kushindwa kufanya ukaguzi kwa Balozi na Misheni 43 kutokana na Ugonjwa wa UVIKO-19

#JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji #WAJIBU
TANGA: AJALI YAUA, MASHUHUDA WA AJALI NAO WAGONGWA

Watu kadhaa wamefariki dunia na wengine kujeruhiwa katika ajali iliyotokea Sindeni, Wilayani Handeni Mkoani humo Machi 16, 2022

DC wa Handeni, Siriel Mchembe amethibitisha kutokea ajali hiyo

Soma > https://jamii.app/TangaAjali
Wizara ya Mambo ya Nje ya Urusi imesema Rais wa Marekani, Joe Biden na Maafisa wengine 12 wamepigwa marufuku kuingia Nchini humo

Vikwazo hivyo pia vitamuhusu Katibu Mkuu Kiongozi, Antony Blinken na Waziri wa Ulinzi, Lloyd Austin

Soma - https://jamii.app/RussiaSanctionBiden
#RussianUkraineWar
JE, WAJUA: MSANII HUTAKIWA KULIPA TSH. 50,000 AKIENDA NJE YA NCHI KWA KAZI ZA SANAA

Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limesema Sheria zinawataka Wasanii kulipa Tsh. 50,000 kupata Kibali kila wanapoenda nje ya Nchi kufanya kazi za kisanaa

Soma https://jamii.app/KibaliSanaa

#Burudani
Zaidi ya Wanajeshi 10 wa #Kenya ambao ni sehemu ya kikosi cha Walinda Amani wa AU wameuawa kwa kilipuzi kilichotegwa eneo la Gedo karibu na mpaka wa Kenya na #Somalia

Vilipuzi vimedaiwa kuwekwa na kundi la Al-Qaeda lenye uhusiano na Al-Shabaab

Soma - https://jamii.app/KenyaWanajeshi
πŸ‘1
SHINYANGA: ASKARI ANAYEMLINDA MWEKEZAJI ADAIWA KUUA RAIA KWA RISASI

Cosmas Hamis Kusililwa (25) aliyekuwa akichimba Madini Kijiji cha Mwang’holo, anadaiwa kuuawa kwa kupigwa risasi na Polisi wanaolinda eneo la Kampuni ya El-Hillal Minerals Ltd

Soma - https://jamii.app/PoliceShy
MDAU: KABLA HAUJAPIGA PICHA YA UTUPU, FIKIRIA MADHARA YAKE

Ameshauri Watu kufikiria madhara ya picha hizo kabla ya kupiga na kuzisambaza akisema ni muhimu kutumia Maendeleo ya #Teknolojia kujijenga kiuchumi badala ya kuchapisha picha mbaya

Soma - https://jamii.app/UtupuPicha
#JFLeo
Rais Samia amewataka watanzania washughulike na masuala ya unyanyasaji kuanzia ngazi za familia

> Ametaja changamoto iliyopo ni watu kuongea na kumaliza suala la unyanyasaji kifamilia hali inayofanya unyanyasaji kuendelea kwa Watu wenye Ulemavu

Soma https://jamii.app/Unyanyasaji
Jamii Forums inakualika kushiriki kwenye Mazungumzo ya Demokrasia Nchini #Tanzania kupitia Digitali. Mazungumzo yatafanyika Machi 17, kuanzia saa 3 asubuhi yakiongozwa na Balozi wa #Sweden, Anders SjΓΆberg

Lengo ni kujenga na kubadilishana uzoefu kati ya Viongozi Wakuu kama Wanasiasa, Watumishi wa Umma, Wawakilishi wa Mashirika ya kiraia kuhusu #Demokrasia ya Kidigitali kama njia ya kuimarisha Maendeleo

Ungana nasi kupitia Kurasa zetu za Mitandao ya Kijamii ikiwemo Twitter, #Facebook, Instagram na #Telegram kufuatilia yatakayojiri.

#JamiiForums #Democracy
Rais Samia Suluhu Hassan amewataka Maafisa Ustawi wa Jamii kuweka mkazo katika kushughulikia changamoto za Watu wenye Ulemavu

> Amesema Maafisa hao wanashughulikia Mirathi na migogoro ya Ndoa kwa kuwa shauri likiisha watu hutoa chochote

Soma https://jamii.app/UstawiJamii

#JFLeo
Mazungumzo haya yanatoa fursa ya mjadala wa Umma kuhusu namna #Teknolojia za Kidigitali zinavyoweza kupanua fursa kwa Watanzania kushiriki ipasavyo katika Utawala wa Nchi na jinsi Serikali inavyoweza kutoa motisha kufikia Azma hiyo

Dhana ya Mazungumzo ya #Demokrasia ni juhudi za kufanya Demokrasia kuwa thabiti, na kuchangia katika Malengo ya Maendeleo Endelevu.

#JamiiForums #Democracy #HumanRights
HAITI: Madaktari, Wauguzi na Wahudumu wengine wa Sekta ya #Afya wamefanya mgomo kupinga wimbi la Utekaji nyara uliokithiri kwa Watu wa Sekta hiyo

Waliotekwa 2021 ni 655, ambapo Serikali inasema idadi inaweza kuwa kubwa zaidi

Soma - https://jamii.app/DrsStrikeHaiti
#HumanRightsViolations
KIGOMA: Kituo cha Sheria na #HakiZaBinadamu (LHRC) kimelaani mauaji ya Juma Ramadhan (35) aliyepigwa risasi na Askari wakati vurugu zikidhibitiwa Uwanja wa Lake Tanganyika

Kimetoa wito wa kuundwa Tume Huru ya uchunguzi

Soma - https://jamii.app/KgmPolice

#HumanRights #JamiiForums
HANDENI, TANGA: AJALI YAUA WATU WANNE NA KUJERUHI 37

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Safia Jongo amesema Basi dogo la Abiria aina ya Coaster iligonga Toyota Hiace na watembea kwa miguu na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi 37

Soma - https://jamii.app/TangaAjali

#JFLeo
Tanzania ni miongoni mwa Nchi zinazokua kwa kasi katika Masoko ya Kidigitali Barani Afrika. Idadi ya Watumiaji wa Huduma za Intaneti imeongezeka kutoka milioni 28 Machi 2021 hadi milioni 30 Februari 2022, sawa na ongezeko la asilimia 7.1.

Mazungumzo ya Machi 17, 2022 kuhusu Demokrasia ya Kidigitali Nchini #Tanzania yanalenga kutoa Jukwaa kwa Watendaji wa Serikali na wasio wa Serikali ili kuonesha mwelekeo wa Demokrasia kupitia #Teknolojia na changamoto zake

#JamiiForums #Democracy #HumanRights
ULIPOKUWA MTOTO ULITAKA KUFANYA KAZI GANI?

Swali 'Unataka kufanya kazi gani?' ni la kawaida kuulizwa ukiwa Mtoto, na wakati mwingine unaweza kuwa na ndoto za kuwa fulani Maishani mwako

Ukiwa Mtoto ulitaka kazi gani, na sasa unafanya nini?

Mjadala > https://jamii.app/KaziMtoto
Jopo la Wazungumzaji litahusisha hadhira inayowakilisha Serikali, Mashirika ya kiraia na Wabunifu.

Wadau wakuu watazungumza kuhusu hali ya sasa ya Demokrasia ya Kidigitali Nchini #Tanzania pamoja na matarajio yake. Kuangazia mafanikio yaliyopatikana na changamoto kupitia #Teknolojia za Kidigitali ili kukuza Serikali iliyo wazi na ushiriki hai wa Wananchi.

#JamiiForums #Democracy #DigitalSpaces