JamiiForums
βœ”
52.6K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Kampuni ya kutengeneza Ndege ya Marekani ya #Boeing (BA.N) imesitisha usambazaji wa Vifaa, matengenezo na usaidizi wa kiufundi kwa Mashirika ya Ndege ya Urusi kama sehemu ya vikwazo vilivyowekwa kutokana na uvamizi wake #Ukraine

Soma - https://jamii.app/BoeingRussia
#RussiaUkraineWar
Kuelekea Siku ya Usikivu Duniani (Machi 03, 2022), Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema zaidi ya Watu Bilioni 1 Duniani wapo katika hatari ya kupoteza uwezo wa kusikia kutokana na mazoea ya kusikiliza muziki kwa sauti kubwa, na kwa muda mrefu

Soma - https://jamii.app/WHD2022
NJOMBE: WANANCHI WALIOIBIWA MASUFURIA YA WALI WAITWA POLISI

Wananchi #Njombe wameitwa kituoni kutambua mali zilizokamatwa wakati wa doria ya Polisi

Baadhi ya mali ni magodoro, pikipiki, sufuria, mitungi ya gesi, jiko, laptop na TV

Soma - https://jamii.app/SufuriaNjombe
#JamiiForums
APPLE YASITISHA KUUZA BIDHAA URUSI

Kampuni hiyo kubwa ya Teknolojia pia imesema huduma nyingine zikiwemo Apple Pay na Apple Maps zitadhibitiwa kufuatia uvamizi uliofanywa na Urusi dhidi ya #Ukraine, na kupekelea maelfu kukimbilia Mataifa jirani

Soma - https://jamii.app/AppleUrusi
TETESI: ABRAMOVICH KUIUZA CHELSEA

Bilionea wa Uswisi, Hansjorg Wyss (86) amedai amepewa nafasi ya kujiunga na Wawekezaji 6 au 7 kuinunua Chelsea

Amedai β€œAbramovich anataka fedha nyingi, anaidai Chelsea Β£2bn na Chelsea haina pesa. Hadi sasa hatujui bei halisi ya kuinunua”

#JFSports
#AFYA: Maziwa Mtindi huwa na Protini nyingi, Calcium, Vitamini, na Bakteria wazuri ambao husaidia kubadilisha Sukari. Mtindi husaidia kutoa ulinzi kwenye Mifupa na Meno na pia kuzuia matatizo ya Usagaji wa Chakula

Aidha, Mtindi umeonesha kuwa na uwezo mkubwa wa kutoa kinga dhidi ya Maradhi ya kuambukiza Ukeni (Vaginal infections)

Soma - https://jamii.app/BenefitsYoghurt
#JamiiForums #HealthCare
UGANDA: MWANDISHI ALIYEKIMBIA NCHI AFUNGUA KESI DHIDI YA SERIKALI

Kakwenza Rukirabashaija amedai aliteswa alipokuwa chini ya ulinzi, akitaka Mahakama ya Haki Afrika Mashariki iseme kukamatwa na kuteswa kwake ni kinyume cha Sheria

Soma - https://jamii.app/UGGovtSued

#JFLeo
SONGWE: Wakazi wa eneo la Old Vwawa wamekutana na kinachodaiwa ni mabaki ya mwili wa binadamu katika shimo ambalo lilichimbwa kwa ajili ya kusimika nguzo ya umeme

> Wakazi hao wamedai kukuta mifupa ya binadamu, cheni, bangili na jino

Soma - https://jamii.app/Songwe

#JamiiForums
Kutokana na utelekezaji wa Sera ya Elimu Msingi bila malipo ya Mwaka 2015/16, kumekuwa na ongezeko la Wanafunzi kila mwaka.

Ongezeko la Wanafunzi lilipaswa kwenda sambamba na uboreshwaji wa Miundombinu ya Shule kama vile Vyumba vya Madarasa, Madawati, Matundu ya Vyoo nk.

#JamiiForums #JFUwajibikaji #WAJIBU #Accountability #JFPartnership
VIONGOZI WA DINI: BUSARA ITUMIKE KUMALIZA KESI YA MBOWE

Wakiwa Ikulu, Dar wameomba Mamlaka husika kutumia busara na kuangalia namna ya kumaliza kesi hiyo

Pia, wamependekeza kuwe na Mjadala kuhusu Mfumo mpya wa Elimu utakaokidhi mahitaji ya sasa

Soma - https://jamii.app/ViongoziDiniIkulu
UKRAINE - UPDATES: Jeshi la Urusi linadaiwa kushambulia Shule 3 Mjini #Kharkiv. Pia inaripotiwa kuwa Majengo kadhaa ya Makazi ya Watu huko #Okhtyrka nayo yameharibiwa kutokana na mashambulizi yanayoendelea

Watu zaidi ya Milioni 1 wamekimbia #Ukraine

Soma https://jamii.app/UkraineUrusi
MSUMBIJI: MAWAZIRI SITA WAONDOLEWA KAZINI

Rais Filipe Nyusi amewatoa kwenye nafasi zao Mawaziri sita wakiwemo Waziri wa Fedha na Waziri wa Madini na Nishati

Ni Mabadiliko makubwa ya pili kufanyika kwenye Baraza la Mawaziri miezi ya hivi karibuni

Soma - https://jamii.app/MinisterSackMoz
URUSI: Waziri wa Ulinzi, Meja Jenerali Igor Konashenkov amesema Wanajeshi wa #Urusi 498 wameuawa na 1,597 wamejeruhiwa ktk mapigano na #Ukraine

> Aidha, Rais wa Ukraine amesema Wanajeshi wa Urusi 7,000 wameuawa ktk mapigano hayo

Soma https://jamii.app/UrusiWapiganaji

#RussiaUkraineConflict
Machi 03, 2022 ni Siku ya Usikivu Duniani ambapo inaelezwa takriban Watu Bilioni 1.5 Duniani kote wanaishi na tatizo la usikivu. Wataalamu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) wanasema idadi hii inaweza kuongezeka hadi Bilioni 2.5 kufikia Mwaka 2030

Kaulimbiu ya Mwaka 2022 inasema, "Ili kusikia maisha yote, sikiliza kwa uangalifu!"

Soma - https://jamii.app/TatizoUsikivu

#WorldHearingDay2022
DAR: Daniel Muga, mkazi wa Bombambili anasakwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua mtoto wake wa miaka mitatu kwa kumpiga na kitu kizito kichwani

> Kamanda wa Polisi Dar, ACP Muliro Jumanne Muliro amesema tukio hilo lilitokea Februari 28, 2022

Soma - https://jamii.app/Mauaji
AFYA: MAMBO UNAYOTAKIWA KUYAFAHAMU
KUHUSU KUCHANGIA DAMU


Huwezi kupata Maambukizi ya Magonjwa kwa kuchangia Damu kwasababu zoezi la kuchangia Damu ni salama na huendeshwa na Watumishi wenye ujuzi na vifaa vinavyotumika ni salama

Mtu mwenye #Afya ana wastani wa Lita 6 - 7 za Damu na anaweza kuchangia mara kwa mara, chupa moja ya Damu ina ujazo usiozidi Mililita 450. Pia, Mtu mwenye uzito wa Kilo 50 na kuendelea ana Damu ya kutosha kuweza kuchangia.

#JamiiForums #HealthCare #BloodDonation
Ripoti ya ukaguzi ya Mwaka 2019/20 inaonesha kati ya mapendekezo 15 yaliyotolewa na CAG Mwaka 2018/19, OR – TAMISEMI haikutekeleza pendekezo lolote kikamilifu

Ripoti hiyo pia inaonesha kati ya mapendekezo 3,126 yaliyotolewa Mwaka 2018/19, ni mapendekezo 1,071 sawa na 34% ndiyo yametekelezwa kikamilifu.

#JamiiForums #JFUwajibikaji #Accountability #WAJIBU #JFPartnership
MDAU: VIJANA WASHIRIKISHWE ZAIDI KWENYE SHUGHULI ZA MAENDELEO

Asema nyenzo ya uhusishwaji/ushikishwaji Vijana ktk Mipango na Utekelezaji wa shughuli za Maendeleo isipotumika vizuri, inaweza kuchangia Vijana na Serikali kulaumiana

Soma https://jamii.app/VijanaSerikaliSOC

#StoriesOfChange
LIBYA HATARINI KUTUMBUKIA ZAIDI KWENYE MGOGORO WA KISIASA

Bunge linajiandaa kuapisha Serikali ya Fathi Bashagha huko Tobruk, Mashariki mwa #Libya lakini Waziri Mkuu aliye Madarakani, Abdulhamid al-Dbeibah ameapa kutoachia madaraka

Soma - https://jamii.app/SiasaLibya

#JFLeo
WANACHAMA WA UN WAPIGA KURA YA MZOZO WA URUSI NA UKRAINE

Nchi 141 zimelaani #Russia na kuridhia kuwekewa vikwazo mbalimbali vya Kimaendeleo

Nchi 4 zimekubaliana na Urusi. Nchi 35 hazijafungamana na upande wowote ikiwemo #Tanzania, China na Uganda

Soma - https://jamii.app/UNVoteUkraine