JamiiForums
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
WAZIRI NAPE: SHERIA YA ULINZI WA DATA NI YA MUHIMU

Amesema ni ya msingi katika Tanzania ya kidijitali ili watu wajiamini na kuwa huru

JamiiForums imekuwa mstari wa mbele kuitetea Haki ya Faragha kwa mujibu wa Ibara ya 16 ya Katiba

Soma https://jamii.app/NapeData

#DataProtection #DataPrivacy
MAREKANI YADAI INA ORODHA YA WANAOPASWA KUUAWA NA URUSI ITAKAPOIVAMIA UKRAINE

Marekani imedai miongoni mwa walengwa ni wapinzani wa kisiasa na makundi madogo ya watu wa Dini

Urusi imeendelea kukanusha kuwa na mpango wa kushambulia Ukraine

Soma - https://jamii.app/UrusiUkraine
#JFLeo
TANZANIA KUPATA MKOPO WA TRILIONI 1.5 KUTOKA BENKI YA DUNIA

Benki ya Dunia (WB) na #Tanzania zimesaini Mikataba ya Mkopo wa masharti nafuu wa Dola Milioni 650 kwa ajili ya Miradi ya kuboresha #Elimu na kuimarisha Usalama na umiliki ardhi

Soma - https://jamii.app/MkoboTrilioni

#Governance
HOJA: UNATAMANI UZEE WAKO UWEJE?

Mdau wa JamiiForums.com anasema akifikisha Miaka 60 hataki kutumia nguvu nyingi kutafuta riziki

Anatamani uwe wakati wa kukaa na Wajukuu zake. Pia, hatamani kuishi Mjini ambako kuna msongamano wa Watu

Je, nawe unataka Uzee wako uweje?

Mjadala - https://jamii.app/TamaaUzee
#Maisha
#MALI: Bunge la Mpito limepitisha kwa Kura zote Muswada wa kutawaliwa na Jeshi kwa miaka mitano. Mali iliingia katika Utawala wa Kijeshi baada ya Mapinduzi ya Mei 2021

Jumuiya mbalimbali zinashinikiza Utawala wa Kiraia kurejeshwa

Soma - https://jamii.app/MaliJeshi

#Democracy
Umoja wa Ulaya umewawekea Vikwazo Maafisa wa #Myanmar pamoja na #Biashara za Mafuta na Gesi kutokana na Mapinduzi ya Mwaka mmoja uliopita

50% ya Mapato ya Myanmar yanatokana na Fedha za Kigeni zinazopatikana kupitia rasilimali ya Gesi

Soma - https://jamii.app/EUBanMyanmar

#Democracy
BRAZIL: MAFURIKO YAUA WATU 176

Mvua kubwa iliyonyesha huko #Petropolis iliwafunika watu wengi kwenye tope na hadi sasa watu zaidi ya 110 bado hawajulikani walipo

Mvua zimesababisha mafuriko na maporomoko maeneo mbalimbali Nchini #Brazil

Soma - https://jamii.app/BrazilVifo176
#JFLeo
#PAKISTAN: WANAOKOSOA MAMLAKA MTANDAONI KUFUNGWA HADI MIAKA 5

Wanaokosoa Jeshi, Mahakama au Maafisa wa Umma Mtandaoni watafungwa Miaka 5 na hakuna dhamana

Wanaharakati wanasema Sheria inazidi kuminya Uhuru wa Kujieleza ktk Taifa hilo

Soma - https://jamii.app/PakistanLawSM
#FreeSpeech
JE, WAJUA; Leo 22/02/2022 ni #Palindrome, ikimaanisha Namba inaweza kusomeka kwa kwenda mbele au kurudi nyuma bila kupoteza thamani

Pia leo ni 'Ambigram' ambayo humaanisha Sanaa inayoweza kufanya neno/namba lisomeke juu chini, na chini juu

Soma https://jamii.app/Paliondrome

#TwosDay
DAKTARI: MATUMIZI YA P2 HUCHANGIA MIMBA KUTUNGA NJE YA KIZAZI

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Wanawake, Godfrey Chale akizungumza na Global amesema utafiti uliofanyika #Ghana 2003 ulionesha Vidonge vya P2 husababisha Mimba kutungwa nje hasa kwa wanakosea matumizi

Soma - https://jamii.app/P2EctopicPreg
#Afya
SERIKALI: SHERIA YA MAKOSA YA MTANDAO YA 2015 INGETUMIKA IPASAVYO MAHABUSU ZINGEJAA

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Habari, Kundo Mathew ambaye pia amesema kuna mkanganyiko kati ya Ofisi ya DCI na TCRA kutokana na Sheria hiyo

Soma - https://jamii.app/CyberCrimeAct

#DigitalRights
BURKINA FASO: WATU 60 WAFARIKI DUNIA KUTOKANA NA MLIPUKO MGODINI

Mamlaka zimesema mlipuko uliotokea mwenye Mgodi wa Dhahabu umetokana na vilipuzi vinavyotumika machimboni

Machimbo yasiyoidhinishwa yametajwa kuwa na ajali za mara kwa mara

Soma - https://jamii.app/BurkinaFasoMlipuko

#JFLeo
RAIS SAMIA: KAMA UNAMJUA MUNGU HUWEZI KUMUUA MWENZIO

Asema "Kama unamjua Mungu huwezi kumuua mwenzio kwa Urithi, Kisasi au umeambiwa amekuroga hukuvuna"

Awaomba Viongozi wa Kimila kuwaambia Watu kinachotokea sicho tulichoamrishwa kwa Dini wala Mila

Soma https://jamii.app/SamiaMauajiTZ
Rais Samia Suluhu Hassan amesema hana tabia ya kutukuzwa wala kulinganishwa na Mungu na atajitahidi kuwa na Hekima na Uvumilivu

Amesema hayo leo, Februari 22, 2022 katika sherehe za Jubilee ya Miaka 25 ya Askofu Niwemugizi iliyofanyika Wilayani Ngara Mkoani Kagera.

#JamiiForums
KITU GANI KILIKUSAIDIA KUPATA KAZI?

Baadhi ya Wadau ndani ya JamiiForums.com wametaja vitu vilivyowasaidia kupata Kazi ikiwemo Maombi, kutembeza CV kwenye kila Ofisi, Kujitolea, Kujiamini kwenye Usahili na 'Connection'

Je, Wewe uliwezaje kupata Kazi?

Mjadala zaidi - https://jamii.app/MbinuAjira
#Maisha
DKT. KIGWANGALLA KUIPINGA SERIKALI JUU YA UJENZI WA MAKAO MAKUU YA WILAYA NZEGA

Waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa ameelekeza Makao Makuu kujengwa Lubisu badala ya Ndalla

Mbunge huyo wa Nzega Vijijini asema mchakato haujafuata Sheria na Kanuni

Soma https://jamii.app/NzegaDktKigwangalla
COLOMBIA YAHALALISHA UTOAJI MIMBA YA HADI MIEZI SITA

Mahakama ya Kikatiba imeruhusu utoaji Mimba hadi yenye wiki 24. Mashirika ya kutetea Haki za Wanawake yameripoti kuwa Wanawake 400,000 kila mwaka Nchini humo walikuwa wanatoa Mimba kwa siri

Soma - https://jamii.app/AbortionColombia
MDAU: MKOPESHE RAFIKI/NDUGU KIASI CHA FEDHA UNACHOWEZA KUSAMEHE

Anasema ili kulinda Heshima baina yako na Rafiki au Ndugu zako linapokuja suala la Fedha inabidi uwe na Akili sana

Utakapokuwa na uhitaji halafu uliyemkopesha anakuzungusha utabaki kuumia Moyoni, na kupotezeana Heshima huanzia hapo

Unakubaliana na Mdau huyu?

Mjadala - https://jamii.app/MkopoNduguRafiki

#JamiiForums #Maisha
NACTE YAONGEZEWA MAJUKUMU YA VETA

Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) limekuwa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) kutokana na mabadiliko ya Sheria

> Mabadiliko hayo yanalenga kuongeza ufanisi

Soma https://jamii.app/NACTVET
#JFLeo
UGANDA: Muswada wa Sheria Mpya ya Afya ya Umma umependekeza faini ya Ush. Milioni 4 (Tsh. Milioni 2.6) kwa watakaokataa chanjo huku watakaoshindwa kulipa faini hiyo wanaweza kwenda jela

> Haijafahamika ni lini Muswada huo utapelekwa Bungeni

Soma https://jamii.app/FainiChanjoUg