JamiiForums
βœ”
52.9K subscribers
34.3K photos
2.42K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MALAWI: BARAZA LA MAWAZIRI LAVUNJWA KWA KASHFA ZA UFISADI

Kashfa za ubadhirifu wa mali za umma za baadhi ya Mawaziri zikijumuisha kuchepusha fedha za #COVID19 na kuingia mikataba ya kifisadi imepelekea Rais Chakwera kulivunja Baraza la Mawaziri

Soma https://jamii.app/MalawiCabinet

#Accountability
CAMEROON: WATU SITA WAFARIKI NA 40 WAJERUHIWA KTK MKANYAGANO

Watu takriban 50,000 walikuwa wakitaka kushuhudia mechi kati ya #TeamCameroon na #TeamComoros ktk michuano ya #AFCON2022

Hospitali iliyo jirani na uwanja wa Olembe imepokea majeruhi 40

Soma - https://jamii.app/6AFCON

#JFSports
LINDA TAARIFA ZAKO BINAFSI MTANDAONI

Taarifa binafsi kama Jina lako, Namba ya Simu na Anwani huweza kuleta madhara zikiwa mtandaoni bila kulindwa, kwani ni rahisi kudukuliwa

Weka Password imara kwenye kifaa chako cha kielektroniki

Soma - https://jamii.app/UlinziTaarifa

#DataProtection
JE, WAJUA: Kahawa aina ya Arabika inauzwa kwa bei kubwa kuliko Robusta ktk soko la dunia

Kwa kipindi cha Mwaka 2002 hadi 2021 Arabika iliuzwa hadi kwa Tsh. 15,250 kwa Kg, na bei kubwa ya Robusta iliyorekodiwa kwa kipindi hiko ni Tsh. 8,550

Soma - https://jamii.app/ArabikaRobusta

#JFBiashara
WHO: CORONA INAWEZA KUISHA MWISHO WA MWAKA 2022

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema ikiwa nchi zote zitachukua hatua zinazostahili, #COVID19 inaweza kuisha kufikia mwishoni mwa 2022

Soma https://jamii.app/Corona2022

#JFAfya #UVIKO3
πŸ‘1
SARATANI NI NINI?

Miili yetu ina chembechembe hai nyingi ambazo huzaliana, hukua, na kufa kwa mpangalio maalum

Chembechembe za Saratani zinazaliana haraka zaidi bila mpangilio na kukua haraka

Zisipotibiwa mapema zinaweza kusambaa na kuota sehemu nyingine mwilini

Soma - https://jamii.app/SarataniOR

#JFAfya #Cancer #Saratani
TMA YATABIRI UPEPO MKALI NA MAWIMBI

Tahadhari ya Upepo mkali unaozidi Kilomita 40 kwa saa pamoja na mawimbi makubwa imetolewa kwa baadhi ya maeneo ya Ukanda wa Pwani ya Bahari ya Hindi yakiwemo Dar, Tanga, Mtwara, Visiwa vya Unguja na Pemba

Soma - https://jamii.app/UpepoTMA

#JFMatukio
DAR: MACHINGA WAOMBA UWAKILISHI KWENYE VYOMBO MBALIMBALI

Pia, wamesema maeneo mengi waliyopelekwa baadhi yao hayana miundombinu rafiki, na yana ukosefu wa wateja

Wapendekeza maeneo hayo kuboreshwa ili wasirudi walipohamishwa

Soma - https://jamii.app/MachingaRaisIkulu

#JFBiashara
πŸ‘1
MACHINGA KUWA MIONGONI MWA MAKUNDI MAALUM

Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali inawatambua rasmi Machinga kama kundi maalum, na litakuwa moja ya Makundi yatakayohudumiwa na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Makundi Maalum

Soma - https://jamii.app/MachingaRaisIkulu

#JFBiashara
Rais Samia Suluhu Hassan amesema Serikali ina mipango kadhaa ya kuhakikisha Wafanyabiashara wadogo wanapata mitaji kwa urahisi

Aidha, ameagiza Benki kuja na Mifumo kwaajili ya kuwasaidia Wanawake na Vijana, ambayo itakuwa ikitoa huduma ya Mikopo

Soma - https://jamii.app/ProgramBenki

#JFSiasa
RAIS SAMIA AWATAKA VIONGOZI WAENDELEE KUSIMAMIA UTOAJI CHANJO

Asema waliopata Chanjo hawapati madhara kama wasiopata Chanjo

Ameongeza Tanzania imekumbwa na mawimbi kadhaa na kwasasa kuna wimbi la 4 ambalo halijaua sana kama yaliyotangulia

Soma - https://jamii.app/ChanjoViongozi

#UVIKO3 #JFAfya
Rais Samia amesema baada ya kujenga Masoko na kuboresha maeneo wataweka Kodi itakayotakiwa kulipwa na Machinga ambapo amewaasa walipe kadiri itakavyowekwa

Pia, amewaasa kutotumika na wenye Maduka kusambaza Bidhaa hali inayoinyima Serikali Kodi

Soma - https://jamii.app/KodiMachinga

#JFSiasa
KENYA YARUHUSU NDEGE ZA ABIRIA KUTOKA UMOJA WA FALME ZA KIARABU KUTUA

Januari 10, 2022, Kenya ilizuia Ndege za Abiria toka Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kutua Nchini humo baada ya marufuku iliyowekwa na UAE dhidi ya Ndege za Abiria toka Kenya

Soma https://jamii.app/UAEVsKenya

#JFSiasa
NINI HUSABABISHA SARATANI?

Hakuna sababu moja, Saratani tofauti zina vyanzo vyake. Miongoni mwa Visababishi visivyozuilika ni Umri

Umri unapokuwa mkubwa, uwezekano wa kutokea dosari katika mabadiliko ya DNA yanayosababisha Kansa huongezeka

Baadhi ya Visababishi vinavyozuilika ni pamoja na uvutaji wa sigara, ulaji mbovu, kutumia pombe kupita kiasi na kutofanya mazoezi

Soma - https://jamii.app/SarataniOR

#JFAfya #Cancer #Saratani
MDAU: FIKRA BORA NA UHURU WA MAONI VITACHOCHEA MAPINDUZI YA KIUCHUMI

Anashauri;

1) Mfumo wa Elimu ulenge kujenga zaidi uwezo: Anasema bado Tanzania ina changamoto kwani Jamii imeshaamini kusoma ni kuruka Vidato na sio kupima mtu anafahamu nini

2) Kuondoa Sheria zinazominya Uhuru wa Maoni: Kuwa na jamii iliyofungwa mdomo humaanisha Serikali itabaki kuamini Sera zake ni nzuri hata kama si uhalisia

Soma - https://jamii.app/FikraUhuruSOC

#StoriesOfChange #JFMaarifa
RIPOTI: ONGEZEKO LA UFISADI LINAKANDAMIZA HAKI ZA BINADAMU

Ripoti ya Transparency International inasema #COVID19 imetumiwa na Nchi nyingi kama kisingizio cha kuacha kufanya ukaguzi

Serikali zatakiwa kuwa wazi kuhusu namna Fedha zinavyotumika

Soma - https://jamii.app/RipotiUfisadi

#HumanRights
JE, UNAYAFAHAMU MAGARI YENYE UWEZO WA KUTEMBEA NCHI KAVU NA MAJINI?

Yanaitwa β€˜Amphibious Vehicles’ ambapo huwa na Injini kwa ajili ya kutembea Nchi kavu na propela ili kutembea Majini

Magari haya hayahitaji uwepo wa gati kuingia kwenye Maji

Soma https://jamii.app/AmphibiousVehicles

#JFMaarifa #JFGarage
#AFCON2021: SENEGAL YAFUZU KUCHEZA ROBO FAINALI

- #TeamSenegal imefuzu baada ya kuifunga #TeamCapeVerde goli 2-0 ndani ya dk 90. Wachezaji wawili wa Cape Verde walipewa kadi nyekundu

- Senegal itakutana na mshindi wa mechi kati ya #TeamMali na #TeamEquatorialGuinea

#JFSports
MOROCCO YAFUZU KUCHEZA ROBO FAINALI #AFCON2021

- #TeamMorocco imefuzu kwa kuifunga #TeamMalawi goli 2-1 ndani ya dk 90

- Morocco itakutana na mshindi kati ya #TeamCotedIvoire na #TeamEgypt

- Hii ilikuwa ni mechi ya 10 ya Malawi kwenye michuano na imeshinda mechi 2

#JFSports
MTWARA: MAAFISA POLISI 7 WAFIKISHWA MAHAKAMANI KWA MAUAJI

Wanatuhumiwa kwa mauaji ya Mfanyabishara Mussa Hamisi Hamisi aliyekuwa akiwadai Maafisa hao zaidi ya Tsh. Milioni 33.7

Inadaiwa walijipatia fedha hizo wakati wakimfanyia upekuzi

Soma - https://jamii.app/MaafisaPolisiMauaji

#JFUwajibikaji