JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
#LIBERIA: WATU 29 WAFARIKI KWENYE MKANYAGANO WA MAOMBI

Polisi wasema vifo huenda vikaongezeka kwasababu baadhi ya waliojeruhiwa wana hali mbaya

Mchungaji Abraham Kromah aliandaa kusanyiko la Maombi la Siku 2 lililofanyika ktk Uwanja wa Mpira

Soma https://jamii.app/29DeadStampede

#JFMatukio
Mlipuko mkubwa wa #Ebola tangu kugundulika kwake, ulitokea Afrika ya Magharibi Mwaka 2014 - 2016

Ulianzia #Guinea na kusambaa hadi #SierraLeone na #Liberia. Katika mlipuko huo kulikuwa na Wagonjwa na Vifo vingi kuliko jumla ya kwenye milipuko mingine yote kwa pamoja

#JFAfya
#DEMOKRASIA: Wananchi wa #Liberia wanatarajiwa kupiga kura leo Novemba 14, 2023 kumchagua Rais katika Awamu ya Pili ya Uchaguzi unaowakutanisha wagombea wawili, #GeorgeWeah anayetetea nafasi hiyo na #JosephBoakai baada ya kutofautiana kwa kura chache katika Awamu ya Kwanza

Weah (57) aliongoza katika kura zilizopigwa Oktoba 2023 kwa kupata 43.8% wakati Boakai (78) ambaye alikuwa Makamu wa Rais 2006 hadi 2018 alipata 43.4%, hivyo hakukuwa na Mshindi kwa kuwa hakukuwa na aliyefikisha 50% ya Kura kama Sheria inavyotaka

Soma https://jamii.app/LiberiaElection23

#Democracy #Governance #JamiiForums
👍21
LIBERIA: Rais #GeorgeWeah amempigia simu mpinzani wake katika kinyang'anyiro cha Urais, #JosephBoakai kumpongeza kwa ushindi wake. Akihutubia Taifa amesema "Watu wa #Liberia wameongea na tumesikia sauti yao."

Boakai anaongoza kwa kura 28,000 huku takriban kura zote zikiwa zimehesabiwa. Hapo awali Tume ya Uchaguzi ilitangaza kuwa Boakai, mwenye umri wa Miaka 78 alikuwa na Asilimia 50.89 ya kura zote, huku Rais Weah akiwa na 49.11%

Weah, Nyota wa zamani wa Soka, amekuwa madarakani tangu Mwaka 2018, atakabidhi madaraka Januari 2024

Soma https://jamii.app/UraisLiberia

#JamiiForums #Governance #Demokrasia #Democracy #LiberiaElections
👍2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
LIBERIA: Rais Joseph Boakai, (79) alishindwa kumaliza hotuba yake baada ya Uapisho ambapo aliongea kwa dakika 30 na kupata changamoto iliyomlazimu kupewa msaada wa kuondoka Jukwaani wakati wa sherehe ya kuapishwa kwake

Rais #Boakai alishindwa mara mbili kuendelea na hotuba yake, na sherehe ikasitishwa. Baadhi ya Ripoti zimedai kwamba alipatwa na uchovu uliotokana na Joto kali

#JosephBoakai ndiye Rais mwenye Umri Mkubwa zaidi katika Historia ya Marais wa #Liberia

Soma https://jamii.app/UapishoLiberia

#JamiiForums #Democracy #Governance
👍2💩21
#JuliaSebutinde ambaye amechaguliwa kwa kipindi cha Miaka 3 amekuwa Jaji wa ICJ kwa zaidi ya Miaka 10. Hapo awali aliendesha kesi kadhaa za uhalifu wa kivita, ikiwa ni pamoja na kufunguliwa mashtaka kwa Rais wa zamani wa #Liberia Charles Taylor

Sebutinde mzaliwa wa #Uganda alikuwa Jaji pekee katika jopo la Wanachama 17 wa Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kupiga kura dhidi ya hatua zote 6 zilizopitishwa na Mahakama ya ICJ katika kesi iliyofunguliwa na Afrika Kusini, ambapo Israel iliamriwa ichukue hatua za haraka kuzuia Mauaji ya halaiki inapopambana na Wanamgambo wa #Hamas huko #Gaza

Serikali ya Uganda ilijitenga na maoni pinzani ya Jaji Sebutinde ikisema hawakilishi msimamo wa nchi hiyo katika mzozo huo

Soma https://jamii.app/JajiSebutinde

#JamiiForums #Democracy #Diplomacy #Governance
👍1
#LIBERIA: Waziri wa Ulinzi, Prince Charles Johnson III amejiuzulu baada ya Wake wa Maafisa wa Jeshi kuandamana kwa malalamiko ya Waume zao kutoongezewa Mshahara huku wakiishi Maisha duni katika Kambi za Kijeshi

Wanawake hao waliandamana na kuweka Vizuizi kwenye Barabara zinazoingia katika Jiji la #Monrovia na maeneo mengi ya Nchi wakishinikiza Rais #JosephBoakai kusitisha Sherehe za Kitaifa za Jeshi huku wakimtuhumu Waziri huyo kufuja Fedha za Wanajeshi wanaorejea kutoka Vitani

Pia, wamedai Wanajeshi wamekuwa na hali mbaya kwenye Mifuko ya Hifadhi ya Jamii, Kutokuwepo kwa Umeme wa Uhakika kwenye Makazi yao pamoja na ongezeko la Rushwa miongoni mwa Vikosi vya Jeshi

Soma https://jamii.app/LiberiaCS

#JamiiForums #SocialJustice #Governance #Accountability #JFSC
👍43😁2
Mitandao ya #Netblocks na #CloudflareRadar inayohusika na ufuatiliaji wa Huduma za Intaneti na Usalama Mtandaoni imesema baadhi ya Nchi Barani Afrika zimepatwa na tatizo la kukatika kwa Huduma za Intaneti, sababu ikidaiwa ni kukatika kwa nyaya katika Mkongo wa Mawasiliano wa Baharini

Baadhi ya Nchi zilizoripoti kupata shida kwenye mawasiliano ni Tanzania, #IvoryCoast ambayo imeripoti kushuka kwa ubora kwa Intaneti hadi 4%, #Benin 14% na #Ghana kwa 25% huku nchi nyingine zilizopata shida zikiwa ni Afrika Kusini, #Nigeria, #Liberia, na #BurkinaFaso

Nchini #Tanzania, Mtandao wa #Vodacom umekiri kutokea kwa tatizo kwenye huduma za intaneti huku wakisema huduma za M-PESA, Kupiga na Kupokea Simu zinapatikana. Pia, Serikali za Nigeria na Liberia zimesema zimebaini uwepo wa tatizo la Intaneti

Vipi Mdau, umepata changamoto za Mawasiliano ya Simu au Intaneti wiki hii?

Soma https://jamii.app/ComsDisrupt

#JamiiForums #DigitalRights #AccessNow #InternetDisruption #ServiceDelivery
👍8👎1