Unapocheka, haujifurahishi tu bali pia unapunguza msongo wa mawazo, unaimarisha kinga ya mwili na kulinda moyo wako.
Kwa kifupi, kicheko ni afya — basi jitafutie sababu ya kucheka kila siku. 😄
Tembelea JamiiForums.com kushiriki kwenye mijadala mbalimbali yenye tija.
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
Kwa kifupi, kicheko ni afya — basi jitafutie sababu ya kucheka kila siku. 😄
Tembelea JamiiForums.com kushiriki kwenye mijadala mbalimbali yenye tija.
#JamiiAfrica #JamiiForums #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
😁1
KATAVI: Mdau wa JamiiForums.com aliyejitambulisha kuwa Mkazi wa Wilaya ya Mpanda anatoa wito kwa Shirika la Umeme Tanzania (#TANESCO) kushughulikia changamoto ya umeme kukatika mara kwa mara, akihoji mbona wanapodai madai yao hutumia magari ya matangazo kuzunguka Mtaani kufikisha ujumbe, lakini suala la kukata umeme hutumia makundi ya WhatsApp ambayo Wananchi wengi hawana au hawatumii?
Zaidi soma https://jamii.app/UmemeMpanda
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
Zaidi soma https://jamii.app/UmemeMpanda
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Akizungumza Agosti 18, 2025, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Prof. Palamagamba Kabudi, amesema "Uchaguzi wetu kila baada ya Miaka mitano ni jambo muhimu sana kwa Taifa letu, ndiyo kielelezo cha #Demokrasia ya #Tanzania. Nchi hii haijawahi kuahirisha uchaguzi hata mara moja na katika mazingira magumu kuliko sasa. Wanaotaka Uchaguzi uahirishwe hawaelewi historia ya nchi hii."
Zaidi soma https://jamii.app/KabudiUchaguziMkuu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
Zaidi soma https://jamii.app/KabudiUchaguziMkuu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
ETHIOPIA: Wizara ya Elimu imetoa mwongozo unaopiga marufuku utoaji wa Shahada za Heshima (Honorary Doctorate) kwa Viongozi wa Serikali na Wanasiasa walioko madarakani, agizo hilo limetiwa saini na Waziri wa Elimu, Profesa Berhanu Nega, na limeelekezwa kwa Vyuo Vikuu na taasisi zote za elimu.
Mwongozo huo umeweka masharti mapya, ukiwataka wanaotunukiwa wawe ni waliotoa mchango mkubwa katika taaluma au kazi zao. Viongozi walioko kazini na Wafanyakazi wa Vyuo Vikuu na Wajumbe wa Seneti, hawataruhusiwa kupokea shahada hizo wakiwa bado kazini.
Aidha, vyuo vitakavyotoa shahada ya heshima vinapaswa kutoa kozi za PhD, viwe na angalau awamu nane za wahitimu, na viwe vinatambulika Kitaifa na Kimataifa.
Upande wa Tanzania, miongoni mwa waliotunukiwa Shahada za Heshima na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni Hayati Mwalimu Julius Nyerere (1966, 1986), Balozi Juma Mwapachu (2005), na Rais Mstaafu Hayati Benjamin Mkapa (2006). Licha ya mchango wao mkubwa, hawakuwahi kutumia cheo cha “Daktari wa Heshima”.
Zaidi soma https://jamii.app/EthiopiaMarufukuPhD
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
Mwongozo huo umeweka masharti mapya, ukiwataka wanaotunukiwa wawe ni waliotoa mchango mkubwa katika taaluma au kazi zao. Viongozi walioko kazini na Wafanyakazi wa Vyuo Vikuu na Wajumbe wa Seneti, hawataruhusiwa kupokea shahada hizo wakiwa bado kazini.
Aidha, vyuo vitakavyotoa shahada ya heshima vinapaswa kutoa kozi za PhD, viwe na angalau awamu nane za wahitimu, na viwe vinatambulika Kitaifa na Kimataifa.
Upande wa Tanzania, miongoni mwa waliotunukiwa Shahada za Heshima na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni Hayati Mwalimu Julius Nyerere (1966, 1986), Balozi Juma Mwapachu (2005), na Rais Mstaafu Hayati Benjamin Mkapa (2006). Licha ya mchango wao mkubwa, hawakuwahi kutumia cheo cha “Daktari wa Heshima”.
Zaidi soma https://jamii.app/EthiopiaMarufukuPhD
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
DAR: Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), leo Agosti 20, 2025 limeeleza kuwa mechi ya Ngao ya Jamii itakayozindua msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara 2025/26 itachezwa Septemba 16, 2025 ikizikutanisha Young Africans SC (Yanga) dhidi ya Simba SC.
TFF imesema marekebisho yametokana na ratiba nyingi za Fainali za Kombe la Mataifa la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (#CHAN) 2025 na michezo ya mchujo ya Kombe la Dunia inayohusisha timu ya Taifa #TaifaStars.
Hivyo, mechi hiyo itachezwa kwa mchezo mmoja badala ya mfumo wa mechi tatu kama ilivyokuwa msimu uliopita ili kuepuka msongamano wa ratiba na kurahisishia maandalizi ya klabu katika mashindano ya #CAF.
Zaidi soma https://jamii.app/WataniKwenyeNgaoYaJamii
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports
TFF imesema marekebisho yametokana na ratiba nyingi za Fainali za Kombe la Mataifa la Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (#CHAN) 2025 na michezo ya mchujo ya Kombe la Dunia inayohusisha timu ya Taifa #TaifaStars.
Hivyo, mechi hiyo itachezwa kwa mchezo mmoja badala ya mfumo wa mechi tatu kama ilivyokuwa msimu uliopita ili kuepuka msongamano wa ratiba na kurahisishia maandalizi ya klabu katika mashindano ya #CAF.
Zaidi soma https://jamii.app/WataniKwenyeNgaoYaJamii
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFSports
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Mhariri Mwandamizi kutoka Baraza la Kiswahili Tanzania (#BAKITA), Onni Sigala amefafanua kuwa neno ‘Ngono’ limepoteza maana yake halisi kwenye jamii, na kuongeza kuwa halina uhusiano kabisa na maana ambayo wengi kwenye jamii wanayoifahamu.
Kwa mjadala zaidi bofya https://jamii.app/MaanaNgono
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFKiswahili #JFLugha
Kwa mjadala zaidi bofya https://jamii.app/MaanaNgono
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFKiswahili #JFLugha
❤1
DAR ES SALAAM: Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Habari na Hoja Mchanganyiko ametoa wito kwa Mamlaka ya Jiji kutafuta suluhisho la Maegesho maeneo ya Ferry ili kuondoa usumbufu kwa madereva wa Taksi Mtandao kukamatwa na kutozwa faini wanaposhusha au kubeba Abiria.
Soma zaidi https://jamii.app/MaegeshoDar
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMdau2025 #ServiceDelivery
Soma zaidi https://jamii.app/MaegeshoDar
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMdau2025 #ServiceDelivery
MWANZA: Mwanachama wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Fichua Uovu ametoa wito kwa mamlaka husika kufuatilia changamoto ya muda mrefu ya Walimu ambao ni Ajira Mpya kutopata malipo ya Fedha ya Kujikimu Wilayani Sengerema licha ya kufuatilia kwa takribani miezi sita.
Mdau anaandika "Majibu ya Afisa Elimu tukiulizia tunaambiwa Mwezi Julai (2025) huwa Mifumo ya Fedha haijakaa sawa, kwa hiyo endeleeni kusubiri”.
Soma zaidi https://jamii.app/MdauSengerema
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #Uwajibikaji #JFMdau2025 #ServiceDelivery
Mdau anaandika "Majibu ya Afisa Elimu tukiulizia tunaambiwa Mwezi Julai (2025) huwa Mifumo ya Fedha haijakaa sawa, kwa hiyo endeleeni kusubiri”.
Soma zaidi https://jamii.app/MdauSengerema
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #Uwajibikaji #JFMdau2025 #ServiceDelivery
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Akizungumza leo Agosti 20, 2025 kwa njia ya Mtandao, Mwenyekiti wa #CHADEMA Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi (Sugu) amesema miongoni mwa mabadiliko yanayohitajika ni kuwepo na utaratibu wa kupinga matokeo ya Urais Mahakamani iwapo kutatokea mashaka kwenye ushindi huo.
Zaidi soma https://jamii.app/SuguMatokeoUrais
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Governance
Zaidi soma https://jamii.app/SuguMatokeoUrais
#JamiiForums #JamiiAfrica #Demokrasia #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR ES SALAAM: Akizungumza katika mdahalo kuhusu amani na #demokrasia uliofanyika kwenye Ukumbi wa JNICC, Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar, Jumanne Muliro amesisitiza kuwa Jeshi la Polisi litaendelea kuimarisha ulinzi, amani na utulivu wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2025.
Pia, ametoa onyo kuwa masanduku na vifaa vya uchaguzi vitalindwa, hivyo wanaotarajia kufanya vitendo vyovyote vya uhalifu watawashughulikia Kisheria.
Soma zaidi https://jamii.app/MuliroUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025
Pia, ametoa onyo kuwa masanduku na vifaa vya uchaguzi vitalindwa, hivyo wanaotarajia kufanya vitendo vyovyote vya uhalifu watawashughulikia Kisheria.
Soma zaidi https://jamii.app/MuliroUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UchaguziMkuu2025
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro akizungumza leo Agosti 20, 2025 katika Mdahalo wa Wadau wa Amani kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 29, 2025 amesema "Nina hakika, kwa Jeshi hili sidhani kama yupo anayependa kufa hata kama upo chama gani, wote kwa kushirikiana Tanzania itakuwa salama."
Mjadala zaidi soma https://jamii.app/MuliroJeshiKufa
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Governance #UtawalaBora
Mjadala zaidi soma https://jamii.app/MuliroJeshiKufa
#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #UchaguziMkuu2025 #Governance #UtawalaBora
Mtengenezaji maudhui Mtandaoni, Ritha Johansen amesema ni vizuri Watumiaji wa Mitandao kutumia lugha zenye heshima pamoja na kuthibitisha vyanzo sahihi vya habari kabla ya kuanzisha mijadala Mitandaoni ili kuepusha athari za kauli za chuki.
Kufuatilia mijadala mingine tembelea JamiiForums.com
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
Kufuatilia mijadala mingine tembelea JamiiForums.com
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akizungumza katika mdahalo kuhusu amani na #Demokrasia uliofanyika katika Ukumbi wa JNICC, Waziri Ofisi ya Makamu wa Pili Rais Zanzibar, Hamza Hassan Juma amesema "Kama kuna mtu alisema atakinukisha naona kama sasa hivi ananuka yeye".
Soma zaidi https://jamii.app/Watakaokinukisha
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #UchaguziMkuu2025
Soma zaidi https://jamii.app/Watakaokinukisha
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #UchaguziMkuu2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akizungumza na East Afrika Redio, leo Agosti 20, 2025, Katibu wa Itikadi na Uenezi wa ACT Wazalendo, Monalisa Ndala amesema hakubaliani na utaratibu wa chama chake kuchukua wagombea kutoka Chama Cha Mapinduzi (#CCM), akidai wengi wao wanaenda Upinzani kutafuta jukwaa la kutoa nyongo na kujibizana kisha baada ya Uchaguzi hurudi CCM.
Baadhi ya Wanasiasa wakubwa kutoka CCM waliowahi kuhamia vyama vya upinzani wakati wa Uchaguzi na kisha kurejea ni marehemu Bernard Membe (ACT), Edward Lowassa (#CHADEMA) na Frederick Sumaye (CHADEMA)
Soma https://jamii.app/MpinaNdala
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
Baadhi ya Wanasiasa wakubwa kutoka CCM waliowahi kuhamia vyama vya upinzani wakati wa Uchaguzi na kisha kurejea ni marehemu Bernard Membe (ACT), Edward Lowassa (#CHADEMA) na Frederick Sumaye (CHADEMA)
Soma https://jamii.app/MpinaNdala
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Siasa ameibua hoja kuhusu wimbi la baadhi ya Watu maarufu na Wanasiasa kujipendekeza kwa Watawala maarufu kama ‘uchawa’ hali ambayo imeonekana kuzidi kushamiri kadri joto la Uchaguzi linavyopanda.
Amedai kuwa tabia hiyo haimfurahishi kwani inaleta madhara kwa Taifa, ikiwemo kupotosha Wapiga Kura na kuharibu mwelekeo wa Demokrasia.
Je, Wanasiasa wanaojipendekeza wanatafuta nafasi za Uongozi kwa maslahi ya Taifa na Wananchi, au ni kwa ajili ya maslahi yao binafsi?
Zaidi Soma https://jamii.app/KujipendekezaWagombea
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025
Amedai kuwa tabia hiyo haimfurahishi kwani inaleta madhara kwa Taifa, ikiwemo kupotosha Wapiga Kura na kuharibu mwelekeo wa Demokrasia.
Je, Wanasiasa wanaojipendekeza wanatafuta nafasi za Uongozi kwa maslahi ya Taifa na Wananchi, au ni kwa ajili ya maslahi yao binafsi?
Zaidi Soma https://jamii.app/KujipendekezaWagombea
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025
❤1👍1
Salum Mwalimu alianza safari yake ya #Siasa kikamilifu Mwaka 2014 ambapo aliteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa #CHADEMA upande wa Zanzibar, alishika nafasi mbalimbali katika chama hicho na sasa amechaguliwa kugombea nafasi ya Urais kupitia Chama cha #CHAUMMA.
Uamuzi wa kuhamia CHAUMMA alitangaza rasmi Mei 19, 2025 baada ya maamuzi ya Salum na Wanachama wengine wa CHADEMA kujitoa katika chama hicho kutokana na kutoridhishwa na maamuzi ya Uongozi mpya ikiwemo kutoshiriki Uchaguzi Mkuu 2025 pamoja na madai ya chama kupoteza dira.
Zaidi https://jamii.app/SalumMwalimuWasifu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Transparency #UchaguziMkuu2025 #PresidentialCandidates #Siasa
Uamuzi wa kuhamia CHAUMMA alitangaza rasmi Mei 19, 2025 baada ya maamuzi ya Salum na Wanachama wengine wa CHADEMA kujitoa katika chama hicho kutokana na kutoridhishwa na maamuzi ya Uongozi mpya ikiwemo kutoshiriki Uchaguzi Mkuu 2025 pamoja na madai ya chama kupoteza dira.
Zaidi https://jamii.app/SalumMwalimuWasifu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Transparency #UchaguziMkuu2025 #PresidentialCandidates #Siasa
Mdau wa JamiiForums.com kutoka Jukwaa la Mahusiano ameeleza changamoto anayopitia katika ndoa yake ya Miaka mitatu, akiwa na mke na Mtoto mmoja wa Kike.
Anasema ana tabia ya kuacha pesa kwenye 'wallet' na alianza kuhisi kama hela zinapungua lakini hakuwa na uhakika hivyo akaamua kuwa makini ili ajue kama kweli pesa yake inatolewa.
Amesema siku moja aliweka Tsh. 70,000 kwenye wallet lakini baada ya siku kadhaa alipokagua alikuta kuna Tsh. 55,000 alimuuliza mke wake kuhusu hela hiyo mwanzo alikataa lakini baadaye akakubali baada ya kumbana na akairudisha, pia alikiri alishawahi kuchukua pesa nyingine bila ruhusa.
Unamshauri nini Mdau kuepuka changamoto hiyo?
Mjadala zaidi soma https://jamii.app/MkeMdokozi
#JamiiForums #Maisha #JFStories #Mikasa #JFLifestyle
Anasema ana tabia ya kuacha pesa kwenye 'wallet' na alianza kuhisi kama hela zinapungua lakini hakuwa na uhakika hivyo akaamua kuwa makini ili ajue kama kweli pesa yake inatolewa.
Amesema siku moja aliweka Tsh. 70,000 kwenye wallet lakini baada ya siku kadhaa alipokagua alikuta kuna Tsh. 55,000 alimuuliza mke wake kuhusu hela hiyo mwanzo alikataa lakini baadaye akakubali baada ya kumbana na akairudisha, pia alikiri alishawahi kuchukua pesa nyingine bila ruhusa.
Unamshauri nini Mdau kuepuka changamoto hiyo?
Mjadala zaidi soma https://jamii.app/MkeMdokozi
#JamiiForums #Maisha #JFStories #Mikasa #JFLifestyle
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA) Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi (#Sugu) akizungumza leo Agosti 20, 2025 amesema “Ifike mahali tukae kama Taifa tuzungumze ili kusaidia nchi yetu, kusaidia isiingie kwenye machafuko ni uzalendo wa kweli kwa Taifa, sio mpaka tuumizane, tuuane wenyewe kwa wenyewe kama ilivyotokea Kenya Mwaka 2007 ndio tukae mezani, haifai.”
Zaidi soma https://jamii.app/SuguMachafuko
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
Zaidi soma https://jamii.app/SuguMachafuko
#JamiiAfrica #JamiiForums #Siasa #Demokrasia #UchaguziMkuu2025 #Governance
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Askofu Gervas Nyaisonga amewaasa vijana kutojishughulisha na dhambi ya mauaji pamoja na matukio ya utekaji akisisitiza kuwa hakuna mtu mwenye haki juu ya uhai wa mtu mwingine.
Ameyasema hayo leo Agosti 20 wakati wa mahubiri kwenye Misa Takatifu ya Ufunguzi wa Kongamano la 6 la Viwawa Taifa ambalo linafanyika Jimbo kuu la Mbeya katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mbeya.
Zaidi soma https://jamii.app/MshirikiDhambiMauaji
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji
Ameyasema hayo leo Agosti 20 wakati wa mahubiri kwenye Misa Takatifu ya Ufunguzi wa Kongamano la 6 la Viwawa Taifa ambalo linafanyika Jimbo kuu la Mbeya katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mbeya.
Zaidi soma https://jamii.app/MshirikiDhambiMauaji
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
JFKUMBUKIZI: Rais Mstaafu Jakaya Kikwete akihojiwa Julai 23, 2023 katika kipindi cha Power Breakfast cha #CloudsTV, alieleza kuwa hakuna kitu kinachoitwa Udikteta nusu. Alifafanua kuwa Udikteta ni kuwanyima Watu fursa ya kutoa maoni.
Zaidi soma https://jamii.app/KikweteUdikteta
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Governance #JFKumbukizi
Zaidi soma https://jamii.app/KikweteUdikteta
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Governance #JFKumbukizi