ISRAEL: Waziri wa Fedha, Bezalel Smotrich na Waziri wa Usalama wa Taifa, Itamar Ben-Gvir, wametishia kujiuzulu na kuvunja Muungano wa Serikali iwapo Waziri Mkuu, #BenjaminNetanyahu atakubali pendekezo la kusitisha mapigano Gaza lililotolewa na Rais #JoeBiden, wakisema wanapinga makubaliano yoyote kabla ya #Hamas kuharibiwa kabisa
Pendekezo la Biden lingeanza na kusitisha mapigano kwa Wiki 6 ambapo Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) lingeondoka maeneo yenye Watu wengi Gaza, Makubaliano ambayo yangesababisha kuachiliwa kwa mateka wote, kusitisha mapigano kwa kudumu na mpango mkubwa wa ujenzi upya wa Gaza
#Netanyahu amesisitiza hakutakuwa na usitishaji wa kudumu wa mapigano hadi uwezo wa kijeshi na wa kiutawala wa Hamas utakapoharibiwa na mateka wote kuachiliwa, huku Kiongozi wa upinzani, Yair Lapid akiahidi kuunga mkono Serikali ikiwa itakubali kusitisha Mapigano
Tangu kuanza kwa Mapigano Oktoba 7, 2023 Zaidi ya Watu 36,000 wameuawa Gaza
Soma https://jamii.app/GazaCeasefire
#JamiiForums #IsraelVsHamas
Pendekezo la Biden lingeanza na kusitisha mapigano kwa Wiki 6 ambapo Jeshi la Ulinzi la Israel (IDF) lingeondoka maeneo yenye Watu wengi Gaza, Makubaliano ambayo yangesababisha kuachiliwa kwa mateka wote, kusitisha mapigano kwa kudumu na mpango mkubwa wa ujenzi upya wa Gaza
#Netanyahu amesisitiza hakutakuwa na usitishaji wa kudumu wa mapigano hadi uwezo wa kijeshi na wa kiutawala wa Hamas utakapoharibiwa na mateka wote kuachiliwa, huku Kiongozi wa upinzani, Yair Lapid akiahidi kuunga mkono Serikali ikiwa itakubali kusitisha Mapigano
Tangu kuanza kwa Mapigano Oktoba 7, 2023 Zaidi ya Watu 36,000 wameuawa Gaza
Soma https://jamii.app/GazaCeasefire
#JamiiForums #IsraelVsHamas
👍4