JamiiForums
52.5K subscribers
34.4K photos
2.47K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
HAKI INAYOCHELEWESHWA NI HAKI INAYOZUILIWA

Ucheleweshwaji wa taratibu za Kisheria unaweza kusababisha upotevu wa Imani ya Wananchi katika Mifumo ya Haki na kuhatarisha upatikanaji wa Haki na Usawa kwa Jamii

Aidha, katika Mazingira mengine huweza kuongezeka Uhamasishaji wa Kujichukulia Sheria Mkononi

Soma https://jamii.app/DelayLegalProcedings

#JamiiForums #JusticeSystem #HumanRights #Democracy #Accountability
👍31
Uahirishaji wa mara kwa mara wa Kesi unachangia kucheleweshwa kwa Haki Nchini na kusababisha msongamano wa kesi

Pia, husababisha ongezeko la gharama za kisheria kwasababu Wahusika hulazimika kuendelea kuajiri Mawakili na kuwekeza muda

Aidha, Mashahidi huweza kusahau ukweli na walalamikaji kupoteza Imani na Mfumo wa Haki kutokana na kucheleweshwa kwa kesi zao

Soma https://jamii.app/UahirishajiKesi

#HumanRights #CivilRights #JusticeSystem #SocialJustice #Accountability #JamiiForums
👍6
Siku chache baada ya Rais #SamiaSuluhuHassan kusaini Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi na Sheria ya Masuala ya Vyama vya Siasa na Gharama za Uchaguzi zote za Mwaka 2024, maoni yametolewa kuwa Sheria hizo hazijazingatia baadhi ya mambo muhimu kama ilivyoshauriwa na Wadau kwenye mchakato wa kutoa maoni

Mkurugenzi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (#LHRC), Anna Henga, amesema “Wadau tulipendekeza maamuzi ya Tume ya Uchaguzi kuhojiwa Mahakamani kwa njia za mapitio au mashauri ya Kikatiba hata hivyo bado maamuzi ya Tume yatakuwa ya mwisho na hayatahojiwa Mahakamani.”

Amesema “Vifungu vya 36(6), 53(6), na 65(7) vya Sheria kuhusu maamuzi ya Tume juu ya mgombea wa Urais, Ubunge na Udiwani kutohojiwa vinakiuka Ibara ya 13(6)(a) ya #Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977.”

Soma https://jamii.app/MaoniYaSheria

#JusticeSystem #JFDemokrasia #Democracy #Governance #JamiiForums
👍6
Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimesema Sheria ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani, Sheria ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, na Sheria ya Masuala ya Vyama vya Siasa na Gharama za Uchaguzi zilizosainiwa hivi karibuni hazijazingatia maoni muhimu ya Wadau

LHRC imesema ilipendekezwa Vyombo vya Habari vinavyokiuka taratibu wakati wa Kampeni na kumpendelea Mgombea mmoja kuwajibishwa

Pia, ilipendekezwa mabadiliko ya upatikanaji wa Wabunge na Madiwani Wanawake wa Viti Maalumu uipe fursa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuweka utaratibu lakini Vyama vya Siasa vimebaki kuwa na Mamlaka hayo

Soma https://jamii.app/MaoniYaSheria

#JusticeSystem #Demokrasia #Democracy #Governance #JamiiForums
👍2