JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Usaili wa kazi ni hatua muhimu katika mchakato wa kuajiriwa. Ni fursa ya kuonesha jinsi unavyoweza kuleta mchango mzuri kwa Kampuni.

#JamiiForums #InterviewTips #FanyaUsailiNaJF #InterviewQuestions #JobInterviewTips
👍1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Jinsi Mwonekano wako unaweza kuwa na athari chanya au hasi wakati wa Usaili wa kazi.

#JamiiForums #InterviewTips #FanyaUsailinaJF #InterviewQuestions #JobInterviewTips
👍31
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Kumbuka Mwonekano wako unaweza kuwa na athari chanya au hasi wakati wa Usaili wa kazi, hivyo hakikisha unaenda katika Usaili husika ukiwa nadhifu

Aidha, ni muhimu kufanya utafiti kidogo kuhusu Kampuni, Taasisi na Nafasi uliyoitiwa ili kupanga mavazi yanayoendana na nafasi hiyo

Soma https://jamii.app/MavaziYaInterview

#JamiiForums #InterviewTips #FanyaUsailinaJF #InterviewQuestions #JobInterviewTips
1🔥1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Kuitwa kwenye Usaili wa kazi ni hatua muhimu katika mchakato wa kuajiriwa, pia ni fursa ya kuonesha jinsi unavyoweza kuongeza thamani kwa kampuni au taasisi husika

Ni muhimu kujiridhisha kwa kufuatilia taarifa muhimu zinazoihusu Kampuni au Taasisi husika kabla ya usaili ili kujiandaa kikamilifu na kujiongezea nafasi ya kufanikiwa katika usaili wako, kwasababu utaepuka kufanya vitu visivyoendana na sera za Kampuni

Pia, Waajiri wengi hupenda kuona umechukua muda kujifunza kuhusu kampuni au Taasisi yao. Hii itaonesha kuwa unajali na una nia ya kweli ya kujiunga nao

Soma https://jamii.app/JobInterviewABCs

#JamiiForums #InterviewTips #FanyaUsailiNaJF #InterviewQuestions #JobInterviewTips
👍3
Swali la 'Tell us about yourself' (tuambie kuhusu wewe) kwenye usaili, huwa linaogopeka sana lakini ni swali muhimu ambalo ukishindwa kujibu vizuri linaweza kukupunguzia nafasi ya kupata fursa au ajira uliyoitiwa

Lengo la Swali hili ni kujenga picha kamili na thabiti ya jinsi ulivyo na jinsi unavyoweza kuleta thamani katika nafasi unayoiomba, hivyo jibu kwa ufupi kuhusu elimu yako, uzoefu wako wa kazi, majukumu uliyokuwa nayo, na jinsi yanavyohusiana na nafasi unayoomba

Vile vile, kwa ufupi elezea ujuzi maalum na stadi ulizonazo zitavyosaidia katika kazi unayoiomba. Pia, eleza jinsi nafasi unayoomba inavyoendana na malengo yako ya muda mrefu kulingana na taaluma yako.

Zaidi https://jamii.app/InterviewTips

#JamiiForums #Fursa #Ajira #InterviewTips
👍32