Akizungumza katika mjadala wa "Kuelekea Uchaguzi, Tunatofautishaje Zawadi na Rushwa?", Mwanasiasa (ACT Wazalendo), Zitto Kabwe amesema “Hakuna anayeweza kubisha kuwa kuna matumizi makubwa ya Fedha katika Chaguzi zetu kiasi kwamba ni jambo gumu kutofautisha Rushwa na Zawadi nyakati za Uchaguzi na hasa katika Mwaka wa Uchaguzi”
Ameongeza kuwa “Hali ya Rushwa sio tu kwa Wanasiasa bali pia hata kwa Dola, ndio maana nyakati za Uchaguzi unaweza kukuta Viongozi wakubwa wakitoa ahadi ambazo zinaweza kutafsiriwa au kutumika kama sehemu ya ushawishi wa nguvu zao kuelekea kwa Dola”
Amesema unaweza kukuta Mgombea ni Rais au Waziri anaweza kutumia nafasi yake wakati wa Kampeni za Uchaguzi kutoa maelekezo ya kimamlaka na hivyo kutumika kama sehemu ya ushawishi wakati ni jambo ambalo halitakiwi kufanyika hivyo
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Ameongeza kuwa “Hali ya Rushwa sio tu kwa Wanasiasa bali pia hata kwa Dola, ndio maana nyakati za Uchaguzi unaweza kukuta Viongozi wakubwa wakitoa ahadi ambazo zinaweza kutafsiriwa au kutumika kama sehemu ya ushawishi wa nguvu zao kuelekea kwa Dola”
Amesema unaweza kukuta Mgombea ni Rais au Waziri anaweza kutumia nafasi yake wakati wa Kampeni za Uchaguzi kutoa maelekezo ya kimamlaka na hivyo kutumika kama sehemu ya ushawishi wakati ni jambo ambalo halitakiwi kufanyika hivyo
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Akichangia katika mjadala wa "Kuelekea Uchaguzi, Tunatofautishaje Zawadi na Rushwa?", Assenga Kimaro (Mdau) amesema “Suala sio zawadi, bali kitu kinachotolewa kwa Wananchi wakati au kuelekea katika Uchaguzi kwa asilimia zote hiyo ni Rushwa, sababu Wananchi wao hawatoi ila wanapokea kutoka kwa Wagombea au Watiania”
Amesisitiza “Tunasema ni zawadi kwa Wananchi, Mgombea anawapongeza nini Wananchi? Hiyo ni Rushwa ila tu inatumika katika jina tofauti”
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Amesisitiza “Tunasema ni zawadi kwa Wananchi, Mgombea anawapongeza nini Wananchi? Hiyo ni Rushwa ila tu inatumika katika jina tofauti”
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Wakili William Maduhu (LHRC) amesema “Kuna wakati Viongozi wanatumia Madaraka yao kutoa ahadi na kutoa vitisho kwa Wananchi kuwa hawatakiwi kuwachagua wapinzani wakati wa Uchaguzi lakini huwezi kuwasikia TAKUKURU wakiingilia kati hapo”
Amesisitiza kwa kutolea mfano Wabunge wa sasa waliopo Madarakani wanaenda kwenye Majimbo kutoa vitu mbalimbali ikiwemo Pikipiki, Baiskeli n.k. lakini watia nia wengine wakienda kufanya hivyo TAKUKURU wanawakamata
Ameongeza kuwa “Inavyofanyika ni kuwa Mbunge ambaye ana nia ya kugombea tena akifanya hivyo ni sawa lakini yule mwenye nia ya kugombea yeye akifanya hivyo anaambiwa anatoa Rushwa
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Amesisitiza kwa kutolea mfano Wabunge wa sasa waliopo Madarakani wanaenda kwenye Majimbo kutoa vitu mbalimbali ikiwemo Pikipiki, Baiskeli n.k. lakini watia nia wengine wakienda kufanya hivyo TAKUKURU wanawakamata
Ameongeza kuwa “Inavyofanyika ni kuwa Mbunge ambaye ana nia ya kugombea tena akifanya hivyo ni sawa lakini yule mwenye nia ya kugombea yeye akifanya hivyo anaambiwa anatoa Rushwa
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Wakili (LHRC) William Maduhu amesema “Pamoja na yote kuna kawaida ambayo inachangia Rushwa, Wananchi tumewageuza Wabunge kuwa ATM”
Amechangia mjadala huu kwa kusema kuwa Mtu akiwa na shida anamfuata Mbunge kumuomba msaada, hivyo Mwananchi wa aina hiyo akipewa zawadi baadaye lazima ashawishike
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Amechangia mjadala huu kwa kusema kuwa Mtu akiwa na shida anamfuata Mbunge kumuomba msaada, hivyo Mwananchi wa aina hiyo akipewa zawadi baadaye lazima ashawishike
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Mwanasiasa (ACT Wazalendo), Zitto Kabwe amesema “Wakati wa Kura za maoni za CCM huwa ni kawaida kuwasikia sana TAKUKURU lakini baada ya hapo huwezi kuwasikia tena”
Ameongeza kwa kusema “TAKUKURU ni kama wanakuwa na jukumu la kudhibiti Rushwa ndani ya CCM lakini huwaoni wakati wa Uchaguzi Mkuu, hata unapotoa taarifa kwa Mamlaka nyingine za Usalama, inachukuliwa kawaida kwa maana hakuna anayechukua hatua”
Amesema kuwa kwa sasa sio mjadala tena kuwa kuna Rushwa au hakuna wakati wa Uchaguzi, inajulikana kinachoendelea
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Ameongeza kwa kusema “TAKUKURU ni kama wanakuwa na jukumu la kudhibiti Rushwa ndani ya CCM lakini huwaoni wakati wa Uchaguzi Mkuu, hata unapotoa taarifa kwa Mamlaka nyingine za Usalama, inachukuliwa kawaida kwa maana hakuna anayechukua hatua”
Amesema kuwa kwa sasa sio mjadala tena kuwa kuna Rushwa au hakuna wakati wa Uchaguzi, inajulikana kinachoendelea
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Mwenyekiti wa Bodi (JUKATA), Dkt Ananilea Nkya amesema “Rushwa imetokana na Wananchi kutoamini mifumo ya Uchaguzi, wanaona bora wachukue hela kwa kuwa wanaowachagua wakifika kwenye Uongozi wanaenda kuchukua hela nyingi, hivyo nao wanachukua chao mapema”
Ameongeza kuwa “Kupunguza Rushwa katika Uchaguzi tunatakiwa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi, hapo namaanisha ni Tume ambayo haichaguliwi na Rais aliyepo Madarakani, inatakiwa iwe inajitegemea na hata upatikanaji wa wafanyakazi uwe wa tofauti na ulivyo sasa”
Amesema kuwa “Sasa hivi Mgombea anaweza kuwa hata na Tsh. Milioni 500 katika Uchaguzi na akakwama kushinda. Sasa hivi wale waliopo Madarakani na wana nia ya kugombea ndio wanakuwa na hela nyingi na nguvu pia”
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Ameongeza kuwa “Kupunguza Rushwa katika Uchaguzi tunatakiwa kuwa na Tume Huru ya Uchaguzi, hapo namaanisha ni Tume ambayo haichaguliwi na Rais aliyepo Madarakani, inatakiwa iwe inajitegemea na hata upatikanaji wa wafanyakazi uwe wa tofauti na ulivyo sasa”
Amesema kuwa “Sasa hivi Mgombea anaweza kuwa hata na Tsh. Milioni 500 katika Uchaguzi na akakwama kushinda. Sasa hivi wale waliopo Madarakani na wana nia ya kugombea ndio wanakuwa na hela nyingi na nguvu pia”
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Akichangia mjadala Mwenyekiti wa Bodi (JUKATA), Dkt Ananilea Nkya amesema “Tuliona katika Uchaguzi uliopita kuna Kiongozi aliyekuwa Madarakani yeye ndio alikuwa anaamua nani ashinde”
Amesema Wagombea wanapitishwa na wenye Mamlaka kwa kuangalia “Huyu yupo karibu na mimi”, Huyu atanihoji maswali mengi” n.k. Yote hayo yanatokana na kuwepo kwa Mifumo mibovu ya kuchagua Watu
Amesema kuwa “Tukiendelea hivi tutakuja kujutia kwa kuwa kunaweza kuwa na hatari kubwa zaidi, ninakubaliana na wale wanaosema 'No reform No election'”
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Amesema Wagombea wanapitishwa na wenye Mamlaka kwa kuangalia “Huyu yupo karibu na mimi”, Huyu atanihoji maswali mengi” n.k. Yote hayo yanatokana na kuwepo kwa Mifumo mibovu ya kuchagua Watu
Amesema kuwa “Tukiendelea hivi tutakuja kujutia kwa kuwa kunaweza kuwa na hatari kubwa zaidi, ninakubaliana na wale wanaosema 'No reform No election'”
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Mwanasiasa (ACT Wazalendo), Zitto Kabwe amesema jamii ikiamua kudhibiti Rushwa inawezekana, wakati wa Uchaguzi wa Chama kimoja Rushwa ilidhibitiwa sana, baadaye uchaguzi wa Vyama vingi matumizi ya Fedha hayakuwa makubwa lakini kadiri Miaka inavyoenda matumizi ya Fedha yanazidi kuongezeka
Ameongeza kwa kusema “Ni lazima tuwe na Katiba imara ambayo inaweza kukataa mifumo na njia za Rushwa. Tunapokuwa na Chaguzi ambazo mtu mmoja anakuwa na nguvu ya kumpitisha Mgombea fulani kutokana na nafasi yake itakuwa ngumu kudhibiti Rushwa”
Amesema kuwa #Rushwa ya Uchaguzi ndio inazaa Rushwa nyingine na kukosekana kwa Uwajibikaji, kwani Kiongozi akishafanya hivyo akashinda lazima atatafuta namna ya kurejesha Fedha alizozipoteza awali
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Ameongeza kwa kusema “Ni lazima tuwe na Katiba imara ambayo inaweza kukataa mifumo na njia za Rushwa. Tunapokuwa na Chaguzi ambazo mtu mmoja anakuwa na nguvu ya kumpitisha Mgombea fulani kutokana na nafasi yake itakuwa ngumu kudhibiti Rushwa”
Amesema kuwa #Rushwa ya Uchaguzi ndio inazaa Rushwa nyingine na kukosekana kwa Uwajibikaji, kwani Kiongozi akishafanya hivyo akashinda lazima atatafuta namna ya kurejesha Fedha alizozipoteza awali
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Mkurugenzi wa Elimu kwa Umma (TAKUKURU), Joseph Kasongwa amesema kuwa #Rushwa ni tabia, kwenye Uchaguzi Rushwa inapotolewa pande zote zinakuwa na furaha, hiyo imechangia kuwa changamoto kumpata Mtuhumiwa
Ameongeza kwa kusema “ Imefika hatua hatuoni kama Rushwa ni adui, hiyo inachangia ugumu wa kupambana nayo, mfano wakati Tanzania ikipambana na Idd Amini, Watanzania wote tulikuwa kitu kimoja, lakini kama wote tukiwa hatuna mtazamo sawa ni vigumu kuizuia Rushwa”
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Ameongeza kwa kusema “ Imefika hatua hatuoni kama Rushwa ni adui, hiyo inachangia ugumu wa kupambana nayo, mfano wakati Tanzania ikipambana na Idd Amini, Watanzania wote tulikuwa kitu kimoja, lakini kama wote tukiwa hatuna mtazamo sawa ni vigumu kuizuia Rushwa”
#ChaguaKiongoziSioPesa #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Rushwa ya uchaguzi inawafanya viongozi waliochaguliwa kwa njia isiyo halali kutowajibika kwa Wananchi, kupuuza mahitaji ya msingi kama elimu, afya, miundombinu na ajira na badala yake kujikita katika kulinda maslahi yao binafsi
Matokeo yake ni ufisadi, ukosefu wa maendeleo na maisha magumu kwa Wananchi wa kawaida. Kataa kununuliwa. Chagua kiongozi kwa misingi ya uwezo, maadili na dhamira ya kweli ya kuleta maendeleo kwa wote.
#ChaguaKiongoziSioPesa #KemeaRushwa25 #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Matokeo yake ni ufisadi, ukosefu wa maendeleo na maisha magumu kwa Wananchi wa kawaida. Kataa kununuliwa. Chagua kiongozi kwa misingi ya uwezo, maadili na dhamira ya kweli ya kuleta maendeleo kwa wote.
#ChaguaKiongoziSioPesa #KemeaRushwa25 #Accountability #Demokrasia #ServiceDelivery #Uwajibikaji
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mkuu wa Mkoa, Albert Chalamila amethibitisha kuwa miili mitatu imetolewa chini ya Lori lililoanguka katika eneo la Kimara Stop Over mpaka kufikia majira ya saa 9 Usiku wa kuamkia leo (Februari 14, 2025)
Pia, Bodaboda sita zimetolewa chini ya Lori hilo ambalo liliacha njia na kuparamia Abiria na Madereva wa Bodaboda waliokuwa pembezoni mwa Barabara
Chalamila amesema walifanikiwa kulinyanyua Lori kwa zaidi ya asilimia 95% na taarifa zaidi za Ajali hiyo zitaendelea kutolewa na Jeshi la Polisi
Soma https://jamii.app/AjaliLoriStopOver
Video Credits: Clouds TV
#JamiiForums #JFMatukio
Pia, Bodaboda sita zimetolewa chini ya Lori hilo ambalo liliacha njia na kuparamia Abiria na Madereva wa Bodaboda waliokuwa pembezoni mwa Barabara
Chalamila amesema walifanikiwa kulinyanyua Lori kwa zaidi ya asilimia 95% na taarifa zaidi za Ajali hiyo zitaendelea kutolewa na Jeshi la Polisi
Soma https://jamii.app/AjaliLoriStopOver
Video Credits: Clouds TV
#JamiiForums #JFMatukio
MBEYA: Siku chache baada ya Mwanachama wa JamiiForums.com kueleza kukerwa na vifusi vilivyomwagwa na TARURA tangu mwaka 2024 katika Barabara ya Sangu kwenda Benki Kuu, vifusi hivyo vimeanza kusambazwa Februari 12, 2025
Mdau alidai vifusi hivyo vimesababisha changamoto ya usafiri kwa kufanya barabara hiyo kuwa nyembamba na kusababisha usumbufu kwa wanaopita na magari
Soma https://jamii.app/VifusiKusambazwaMbeya
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #HudumaZaKijamii #JFMdau2025
Mdau alidai vifusi hivyo vimesababisha changamoto ya usafiri kwa kufanya barabara hiyo kuwa nyembamba na kusababisha usumbufu kwa wanaopita na magari
Soma https://jamii.app/VifusiKusambazwaMbeya
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #HudumaZaKijamii #JFMdau2025
KILIMANJARO: Mdau wa JamiiForums.com kutokea Kitefure Longuo A, Moshi Vijijini anasema eneo hilo lina changamoto ya kutokuwa na Huduma ya Maji hali ambayo inaathiri Watu wengi huku ikiwa imedumu kwa muda mrefu sasa
Ameomba Mamlaka husika kushughulikia changamoto hiyo kwasababu kuna wakati Maji yanapatikana mara moja kwa Wiki au baada ya Siku 9 - 10
Soma https://jamii.app/KitefureMajiHakuna
#JamiiForums #HudumaZaKijamii #ServiceDelivery
Ameomba Mamlaka husika kushughulikia changamoto hiyo kwasababu kuna wakati Maji yanapatikana mara moja kwa Wiki au baada ya Siku 9 - 10
Soma https://jamii.app/KitefureMajiHakuna
#JamiiForums #HudumaZaKijamii #ServiceDelivery
Kabla Mshukiwa hajakamatwa na Polisi ana Haki ya kuelezwa kwanini anakamatwa. Aidha, Polisi mkamataji ni lazima ajitambulishe na kueleza kituo cha Polisi anachotoka
Raia aliyekamatwa ana Haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa Kituo cha Polisi endapo kosa lake linastahili dhamana
Pia, ana Haki ya kufikishwa Mahakamani katika muda usiozidi Saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha Polisi
Soma zaidi https://jamii.app/HakiKukamatwaPolisi
#JamiiForums #HakiZaKiraia #CivilRights #HumanRights #KesiYaHaki #HakiZaBinadamu #UtawalaWaSheria
Raia aliyekamatwa ana Haki ya kuomba na kupewa dhamana wakati akiwa Kituo cha Polisi endapo kosa lake linastahili dhamana
Pia, ana Haki ya kufikishwa Mahakamani katika muda usiozidi Saa 24 tangu alipokamatwa na kufikishwa kituo cha Polisi
Soma zaidi https://jamii.app/HakiKukamatwaPolisi
#JamiiForums #HakiZaKiraia #CivilRights #HumanRights #KesiYaHaki #HakiZaBinadamu #UtawalaWaSheria
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Jana, Februari 13, 2025, Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba aliwasilisha mapendekezo ya nyongeza ya Tsh. bilioni 945.7 kwenye Bajeti Kuu ya Serikali ya 2024/25 kutoka kwenye ile ya awali ya Tsh. Trilioni 49.3 iliyowasilisha Bungeni Juni 13, 2024
Leo Februari 14, 2025 Wabunge watajadili kuhusu Mapendekezo hayo pamoja na Muhtasari wa Tamko la Sera ya Fedha – Mapitio ya Nusu Mwaka 2024/2025.
Soma https://jamii.app/NyongezaBajeti
#JamiiForums #Governance
Leo Februari 14, 2025 Wabunge watajadili kuhusu Mapendekezo hayo pamoja na Muhtasari wa Tamko la Sera ya Fedha – Mapitio ya Nusu Mwaka 2024/2025.
Soma https://jamii.app/NyongezaBajeti
#JamiiForums #Governance
DAR: Mdau wa JamiiForums.com ametoa wito kwa mamlaka kushughulikia ujenzi na uboreshaji wa Barabara ya Kichangani kuanzia Shule, Kisimani hadi Msikiti wa Mzee Nandule zilizopo Kisarawe kwani hazipitiki na kupelekea changamoto ya usafiri kwa wakazi wa eneo hilo
Soma https://jamii.app/BarabaraKisaraweIrekebishe
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #ServiceDelivery
Soma https://jamii.app/BarabaraKisaraweIrekebishe
#JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji #ServiceDelivery
MWANZA: Mwanachama wa JamiiForums.com anasema licha ya uzuri wa Stendi ya Daladala ya Buzuruga ila ukosefu wa Vifaa vya kuwekea uchafu unachafua taswira ya eneo hilo na kuhatarisha #Afya ya Watumiaji
Ameshauri Wasimamizi wa stendi hiyo ambao ni Halmashauri ya Ilemela kuweka vyombo vya kuwekea Uchafu ili kuzuia utupaji holela wa taka na kurundika taka maeneo yasio stahiki.
Soma https://jamii.app/UchafuStendiBuzuruga
#JamiiForums #HudumaZaKijamii #Uwajibikaji #Accountability #JFMdau2025 #ServiceDelivery
Ameshauri Wasimamizi wa stendi hiyo ambao ni Halmashauri ya Ilemela kuweka vyombo vya kuwekea Uchafu ili kuzuia utupaji holela wa taka na kurundika taka maeneo yasio stahiki.
Soma https://jamii.app/UchafuStendiBuzuruga
#JamiiForums #HudumaZaKijamii #Uwajibikaji #Accountability #JFMdau2025 #ServiceDelivery