JamiiForums
βœ”
55.7K subscribers
33.2K photos
1.96K videos
30.2K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MAHAKAMA YA ICC KUCHUNGUZA UHALIFU WA KIVITA UKRAINE

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) imesema ktk uchunguzi wa awali imeridhika kuna sababu za msingi za kuamini madai ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya Binadamu umefanyika Nchini Ukraine

Soma https://jamii.app/ICCUkraine
RAIS BIDEN: PUTIN ALIKATAA DIPLOMASIA, HAJUI KILICHOPO MBELE

Asema Vita dhidi ya #Ukraine ilipangwa bila kuchochewa, na Rais Putin alifikiri Nchi za Magharibi hazitojibu

Marekani itapiga marufuku Ndege za Urusi kwenye Anga lake

Soma - https://jamii.app/BidenPutin

#RussiaUkraine
LEO NI JUMATANO YA MAJIVU. KWARESMA KUANZA

- Siku ya kwanza ya Kwaresma huitwa Jumatano ya Majivu kutokana na tendo la kupakwa Majivu

- Kwaresma ni siku 40 za kufunga, kusali, kutafakari Neno la Mungu na kufanya matendo ya huruma

Kwa Historia, soma - https://jamii.app/Kwaresima
JE, WAJUA?: Chupa moja ya Damu inaweza kuokoa Maisha ya Watu Watatu. Mwanamke anaweza kuchangia Damu kila baada ya Miezi 4 na Mwanaume anaweza kuchangia kila baada ya Miezi Mitatu

Kila unapotoa Damu unafanyiwa uchunguzi mdogo wa #Afya. Damu inayochangiwa huchunguzwa Virusi vya UKIMWI, Kaswende na Homa ya Ini (Hepatitis B&C). Matokeo ya uchunguzi hayatolewi hadharani, bali ni mtoaji tu ndiye atakayepewa.

#JamiiForums #BloodDonation #DidYouKnow
MDAU: UTHUBUTU NI SILAHA YA MAFANIKIO

Anasema woga wa kufanya makosa ni tabia iliyowafungia wengi nje ya fursa nono, ikiwapotezea muda na ujasiri. Hatua mojawapo kutoka kwenye umasikini na unyonge ni kutoogopa gharama za makosa

Soma - https://jamii.app/UthubutuSOC

#StoriesOfChange
Kampuni ya kutengeneza Ndege ya Marekani ya #Boeing (BA.N) imesitisha usambazaji wa Vifaa, matengenezo na usaidizi wa kiufundi kwa Mashirika ya Ndege ya Urusi kama sehemu ya vikwazo vilivyowekwa kutokana na uvamizi wake #Ukraine

Soma - https://jamii.app/BoeingRussia
#RussiaUkraineWar
Kuelekea Siku ya Usikivu Duniani (Machi 03, 2022), Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema zaidi ya Watu Bilioni 1 Duniani wapo katika hatari ya kupoteza uwezo wa kusikia kutokana na mazoea ya kusikiliza muziki kwa sauti kubwa, na kwa muda mrefu

Soma - https://jamii.app/WHD2022
NJOMBE: WANANCHI WALIOIBIWA MASUFURIA YA WALI WAITWA POLISI

Wananchi #Njombe wameitwa kituoni kutambua mali zilizokamatwa wakati wa doria ya Polisi

Baadhi ya mali ni magodoro, pikipiki, sufuria, mitungi ya gesi, jiko, laptop na TV

Soma - https://jamii.app/SufuriaNjombe
#JamiiForums
APPLE YASITISHA KUUZA BIDHAA URUSI

Kampuni hiyo kubwa ya Teknolojia pia imesema huduma nyingine zikiwemo Apple Pay na Apple Maps zitadhibitiwa kufuatia uvamizi uliofanywa na Urusi dhidi ya #Ukraine, na kupekelea maelfu kukimbilia Mataifa jirani

Soma - https://jamii.app/AppleUrusi
TETESI: ABRAMOVICH KUIUZA CHELSEA

Bilionea wa Uswisi, Hansjorg Wyss (86) amedai amepewa nafasi ya kujiunga na Wawekezaji 6 au 7 kuinunua Chelsea

Amedai β€œAbramovich anataka fedha nyingi, anaidai Chelsea Β£2bn na Chelsea haina pesa. Hadi sasa hatujui bei halisi ya kuinunua”

#JFSports
#AFYA: Maziwa Mtindi huwa na Protini nyingi, Calcium, Vitamini, na Bakteria wazuri ambao husaidia kubadilisha Sukari. Mtindi husaidia kutoa ulinzi kwenye Mifupa na Meno na pia kuzuia matatizo ya Usagaji wa Chakula

Aidha, Mtindi umeonesha kuwa na uwezo mkubwa wa kutoa kinga dhidi ya Maradhi ya kuambukiza Ukeni (Vaginal infections)

Soma - https://jamii.app/BenefitsYoghurt
#JamiiForums #HealthCare
UGANDA: MWANDISHI ALIYEKIMBIA NCHI AFUNGUA KESI DHIDI YA SERIKALI

Kakwenza Rukirabashaija amedai aliteswa alipokuwa chini ya ulinzi, akitaka Mahakama ya Haki Afrika Mashariki iseme kukamatwa na kuteswa kwake ni kinyume cha Sheria

Soma - https://jamii.app/UGGovtSued

#JFLeo
SONGWE: Wakazi wa eneo la Old Vwawa wamekutana na kinachodaiwa ni mabaki ya mwili wa binadamu katika shimo ambalo lilichimbwa kwa ajili ya kusimika nguzo ya umeme

> Wakazi hao wamedai kukuta mifupa ya binadamu, cheni, bangili na jino

Soma - https://jamii.app/Songwe

#JamiiForums
Kutokana na utelekezaji wa Sera ya Elimu Msingi bila malipo ya Mwaka 2015/16, kumekuwa na ongezeko la Wanafunzi kila mwaka.

Ongezeko la Wanafunzi lilipaswa kwenda sambamba na uboreshwaji wa Miundombinu ya Shule kama vile Vyumba vya Madarasa, Madawati, Matundu ya Vyoo nk.

#JamiiForums #JFUwajibikaji #WAJIBU #Accountability #JFPartnership
VIONGOZI WA DINI: BUSARA ITUMIKE KUMALIZA KESI YA MBOWE

Wakiwa Ikulu, Dar wameomba Mamlaka husika kutumia busara na kuangalia namna ya kumaliza kesi hiyo

Pia, wamependekeza kuwe na Mjadala kuhusu Mfumo mpya wa Elimu utakaokidhi mahitaji ya sasa

Soma - https://jamii.app/ViongoziDiniIkulu
UKRAINE - UPDATES: Jeshi la Urusi linadaiwa kushambulia Shule 3 Mjini #Kharkiv. Pia inaripotiwa kuwa Majengo kadhaa ya Makazi ya Watu huko #Okhtyrka nayo yameharibiwa kutokana na mashambulizi yanayoendelea

Watu zaidi ya Milioni 1 wamekimbia #Ukraine

Soma https://jamii.app/UkraineUrusi
MSUMBIJI: MAWAZIRI SITA WAONDOLEWA KAZINI

Rais Filipe Nyusi amewatoa kwenye nafasi zao Mawaziri sita wakiwemo Waziri wa Fedha na Waziri wa Madini na Nishati

Ni Mabadiliko makubwa ya pili kufanyika kwenye Baraza la Mawaziri miezi ya hivi karibuni

Soma - https://jamii.app/MinisterSackMoz
URUSI: Waziri wa Ulinzi, Meja Jenerali Igor Konashenkov amesema Wanajeshi wa #Urusi 498 wameuawa na 1,597 wamejeruhiwa ktk mapigano na #Ukraine

> Aidha, Rais wa Ukraine amesema Wanajeshi wa Urusi 7,000 wameuawa ktk mapigano hayo

Soma https://jamii.app/UrusiWapiganaji

#RussiaUkraineConflict
Machi 03, 2022 ni Siku ya Usikivu Duniani ambapo inaelezwa takriban Watu Bilioni 1.5 Duniani kote wanaishi na tatizo la usikivu. Wataalamu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) wanasema idadi hii inaweza kuongezeka hadi Bilioni 2.5 kufikia Mwaka 2030

Kaulimbiu ya Mwaka 2022 inasema, "Ili kusikia maisha yote, sikiliza kwa uangalifu!"

Soma - https://jamii.app/TatizoUsikivu

#WorldHearingDay2022
DAR: Daniel Muga, mkazi wa Bombambili anasakwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua mtoto wake wa miaka mitatu kwa kumpiga na kitu kizito kichwani

> Kamanda wa Polisi Dar, ACP Muliro Jumanne Muliro amesema tukio hilo lilitokea Februari 28, 2022

Soma - https://jamii.app/Mauaji