Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
ARUSHA: Akizungumza na Waandishi wa Habari, Agosti 16, 2025, Katibu wa Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM, Saipulan Ramsey amesema “Chama Cha Mapinduzi hakijatoa kwa Mwanachama yeyote wala Mwananchi yeyote wala kutoa ruksa ya utengenezaji wa Namba za 'SSH 2530'. Ziko mamlaka husika zinazohusika na utoaji wa vibao vya namba za magari.”
Ameongeza “Chama hakina mamlaka ya kutengeneza vibao vya namba za magari, zipo mamlaka husika zinazoshughulika na jukumu hilo. Naomba mamlaka zinazohusika na utoaji wa namba za magari pamoja na usafirishaji zifuatilie yeyote aliyeweka namba hizo awaeleze amezipata wapi.”
Video Credit: Arusha Zone
Soma zaidi https://jamii.app/NambaZaSSH2530
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
Ameongeza “Chama hakina mamlaka ya kutengeneza vibao vya namba za magari, zipo mamlaka husika zinazoshughulika na jukumu hilo. Naomba mamlaka zinazohusika na utoaji wa namba za magari pamoja na usafirishaji zifuatilie yeyote aliyeweka namba hizo awaeleze amezipata wapi.”
Video Credit: Arusha Zone
Soma zaidi https://jamii.app/NambaZaSSH2530
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
❤2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MWANZA: Mkuu wa Mkoa, Said Mtanda, leo Jumatatu Agosti 18, 2025 amefafanua suala la Mtoto Mkazi wa Nyakato, Wilayani Ilemela aliyesemekana kulawitiwa na Steven Ibasa (Baba Claudia), kwa kueleza kuwa suala hilo limefikishwa Mahakamani na kwamba mtuhumiwa amekosa mtu wa kumdhamini, amepelekwa Gerezani Butimba.
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Akiwa ofisini kwake, RC Mtanda amewataka Wananchi kuwa na imani na Muhimili wa Mahakama kwakuwa utatenda haki katika suala hilo.
Ikumbukwe, suala hilo liliibuliwa na Mdau wa JamiiForums.com akidai kuna mazingira ya kumlinda Mtuhumiwa huyo ambaye alishikiliwa katika Kituo cha Polisi Nyakato kisha Kituo cha Polisi Kirumba, hivyo akaomba Mamlaka za Juu kuingilia kati ili Haki ipatikane.
Soma zaidi https://jamii.app/SaidMtandaUpdates
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Akizungumza Agosti 18, 2025, Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, David Misime amesema "Tukiona moshi unafuka hatutasubiri moto uwake, tutachukua hatua. Tukiona matamshi ambayo hayastahili, tunajua huku anakoelekea huyu siyo sahihi, lazima tuzuie kabla ya kutokea madhara."
Soma https://jamii.app/MishimeMoshi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
Soma https://jamii.app/MishimeMoshi
#JamiiAfrica #JamiiForums #UtawalaBora #Uwajibikaji #Accountability #UchaguziMkuu2025
❤1👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MWANZA: Kulwa Steven Ibasa (37) anayetuhumiwa kumlawiti Mtoto wa Kiume (4), amefikishwa Mahakama ya Ilemela, jana Agosti 18, 2025 na baada ya shauri lake kutajwa alikosa Mtu wa kumdhamini akapelekwa Gerezani Butimba.
Hati ya Mashtaka imesomwa na Wakili wa Serikali, Mwanahawa Changali mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Juma Opudo imeeleza Kesi hiyo Namba 20028/2025, Ibasa ameshtakiwa kwa shtaka la kulawiti, kinyume na Kifungu cha 154(1)(a)(2) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16, marejeo ya Mwaka 2023.
Mshtakiwa alikana mashtaka ambapo kesi imepangwa kutajwa tena Septemba 1, 2025 kwa ajili ya kuanza kusikilizwa upande wa mashahidi.
Ikumbukwe, Agosti 15, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alihoji ukimya wa Mamlaka kuhusu tukio hilo, Mkuu wa Mkoa, Saidi Mtanda, akatoa maelekezo suala hilo lifanyiwe kazi ndipo Agosti 18 mtuhumiwa akafikishwa Mahakamani.
Zaidi soma https://jamii.app/NyakatoMatukio
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
Hati ya Mashtaka imesomwa na Wakili wa Serikali, Mwanahawa Changali mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Juma Opudo imeeleza Kesi hiyo Namba 20028/2025, Ibasa ameshtakiwa kwa shtaka la kulawiti, kinyume na Kifungu cha 154(1)(a)(2) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16, marejeo ya Mwaka 2023.
Mshtakiwa alikana mashtaka ambapo kesi imepangwa kutajwa tena Septemba 1, 2025 kwa ajili ya kuanza kusikilizwa upande wa mashahidi.
Ikumbukwe, Agosti 15, 2025, Mdau wa JamiiForums.com alihoji ukimya wa Mamlaka kuhusu tukio hilo, Mkuu wa Mkoa, Saidi Mtanda, akatoa maelekezo suala hilo lifanyiwe kazi ndipo Agosti 18 mtuhumiwa akafikishwa Mahakamani.
Zaidi soma https://jamii.app/NyakatoMatukio
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #ChildRights #Accountability
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akizungumza Agosti 18, 2025 kwenye Baraza la Wafanyakazi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza S. Johari ametoa onyo kwa Watumishi wanaovujisha siri za Serikali, akibainisha kuwa ofisi yake itawafuatilia kwa ukaribu na kuchukua hatua za kinidhamu kwani ni kinyume na miongozo, Kanuni na Sheria za nchi, pia kufanya hivyo ni sawa na kujipiga risasi mwenyewe.
Pia, alieleza kusikitishwa na uwepo wa Mawakili wa Serikali wenye tabia za uongo, akisema jambo hilo linaweza kuipunguzia heshima taaluma ya Sheria na kuichafua taswira ya Serikali mbele ya umma.
Soma zaidi https://jamii.app/MwanasheriaSerikali
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
Pia, alieleza kusikitishwa na uwepo wa Mawakili wa Serikali wenye tabia za uongo, akisema jambo hilo linaweza kuipunguzia heshima taaluma ya Sheria na kuichafua taswira ya Serikali mbele ya umma.
Soma zaidi https://jamii.app/MwanasheriaSerikali
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
ARUSHA: Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Habari na Hoja Mchanganyiko ametoa ushauri kwa Mamlaka za Jiji kuangalia changamoto ya baadhi ya Maafisa wa Usalama katika Barabara kati ya Soko Kuu na Sokoine, akidai hawatendi haki kwa baadhi ya madereva wanaopita njia hiyo kiasi kwamba wengine wanatengeneza mazingira ya usumbufu ili 'wamalizana pembeni'.
Soma zaidi https://jamii.app/FainiArusha
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #JFMdau2025 #Accountability
Soma zaidi https://jamii.app/FainiArusha
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #JFMdau2025 #Accountability
👍1
KATAVI: Mdau wa JamiiForums.com aliyejitambulisha kuwa Mkazi wa Wilaya ya Mpanda anatoa wito kwa Shirika la Umeme Tanzania (#TANESCO) kushughulikia changamoto ya umeme kukatika mara kwa mara, akihoji mbona wanapodai madai yao hutumia magari ya matangazo kuzunguka Mtaani kufikisha ujumbe, lakini suala la kukata umeme hutumia makundi ya WhatsApp ambayo Wananchi wengi hawana au hawatumii?
Zaidi soma https://jamii.app/UmemeMpanda
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
Zaidi soma https://jamii.app/UmemeMpanda
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
ETHIOPIA: Wizara ya Elimu imetoa mwongozo unaopiga marufuku utoaji wa Shahada za Heshima (Honorary Doctorate) kwa Viongozi wa Serikali na Wanasiasa walioko madarakani, agizo hilo limetiwa saini na Waziri wa Elimu, Profesa Berhanu Nega, na limeelekezwa kwa Vyuo Vikuu na taasisi zote za elimu.
Mwongozo huo umeweka masharti mapya, ukiwataka wanaotunukiwa wawe ni waliotoa mchango mkubwa katika taaluma au kazi zao. Viongozi walioko kazini na Wafanyakazi wa Vyuo Vikuu na Wajumbe wa Seneti, hawataruhusiwa kupokea shahada hizo wakiwa bado kazini.
Aidha, vyuo vitakavyotoa shahada ya heshima vinapaswa kutoa kozi za PhD, viwe na angalau awamu nane za wahitimu, na viwe vinatambulika Kitaifa na Kimataifa.
Upande wa Tanzania, miongoni mwa waliotunukiwa Shahada za Heshima na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni Hayati Mwalimu Julius Nyerere (1966, 1986), Balozi Juma Mwapachu (2005), na Rais Mstaafu Hayati Benjamin Mkapa (2006). Licha ya mchango wao mkubwa, hawakuwahi kutumia cheo cha “Daktari wa Heshima”.
Zaidi soma https://jamii.app/EthiopiaMarufukuPhD
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
Mwongozo huo umeweka masharti mapya, ukiwataka wanaotunukiwa wawe ni waliotoa mchango mkubwa katika taaluma au kazi zao. Viongozi walioko kazini na Wafanyakazi wa Vyuo Vikuu na Wajumbe wa Seneti, hawataruhusiwa kupokea shahada hizo wakiwa bado kazini.
Aidha, vyuo vitakavyotoa shahada ya heshima vinapaswa kutoa kozi za PhD, viwe na angalau awamu nane za wahitimu, na viwe vinatambulika Kitaifa na Kimataifa.
Upande wa Tanzania, miongoni mwa waliotunukiwa Shahada za Heshima na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ni Hayati Mwalimu Julius Nyerere (1966, 1986), Balozi Juma Mwapachu (2005), na Rais Mstaafu Hayati Benjamin Mkapa (2006). Licha ya mchango wao mkubwa, hawakuwahi kutumia cheo cha “Daktari wa Heshima”.
Zaidi soma https://jamii.app/EthiopiaMarufukuPhD
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Siasa ameibua hoja kuhusu wimbi la baadhi ya Watu maarufu na Wanasiasa kujipendekeza kwa Watawala maarufu kama ‘uchawa’ hali ambayo imeonekana kuzidi kushamiri kadri joto la Uchaguzi linavyopanda.
Amedai kuwa tabia hiyo haimfurahishi kwani inaleta madhara kwa Taifa, ikiwemo kupotosha Wapiga Kura na kuharibu mwelekeo wa Demokrasia.
Je, Wanasiasa wanaojipendekeza wanatafuta nafasi za Uongozi kwa maslahi ya Taifa na Wananchi, au ni kwa ajili ya maslahi yao binafsi?
Zaidi Soma https://jamii.app/KujipendekezaWagombea
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025
Amedai kuwa tabia hiyo haimfurahishi kwani inaleta madhara kwa Taifa, ikiwemo kupotosha Wapiga Kura na kuharibu mwelekeo wa Demokrasia.
Je, Wanasiasa wanaojipendekeza wanatafuta nafasi za Uongozi kwa maslahi ya Taifa na Wananchi, au ni kwa ajili ya maslahi yao binafsi?
Zaidi Soma https://jamii.app/KujipendekezaWagombea
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025
❤1👍1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Askofu Gervas Nyaisonga amewaasa vijana kutojishughulisha na dhambi ya mauaji pamoja na matukio ya utekaji akisisitiza kuwa hakuna mtu mwenye haki juu ya uhai wa mtu mwingine.
Ameyasema hayo leo Agosti 20 wakati wa mahubiri kwenye Misa Takatifu ya Ufunguzi wa Kongamano la 6 la Viwawa Taifa ambalo linafanyika Jimbo kuu la Mbeya katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mbeya.
Zaidi soma https://jamii.app/MshirikiDhambiMauaji
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji
Ameyasema hayo leo Agosti 20 wakati wa mahubiri kwenye Misa Takatifu ya Ufunguzi wa Kongamano la 6 la Viwawa Taifa ambalo linafanyika Jimbo kuu la Mbeya katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki Mbeya.
Zaidi soma https://jamii.app/MshirikiDhambiMauaji
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #JFUwajibikaji
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi cha Taasisi Zinazounda Utatu, Agosti 18, 2025, Jaji Mkuu George Masaju ametaka Mahakama iondoe ucheleweshaji wa mashauri usio na sababu za msingi, akisema hali hiyo inadhoofisha utoaji wa haki, akisema “Kitu mnachoweza kumaliza kwa siku mbili, unasema mpaka umalize Miezi minne?”
Zaidi soma https://jamii.app/MasajuKesiMahakamani
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance #UtawalaBora
Zaidi soma https://jamii.app/MasajuKesiMahakamani
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance #UtawalaBora
👍1
DAR: Baada ya Mdau wa JamiiForums.com kudai huduma ya Kampuni inayokamata Vyombo vya Moto vinavyoegeshwa kimakosa ndani ya Wilaya ya Ubungo na kueleza faini ya Tsh. 80,000 inayotozwa haiendani na kosa, ufafanuzi umetolewa na Mamlaka inayosimamia.
Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imesema dereva anayekutwa na kosa hataruhusiwa kuondoka eneo la tukio hadi awe amelipa faini tofauti na utaratibu wa Polisi ambapo faini inaweza kulipwa baadaye hata baada ya kuondoka eneo la tukio.
Halmashauri hiyo pia imetoa maelekezo kwa Watendaji wa Boss Kazi Ltd kufanya kazi kwa kufuata masharti ya mkataba na Sheria za nchi, kuhudumia Wananchi kwa staha, heshima na weledi, kupiga picha kabla ya kutoa faini ili kuepusha sintofahamu na kutoa elimu ya kutosha kwa kila Mwananchi anayekamatwa kuhusu kosa lake na namna ya kulipa.
Zaidi https://jamii.app/WrongParkingUbungo
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #ServiceDelivery #JFMdau2025 #Accountability
Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo imesema dereva anayekutwa na kosa hataruhusiwa kuondoka eneo la tukio hadi awe amelipa faini tofauti na utaratibu wa Polisi ambapo faini inaweza kulipwa baadaye hata baada ya kuondoka eneo la tukio.
Halmashauri hiyo pia imetoa maelekezo kwa Watendaji wa Boss Kazi Ltd kufanya kazi kwa kufuata masharti ya mkataba na Sheria za nchi, kuhudumia Wananchi kwa staha, heshima na weledi, kupiga picha kabla ya kutoa faini ili kuepusha sintofahamu na kutoa elimu ya kutosha kwa kila Mwananchi anayekamatwa kuhusu kosa lake na namna ya kulipa.
Zaidi https://jamii.app/WrongParkingUbungo
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFHuduma #ServiceDelivery #JFMdau2025 #Accountability
❤2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
MBEYA: Kamanda wa Polisi Mkoa, Benjamin Kuzaga amesema wanawashikilia Watu Tisa kwa tuhuma za kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu kupitia Mitandao ya Kijamii ikiwemo Facebook na WhatsApp, ambapo Watuhumiwa hao walikamatwa Agosti 18, 2025 katika maeneo ya Nsalala na Mapelele, Mbalizi.
Kamanda Kuzaga ameeleza kuwa Watuhumiwa hao walitumia mbinu mbalimbali ikiwemo kutangaza nafasi feki za ajira, kuwatapeli Watu kwa kutumia simu na mitandao kwa mtindo wa “Tuma kwenye namba hii,” na kuwarubuni wengine wachangie fedha kujiunga na Kampuni ya Q NET yenye asili ya Malaysia.
Amewataja waliokamatwa ni Nemia Njonga (23), Ombeni Ambilikile (22), Jacob Peter (23), Baraka Mgala (22), Lusajo Jeremiah (45), Adili Mbeyale (19), Shaban Yasin (23), Ester Kimaro (28) na Abdi Awadhi (21).
Zaidi soma https://jamii.app/WakamatwaUtapeli
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFDigitali #DigitalSafety #Accountability
Kamanda Kuzaga ameeleza kuwa Watuhumiwa hao walitumia mbinu mbalimbali ikiwemo kutangaza nafasi feki za ajira, kuwatapeli Watu kwa kutumia simu na mitandao kwa mtindo wa “Tuma kwenye namba hii,” na kuwarubuni wengine wachangie fedha kujiunga na Kampuni ya Q NET yenye asili ya Malaysia.
Amewataja waliokamatwa ni Nemia Njonga (23), Ombeni Ambilikile (22), Jacob Peter (23), Baraka Mgala (22), Lusajo Jeremiah (45), Adili Mbeyale (19), Shaban Yasin (23), Ester Kimaro (28) na Abdi Awadhi (21).
Zaidi soma https://jamii.app/WakamatwaUtapeli
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFDigitali #DigitalSafety #Accountability
❤1
Mdau wa JamiiForums.com kupitia Jukwaa la Siasa ameeleza katika kipindi hiki cha mchakato wa vyama kuwapata Wagombea, kumekuwa na usambazaji wa vifaa vyenye nembo ya chama. Anadai matukio hayo yanaweza kuibua mjadala kuhusu ushawishi, kwani bado haijathibitishwa kama vinaweza kuathiri maoni ya Wapiga Kura kwa makusudi.
Amehoji, Je, wahusika wanahakikisha hakuna uvunjifu wa Sheria za Uchaguzi wakati wa usambazaji wa vifaa hivyo?
Zaidi Soma https://jamii.app/KablaYaKampeni
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025 #TaarifaZaUchaguzi2025
Amehoji, Je, wahusika wanahakikisha hakuna uvunjifu wa Sheria za Uchaguzi wakati wa usambazaji wa vifaa hivyo?
Zaidi Soma https://jamii.app/KablaYaKampeni
#JamiiForums #Accountability #Misinformation #Disinformation #ElectionInformation2025 #MisDis2025 #TaarifaZaUchaguzi2025
❤2
GEITA: Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita limesema linaendelea kuchunguza tukio la kutoweka kwa Elisha Juma, mkazi wa Mtaa wa Kadisi, Kata ya Katente, Wilaya ya Bukombe, ambaye pia ni mwimbaji wa nyimbo za injili.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Agosti 21, 2025, Polisi wameeleza walipokea malalamiko kwamba mnamo Agosti 19, 2025 saa 10:00 jioni, Elisha alichukuliwa na watu watatu wasiojulikana akiwa studio ya MAS J, Kilimahewa kata ya Bulangwa, waliokuwa na gari jeupe lisilojulikana usajili wake.
Aidha, Jeshi limetoa wito kwa yeyote mwenye taarifa ya kuweza kusaidia kupatikana kwa Elisha asisite kuziwasilisha ili zifanyiwe kazi.
Zaidi soma https://jamii.app/JumaElishaWasiojulikana
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #JFMatukio #UtawalaBora #HakiZaBinadamu
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Agosti 21, 2025, Polisi wameeleza walipokea malalamiko kwamba mnamo Agosti 19, 2025 saa 10:00 jioni, Elisha alichukuliwa na watu watatu wasiojulikana akiwa studio ya MAS J, Kilimahewa kata ya Bulangwa, waliokuwa na gari jeupe lisilojulikana usajili wake.
Aidha, Jeshi limetoa wito kwa yeyote mwenye taarifa ya kuweza kusaidia kupatikana kwa Elisha asisite kuziwasilisha ili zifanyiwe kazi.
Zaidi soma https://jamii.app/JumaElishaWasiojulikana
#JamiiAfrica #JamiiForums #Governance #Accountability #JFMatukio #UtawalaBora #HakiZaBinadamu
❤2
NJOMBE: Mdau wa JamiiForums.com ambaye ni Mkazi wa Njombe Mjini ametoa wito kwa Halmashauri hiyo kuweka wazi ikiwa imetoa maelekezo kwa Shule za Msingi kutoza Wanafunzi hadi Tsh. 10,000 kwa ajili ya mitihani ya kila wiki, na kuongeza kuwa gharama hizo zimekuwa mzigo kwa Wazazi na Walezi.
Zaidi soma https://jamii.app/ShuleNjombeHalmashauri
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
Zaidi soma https://jamii.app/ShuleNjombeHalmashauri
#JamiiForums #JamiiAfrica #JFHuduma #Accountability #JFMdau2025 #JFUwajibikaji
❤1
SOMALIA: Marais watatu wastaafu Sharif Sheikh Ahmed, Abdiqasim Salad Hassan na Mohamed Abdullahi Farmaajo wameungana kutoa tamko dhidi ya Serikali ya Rais Hassan Sheikh Mohamud, wakiilaani kwa uporaji na uuzaji holela wa ardhi ya umma bila kuzingatia taratibu za Kisheria na usimamizi unaostahili.
Viongozi hao wamesema Serikali imekuwa ikihamisha umiliki wa ardhi bila kuhusisha Mamlaka ya Mikataba ya Taifa, na kutoingiza mapato kwenye Hazina ya Taifa. Hali inayosababisha Wananchi maskini wa Mogadishu kufukuzwa na kuondolewa katika makazi yao.
Wametaka Wananchi na Wafanyabiashara kuepuka kununua au kushiriki katika mali zilizopatikana kwa njia zisizo halali, wakisema ni mikataba hatarishi na isiyo na uhalali, hatua ambayo imepongezwa na makundi ya uharakati.
Soma zaidi https://jamii.app/Somalia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance
Viongozi hao wamesema Serikali imekuwa ikihamisha umiliki wa ardhi bila kuhusisha Mamlaka ya Mikataba ya Taifa, na kutoingiza mapato kwenye Hazina ya Taifa. Hali inayosababisha Wananchi maskini wa Mogadishu kufukuzwa na kuondolewa katika makazi yao.
Wametaka Wananchi na Wafanyabiashara kuepuka kununua au kushiriki katika mali zilizopatikana kwa njia zisizo halali, wakisema ni mikataba hatarishi na isiyo na uhalali, hatua ambayo imepongezwa na makundi ya uharakati.
Soma zaidi https://jamii.app/Somalia
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Governance
❤1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (#JAB), Wakili Patrick Kipangula ametoa angalizo kwa Waandishi wa Habari wasiokuwa na ithibati, kuwa hawataruhusiwa kuripoti Uchaguzi Mkuu 2025.
Amefafanua kuwa Mwandishi kufanya kazi bila kitambulisho cha Bodi ya Ithibati ni kosa linaloweza kusababisha faini ya hadi Tsh. Milioni 5 au kifungo cha miaka mitatu hadi mitano. Ameeleza hayo wakati wa Mkutano wa Wadau wa Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki, Agosti 21, 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/JABWaandishiUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFUwajibikaji #Accountability #JFSiasa
Amefafanua kuwa Mwandishi kufanya kazi bila kitambulisho cha Bodi ya Ithibati ni kosa linaloweza kusababisha faini ya hadi Tsh. Milioni 5 au kifungo cha miaka mitatu hadi mitano. Ameeleza hayo wakati wa Mkutano wa Wadau wa Habari na Utangazaji Kanda ya Mashariki, Agosti 21, 2025.
Zaidi soma https://jamii.app/JABWaandishiUchaguzi
#JamiiAfrica #JamiiForums #JFUwajibikaji #Accountability #JFSiasa
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
JF KUMBUKIZI: Akizungumza siku ya Mei Mosi, 1995, katika hotuba yake Mwl. Julius Kambarage #Nyerere alisema kuwa mwenye akili akikupa mawazo ya kipumbavu, ukayakubali, anakudharau.
"Na wewe una akili, anajua unajua kwamba ni ya kipumbavu, ukayakubali, anakudharau."
Zaidi Soma https://jamii.app/MawazoKipumbavu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Siasa #JFKumbukizi #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning
"Na wewe una akili, anajua unajua kwamba ni ya kipumbavu, ukayakubali, anakudharau."
Zaidi Soma https://jamii.app/MawazoKipumbavu
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Siasa #JFKumbukizi #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning
❤5
ARUSHA: Jeshi la Polisi limetoa taarifa kuwa linafanya uchunguzi kuhusiana na tukio la Mtu mmoja aitwaye Bakari Halifa Daud (18) Mkazi wa Sombetini kujeruhiwa kwa kupigwa risasi mguuni na Abdulaziz Abubakari (Dogo Janja).
Kamanda wa Polisi Mkoa, SACP Justine Masejo amesema uchunguzi wa awali umebaini tukio hilo lilitokea Agosti 23, 2025 Saa 5:30 Usiku maeneo ya Sombetini na kwamba Jeshi linawashikilia Watu wawili kuhusiana na tukio hilo huku uchunguzi ukiendelea.
SACP Masejo ameongeza kuwa wakati Abdulaziz Abubakari (30), Mkazi wa Levolosi akiwa anashuka kwenye gari alidai kutaka kuvamiwa na Bakari akiwa na mwenzake kwa kutumia silaha ya jadi hali iliyosababisha kutumia silaha aliyokuwa nayo.
Zaidi https://jamii.app/DogoJanjaKumpigaRisasi
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #Accountability #Uwajibikaji
Kamanda wa Polisi Mkoa, SACP Justine Masejo amesema uchunguzi wa awali umebaini tukio hilo lilitokea Agosti 23, 2025 Saa 5:30 Usiku maeneo ya Sombetini na kwamba Jeshi linawashikilia Watu wawili kuhusiana na tukio hilo huku uchunguzi ukiendelea.
SACP Masejo ameongeza kuwa wakati Abdulaziz Abubakari (30), Mkazi wa Levolosi akiwa anashuka kwenye gari alidai kutaka kuvamiwa na Bakari akiwa na mwenzake kwa kutumia silaha ya jadi hali iliyosababisha kutumia silaha aliyokuwa nayo.
Zaidi https://jamii.app/DogoJanjaKumpigaRisasi
#JamiiAfrica #JamiiForums #HumanRights #Accountability #Uwajibikaji