Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DODOMA: Naibu Waziri Mkuu, Dkt. Doto Biteko amesema Serikali ya Rais Samia Suluhu inathamini Viongozi wa Dini na Dini kwa kuwa inaongoza Wananchi wenye dini, isingependa kuona Haki zao zinapuuzwa au kudogoshwa
Amesema hayo wakati akimwakilisha Rais Samia katika Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Julai 3, 2025
Soma https://jamii.app/Samiahakizakidini
#JamiiAfrica #HakiyaKuabudu #JamiiForums #HumanRights #Uwajibikaji
Amesema hayo wakati akimwakilisha Rais Samia katika Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Julai 3, 2025
Soma https://jamii.app/Samiahakizakidini
#JamiiAfrica #HakiyaKuabudu #JamiiForums #HumanRights #Uwajibikaji
❤3👏1
DAR: Mdau wa JamiiForums.com ametoa wito kwa Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA) kushughulikia kero ya baadhi ya Makondakta wa Daladala kuongeza nauli wakati wa Usiku bila taarifa rasmi
Soma https://jamii.app/NauliKupandaUsiku
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
Soma https://jamii.app/NauliKupandaUsiku
#JamiiAfrica #JamiiForums #Accountability #Uwajibikaji
❤1
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
KENYA: Vijana kadhaa leo Juni 3, 2025 wamevamia na kuchoma moto Kituo cha Polisi cha Mawego kilichopo Rachuonyo Mashariki, Kaunti ya Homa Bay, eneo ambalo Mwanaharakati Albert Ojwang alishikiliwa kabla ya kupigwa na kusababisha kifo chake
Awali, waombolezaji walitakiwa kuaga mwili wa Ojwang katika Shule ya Msingi ya Nyawango, lakini ratiba ilibadilika baada ya Vijana kuzuia msafara wa Jeneza la marehemu na kulazimisha mwili huo upelekwe katika Kituo cha Polisi cha Mawego
Walipofika kituoni vijana hao waliondoa vizuizi vilivyowekwa na Polisi kisha kuchoma kituo hicho kama ishara ya kupinga mauaji ya Ojwang’
Zaidi bofya https://jamii.app/kituochapolisi
#JamiiAfrica #Accountability #HumanRights #Governance #KenyanPolitics
Awali, waombolezaji walitakiwa kuaga mwili wa Ojwang katika Shule ya Msingi ya Nyawango, lakini ratiba ilibadilika baada ya Vijana kuzuia msafara wa Jeneza la marehemu na kulazimisha mwili huo upelekwe katika Kituo cha Polisi cha Mawego
Walipofika kituoni vijana hao waliondoa vizuizi vilivyowekwa na Polisi kisha kuchoma kituo hicho kama ishara ya kupinga mauaji ya Ojwang’
Zaidi bofya https://jamii.app/kituochapolisi
#JamiiAfrica #Accountability #HumanRights #Governance #KenyanPolitics
❤1👍1
Maisha ni kama mchezo kwa sababu kila uamuzi tunaochukua ni kama hatua moja mbele
Hatuna uwezo wa kurudi nyuma kubadilisha tuliyofanya zamani (makosa au mafanikio), lakini tunayo nafasi na uwezo wa kuhakikisha hatua au uamuzi wetu unaofuata unakuwa bora zaidi na unaleta matokeo mazuri.
#JamiiForums #JamiiAfrica #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
Hatuna uwezo wa kurudi nyuma kubadilisha tuliyofanya zamani (makosa au mafanikio), lakini tunayo nafasi na uwezo wa kuhakikisha hatua au uamuzi wetu unaofuata unakuwa bora zaidi na unaleta matokeo mazuri.
#JamiiForums #JamiiAfrica #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
DODOMA: Jeshi la Polisi Mkoanii Geita linawashikilia Ferdinand Antony, Afisa Mtendaji Kijiji cha Liyobahika pamoja na Hussein Ally kwa tuhuma za mauaji ya Enock Mhangwa. Tukio hilo lilitokea Juni 26, 2025 ambapo Watuhumiwa walimshambulia kijana huyo kwa kipigo mpaka kufariki Dunia
Aidha, Watuhumiwa wengine akiwemo Mtendaji wa Kijiji cha Uyovu na mgambo wawili wanaendelea kutafutwa baada ya kukimbia
Video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo JamiiForums.com ilionesha kijana huyo akipigwa fimbo akiwa amefungwa kamba akituhumiwa kuwa mwizi
Zaidi bofya https://jamii.app/MauajiEnock
#JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #HumanRights #Governance #JamiiForums
Aidha, Watuhumiwa wengine akiwemo Mtendaji wa Kijiji cha Uyovu na mgambo wawili wanaendelea kutafutwa baada ya kukimbia
Video iliyosambaa kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo JamiiForums.com ilionesha kijana huyo akipigwa fimbo akiwa amefungwa kamba akituhumiwa kuwa mwizi
Zaidi bofya https://jamii.app/MauajiEnock
#JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #HumanRights #Governance #JamiiForums
❤1
Filamu ya "Squid Game" msimu wa 3 iliyotoka Juni 27, 2025 ni miongoni mwa filamu zinazohusisha michezo hatarishi.
Baadhi ya wadau wamedai kuwa wasingetoboa katika mchezo wa "Hide and Seek" katika filamu hiyo maarufu kama (Kombolela)
Mdau, umeitazama Squid Game 3? Ni mchezo gani unaona kabisa usingetoka salama?
Mjadala zaidi https://jamii.app/squidgame3
#JamiiAfrica #Jamiiforums #JFBurudani #JFEntertainment
Baadhi ya wadau wamedai kuwa wasingetoboa katika mchezo wa "Hide and Seek" katika filamu hiyo maarufu kama (Kombolela)
Mdau, umeitazama Squid Game 3? Ni mchezo gani unaona kabisa usingetoka salama?
Mjadala zaidi https://jamii.app/squidgame3
#JamiiAfrica #Jamiiforums #JFBurudani #JFEntertainment
🔥2❤1
DAR: Baada ya Mdau kushauri Hospitali ya Amana kuboresha huduma ikiwemo ya "Ambulance", akidai kuna gari mbili na Dereva mmoja, hivyo kasi kuwa ndogo ya kubeba Wagonjwa huku akiongeza kuwa baadhi ya Wauguzi wajirekebishe katika kauli zao wakati wa huduma, Uongozi wa Hospitali umetoa majibu
Kuhusu Mgonjwa kusubiri gari kuanzia Jioni hadi Saa Saba Usiku, Juni 23, 2025, Amana imeeleza “Kulikuwa na Wagonjwa sita wa rufaa, wawili walipelekwa Muhimbili – Mloganzila, wanne walipelekwa Muhimbili Upanga, mgonjwa wa mwisho alipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kabla ya Saa Saba Usiku”
Taarifa ya Hospitali imeeleza “Amana ina Ambulance mbili, lakini kutokana Serikali kufanya maboresho ya huduma za Afya, idadi ya Wagonjwa wanaopewa Rufaa kutoka Amana imepungua na muda mwingine kuweka dereva mmoja kwa zamu za usiku, na hata siku hiyo ya Juni 23, 2025 alipangwa dereva mmoja
Soma https://jamii.app/AmanaHospitali
#JamiiForums #JamiiAfrica #ServiceDelivery #Accountability
Kuhusu Mgonjwa kusubiri gari kuanzia Jioni hadi Saa Saba Usiku, Juni 23, 2025, Amana imeeleza “Kulikuwa na Wagonjwa sita wa rufaa, wawili walipelekwa Muhimbili – Mloganzila, wanne walipelekwa Muhimbili Upanga, mgonjwa wa mwisho alipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili kabla ya Saa Saba Usiku”
Taarifa ya Hospitali imeeleza “Amana ina Ambulance mbili, lakini kutokana Serikali kufanya maboresho ya huduma za Afya, idadi ya Wagonjwa wanaopewa Rufaa kutoka Amana imepungua na muda mwingine kuweka dereva mmoja kwa zamu za usiku, na hata siku hiyo ya Juni 23, 2025 alipangwa dereva mmoja
Soma https://jamii.app/AmanaHospitali
#JamiiForums #JamiiAfrica #ServiceDelivery #Accountability
❤1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Mbunge wa Jimbo la Tandahimba, Katani Ahmed Katani amesema "Upige picha kwenye barabara za Doha-Qatar, halafu upite barabara za Tandahimba na uweke kwenye mtandao huwezi kuona tofauti"
Ameyasema hayo Julai 3, 2025 katika mahojiano kwenye kipindi cha Wasafi cha 'One on One'
Watu wa Tandahimba, tuambieni hali ikoje?
Soma https://jamii.app/Tandahimbakamadoha
#JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #ServiceDelivery #Governance #JamiiForums #KuelekeaUchaguzi2025
Ameyasema hayo Julai 3, 2025 katika mahojiano kwenye kipindi cha Wasafi cha 'One on One'
Watu wa Tandahimba, tuambieni hali ikoje?
Soma https://jamii.app/Tandahimbakamadoha
#JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji #ServiceDelivery #Governance #JamiiForums #KuelekeaUchaguzi2025
❤1🤣1
DAR: Rais wa Shirikisho la Soka la Tanzania (#TFF), Wallace Karia amesalia kuwa Mgombea pekee wa nafasi ya Urais wa Shirikisho hilo katika Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Agosti 16, 2025 baada ya Wagombea wengine kukosa vigezo kwa mujibu wa taarifa ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF iliyoeleza amepita kwenye mchujo wa awali
Wagombea wengine wa nafasi hiyo Ally Mayay Tembele, Mbette Mshindo Msolla, Mustapha Salumu Himba na Shija Richard Shija wamekosa vigezo huku Ally Thabit Mbingo hakufika katika usaili
Nafasi ya Kamati ya Utendaji ya TFF wamepita Wagombea 10 kati ya 17 ambao walifika kwenye usaili wa awali, hivyo Kamati ya Uchaguzi inasubiri kupokea Rufaa za Wagombea watakaokata rufaa ambayo inatakiwa kukatwa ndani ndani ya siku 6
Soma https://jamii.app/kariamgombeaurais
#JamiiForums #JFSports #JamiiAfrica
Wagombea wengine wa nafasi hiyo Ally Mayay Tembele, Mbette Mshindo Msolla, Mustapha Salumu Himba na Shija Richard Shija wamekosa vigezo huku Ally Thabit Mbingo hakufika katika usaili
Nafasi ya Kamati ya Utendaji ya TFF wamepita Wagombea 10 kati ya 17 ambao walifika kwenye usaili wa awali, hivyo Kamati ya Uchaguzi inasubiri kupokea Rufaa za Wagombea watakaokata rufaa ambayo inatakiwa kukatwa ndani ndani ya siku 6
Soma https://jamii.app/kariamgombeaurais
#JamiiForums #JFSports #JamiiAfrica
❤1
MAREKANI: Chama cha Democratic kimemteua Zohran Mamdani, mwenye asili ya Uganda na India, kuwa mgombea katika kinyang’anyiro cha Umeya wa Jiji la New York baada ya kushinda mchujo wa ndani wa chama hicho uliofanyika Juni 25, 2025.
Mamdani amezaliwa Uganda, na anatoka katika familia yenye asili ya Kihindi. Baba yake, Mahmood Mamdani, ni profesa maarufu katika Chuo Kikuu cha Columbia nchini Marekani, huku mama yake, Mira Nair akiwa ni mtayarishaji wa filamu kimataifa.
Aliwasili Marekani akiwa na umri wa miaka 7 na alipata uraia mwaka 2018. Iwapo atachaguliwa kwenye Uchaguzi utakaofanyika Novemba 4 2025, Mamdani atakuwa Meya wa kwanza Muislamu wa jiji hilo na pia Meya wa kwanza nchini Marekani mwenye asili ya Kihindi na Uganda
Soma pia: https://jamii.app/mamdanimeya
#JamiiAfrica #Democracy #Governance #JamiiForums
Mamdani amezaliwa Uganda, na anatoka katika familia yenye asili ya Kihindi. Baba yake, Mahmood Mamdani, ni profesa maarufu katika Chuo Kikuu cha Columbia nchini Marekani, huku mama yake, Mira Nair akiwa ni mtayarishaji wa filamu kimataifa.
Aliwasili Marekani akiwa na umri wa miaka 7 na alipata uraia mwaka 2018. Iwapo atachaguliwa kwenye Uchaguzi utakaofanyika Novemba 4 2025, Mamdani atakuwa Meya wa kwanza Muislamu wa jiji hilo na pia Meya wa kwanza nchini Marekani mwenye asili ya Kihindi na Uganda
Soma pia: https://jamii.app/mamdanimeya
#JamiiAfrica #Democracy #Governance #JamiiForums
❤1
Wakati mwingine picha, video au maneno yanayodhalilisha dini, kabila, jinsia au Watu fulani husambazwa kwa mzaha, lakini kwa Mtu anayelengwa, si mzaha, ni tusi, ni kejeli, ni maumivu
Chuki huanza kwa utani, huishia kwa madhara makubwa. Inaweza kuchochea fujo, kuchafua sifa ya Mtu, au hata kumweka hatarini
Ni wajibu wetu kama Vijana kuhoji kila tunachotaka kusambaza
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
Chuki huanza kwa utani, huishia kwa madhara makubwa. Inaweza kuchochea fujo, kuchafua sifa ya Mtu, au hata kumweka hatarini
Ni wajibu wetu kama Vijana kuhoji kila tunachotaka kusambaza
#JamiiForums #JamiiAfrica #HumanRights #KauliZaChuki #StopHateSpeech #DigitalPeace #NoToHateSpeech #ResponsiblePosting #JamiiYenyeUelewa
Sio lazima kila mtu akubaliane na wewe
Wengine hawaoni mambo kama unavyoyaona, na hiyo haimaanishi wako sahihi au wamekosea, ni mtazamo tu tofauti.
#JamiiForums #JamiiAfrica #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
Wengine hawaoni mambo kama unavyoyaona, na hiyo haimaanishi wako sahihi au wamekosea, ni mtazamo tu tofauti.
#JamiiForums #JamiiAfrica #AmkaNaJamiiAfrica #GoodMorning #Maisha
KENYA: Rais #WilliamRuto amesema hatamuomba yeyote msamaha kwa kitendo cha yeye kujenga Kanisa ndani ya Ikulu, akiongeza kuwa anawashangaa wanaomsema kuhusu ujenzi huo kwani atatumia pesa zake mwenyewe na sio kutoka Serikalini
Ametoa msimamo huo Julai 4, 2025, na kusisitiza kuwa hajajenga Kanisa jipya bali anaboresha alilolikuta lililokuwa limejengwa kwa mabati ambalo haliendani na hadhi ya Ikulu
Zaidi bofya https://jamii.app/KujengaKanisaIkulu
#JamiiAfrica #Accountability #KenyanPolitics #Uwajibikaji
Ametoa msimamo huo Julai 4, 2025, na kusisitiza kuwa hajajenga Kanisa jipya bali anaboresha alilolikuta lililokuwa limejengwa kwa mabati ambalo haliendani na hadhi ya Ikulu
Zaidi bofya https://jamii.app/KujengaKanisaIkulu
#JamiiAfrica #Accountability #KenyanPolitics #Uwajibikaji