JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.44K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Baadhi ya Waumini wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania (Kanisa la Ufufuo na Uzima) linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima ambalo Juni 2, 2025 lilifungiwa, wamejitokeza eneo la pembezoni mwa Kanisa hilo lililopo Ubungo wakipiga maombi huku Kanisa hilo likiwa limezungukwa na Askari Polisi

Juni 14, 2025, kupitia ukurasa wake wa Instagram, Askofu Gwajima alitangaza uwepo wa ibada leo Juni 15, 2025 eneo la Ubungo

Soma https://jamii.app/WauminiGwajimaWasaliNje

#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio
Ajira kwa Vijana ni nyenzo muhimu kwa maendeleo ya Mtu Binafsi, Jamii na Taifa kwa ujumla. Ajira humfanya mtu awe na ari ya kutosha, kuwajibika na kushiriki kikamilifu katika nyanja zote za Kijamii na Kiuchumi

Kwa mujibu wa Utafiti wa Nguvu Kazi (ILFS 2021), Tanzania, ilikuwa na nguvu kazi ya Watu wapatao 25,861,023 ambapo kati ya Nguvu kazi hiyo, Vijana ni 14,219,191 sawa na 55.6%.

Soma https://jamii.app/UwajibikajiWaVijana

#JamiiAfrica #JamiiForums #JFVijana #RestlessDevelopment #UshirikiWaVijana
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Baadhi ya Waumini wa Kanisa la Glory of Christ Tanzania Church (Nyumba ya Ufufuo na Uzima) waliokuwa wamekusanyika leo Juni 15, 2025 kwaajili ya ibada wametawanywa na Askari Polisi waliokuwa wanalinda eneo hilo baada ya Waumini kujikusanya na kuanza kuelekea katika kanisa hilo

Awali, Waumini hao walikusanyika eneo la umbali wa takriban mita 300 tokea lilipo Kanisa hilo ambalo limezungukwa na Askari, ambapo walifanya maombi na kuimba nyimbo

Soma https://jamii.app/WauminiGwajimaWatawanywishwa

#JamiiAfrica #JamiiForums #JFMatukio
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Jaji Mkuu mstaafu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma amesema "Sijawahi hata siku moja kukaa na Mheshimiwa Rais, Spika au Waziri Mkuu na kuzungumzia kesi, kwanza sina hata majalada hapa. Tunazungumza mambo ya masilahi mapana ya Taifa" akifafanua kuhusu ufuatiliaji wa masuala ya Mahakama unaofanywa na viongozi wa Serikali haumaanishi kuingilia uhuru wa Mhimili huo

Amesema hayo leo, Juni 15, 2025 katika hafla ya kuapishwa kwa Jaji George Masaju kuwa Jaji Mkuu wa Tanzania, iliyofanyika Ikulu Jijini Dodoma

Soma https://jamii.app/RaisHaingiliiMahakama

#JamiiForums #JamiiAfrica #ConstituonalRights
Mdau wa Jukwaa la JF Chit-Chats and Jokes ndani ya JamiiForums.com ameanzisha mjadala wa Siku gani unazipenda katika wiki

Ni kitu gani kinakufanya uwe na siku pendwa katika wiki?

Mjadala zaidi https://jamii.app/SikuIpi

#JamiiForums #JamiiAfrica #JFChitChats
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson akizungumza katika ghafla ya kumuapisha Jaji Mkuu mpya George Masaju amesema "Lazima wananchi wafike mahali waelewe kazi ya mihimili hii na kumuweka Rais mahali anapostahili, kumtofautisha na Jaji Mkuu, Spika, lakini pia kuelewa Rais anavyofanya kazi kama Mkuu wa mhimili"

Ameyasema hayo Juni 15, 2025 Jijini Mbeya akisisitiza kuwa ni muhimu Wananchi na Viongozi waelewe majukumu ya mihimili ya dola na kuheshimu mipaka yake ili kulinda utawala wa Sheria na Demokrasia ya kweli

Soma https://jamii.app/RaisKuingiliaMahakama

#JamiiForums #JamiiAfrica #ConstituonalRights
1
Kusoma kwa undani habari hizi na nyingine zilizojiri juma lililopita bofya https://jamii.app/YaliyojiriJumaLililopita

#JamiiForums #YaliyojiriJumaLililopita #JFToons
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, Tundu Antipas Lissu amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akiwa chini ya ulinzi mkali wa Polisi leo Juni 16, 2025, ili kusikiliza kesi zinazomkabili

Ikumbukwe Juni 2, 2025 Mahakama iliagiza upande wa Jamhuri kuhakikisha unaharakisha na kutoa taarifa za mwenendo wa upelelezi wa kesi ya Uhaini ili shauri lianze kusikilizwa mapema

Soma https://jamii.app/KesiLissuKurindimaLeo

#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights #Kuelekea2025
3
DAR: Jeshi la Polisi limeimarisha ulinzi katika maeneo ya karibu na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo Mashauri yanayomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, #TunduLissu, yanaendelea Mahakamani hapo

Baadhi ya Viongozi mbalimbali wa #CHADEMA wameshawasili Mahakamani kufuatilia kinachoendelea

Soma https://jamii.app/KesiLissuKurindimaLeo

#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights #Kuelekea2025
1
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa, #TunduLissu ambaye anakabiliwa na Kesi mbili kwenye Mahakama ya Kisutu amesema kwa siku 68 ambazo amekuwa Gerezani, amenyimwa haki ya kuzungumza kwa faragha na Mawakili wake ambao wamekuwa wakienda kuonana naye

Ameongeza kuwa licha ya hivyo yeye pamoja na Mawakili wake hawapati nafasi ya kubadilishana nyaraka kwaajili ya kushughulikia kesi zinazomkabili

Lissu akiwa kizimbani amesema amekuwa akizungumza na Mawakili kwenye simu akiwa eneo ambalo halimpi nafasi ya kufanya mazungumzo ya faragha, ambapo amesema kuwa, kupitia mawasiliano ya simu au eneo chumba anachotumia kuwasiliana na Mawakili wake kuna uwezekano wa kupokwa kwa Haki ya Faragha

Amesema mazingira ya aina hiyo ni kinyume na Sheria

Soma https://jamii.app/LissuNaMawakili

#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights #Kuelekea2025
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Mwenyekiti ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (#CHADEMA) Taifa, #TunduLissu ameomba Mahakamani ajitetee mwenyewe katika mashauri yanayoendelea dhidi yake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo Juni 16, 2025 wakati kesi yake ikianza kusikilizwa

Lissu ambaye alikuwa anawakilishwa na Mawakili zaidi ya 30, anakabiliwa na kesi ya uhaini pamoja na kesi ya kuchapisha taarifa za uwongo Mtandaoni

Soma https://jamii.app/LissuKujibuHoja

#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Wakili wa Serikali Mkuu, Nassoro Katuga ameieleza Mahakama kuwa jalada la uchunguzi la kesi ya uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu tayari limepelekwa kwa Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali (DPP) kwaajili ya kupitiwa kabla ya kuamriwa kupelekwa Mahakama Kuu

Upande wa Utetezi uliomba Mahakama kuitaka Jamhuri kukamilisha uchunguzi katika shauri hilo, ambapo Mahakama ilitoa maelekezo kwa upande wa Jamhuri kuharakisha uchunguzi

Hata hivyo, shauri hilo limekuwa likitajwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu bila kusikilizwa, kwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kisheria kulisikiza

Baada ya Jamhuri kueleza hatua hiyo na mshtakiwa kukubaliana nayo, Mahakama imeahirisha shauri hilo mpaka Julai 1, 2025

Soma https://jamii.app/KesiLissuKurindimaLeo

#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights
DAR: Mdau anadai tangu kuanza kwa Mwaka 2025, hajaona gari la taka katika Mtaa anaoishi (Mbezi Beach), ambapo Wananchi hulazimika kuwakodi Vijana wenye mikokoteni ili kuzoa taka na kuondoka nazo, bila kujua zinaenda kutupwa wapi

Mdau anadai Mamlaka inayosimamia mazingira (NEMC) imekuwa kimya katika suala hilo, akihoji au inasubiri mlipuko wa Magonjwa utokee ndio watoe tamko na kuchukua hatua, halafu ukiisha 'wapige kimya' tena?

Soma https://jamii.app/UzoajiTaka

#Accountability #JamiiForums
Siku ya Mtoto wa Afrika huadhimishwa kila Mwaka tarehe 16 Juni, ikiwa ni kumbukumbu ya Maandamano ya Wanafunzi huko Soweto, Afrika Kusini Mwaka 1976, ambapo walidai Haki yao ya kupata Elimu bora

Ulimwenguni kote, Watoto wanaendelea kukabiliwa na vitisho vinavyoingiliana, kutoka Umasikini na njaa hadi upatikanaji mdogo wa Elimu bora na Huduma za Afya. Kwa mujibu wa Shirika la #UNICEF (2023), zaidi ya Watoto Bilioni moja Duniani kote wanakabiliwa na angalau aina moja ya kunyimwa mahitaji muhimu

Hili ni suala la dharura hasa Barani Afrika, ambalo lina idadi ya Watoto inayokua kwa kasi zaidi Duniani, kukiwa na zaidi ya Watoto Milioni 540, karibu 50% ya idadi ya Watu Barani kote. Ifikapo Mwaka 2055, Afrika itakuwa na idadi kubwa zaidi ya Watoto Duniani

Soma https://jamii.app/DAC2025

#AfricanChildDay #InvestInChildren #DAC2025 #DayOfTheAfricanChild #JamiiForums #JamiiAfrica
1
KENYA: Naibu Mkuu wa Jeshi la Polisi (DIG), Eliud Kipkoech Lagat, ametangaza kujiondoa kwa muda kazini wakati uchunguzi ukiendelea kuhusu kifo cha Mwanaharakati Albert Ojwang’, ambaye alikamatwa kufuatia malalamiko ya kashfa yanayodaiwa kuwasilishwa na Afisa huyo

Katika taarifa iliyotolewa siku ya Jumatatu, Lagat amesema “Leo nimeamua kujiondoa kwa muda kutoka katika Wadhifa wa Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi Kenya hadi uchunguzi utakapokamilika. Majukumu ya Ofisi yataendelea kutekelezwa na Naibu wangu hadi uchunguzi utakapokamilika.”

Ojwang’ alikamatwa muda mfupi baada ya kuchapisha madai ya Ufisadi yaliyomhusisha Lagat, hasa kuhusu upangaji wa kimkakati wa Maafisa ndani ya Idara ya Upelelezi wa Jinai (DCI) na vitengo vya trafiki, nafasi zinazodaiwa kuwa na uhusiano na udhibiti wa mapato na taarifa za Kijasusi

Soma https://jamii.app/DIGResignsKE

#JamiiForums #JamiiAfrica #Accountability #Uwajibikaji
2
Media is too big
VIEW IN TELEGRAM
DAR: Akiongea Mahakamani leo Juni 16, 2025, Mwenyekiti wa #CHADEMA Taifa, #TunduLissu amesema kuwa licha ya kuwa hajahukumiwa, anakaa upande wa Watu waliohukumiwa kifo katika Gereza la Ukonga

Zaidi https://jamii.app/LissuKuhusuGerezani

#JamiiForums #JamiiAfrica #Siasa #Democracy #Governance #HumanRights
This media is not supported in your browser
VIEW IN TELEGRAM
SIMIYU: Rais Samia Suluhu ametoa wito kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kukusanya mapato kwa njia rafiki, lakini sio kubembelezana anayekataa asilipe. Amesema kila anayepaswa kulipa kodi, alipe

Amesema hayo baada ya kufungua Jengo la Ofisi ya TRA Mkoani humo, leo Juni 16, 2025

Soma https://jamii.app/MikopoYaNje

#JamiiForums #Governance #Accountability