JamiiForums
βœ”
52.7K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
URUSI: MAHAKAMA YASITISHA SHUGHULI ZA FACEBOOK NA INSTAGRAM

Ofisi ya Mwendesha Mashtaka imesema kumekuwa na machapisho makali kwenye Mitandao hiyo ya Kijamii, yakitoa wito wa vurugu dhidi ya raia wa Urusi na Wanajeshi wake walioko #Ukraine

Soma https://jamii.app/FBIGBanRussia
#DigitalRights
Waziri wa Utamaduni, #Sanaa na #Michezo, Mohamed Mchengerwa amelitaka BASATA kuwaita Viongozi wa Shirikisho la Muziki kushughulikia mgogoro unaoendelea baada ya Steven Mengele (Steve Nyerere) kuteuliwa kuwa Msemaji

Aidha, Steve amesema hawezi kujiuzulu nafasi hiyo bila utaratibu au kutokana na mashinikizo kutoka kwa Wasanii

Soma - https://jamii.app/BasataVsSteve
Kuingilia Vyombo vya Habari kunaweza kuzuia Uhuru wa Kujieleza unaotolewa na Demokrasia. Hatua hizi zinaweza kuchochea rushwa na kukosekana kwa Uwajibikaji

Kwa mujibu wa Corruption Perceptions Index (CPI) ya Mwaka 2021 ni kuwa licha ya ahadi kwenye karatasi Nchi 131 hazijapiga hatua kubwa dhidi ya Rushwa/Ufisadi katika muongo uliopita

Soma - https://jamii.app/UwaziKodiUmma
#Accountability
MCHENGERWA: HAKUNA MSANII MKUBWA KULIKO NCHI

Waziri wa #Sanaa na Michezo amewataka BASATA na COSOTA kuhakikisha Wasanii wote wanasajiliwa hususani wakubwa

Amesema Wasanii wakongwe wapewe nafasi mbalimbali hasa za BASATA ili wasimamie #Biashara zao

Soma - https://jamii.app/UsajiliWasanii
EU: AFRIKA IUNGANE NA DUNIA KUIPINGA URUSI

Umoja wa Ulaya (EU) umeshawishi Afrika kujitokeza kupinga Urusi kuivamia #Ukraine Kijeshi

Tamko hilo limetolewa Dar na Mabalozi wa Nchi za Ulaya Nchini Tanzania walio Wanachama wa EU

Soma - https://jamii.app/EUTZ
#RussianUkraineWar
URUSI: Mahakama imemhukumu mkosoaji wa Serikali ya Urusi, Alexei Navalny kifungo cha Miaka 9 kwa ufujaji Fedha na kutoheshimu Mahakama

Haijabainika ikiwa Miaka hiyo tisa itaenda sambamba na hukumu ya Miaka 2 na nusu anayotumikia sasa

Soma - https://jamii.app/Navalny9Yrs
#HumanRights
#UPDATES AJALI YA NDEGE (BOEING 737)

Shirika la Habari la Serikali ya China limesema hakuna Abiria hai aliyepatikana kwenye mabaki ya Ndege iliyoanguka na Abiria 132

Hii ndiyo ajali mbaya zaidi ya Ndege kuikumba #China kwa zaidi ya muongo mmoja

Soma - https://jamii.app/Boeing737Crash
MGOGORO WA #UKRAINE NA #URUSI: Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa asema NATO ingesikiliza maonyo kusingekuwa na mgogoro uliopo

> Aidha, baadhi ya Wachambuzi wamesema ushawishi wa Ramaphosa kama Mpatanishi umepungua baada ya kuilaumu NATO

Soma https://jamii.app/RamaphosaNATO
Ukaguzi wa CAG umebaini Deni la Serikali katika Bohari Kuu ya Dawa limeongezeka kwa Tsh. bilioni 56.01 kutoka Tsh. bilioni 200.91 mwaka 2017/18 hadi kufikia Tsh. bilioni 256.92 mwaka 2019/20

Kuongezeka kwa Deni hilo kumetokana na ulipaji hafifu wa Madeni ya Hospitali, Vituo vya #Afya vya Serikali na Taasisi nyingine za Umma baada ya kupelekewa Dawa na Vifaa Tiba kutoka MSD

#JamiiForums #Accountability #WAJIBU #JFUwajibikaji
NAIBU WAZIRI: HAKUNA SERIKALI DUNIANI INAPANGA KUUA WATU WAKE

Mbunge wa Butiama, Jumanne Abdallah Sagini ambaye ni Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani amewataka Wananchi kuamini taarifa ya Kamati Maalumu kuchunguza mabadiliko ya Maji ndani ya Mto Mara

Soma - https://jamii.app/SaginiMtoMara
UKRAINE: Maksym Levin ambaye ni Mwanahabari Picha wa #Ukraine aliyekuwa anapiga picha Mjini #Kyiv hajulikani alipo

> Rafiki yake amesema inawezekana amejeruhiwa au kutekwa na Wanajeshi wa #Urusi walioko nchini Ukraine

Soma https://jamii.app/Photojournalist
#RussiaUkraineConflict
DAR ES SALAAM: Rais Samia Suluhu Hassan amewapa Wananchi miezi mitatu ya kupumzika kuchangia gharama za uendeshaji wa Nyumba 644 za Makazi za Magomeni Kota

> Aidha, Rais Samia amewataka Wananchi hao kutunza nyumba hizo

Soma https://jamii.app/Nyumba644
#JamiiForums #RaisSamia
JAMAICA: Wanaharakati walikusanyika Ubalozi wa #Uingereza nchini humo wakitaka Uingereza kuomba radhi na kulipa fidia kutokana na madhara yaliyosababishwa na Utumwa

> Hayo yamejiri Mwana Mfalme, William alipotembelea #Kingston Machi 22, 2022

Soma https://jamii.app/JamaicaReparation
πŸ‘1
MALEZI: JINSI YA KUMSAIDIA MTOTO ANAPOPATA MLIPUKO WA HASIRA

Mtoto anapokasirika huweza kuanza kupiga kelele, kutupa vitu, kupiga piga miguu na kujigaragaza chini

1. Shikilia msimamo wako: Ikiwa unampa Mtoto wako kila kitu anachotaka kwasababu tu amekasirika tambua ataendelea kufanya hivyo kila anapotaka kitu fulani. Mwoneshe msimamo wako haubadiliki ovyo

Zaidi, soma - https://jamii.app/HasiraWatoto
#Malezi
#COVID19: Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema waliopata chanjo ya #Corona hadi sasa ni asilimia 9.81 kati ya wote wanaostahili kupata

> Waziri amesema hayo wakati akipokea chanjo aina ya #Sinovac dozi milioni 1 kutoka Serikali ya Uturuki

Soma - https://jamii.app/Uviko19
#JamiiForums
IRINGA: Mahakama ya Rufani Tanzania imeiondoa Mahakamani kesi iliyomkabili Abdul Nondo baada ya DPP kukosa nia ya kuendelea nayo

> Alishtakiwa kwa makosa ya kuchapisha taarifa za uongo Mtandaoni na kutoa taarifa za uongo kwa Mtumishi wa Umma Mafinga

Soma https://jamii.app/NondoKesi
KUELEKEA NDOA YA MREMA: Mwenyekiti wa TLP, Augustino Lyatonga #Mrema anatarajia kufunga ndoa Machi 24, 2022

> Mrema amesema ikitokea ameshindwa kufika Kanisani kutokana na hali yake ya kiafya, ndoa hiyo itafungiwa hata chumbani kwake

Soma > https://jamii.app/MremaNdoa
#JamiiForums
MATUMIZI YAKO YA SIMU YANAJENGA AU KUDHOOFISHA FAMILIA YAKO?

Mdau anasema kwa Dunia ya leo imekuwa ni changamoto kuweza kuhusiana vema Majumbani, Simu ikiwa moja ya sababu ya upungufu huo

Anasema baadhi ya Makosa ambayo Wazazi/Walezi huyafanya na Simu ni kuona Teknolojia ya Kidigitali haifai kwa Mtoto. Wengine hukosea kwa kummilikisha Mtoto kifaa cha Kidigitali bila misingi ya matumizi

Zaidi, soma - https://jamii.app/SimuFamilia
#DigitalSafety #Familia
MADEREVA WANAOSABABISHA AJALI KUPELEKWA MAHAKAMANI

Kamanda wa Polisi, Wilbroad Mutafungwa akiwa Kituo cha Mabasi cha Magufuli amesema β€œDereva atakayekutwa anaendesha Gari bila kufuata #Sheria atapelekwa Mahakamani na sio kulipa faini kama awali”

Soma - https://jamii.app/DerevaAjaliJela
MGOGORO WA #UKRAINE NA #URUSI: Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China, Wang Wenbin amesema hakuna nchi kati ya zilizopo ktk G20 inayoweza kumfukuza Uanachama Nchi nyingine

> Hii ni baada ya Marekani kuomba Urusi iondolewe G20

Soma https://jamii.app/G20
#RussiaUkraineConflict