JamiiForums
βœ”
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
KIGOMA: MAJAMBAZI WAUA MFANYABIASHARA NA KUPORA FEDHA

Daglas Kinungunyi, Mfanyabiashara na Mkazi wa Nyamidaho Wilayani Kasulu ameuawa kwa kupigwa risasi Mkono wa kulia na kwenye Nyonga kisha kuporwa Fedha ambazo hazijajulikana kiasi chake

Soma - https://jamii.app/MajambaziKasulu
#JFLeo
BIDEN AIONYA CHINA KUHUSU KUISAIDIA URUSI

Rais wa #Marekani, Joe Biden amemuonya Rais wa #China, Xi Jinping ikiwa wataisaidia vifaa vya kivita #Urusi

> Aidha, Rais Xi ametoa wito kwa NATO kuzungumza na Urusi ili kuondoa mzizi wa mgogoro uliopo

Soma https://jamii.app/ChinaUrusi
BRAZIL: TELEGRAM YAZUILIWA KWA KUTOFUATA SHERIA

Mahakama Kuu imezuia matumizi ya Telegram baada ya kutofuata Sheria inayotaka udhibiti wa taarifa zisizo sahihi

#Telegram inatumiwa sana na Rais Jair Bolsonaro na wafuasi wake

Soma - https://jamii.app/TelegramBrazil

#DigitalRights
KAMATI: KINYESI NA MIKOJO YA MIFUGO VILISABABISHA VIFO VYA SAMAKI MTO MARA

Kamati imebaini uwepo wa kinyesi cha ng'ombe tani milioni 1.8 na mkojo lita bilioni 1.5

> Hali hiyo imebadilisha rangi ya maji, harufu na samaki kufa kwa kukosa Oksijeni

Soma https://jamii.app/MtoKinyesi
UKRAINE: Wanajeshi wa Urusi wameripotiwa kuingia katika Mji wa #Mariupol na kupelekea kufungwa kwa Kampuni kuu ya chuma cha Pua

Afisa wa Polisi wa Mariupol amesema Watoto na Wazee wanafariki zaidi kutokana na mashambulizi

Soma - https://jamii.app/RussiaMauripol
#RussiaUkraineWar
UNICEF: 4% YA WATOTO WALIO MTANDAONI WALIFANYIWA UNYANYASAJI MWAKA 2021

Utafiti umeonesha Watoto wa miaka 12 - 17 wamekuwa wakitumiwa ujumbe wa vitisho au kutakiwa kushiriki ngono kwa malipo

Picha zao za utupu zilisambazwa mitandaoni bila ruhusa

Soma - https://jamii.app/OnlineChildren
VIFO VYA SAMAKI MTO MARA: MDAU ACHAMBUA RIPOTI ZINAZOKINZANA

Anasema, "Ikitokea Samaki wengi wamekufa ndani ya muda mfupi kuna tatizo. Kuhusu Maji kubadilika rangi hoja ya wingi wa Mafuta ingeeleweka, kinyesi na mkojo ni ngumu kubadilisha rangi"

Msome - https://jamii.app/Mara
RAIS ZELENSKY: KUSHINDWA KWA MAZUNGUMZO KUTAMAANISHA VITA YA 3 YA DUNIA

Rais wa #Ukraine, Volodymyr Zelensky amesema yuko tayari kwa mazungumzo ila hatokubali kutambua maeneo yanayojitenga

Amesema wangekuwa Wanachama wa NATO vita isingeanza

Soma https://jamii.app/MazungumzoUkraine
#JFLeo
#UKRAINE: Shirika la wakimbizi Duniani (UNHCR) limesema Watu milioni 10 wamekimbia kutokana na vita

90% ya waliokimbia ni Wanawake na Watoto. Watoto milioni 1.5 wako hatarini kukabiliwa na biashara haramu ya usafirishaji Binadamu

Soma - https://jamii.app/Refugees10MUkraine
#RussiaUkraineWar
JE, WAJUA? - Nyoka aina ya Koboko (Black Mamba) wana uwezo wa kurefuka hadi kufikia futi 14. Ndiyo Nyoka mrefu kuliko Nyoka wote wenye sumu Barani Afrika

Anakimbia kwa kasi kuliko Nyoka wote Duniani (20km/h). Akiwa na hasira ana uwezo wa kuinua moja ya tatu (1/3) ya Mwili wake

Soma zaidi - https://jamii.app/BlackMamba
#WildLife #Animals
Mtaalamu wa Afya ya Umma, Dkt. Katanta Simwanza amewashauriwa Wanawake kuacha kuweka ktk sehemu za siri dawa za kuongeza hamu ya ngono ambazo hazijapimwa na Wataalamu, kwani kufanya hivyo kunawaweka hatarini kupata Saratani ya Shingo ya Kizazi

Soma > https://jamii.app/AfyaSaratani
KIKOSI KAZI CHAPENDEKEZA MCHAKATO WA KATIBA MPYA UANZE BAADA YA 2025

Akiwasilisha taarifa ya Kikosi Kazi cha kuratibu maoni ya wadau wa #Demokrasia ya Vyama vingi vya Siasa, Profesa Rwekaza Mukandala amesema kuna ambao wanaona hakuna haja ya kuwa na #Katiba Mpya kwani ya sasa inaweza kufanyiwa marekebisho

Soma - https://jamii.app/KikosiKatiba2025
#Democracy
Rais Samia Suluhu Hassan ameagiza Kanuni za Uendeshaji Vyama vya Siasa zirekebishwe ili kuondoa upungufu

Amefafanua akisema β€œMwangalie zisikandamize, zisiuwe Vyama vya Siasa. Zilete Siasa zenye tija, isiwe kila siku tuko BBC, CNN, sio ustaarabu.”

Soma -https://jamii.app/SamiaVyamaSiasa
Kauli za Rais Samia Suluhu Hassan kuhusu #Katiba na Tume Huru ya Uchaguzi

#Demokrasia #Democracy #JamiiForums
Bunge la #Pakistan kukutana ili kupiga kura ya kutokuwa na imani na Waziri Mkuu, Imran Khan aliyeingia madarakani 2018

Mapema mwezi huu Muungano wa Vyama vya Upinzani uliwasilisha hoja ukisema Khan amepoteza idadi kubwa ya uungwaji mkono #Bungeni

Soma https://jamii.app/KuraImanPakistan
#JFLeo
Ili kuweza kutuma Maombi ya nafasi hizi tembelea - https://jamii.app/NafasiAjira

#JamiiForums