JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
Machi 8 ni Siku ya Wanawake Duniani

> Tunaungana na Watu wote kuadhimisha Siku hii, na tunawatakia Maadhimisho mema ya Siku ya Wanawake Duniani

#JamiiForums #IWD2022 #InternationalWomensDay
👍1
Takwimu zilizotolewa na Chuo Kikuu cha Johns Hopkins zimeonesha idadi ya Vifo vilivyotokana na #COVID19 vimefikia 5,999,158

Nchi nyingi zimelegeza masharti huku Safari na #Biashara zikianza kurejea. Aidha, kupata chanjo bado kunasisitizwa

Soma - https://jamii.app/COVID19Duniani

#UVIKO3
#UGANDA: Gabriel Rwotomiya amefariki kwa kupigwa risasi wakati Polisi wakituliza vurugu za Wanafunzi wa Sekondari Gulu baada ya kuzuiwa kutazama Mechi ya Man City na Man U, Machi 6

Wanafunzi wamerejeshwa Nyumbani na Shule kufungwa kwa muda

Soma - https://jamii.app/Uganda

#JFLeo
Katika Mwaka wa Fedha 2019/20, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) alipata taarifa za makusanyo ya Mapato katika Halmashauri 135

Alibaini Bilioni 18.77 zilikusanywa kutoka vyanzo mbalimbali, lakini hakuna ushahidi Mapato hayo yaliwasilishwa Benki

#JamiiForums #WAJIBU #JFUwajibikaji #Accountability
Katika kuadhimisha #InternationalWomensDay ni muhimu kuangazia changamoto mbalimbali zinazowakabili na kuhamasisha jitihada za kukomesha ukosefu wa #UsawaWaKijinsia

Leo, tunasherehekea na kutambua Uongozi, nguvu, uwezo, ujasiri na mchango walionao Wanawake wote katika Jamii

Maadhimisho ya Mwaka 2022 yanabeba Kaulimbiu isemayo, "Kizazi cha Haki na Usawa kwa Maendeleo Endelevu"

#JamiiForums #BreakTheBias #IWD2022
MDAU: WATUMISHI WAFUNDISHWE NAMNA BORA YA KUTUMIA MIKOPO WANAYOCHUKUA

Anasema Watumishi wa Serikali huvutiwa huchukua Mikopo wakiamini ni ya gharama nafuu hali inayowafanya wawe na madeni hadi wanastaafu

Ameshauri kiundwe chombo maalum cha kudhibiti usimamizi na uendeshaji wa Taasisi zote za Kifedha. Sheria ya Mafao iboreshwe ili kuwezesha Watumishi wanapostaafu wawe wanajengewe Nyumba za Makazi

Soma - https://jamii.app/WatumishiMadeni

#StoriesOfChange
Rushwa ya Ngono inatajwa kuwa tatizo linalowatafuna Wanawake ndani kwa ndani hasa maeneo ya Kazi

Utafiti wa Asasi ya Wanawake katika Habari Afrika (WIN) ulibaini 41% ya Wanawake wanahabari waliwahi kufanyiwa Unyanyasaji wa Kingono kazini

Soma - https://jamii.app/Womenday

#IWD2022
Rais Samia ametoa wito kwa Wananchi kujitokeza ktk zoezi la Sensa huku akisema suala jipya lililoongezwa ni swali kuhusu Anuani za Makazi

Asema hakutakuwa na swali kuhusu Dini kwa kuwa suala hilo lilishakataliwa tangu enzi za Mwl. Nyerere

Soma - https://jamii.app/DiniSensa
#JFLeo
MDAU: JAMII HAIWEZI KUCHOCHEA USTAWI BILA MAWAZO HURU

Anasema kukabiliana na changamoto kutahitaji sauti, uwazi na ukweli hivyo walio Madarakani wanahitaji kukosolewa

Jamii ikifungwa, watu wake wanakuwa kama Watumishi waoga badala ya Raia huru

Soma - https://jamii.app/UhuruKujieleza
Rais Samia Suluhu Hassan amesema kupanda kwa bei ya Mafuta kwa kiasi inasababishwa na Mgogoro kati ya Urusi na #Ukraine

Amesema “#Tanzania hatutanusurika, bidhaa zote zitapanda bei, nauli zitapanda bei, thamani ya kila kitu itapanda juu"

Soma - https://jamii.app/WomanDay

#IWD2022
Balozi wa #Urusi katika Umoja wa Mataifa (UN), Vassily Nebenzia, amesema Nchi yake itasitisha mapigano ili kuruhusu raia waliopo Kiev, Cher-nigov, Sumy na Mariupol kuondoka bila masharti kwa raia wanaopitia Urusi

Soma - https://jamii.app/RaiaWapite
#JamiiForums #RussiaUkraineConflict
KILIMANJARO: Grace Pima anashikiliwa na Polisi akidaiwa kumchoma Moto Mtoto wake wa Miaka Mitano Mdomoni na Puani kwa kosa la kutukana

Alifanya unyama huo Februari 28 na kumfungia Mtoto ndani kwa Saa 48 akimtibu kwa Dawa za Asili.

Soma - https://jamii.app/MotoMtoto
#UkatiliMtoto
#ZANZIBAR: Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (ZURA) imetangaza kuanzia Machi 9, Petroli itauzwa Tsh. 2,459, Dizeli Tsh. 2,500 na Mafuta ya Taa Tsh. 1,811 kwa Lita

Ongezeko limetokana na kupungua thamani ya Shilingi na tozo za Serikali

Soma https://jamii.app/MafutaZanzibar
UPDATE: Ofisi ya #HakiZaBinadamu ya Umoja wa Mataifa inasema Raia wa #Ukraine wapatao 474 wameuawa tangu uvamizi wa Urusi kuanza, lakini inahofiwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi

Ukraine imesema Vikosi vya Urusi vimeharibu takriban Hospitali 61

Soma - https://jamii.app/VifoUkraine
Mapungufu kadhaa kwenye ulipaji wa Mishahara kwa Watumishi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa yaliainishwa na CAG Mwaka 2019/20

Miongoni mwao ni Mamlaka 46 kushindwa kuwasilisha Makato ya Kisheria ya Mishahara yenye thamani ya Tsh. Bilioni 5.08 kwa Taasisi husika zikiwemo TRA (Tsh. Milioni 149.9) na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (Tsh. Bilioni 3.92)

#JamiiForums #WAJIBU #JFUwajibikaji #Accountability
KAMPUNI ZAENDELEA KUSITISHA BIASHARA URUSI

Coca-Cola, Starbucks, Pepsi na McDonald's zasitisha Biashara kufuatia uvamizi wa #Ukraine

Kumekuwepo na shinikizo kutaka Kampuni za Biashara kuchukua hatua kama ishara ya kupinga mateso wanayopata Raia

Soma - https://jamii.app/BiasharaUrusi
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Hussein Kattanga amesema ili kuikuza #Teknolojia ktk Uchumi wa Kidigitali ni lazima kuwa na mazingira wezeshi

Amesema Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) inapaswa kuwa Mlezi badala ya Mdhibiti/Ubabe

Soma - https://jamii.app/MleziTCRA

#DigitalRights
MDAU: TAIFA LINALOONGOZWA KIDEMOKRASIA LAZIMA LIFUATE MISINGI YAKE

Anasema Nchi inayoongozwa kwa Misingi ya Demokrasia inalazimika kutoa nafasi kwa Wananchi kumchagua Kiongozi wanayemhitaji bila udanganyifu wowote

Mihimili mikuu inayojenga Serikali inapaswa kufanya kazi kwa Uhuru bila kuingiliana kimajukumu

Soma - https://jamii.app/DemocracySOC

#StoriesOfChange
JE, WAJUA?: Kwenye Mgogoro wa #Ukraine na Urusi baadhi ya Watu wamebainika kuunga mkono vita kwa kutumia herufi ‘Z’ ikimaanisha ‘Za popedy’ yaani ushindi

Mwanariadha wa Kirusi, Ivan Kuliak anakabiliwa na kesi ya kinidhamu kwa kuonesha herufi hiyo

Soma - https://jamii.app/RussiaZ
SERIKALI YATOA TAHADHARI YA HOMA YA MANJANO

Waziri Ummy Mwalimu aagiza Maafisa wa Afya Mipakani kuhakikisha Wasafiri kutoka Nchi zenye Maambukizi wana vyeti vya Chanjo

Wananchi wametakiwa kuchukua tahadhari na kujua dalili za Ugonjwa huo

Soma - https://jamii.app/HomaManjano

#JFLeo