JamiiForums
52.8K subscribers
34.4K photos
2.45K videos
31.3K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
UGAWAJI WA MIRABAHA WAKOSOLEWA

Mtandao wa Sekta ya Ubunifu Tanzania(CINT) umesema mirabaha inapaswa kulipwa kwa kazi zote za ubunifu sio wanamuziki pekee

> COSOTA imekosolewa kukosa uwazi wa kanuni iliyotumika kugawa mirabaha

Soma https://jamii.app/MirabahaCOSOTA

#JFBurudani
NAPE: SHERIA INALENGA KUADHIBU MWANAHABARI SIO CHOMBO

Waziri wa Habari, Nape Nnauye amesema Sheria ya Habari ya 2016 inalenga kutoa leseni kwa wanahabari ili likitokea kosa aadhibiwe mtu sio Chombo cha Habari

> Nia ni kufanya tasnia ya habari kuwa taaluma

Soma https://jamii.app/KufungiaMtu

#PressFreedom
RUKWA: AMCHAPA MKEWE VIBOKO MPAKA KIFO

Kamanda wa Polisi Rukwa, ACP William Mwampaghale amesema Mwanaume huyo alianza kumshambulia Mkewe kwa fimbo maeneo mbalimbali ya Mwili na kusababisha kuvuja Damu nyingi kwa ndani na baadaye kusababisha mauti

Soma - https://jamii.app/KifoViboko

#JFMatukio #UkatiliKijinsia
SIKU YA KIMATAIFA YA HAKI ZA KIJAMII

Siku hii huangazia hitaji la kukuza Haki za Kijamii ambazo zinahusisha jitihada za kushughulikia masuala mbalimbali kama Umasikini, Ukosefu wa Usawa wa Kijinsia, Ajira na #HakiZaBinadamu

Soma - https://jamii.app/SJD2022

#SocialJusticeDay #SocialJustice
KAMATI YA KUCHUNGUZA MAUAJI YA MTWARA NA TANGA YAONGEZEWA SIKU 7

Kamati hiyo iliyoanza kazi Februari 4, 2022 ilipaswa kukamilisha ripoti yake Februari 17, 2022 ila imeomba muda zaidi kutokana na ukubwa wa kazi na kujiridhisha na baadhi ya masuala

Soma - https://jamii.app/KamatiMauaji7

#Accountability
NINI MAANA YA DHANA YA HAKI ZA KIJAMII?

Humaanisha uwepo wa Haki sawa kwa watu wote na uwezekano wa kila mtu, bila ubaguzi, kufaidika na Maendeleo ya Kiuchumi na Kijamii

Baadhi ya Haki za Kijamii ni pamoja na Usawa mbele ya #Sheria na Haki ya kupata Huduma za Afya

Soma - https://jamii.app/SJD2022

#SocialJusticeDay #SocialJustice
NIGER: Watoto saba (7) wameuawa na wengine watano (5) kujeruhiwa vibaya nchini humo baada ya shambulizi la anga la Jeshi la #Nigeria lililolenga wapiganaji walioko mpakani

> Mamlaka zinaendelea kufuatilia tukio hilo

Soma https://jamii.app/NigeriaNiger

#JFMatukio
HISTORIA: Chips za Viazi (Crisps) zilianza kutengenezwa Mwaka 1853 baada ya Mmarekani mweusi, George Speck (Mpishi) kupokea malalamiko ya Mteja akimlaumu kuwekewa Viazi vyenye mapande makubwa sana

Inadaiwa ili kuwakomoa Wateja, Speck alianza kukata vipande vidogovidogo mfano wa Karatasi lakini Wateja wakatokea kuvipenda sana.

Soma zaidi - https://jamii.app/SaratogaChips

#JFHistoria
40% YA WATU HAWATUMII LUGHA MAMA KWENYE ELIMU

Shirika la UN linalohusika na Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limesema Jamii hizo zimelazimika kufahamu Lugha zaidi ya moja

Februari 21 ni Siku ya Kimataifa ya Lugha Mama

Soma - https://jamii.app/LughaMama

#MotherLanguageDay #JFLugha
MALEZI: TUNZA AFYA YA MTOTO KWA KUMFUNDISHA USAFI

Usafi wa Kinywa: Mpigishe Mtoto Mswaki kila siku Asubuhi na ikiwezekana kila baada ya kula. Mfundishe namna ya kuswaki vizuri ili kuzuia kuoza kwa Meno na Magonjwa ya Fizi

Usafi wa Mikono: Wafundishe Watoto kunawa Mikono kwa Maji safi na sabuni kila wanapotoka Kucheza, kabla ya Kula, baada ya Kula na baada ya kutoka Maliwato

Soma - https://jamii.app/UsafiWatotoAfya

#JFMalezi #Parenthood
Uwajibikaji unapima kiwango ambacho Serikali inatekeleza majukumu yake katika kueleza na kuhalalisha Maamuzi yake kwa Umma

Ufanisi mkubwa wa #Uwajibikaji unaainishwa kwa namna ambavyo Wadai Haki/Wananchi wanaelezea mahitaji yao, lakini pia unahusiana na Nafasi, Uwezo na Utayari wa Watendaji kuwajibika kwa Matendo

Soma - https://jamii.app/UwajibikajiUfanisi
#Accountability #Democracy
MAGU: WAVUNJA MAKABURI NA KUIBA MISALABA, NONDO

Wananchi wamedai baadhi ya Makaburi yameharibiwa na kuachwa wazi au na mianya mikubwa huku vitu vikiibwa

Mkuu wa Wilaya ya Magu Mkoani Mwanza, Salum Kalli ameagiza wahusika wasakwe na kutiwa nguvuni

Soma - https://jamii.app/MakaburiMagu

#JFUwajibikaji
LINDI: Wanachama Wanne wa CHADEMA wamehukumiwa kifungo cha miaka 8 kwa kosa la kuharibu mali na kujeruhi watu wakiwemo Askari Polisi siku ya Uchaguzi Mkuu (Oktoba 28, 2020)

Katika utetezi walisema wahurumiwe kwa madai wana Familia zinazowategemea

Soma - https://jamii.app/LindiChadema

#JFSiasa
UNHCR: IDADI KUBWA YA WAKIMBIZI DUNIANI HUTOKEA NCHI TANO

Nchi hizo ni #Afghanistan, Myanmar, Sudan Kusini, Syria na #Venezuela

Kwa kila sekunde, kuna Mtu 1 anayakimbia Makazi yake kutokana na Mabadiliko ya Tabianchi/Hali ya Hewa

Soma - https://jamii.app/ClimateRefugees
#HumanRights
SHINYANGA: MBARONI KWA KUIBA MTOTO WA SIKU 20

Rehema Saidi (47) amekamatwa kwa tuhuma ya kuiba Mtoto Kituo cha Afya Lunguya

Wito umetolewa kwa Serikali kuimarisha ulinzi katika Vituo vya Afya na Zahanati ili kudhibiti wizi wa Watoto

Soma - https://jamii.app/WiziMtoto

#JFMatukio
WAZIRI NAPE: SHERIA YA ULINZI WA DATA NI YA MUHIMU

Amesema ni ya msingi katika Tanzania ya kidijitali ili watu wajiamini na kuwa huru

JamiiForums imekuwa mstari wa mbele kuitetea Haki ya Faragha kwa mujibu wa Ibara ya 16 ya Katiba

Soma https://jamii.app/NapeData

#DataProtection #DataPrivacy
MAREKANI YADAI INA ORODHA YA WANAOPASWA KUUAWA NA URUSI ITAKAPOIVAMIA UKRAINE

Marekani imedai miongoni mwa walengwa ni wapinzani wa kisiasa na makundi madogo ya watu wa Dini

Urusi imeendelea kukanusha kuwa na mpango wa kushambulia Ukraine

Soma - https://jamii.app/UrusiUkraine
#JFLeo
TANZANIA KUPATA MKOPO WA TRILIONI 1.5 KUTOKA BENKI YA DUNIA

Benki ya Dunia (WB) na #Tanzania zimesaini Mikataba ya Mkopo wa masharti nafuu wa Dola Milioni 650 kwa ajili ya Miradi ya kuboresha #Elimu na kuimarisha Usalama na umiliki ardhi

Soma - https://jamii.app/MkoboTrilioni

#Governance
HOJA: UNATAMANI UZEE WAKO UWEJE?

Mdau wa JamiiForums.com anasema akifikisha Miaka 60 hataki kutumia nguvu nyingi kutafuta riziki

Anatamani uwe wakati wa kukaa na Wajukuu zake. Pia, hatamani kuishi Mjini ambako kuna msongamano wa Watu

Je, nawe unataka Uzee wako uweje?

Mjadala - https://jamii.app/TamaaUzee
#Maisha
#MALI: Bunge la Mpito limepitisha kwa Kura zote Muswada wa kutawaliwa na Jeshi kwa miaka mitano. Mali iliingia katika Utawala wa Kijeshi baada ya Mapinduzi ya Mei 2021

Jumuiya mbalimbali zinashinikiza Utawala wa Kiraia kurejeshwa

Soma - https://jamii.app/MaliJeshi

#Democracy