JamiiForums
52.6K subscribers
34.4K photos
2.46K videos
31.4K links
Official Telegram Channel | Inform x Engage x Empower
Download Telegram
MDAU: MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOTAKA KUJENGA NIDHAMU BINAFSI ILI KUFIKIA MALENGO

Muda: Jifunze kusema 'Hapana' kwenye matukio yanayopoteza muda wako na wekeza muda mwingi kwenye masuala yanayokuongezea ujuzi

Fedha: Nidhamu bora ya fedha huchochea kutengeneza uwezekano wa ndoto zako. Wekeza katika maeneo yanayoendana na ndoto zako

Soma Makala - https://jamii.app/NidhamuSOC

#StoriesOfChange #JFMdau
TANZIA: MZEE KAMBAULAYA AFARIKI DUNIA

Msanii maarufu na Mwanahabari mkongwe, Barnabas Maro maarufu kama Mzee Kambaulaya au Baba Bishanga amefariki dunia Januari 4, 2022 Hospitali ya Taifa ya Muhimbili akipatiwa matibabu

Soma https://jamii.app/Kambaulaya
IRAN YATAKA TRUMP AWAJIBISHWE KWA MAUAJI YA SOLEIMANI

Rais Ebrahim Raisi ataka kuundwe Mahakama ambayo Donald Trump, Mike Pompeo na wengine watashtakiwa kwa mauaji ya Jenerali Qassem Soleimani yaliyotokea miaka 2 iliyopita, au Iran italipiza kisasi

Soma https://jamii.app/TrumpSoleimani

#JFUwajibikaji #Accountability
ISRAEL YAWA NCHI YA KWANZA KUTOA CHANJO YA NNE YA #COVID19

Ongezeko la maambukizi ya #Omicron limefanya watu wenye umri wa zaidi ya miaka 60 wapewe 'booster' ya pili

Wengine wanaopewa kipaumbele ni wenye Magonjwa Sugu na Wahudumu wa Afya

Soma https://jamii.app/SecondBoosterDose

#UVIKO3 #JFAfya
KENYA: Kiongozi wa ODM, Raila Odinga amehoji chanzo cha Mamilioni ya Fedha ambayo amesema Naibu Rais, William Ruto anamwaga kwenye Kampeni zake

Awataka Wakenya kutomchagua Ruto kuongoza Taifa hilo akisema Uongozi wake utatawaliwa na Ufisadi

Soma https://jamii.app/RailaRutoKE

#Accountability
MDAU: NAMNA SERIKALI INAVYOWEZA KUWASAIDIA WAHITIMU KATIKA UTAFUTAJI

1. Serikali na Sekta Binafsi zinapaswa kuwaamini Vijana na kuondoa kigezo cha uzoefu

2. Serikali itengeneze mahusiano mazuri na mataifa mengine, kwani hii itasaidia kupanua soko la nje

3. Kuwepo uwazi katika masuala ya Ajira kuanzia Serikali mpaka Mashirika Binafsi. Ukabila, Rushwa na Udini viepukwe

Soma - https://jamii.app/WahitimuSerikaliSOC

#StoriesOfChange #JFMdau
UTEUZI: Rais Samia amteua Dkt. Baghayo Saqware kuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA)

Charles Itembe ateuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Eneo Maalum la Mauzo ya Nje (EPZA), na Ernest Mchanga Katibu wa Tume ya Pamoja ya Fedha

Soma - https://jamii.app/Uteuzi3Rais

#Governance
MSUMBIJI: Rais Filipe Nyusi na mkewe Isaura Nyusi wamekutwa na #COVID19 na wamelazimika kujitenga

> Nchi hiyo imethibitisha kuwa na watu 193,000 wanaougua COVID-19, na vifo 2,031

Soma https://jamii.app/FilipeNyusi

#UVIKO3 #JFAfya
SUDAN: WANAHARAKATI WAITISHA MAANDAMANO ZAIDI

Wanaoongoza Kampeni dhidi ya Utawala wa Kijeshi wamesema Waandamanaji watakuwa wakielekea Ikulu hadi ushindi utakapopatikana

Idadi ya waliopoteza maisha tangu Mapinduzi kufanyika imefikia 56

Soma - https://jamii.app/ProtestsSdn

#Democracy
UTAJIRI WA KAMPUNI YA APPLE WAZIDI GDP YA AFRIKA

Kampuni ya Apple imefikisha thamani ya Dola trilioni 3 (takriban Tsh. Trilioni 6,920.88) katika Soko la Hisa

Pato la Ndani la Afrika (GDP) ni Dola Trilioni 2.6 sawa na Tsh. Trilioni 5,998.1

Soma - https://jamii.app/AppleUtajiri

#JFTech
MWIGULU: DENI NI HIMILIVU, TUTAENDELEA KUKOPA

Asema Mkopo sio Msaada na hutolewa kwa mwenye chanzo cha kulipa

Pia, amesema sio uungwana kusema Rais anakopa akisisitiza Marais hawakopi bali ni Serikali akisema "Hilo si jambo la Familia, ni la Nchi"

Soma https://jamii.app/MwiguluDeni

#Governance
👍1
RAIS SAMIA: TANZANIA IMEKUWA IKIKOPA TANGU UHURU

Amesema inashangaza Mtu anayetegemewa kushirikiana na Serikali kwenye safari ya maendeleo 'kuargue' kuhusu Tozo na Mkopo wa Trilioni 1.3 akisema, "Ni homa (fever) ya 2025, wasameheni"

Asema "Toka tunapata Uhuru ni Mikopo kwenda mbele. Na katika Mikopo yote huu ni mkopo mzuri zaidi"

Soma - https://jamii.app/RaisTozoMikopo

#Governance
RAIS SAMIA: TAIFA HALIWEZI KUENDESHWA NA TOZO PEKEE

Rais Samia asema kumekuwepo watu wanaohoji kwanini Nchi imekopa japokuwa kuna fedha za tozo, akifafanua kuwa Taifa haliwezi kwenda na fedha za tozo pekee

Amesema kuleta ustawi wa Nchi sio miujiza na ni lazima kutumia mbinu zote zilizopo

Soma - https://jamii.app/SSHTozo

#Governance
RAIS SAMIA KUFANYA MABADILIKO YA BARAZA LA MAWAZIRI HIVI KARIBUNI

Amesema ataenda na wale wote anaohisi wanaweza kwenda naye kuleta maendeleo kwa Watanzania na kwamba wale ambao anahisi ndoto zao ni "kule" atawapa nafasi waende kujiandaa

Asema, "Wakajitayarishe vizuri huko nje kwasababu nikiwatuma ndani nitawasumbua"

Soma - https://jamii.app/RaisBarazaMawaziri

#Governance
RAIS SAMIA: UMEME HAUWEZI KUUNGANISHWA KWA ELFU 27

Rais Samia Suluhu amesema ni ngumu kwa TANESCO kuwaunganishia umeme Watanzania kwa Tsh. 27,000

> Amesema Wananchi wamelipa lakini wanashindwa kuunganishiwa umeme kwa kuwa TANESCO hawana nguzo

Soma - https://jamii.app/Tsh27kTANESCO

#ServiceDelivery
PEMBA: WATU TISA WAFARIKI KWA AJALI YA BOTI

Boti iliyokuwa inatokea Chakechake kuelekea Panza kwa shughuli za mazishi imezama usiku wa kuamkia Januari 5, 2022

> Uokoaji ulisitishwa kwasababu ya giza ambapo maiti 9 ziliopolewa, na Watu 6 waliokolewa

Soma https://jamii.app/PembaAjalii

#JFMatukio
KAZAKHSTAN: SERIKALI YAJIUZULU KUFUATIA MAANDAMANO YA KUPINGA BEI ZA MAFUTA

Rais Kassym-Jomart Tokayev ametangaza Hali ya Dharura kwa wiki mbili katika baadhi ya maeneo

Hatua kadhaa za dharura zimetangazwa ikiwemo marufuku ya mikusanyiko

Soma - https://jamii.app/GovtResigns

#Accountability #JFUwajibikaji
HONG KONG YAPIGA MARUFUKU NDEGE KUTOKA NCHI 8

Miongoni mwa Nchi hizo ni Canada, Marekani na India. Mamlaka zimeweka marufuku hiyo kutokana na hofu ya Wimbi la Tano la #COVID19

Baa, klabu na makumbusho kufungwa ili kudhibiti maambukizi

Soma - https://jamii.app/FlightBanHK

#UVIKO3 #JFAfya #Governance
Wateja wa njia moja watalipia Tsh. 320,960, Tsh. 515,618 na Tsh. 696,670 kwa Mita 30, 70 na 120 ili kuunganishiwa umeme

Kwa njia 3 ni Tsh. 912,014, Tsh. 1,249,385 na Tsh. 1,639,156 kwa Mita 30, 70 na 120 mtawalia. Kwa Watu wa Kijijini ni Tsh. 27,000

Soma https://jamii.app/BeiKuunganisha

#ServiceDelivery
MDAU: NJIA ZA KUTATUA TATIZO LA AJIRA KWA VIJANA NCHINI

Kuanzisha Programu za Ujuzi, Elimu na Mafunzo: Serikali inatakiwa kuanzisha Mitaala Maalum itakayoweza kutumika kuanzia ngazi ya Msingi mpaka Vyuo

Kuboresha Sayansi na Teknolojia: Vijana wafunzwe ujuzi wa kubuni, kutengeneza na kutumia vifaa au programu zenye kulenga kutatua kero za kijamii

Soma - https://jamii.app/TatizoAjiraSOC

#StoriesOfChange #JFMdau